< 2 Reyes 16 >

1 Acaz, hijo de Jotam, llegó a ser rey de Judá en el año diecisiete del reinado de Peca, hijo de Remalías.
Katika mwaka wa kumi na saba wa utawala wa Peka mwana wa Remalia, Ahazi mwana wa Yothamu mfalme wa Yuda alianza kutawala.
2 Acaz tenía veinte años cuando llegó a ser rey, y reinó en Jerusalén durante dieciséis años. Pero a diferencia de David, su antepasado, no hizo bien las cosas a los ojos del Señor, su Dios.
Ahazi alikuwa na miaka ishirini alipoanza kutawala, akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na sita. Tofauti na Daudi baba yake, hakufanya yaliyo mema machoni pa Bwana, Mungu wake.
3 Siguió los caminos de los reyes de Israel, e incluso sacrificó a su hijo en el fuego, participando en las prácticas repugnantes de las naciones que el Señor había expulsado ante los israelitas.
Akaenenda katika njia za wafalme wa Israeli, na hata akamtoa mwanawe kafara katika moto, akifuata njia za machukizo za mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele ya Waisraeli.
4 Sacrificó y presentó holocaustos en los lugares altos y en las colinas, y bajo todo árbol verde.
Akatoa kafara na kufukiza uvumba katika mahali pa juu pa kuabudia miungu, juu ya vilima, na chini ya kila mti uliotanda.
5 Rezín, rey de Harán, y Peca, hijo de Remalías, rey de Israel, llegaron y atacaron Jerusalén. Asediaron a Acaz, pero no pudieron derrotarlo.
Kisha Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli wakaondoka kwenda kupigana dhidi ya Yerusalemu na kumzunguka Ahazi kwa jeshi, lakini hawakuweza kumshinda.
6 Fue entonces cuando Rezín, rey de Harán, recuperó Elat para Edom. Expulsó al pueblo de Judá y envió a los edomitas a Elat, donde todavía viven.
Wakati ule, Resini mfalme wa Aramu akaurudisha Elathi kwa Aramu kwa kuwafukuza watu wa Yuda. Kisha Waedomu wakahamia Elathi, nao wanaishi huko mpaka leo.
7 Ajaz envió mensajeros a Tiglat-pileser, rey de Asiria, diciendo: “Soy tu siervo y tu hijo. Por favor, ven a rescatarme de los reyes de Harán e Israel que me están atacando”.
Ahazi akatuma wajumbe kumwambia Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru kwamba, “Mimi ni mtumishi na mtumwa wako. Njoo na uniokoe kutoka mkononi mwa mfalme wa Aramu na wa mfalme wa Israeli, ambao wananishambulia.”
8 Acaz tomó la plata y el oro del Templo del Señor y de los tesoros del palacio real, y se lo envió al rey de Asiria como regalo.
Naye Ahazi akachukua fedha na dhahabu zilizopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina ya jumba la mfalme, na kuzituma kama zawadi kwa mfalme wa Ashuru.
9 El rey de Asiria le respondió positivamente. Fue y atacó Damasco, y la capturó. Deportó a sus habitantes a Quir y ejecutó a Rezín.
Mfalme wa Ashuru akamwitikia kwa kushambulia Dameski na kuiteka. Akawahamishia wenyeji wake huko Kiri, na kumuua Resini.
10 El rey Acaz fue a Damasco para reunirse con Tiglat-Pileser, rey de Asiria. Durante su visita vio un altar en Damasco, y envió al sacerdote Urías un dibujo del altar, junto con las instrucciones de cómo construirlo.
Kisha Mfalme Ahazi akaenda Dameski kukutana na Tiglath-Pileseri wa Ashuru. Akaona madhabahu huko Dameski, naye akamtumia Uria kuhani mchoro wa hayo madhabahu, pamoja na maelezo ya mpango kamili wa ujenzi wake.
11 El sacerdote Urías construyó el altar siguiendo todas las instrucciones que el rey Acaz había enviado desde Damasco, y lo terminó antes de que el rey Acaz regresara.
Kwa hiyo Uria kuhani akajenga madhabahu kulingana na mipango yote ambayo Mfalme Ahazi alikuwa ameituma kutoka Dameski, na akamaliza ujenzi kabla ya Mfalme Ahazi kurudi.
12 Cuando el rey regresó de Damasco vio el altar. Se acercó a él y ofreció ofrendas en él.
Mfalme aliporudi kutoka Dameski na kuona hayo madhabahu, akayasogelea na kutoa sadaka juu yake.
13 Presentó su holocausto y su ofrenda de grano, derramó su libación y roció sobre él la sangre de sus ofrendas de paz.
Akatoa sadaka yake ya kuteketezwa na sadaka ya nafaka, akamimina sadaka ya kinywaji na kunyunyizia damu ya sadaka zake za amani juu ya hayo madhabahu.
14 También trasladó el altar de bronce que estaba ante el Señor desde el frente del Templo, entre el nuevo altar y el Templo del Señor, y lo colocó al norte del nuevo altar.
Mfalme Ahazi akayaondoa madhabahu ya zamani ya shaba kutoka hapo mbele ya Hekalu la Bwana, yaliyokuwa yamesimama kati ya ingilio la Hekalu na hayo madhabahu mapya, naye akayaweka upande wa kaskazini mwa hayo madhabahu mapya.
15 Entonces el rey Acaz ordenó al sacerdote Urías “Usa este nuevo e importante altar para ofrecer el holocausto de la mañana, la ofrenda de grano de la tarde, el holocausto y la ofrenda de grano del rey, y el holocausto de todo el pueblo, y sus ofrendas de grano y sus libaciones. Rocía sobre este altar la sangre de todos los holocaustos y sacrificios. El viejo altar de bronce lo usaré para la adivinación”.
Ndipo Mfalme Ahazi akatoa amri zifuatazo kwa Uria kuhani: “Juu ya hayo madhabahu kubwa mapya, toa sadaka ya asubuhi ya kuteketezwa na sadaka ya jioni ya nafaka, sadaka ya mfalme ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya nafaka, sadaka ya kuteketezwa ya watu wote wa nchi, pamoja na sadaka yao ya nafaka na sadaka yao ya kinywaji. Unyunyize juu ya hayo madhabahu damu yote ya sadaka za kuteketezwa na dhabihu. Lakini mimi nitatumia hayo madhabahu ya zamani ya shaba kwa ajili ya kutafuta uongozi.”
16 El sacerdote Urías siguió las órdenes del rey Acaz.
Naye Uria kuhani akafanya kama Mfalme Ahazi alivyoagiza.
17 El rey Acaz también quitó los armazones de los carros móviles, y también sacó la pila de bronce de cada uno de ellos. Quitó el Mar de los toros de bronce sobre los que descansaba y lo colocó sobre un pedestal de piedra.
Mfalme Ahazi akaondoa mbao za pembeni na kuondoa masinia kwenye vile vishikilio vilivyohamishika. Akaondoa ile Bahari kutoka kwenye mafahali wa shaba walioishikilia, na kuiweka kwenye kitako cha jiwe.
18 Derribó el dosel del sábado que habían construido en el Templo, así como la entrada exterior del rey al Templo del Señor. Hizo esto para complacer al rey de Asiria.
Kwa heshima ya mfalme wa Ashuru, akaliondoa pia pazia la Sabato lililokuwa limewekwa ndani ya Hekalu, na akaondoa ile njia ya kifalme ya kuingia kwenye Hekalu la Bwana.
19 El resto de lo que sucedió en el reinado de Acaz y todo lo que hizo está registrado en el Libro de las Crónicas de los Reyes de Judá.
Matukio mengine ya utawala wa Ahazi na yale aliyoyafanya, je hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
20 Acaz murió y fue enterrado con sus antepasados en la Ciudad de David. Su hijo Ezequías le sucedió como rey.
Ahazi akalala na baba zake, naye akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Naye Hezekia mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 2 Reyes 16 >