< 1 Timoteo 2 >

1 En primer lugar quiero animarte a orar por todos: haz peticiones y agradece en nombre de ellos.
Awali ya yote, nasihi kwamba dua, sala, maombezi na shukrani zifanyike kwa ajili ya watu wote:
2 De este mismo modo ora por los reyes y por todo tipo de líderes, para que podamos tener una vida tranquila y pacífica, siempre pensando en Dios y tomando la vida con seriedad.
kwa ajili ya wafalme na wale wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi kwa amani na utulivu, katika uchaji wote wa Mungu na utakatifu.
3 Esto es bueno, y es lo que agrada a Dios, nuestro Salvador.
Jambo hili ni jema, tena linapendeza machoni pa Mungu Mwokozi wetu,
4 Porque él desea que todos seamos salvos y comprendamos la verdad.
anayetaka watu wote waokolewe na wafikie kuijua kweli.
5 Pues hay un Dios, y un mediador entre Dios y la humanidad, el hombre Cristo Jesús.
Kwa maana kuna Mungu mmoja na mpatanishi mmoja kati ya Mungu na wanadamu, yaani mwanadamu Kristo Yesu,
6 Él se entregó a fin de que todos pudiéramos ser rescatados nuevamente, demostrando la evidencia a su debido tiempo.
aliyejitoa mwenyewe kuwa fidia kwa ajili ya wanadamu wote: jambo hili lilishuhudiwa kwa wakati wake ufaao.
7 Fui designado para compartir este mensaje y ser su mensajero, ser un maestro para los extranjeros sobre la fe en Dios y la verdad (no miento, digo la verdad).
Nami kwa kusudi hili nimewekwa niwe mhubiri na mtume (nasema kweli katika Kristo wala sisemi uongo), mwalimu wa watu wa Mataifa katika imani na kweli.
8 Lo que realmente quiero es que los hombres en todas partes oren a Dios con sinceridad. ¡Sin enojos ni discusiones!
Nataka kila mahali wanaume wasali wakiinua mikono mitakatifu pasipo hasira wala kugombana.
9 Del mismo modo, las mujeres deben vestir con prudencia, con modestia y apropiadamente. Deben ser atractivas pero no por su corte de cabello o por el uso de oro, perlas o ropas costosas,
Vivyo hivyo nataka wanawake wajipambe kwa adabu na kwa heshima katika mavazi yanayostahili, si kwa kusuka nywele, kuvalia dhahabu, lulu au mavazi ya gharama kubwa,
10 sino por las cosas buenas que hacen, como es apropiado en las mujeres que dicen seguir a Dios.
bali kwa matendo mazuri kama iwapasavyo wanawake wanaokiri kuwa wanamcha Mungu.
11 Las mujeres deben aprender en silencio, respetando su lugar.
Mwanamke na ajifunze kwa utulivu na kwa utiifu wote.
12 Yo no permito que las mujeres sean instructoras, o que dominen a los hombres; háganlas permanecer en silencio.
Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha au kuwa na mamlaka juu ya mwanaume. Mwanamke inampasa kukaa kimya.
13 Pues Adán fue creado primero, y luego Eva.
Kwa maana Adamu aliumbwa kwanza, kisha Eva.
14 Adán no fue engañado, pero Eva sí fue engañada por completo, y cayó en pecado.
Wala si Adamu aliyedanganywa, bali ni mwanamke aliyedanganywa akawa mkosaji.
15 No obstante, las mujeres serán salvadas por convertirse en madres, siempre y cuando sigan con fe y amor, y vivan vidas prudentes en santidad.
Lakini mwanamke ataokolewa kwa kuzaa kwake, kama wakiendelea kudumu katika imani, upendo na utakatifu, pamoja na kuwa na kiasi.

< 1 Timoteo 2 >