< 1 Crónicas 9 >

1 Todo el pueblo de Israel quedó registrado en los registros de las genealogías del libro de los reyes de Israel. Pero el pueblo de Judá fue llevado al cautiverio en Babilonia porque había sido infiel.
Waisraeli wote waliorodheshwa katika koo zilizoandikwa kwenye kitabu cha wafalme wa Israeli. Watu wa Yuda walichukuliwa mateka kwenda Babeli kwa sababu ya kukosa uaminifu kwa Mungu.
2 Los primeros en regresar y reclamar sus propiedades y vivir en sus ciudades fueron algunos israelitas, sacerdotes, levitas y servidores del Templo.
Basi watu wa kwanza kurudi kukaa kwenye milki zao katika miji yao walikuwa baadhi ya Waisraeli, makuhani, Walawi na watumishi wa Hekalu.
3 Algunos de los miembros de las tribus de Judá, Benjamín, Efraín y Manasés volvieron a vivir en Jerusalén. Entre ellos estaban:
Wale waliotoka Yuda, Benyamini, Efraimu na Manase ambao waliishi Yerusalemu walikuwa:
4 Utaí hijo de Ammihud, hijo de Omrí, hijo de Imrí, hijo de Baní, descendiente de Fares, hijo de Judá.
Uthai mwana wa Amihudi, mwana wa Omri, mwana wa Imri, mwana wa Bani, wa wana wa Peresi, mwana wa Yuda.
5 De los silonitas: Asaías (el primogénito) y sus hijos.
Wazao wa Washiloni waliorudi ni: Asaya mzaliwa wa kwanza na wanawe.
6 De los zeraítas: Jeuel y sus parientes, con un total de 690.
Kwa wana wa Zera: Yeueli. Watu wa Yuda jumla yao walikuwa watu 690.
7 De los benjamitas: Salú, hijo de Mesulam, hijo de Hodavías, hijo de Asenúa;
Kwa Benyamini walikuwa: Salu mwana wa Meshulamu, mwana wa Hodavia, mwana wa Hasenua;
8 Ibneías, hijo de Jeroham; Ela, hijo de Uzi, hijo de Micrí; y Mesulam, hijo de Sefatías, hijo de Reuel, hijo de Ibniás.
Ibneya mwana wa Yerohamu, Ela mwana wa Uzi, mwana wa Mikri; na Meshulamu mwana wa Shefatia, mwana wa Reueli, mwana wa Ibniya.
9 Todos ellos eran jefes de familia, según consta en sus genealogías, y en total sumaban 956.
Watu kutoka Benyamini kama walivyoorodheshwa katika koo zao jumla yao ni 956. Watu hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa zao.
10 De los sacerdotes: Jedaías, Joiarib, Yacín,
Wa jamaa za makuhani walikuwa: Yedaya, Yehoyaribu na Yakini;
11 Azarías hijo de Hilcías, hijo de Mesulam, hijo de Sadoc, hijo de Meraiot, hijo de Ajitub. (Azarías era el funcionario principal a cargo de la casa de Dios).
Azaria mwana wa Hilkia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayothi, mwana wa Ahitubu aliyekuwa afisa kiongozi wa nyumba ya Mungu.
12 También Adaías hijo de Jeroham, hijo de Pasur, hijo de Malquías, y Masai hijo de Adiel, hijo de Jazera, hijo de Mesulam, hijo de Mesilemit, hijo de Imer.
Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya; Maasai, mwana wa Adieli, mwana wa Yahzera, mwana wa Meshulamu, mwana wa Meshilemithi, mwana wa Imeri.
13 Los sacerdotes, que eran jefes de familia, sumaban 1.760. Eran hombres fuertes y capaces que servían en la casa de Dios.
Makuhani waliokuwa viongozi wa jamaa zao walikuwa 1,760. Walikuwa watu wenye uwezo, waliowajibika kuhudumu katika nyumba ya Mungu.
14 De los levitas: Semaías, hijo de Jasub, hijo de Azricam, hijo de Hasabías, descendiente de Merari;
Jamaa za Walawi walikuwa: Shemaya, mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, wa wana wa Merari.
15 Bacbacar, Heres, Galal y Matanías, hijo de Mica, hijo de Zicri, hijo de Asaf;
Bakbakari, Hereshi, Galali na Matania mwana wa Mika, mwana wa Zikri, mwana wa Asafu.
16 Abdías, hijo de Semaías, hijo de Galal, hijo de Jedutún; y Berequías, hijo de Asa, hijo de Elcana, que vivían en las aldeas de los netofatitas.
Obadia mwana wa Shemaya, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni. Berekia mwana wa Asa, mwana wa Elikana, ambao waliishi katika vijiji vya Wanetofathi.
17 Los guardas de la puerta del Templo: Salum, Acub, Talmón, Ahimán y sus parientes. Salum era el jefe de los guardianes de la puerta del Templo.
Mabawabu katika Hekalu la Bwana waliorudi walikuwa: Shalumu, Akubu, Talmoni, Ahimani na ndugu zao. Shalumu alikuwa mlinzi wao mkuu.
18 Ellos tenían la responsabilidad hasta ahora de cuidar la Puerta del Rey en el lado Este. Eran los guardianes de los campamentos de los levitas.
Walikuwa wamewekwa katika lango la mfalme lililokuwa upande wa mashariki, mpaka wakati huu. Hawa walikuwa mabawabu wa kutoka kwenye kambi ya Walawi.
19 Salum era hijo de Coré, hijo de Ebiasaf, hijo de Coré. Él y sus parientes, los coreítas, eran responsables de vigilar las entradas del santuario de la misma manera que sus padres se habían encargado de vigilar la entrada de la casa de campaña del Señor.
Shalumu mwana wa Kore, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora, pamoja na mabawabu wenzake kutoka jamaa yake ya Kora waliwajibika kulinda malango ya Hema, kama vile baba zao walivyokuwa wamewajibika kulinda ingilio la Maskani ya Bwana.
20 Anteriormente, Finees hijo de Eleazar, había sido el líder de los porteros. Y el Señor estaba con él.
Hapo zamani Finehasi mwana wa Eleazari alikuwa kiongozi wa mabawabu, naye Bwana alikuwa pamoja naye:
21 Posteriormente, Zacarías hijo de Meselemías fue el portero de la entrada de la tienda de reunión.
Zekaria mwana wa Meshelemia alikuwa bawabu katika ingilio la Hema la Kukutania.
22 En total hubo 212 elegidos para ser porteros en las entradas. Registraron sus genealogías en sus ciudades de origen. David y el profeta Samuel habían seleccionado a sus antepasados por su fidelidad.
Jumla ya waliochaguliwa kuwa mabawabu katika sakafu za kupuria nafaka walikuwa watu 212. Waliandikishwa kwa koo zao kwenye vijiji vyao. Mabawabu hawa waliwekwa katika nafasi zao za kuaminiwa na Daudi pamoja na mwonaji Samweli.
23 Ellos y sus descendientes eran responsables de vigilar la entrada de la casa del Señor, también cuando era una tienda.
Wao na wazao wao walikuwa viongozi wa kulinda malango ya nyumba ya Bwana, nyumba iliyoitwa Hema.
24 Los porteros estaban ubicados en cuatro lados: al este, al oeste, al norte y al sur.
Mabawabu walikuwa pande zote nne: mashariki, magharibi, kaskazini na kusini.
25 Sus parientes en sus pueblos venían cada siete días a ciertas horas para ayudarlos.
Ndugu zao katika vijiji vyao walikuwa wakija mara kwa mara na kuwasaidia katika kazi zao kwa vipindi mbalimbali vya siku saba.
26 Los cuatro porteros principales, que eran levitas, tenían la responsabilidad de cuidar las habitaciones y los tesoros de la casa de Dios.
Lakini mabawabu wanne wakuu, waliokuwa Walawi, walikabidhiwa wajibu kwa ajili ya vyumba na hazina katika nyumba ya Mungu.
27 Pasaban la noche alrededor de la casa de Dios porque tenían que vigilarla y tenían la llave para abrirla por la mañana.
Walikesha mahali walipowekwa kuizunguka nyumba ya Mungu, kwa sababu iliwapasa kuilinda. Pia walitunza funguo kwa ajili ya kufungua mlango kila siku asubuhi.
28 Algunos de los porteros eran responsables de los artículos que se utilizaban en los servicios de culto. Llevaban un inventario de lo que se traía y de lo que se sacaba.
Baadhi yao walikuwa viongozi wa kutunza vifaa vilivyotumika katika huduma ndani ya Hekalu; walivihesabu kila vilipoingizwa ndani na kila vilipotolewa.
29 A otros se les asignaba la tarea de cuidar el mobiliario y el equipo utilizado en el santuario, así como la harina especial, el vino, el aceite de oliva, el incienso y las especias.
Wengine walipangiwa kutunza mapambo na vifaa vingine vya patakatifu, pamoja na unga, divai, mafuta, uvumba na vikolezo.
30 (Sin embargo, algunos de los sacerdotes eran los encargados de mezclar las especias).
Lakini baadhi ya makuhani walifanya kazi ya kuchanganya vikolezo.
31 A Matatías, un levita, que era el hijo primogénito de Salum el coreíta, se le dio la responsabilidad de hornear el pan usado en las ofrendas.
Mlawi aliyeitwa Matithia, mwana mzaliwa wa kwanza wa Shalumu, wa ukoo wa Kora, alikabidhiwa wajibu kwa ajili ya kuoka mikate ya sadaka.
32 Otros coatitas se encargaban de preparar el pan que se ponía en la mesa cada sábado.
Baadhi ya ndugu zao wa ukoo wa Kohathi walikuwa viongozi wa kuandaa mikate ya Wonyesho kwa ajili ya kila Sabato, mikate iliyokuwa inawekwa mezani.
33 Los músicos, jefes de familias de levitas, vivían en las habitaciones del Templo y no debían realizar otras tareas porque estaban de servicio día y noche.
Wale waliokuwa waimbaji, viongozi wa jamaa za Walawi, waliishi katika vyumba vya Hekalu, nao hawakufanya shughuli nyingine yoyote kwa sababu iliwapasa kuwajibika kwa kazi hiyo usiku na mchana.
34 Todos ellos eran jefes de familias de levitas, líderes según sus genealogías, y vivían en Jerusalén.
Hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa za Walawi, wakuu kama walivyoorodheshwa katika koo zao, nao waliishi Yerusalemu.
35 Jeiel era el padre de Gabaón y vivía en Gabaón. Su mujer se llamaba Maaca.
Yeieli alikuwa baba yake Gibeoni naye aliishi huko Gibeoni. Mke wake aliitwa Maaka,
36 Su hijo primogénito fue Abdón, luego Zur, Cis, Baal, Ner, Nadab,
mwanawe mzaliwa wa kwanza alikuwa Abdoni, akafuatiwa na Suri, Kishi, Baali, Neri, Nadabu,
37 Gedor, Ahío, Zacarías y Miclot.
Gedori, Ahio, Zekaria na Miklothi.
38 Miclot fue el padre de Simeam. Ellos también vivían cerca de sus parientes en Jerusalén.
Miklothi akamzaa Shimeamu. Wao pia waliishi karibu na jamaa zao huko Yerusalemu.
39 Ner fue el padre de Cis, Cis fue el padre de Saúl, y Saúl fue el padre de Jonatán, Malquisúa, Abinadab y Es-Baal.
Neri akamzaa Kishi, Kishi akamzaa Sauli. Sauli akamzaa Yonathani, Malki-Shua, Abinadabu na Esh-Baali.
40 El hijo de Jonathan: Merib-Baal, que fue el padre de Miqueas.
Yonathani akamzaa Merib-Baali, naye Merib-Baali akamzaa Mika.
41 Los hijos de Miqueas: Pitón, Melec, Tarea y Acaz.
Wana wa Mika walikuwa: Pithoni, Meleki, Tarea, na Ahazi.
42 Acaz fue el padre de Jada, Jada fue el padre de Alemet, Azmavet y Zimri, y Zimri fue el padre de Mosa.
Ahazi akamzaa Yara, Yara akawazaa Alemethi, Azmawethi na Zimri, naye Zimri akamzaa Mosa.
43 Mosa fue el padre de Bina; Refaías fue su hijo, Elasa su hijo, y Azel su hijo.
Mosa akamzaa Binea, Binea akamzaa Refaya, na mwanawe huyo ni Eleasa, na mwanawe huyo ni Aseli.
44 Azel tuvo seis hijos. Sus nombres eran: Azricam, Bocru, Ismael, Searías, Obadías y Hanán. Estos fueron los hijos de Azel.
Aseli alikuwa na wana sita, na haya ndiyo majina yao: Azrikamu, Bokeru, Ishmaeli, Shearia, Obadia na Hanani. Hawa ndio waliokuwa wana wa Aseli.

< 1 Crónicas 9 >