< 2 Crónicas 4 >

1 Salomón hizo un altar de bronce de veinte codos de largo, veinte de ancho y diez de alto.
Mfalme Solomoni akatengeneza madhabahu ya shaba yenye urefu wa dhiraa ishirini, upana wa dhiraa ishirini na kimo chake dhiraa kumi.
2 Hizo un “Mar” de metal fundido, diez codos de diámetro, cinco de altura y treinta de circunferencia.
Akatengeneza Bahari ya kusubu, yenye umbo la mviringo, ya dhiraa kumi kutoka ukingo hadi ukingo na kimo cha dhiraa tano. Kamba ya urefu wa dhiraa thelathini ingeweza kuizunguka.
3 Debajo de ella había toros ornamentales a su alrededor, diez por codo. Estaban en dos filas cuando todo estaba fundido.
Chini ya huo ukingo, kulikuwa na mafahali kuizunguka, yaani mafahali kumi katika kila dhiraa moja. Hayo mafahali waliyasubu katika safu mbili yakiwa ya kitu kimoja na hiyo Bahari.
4 El Mar estaba sostenido por doce estatuas de toros, tres orientadas al norte, tres al oeste, tres al sur y tres al este. El Mar estaba colocado sobre ellos, con sus espaldas hacia el centro.
Bahari hiyo ilikaa juu ya mafahali kumi na wawili, mafahali watatu walielekeza nyuso zao kaskazini, watatu magharibi, watatu kusini na watatu mashariki. Bahari hiyo ilikaa juu ya hao mafahali, nazo sehemu zao za nyuma zilielekeana.
5 Era tan grueso como el ancho de una mano, y su borde era como el borde acampanado de una copa o de una flor de lis. Contenía tres mil baños.
Unene wake ulikuwa nyanda nne, na ukingo wake ulifanana na ukingo wa kikombe, kama ua la yungiyungi iliyochanua. Iliweza kuchukua bathi 3,000.
6 También hizo diez pilas sobre carros para lavar. Colocó cinco en el lado sur y cinco en el norte. Se usaban para limpiar lo que se usaba en los holocaustos, pero el Mar lo usaban los sacerdotes para lavarse.
Kisha akatengeneza masinia kumi kwa ajili ya kuoshea vifaa, naye akayaweka matano upande wa kusini na matano upande wa kaskazini. Ndani yake ndimo walioshea vifaa vya kutumika katika sadaka za kuteketezwa, lakini ile Bahari ilikuwa ni kwa ajili ya makuhani kunawia.
7 Hizo diez candelabros de oro como se había especificado, y las colocó en el Templo, cinco en el lado sur y cinco en el norte.
Akatengeneza vinara vya taa kumi vya dhahabu kama ilivyoainishwa kwao na kuviweka hekaluni, vinara vitano upande wa kusini na vitano upande wa kaskazini.
8 Además, hizo diez mesas y las colocó en el Templo, cinco en el lado sur y cinco en el norte. También hizo cien pilas de oro.
Akatengeneza meza kumi na kuziweka hekaluni, tano upande wa kusini na tano upande wa kaskazini. Pia akatengeneza mabakuli 100 ya dhahabu ya kunyunyizia.
9 Salomón también construyó el patio de los sacerdotes, el patio grande y las puertas del patio, y cubrió las puertas con bronce.
Akatengeneza ukumbi wa makuhani na ukumbi mwingine mkubwa na milango yake, naye akaifunika hiyo milango kwa shaba.
10 Colocó el Mar en el lado sur, junto a la esquina sureste.
Akaweka ile Bahari upande wa kusini, kwenye pembe ya kusini mashariki ya nyumba.
11 Hiram también hizo las ollas, las palas y las pilas. Hiram terminó el trabajo que había estado haciendo para el rey Salomón en el Templo de Dios:
Pia akatengeneza masufuria, masepetu na mabakuli ya kunyunyizia. Kwa hiyo Huramu akakamilisha kazi katika Hekalu la Mungu kama vile Mfalme Solomoni alikuwa amemwagiza, yaani:
12 las dos columnas; los dos capiteles en forma de cuenco en la parte superior de las columnas; los dos juegos de redes que cubrían las dos cazoletas de los capiteles de la parte superior de las columnas;
zile nguzo mbili; yale mataji mawili yaliyokuwa juu ya hizo nguzo, zile nyavu mbili za kupamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli yaliyowekwa juu ya zile nguzo;
13 las cuatrocientas granadas ornamentales para los dos conjuntos de red -dos filas de granadas para cada red que cubrían las dos cazoletas de los capiteles de la parte superior de las columnas-;
yale makomamanga 400 kwa ajili ya hizo nyavu mbili (safu mbili za makomamanga kwa kila wavu yakipamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo);
14 los carros de agua y las pilas de los carros de agua;
vishikio pamoja na masinia yake;
15 el Mar y las doce estatuas de toros que lo sostenían; las ollas, las palas, los tenedores y todo lo demás.
hiyo Bahari na hao mafahali kumi na wawili chini yake;
16 Todo el trabajo de metal que Hiram hizo para el rey Salomón para la casa del Señor era de bronce pulido.
pia hayo masufuria, masepetu, uma za nyama na vyombo vingine vyote vilivyohusiana. Vitu vyote ambavyo Huramu-Abi alimtengenezea Mfalme Solomoni kwa ajili ya Hekalu la Bwana vilikuwa vya shaba iliyosuguliwa.
17 El rey los fundió en moldes de arcilla en la llanura del Jordán, entre Sucot y Zereda.
Mfalme aliagiza wavisubu vitu hivi kwenye kalibu za udongo wa mfinyanzi katika uwanda wa Yordani kati ya Sukothi na Sereda.
18 Salomón hizo tantas de estas cosas que no se podía medir el peso del bronce utilizado.
Vitu hivi vyote Mfalme Solomoni alivyotengeneza vilikuwa vingi sana hivi kwamba uzito wa shaba haungekadirika.
19 Salomón hizo también todo lo que se utilizaba en el Templo de Dios: el altar de oro; las mesas donde se exponía el Pan de la Presencia;
Solomoni pia akatengeneza samani zote zilizokuwa ndani ya Hekalu la Mungu: madhabahu ya dhahabu; meza za kuweka mikate ya Wonyesho;
20 los candelabros de oro puro y sus lámparas que debían arder delante del Lugar Santísimo, tal como se había especificado;
vinara vya taa vya dhahabu safi pamoja na taa zake ili ziwake mbele ya sehemu takatifu ya ndani kama ilivyoelekezwa;
21 las flores decorativas, las lámparas y las pinzas, todo de oro macizo;
maua ya dhahabu yaliyofanyizwa, taa na makoleo (vilikuwa vya dhahabu bora kabisa);
22 los adornos para las mechas, las jofainas, los platos y los incensarios, todo de oro; y las puertas del Templo: las puertas interiores del Lugar Santísimo y las puertas de la sala principal, todas cubiertas de oro.
mikasi ya dhahabu safi, mabakuli ya kunyunyizia, masinia na vyetezo; milango ya dhahabu ya Hekalu: yaani milango ya ndani ya Patakatifu pa Patakatifu, na milango ya ukumbi mkuu.

< 2 Crónicas 4 >