< 1 Crónicas 8 >

1 Benjamín fue el padre de Bela (su primogénito), Asbel (el segundo), Ahara (el tercero),
Benyamini akamzaa: Bela mzaliwa wake wa kwanza, Ashbeli mwanawe wa pili, Ahara mwanawe wa tatu,
2 Noé (el cuarto) y Rafa (el quinto).
Noha mwanawe wa nne na Rafa mwanawe wa tano.
3 Los hijos de Bela fueron: Adar, Gera, Abiud,
Wana wa Bela walikuwa: Adari, Gera, Abihudi,
4 Abisúa, Naamán, Ahoa,
Abishua, Naamani, Ahoa,
5 Gera, Sefufán y Huram.
Gera, Shefufani na Huramu.
6 Estos fueron los hijos de Aod, jefes de familia que vivían en Geba, y fueron desterrados a Manahat:
Hawa ndio wazao wa Ehudi, waliokuwa viongozi wa jamaa za wale walioishi huko Geba na ambao walihamishiwa Manahathi:
7 Naamán, Ahías y Gera. Gera fue quien los exilió. Era el padre de Uzz y Ahiud.
Naamani, Ahiya na Gera. Gera alikuwa baba yao Uza na Ahihudi na ndiye aliwaongoza kwenda uhamishoni.
8 Saharaim tuvo hijos en Moab después de divorciarse de sus esposas Husim y Baara.
Shaharaimu aliwazaa wana katika nchi ya Moabu baada ya kuwapa talaka wake zake wawili yaani, Hushimu na Baara.
9 Se casó con Hodes y tuvo a Jobab, Zibia, Mesa, Malcam,
Kwa mkewe Hodeshi, akawazaa wana saba: Yobabu, Sibia, Mesha, Malkamu,
10 Jeuz, Saquías y Mirma. Todos estos fueron sus hijos, jefes de familia.
Yeuzi, Sakia na Mirma. Hawa ndio waliokuwa wanawe, viongozi wa jamaa zao.
11 También tuvo hijos con Husim: Abitob y Elpal.
Hushimu alimzalia: Abitubu na Elpaali.
12 Los hijos de Elpal: Éber, Misham, Shemed (construyó Ono y Lod con sus ciudades cercanas),
Wana wa Elpaali walikuwa: Eberi, Mishamu, Shemedi (aliyeijenga miji ya Ono na Lodi, pamoja na vijiji vilivyoizunguka),
13 y Bería y Sema, que eran jefes de familia que vivían en Ajalón y que expulsaron a los que vivían en Gat.
na Beria na Shema, waliokuwa viongozi wa zile jamaa zilizokuwa zinaishi katika mji wa Aiyaloni, na ambao waliwafukuza wenyeji wa Gathi.
14 Ahío, Sasac, Jeremot,
Wana wa Beria walikuwa Ahio, Shashaki, Yeremothi,
15 Zebadías, Arad, Eder,
Zebadia, Aradi, Ederi,
16 Micael, Ispa y Joha eran los hijos de Bería.
Mikaeli, Ishpa, na Yoha.
17 Zebadías, Mesulám, Hizqui, Heber,
Zebadia, Meshulamu, Hizki, Heberi,
18 Ismerai, Jezlías y Jobab fueron los hijos de Elpaal.
Ishmerai, Izlia na Yobabu ndio waliokuwa wana wa Elpaali.
19 Jacim, Zicri, Zabdi,
Yakimu, Zikri, Zabdi,
20 Elienai, Ziletai, Eliel,
Elienai, Silethai, Elieli,
21 Adaías, Beraías, y Simrat fueron los hijos de Simei.
Adaya, Beraya na Shimrathi walikuwa wana wa Shimei.
22 Ispán, Heber, Eliel,
Wana wa Shashaki walikuwa Ishpani, Eberi, Elieli,
23 Abdón, Zicri, Hanán,
Abdoni, Zikri, Hanani,
24 Hananías, Elam, Antotías,
Hanania, Elamu, Anthothiya,
25 Ifdaías y Peniel fueron los hijos de Sasac.
Ifdeya na Penueli.
26 Samsherai, Seharías, Atalías,
Shamsherai, Sheharia, Athalia,
27 Jaresías, Elías, y Zicri fueron los hijos de Jeroham.
Yaareshia, Eliya na Zikri walikuwa wana wa Yerohamu.
28 Todos ellos eran jefes de familia, según su genealogía. Y vivían en Jerusalén.
Hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa zao wakuu, kama ilivyoorodheshwa katika koo zao, nao waliishi Yerusalemu.
29 Jeiel fundó Gabaón y vivió allí. Su mujer se llamaba Maaca.
Yeieli alikuwa baba yake Gibeoni naye aliishi huko Gibeoni. Mke wake aliitwa Maaka.
30 Su hijo primogénito fue Abdón, luego Zur, Cis, Baal, Ner, Nadab,
Mwanawe mzaliwa wa kwanza alikuwa Abdoni, akafuatiwa na Suri, Kishi, Baali, Neri, Nadabu,
31 Gedor, Ahío, Zequer,
Gedori, Ahio, Zekeri,
32 y Miclot. Miclot fue el padre de Simea. También vivían cerca de sus parientes en Jerusalén.
na Miklothi ambaye alikuwa baba yake Shimea. Hawa pia waliishi karibu na jamaa zao huko Yerusalemu.
33 Ner fue el padre de Cis, Cis fue el padre de Saúl, y Saúl fue el padre de Jonatán, Malquisúa, Abinadab y Es-Baal.
Neri akamzaa Kishi, Kishi akamzaa Sauli, Sauli akamzaa Yonathani, Malki-Shua, Abinadabu na Esh-Baali.
34 El hijo de Jonatán fue Merib-Baal, que fue el padre de Miqueas.
Yonathani akamzaa: Merib-Baali, naye Merib-Baali akamzaa Mika.
35 Los hijos de Miqueas fueron Pitón, Melec, Tarea y Acaz.
Wana wa Mika walikuwa: Pithoni, Meleki, Tarea na Ahazi.
36 Acaz fue el padre de Jada; Jada fue el padre de Alemet, Azmavet y Zimri; y Zimri fue el padre de Mosa.
Ahazi akamzaa Yehoada. Naye Yehoada akawazaa Alemethi, Azmawethi na Zimri, naye Zimri akamzaa Mosa.
37 Mosa fue el padre de Bina. Su hijo fue Rafa, padre de Elasa, padre de Azel.
Mosa akamzaa Binea, Binea akamzaa Rafa, na mwanawe huyo ni Eleasa, na mwanawe huyo ni Aseli.
38 Azel tuvo seis hijos. Estos fueron sus nombres: Azricam, Bocru, Ismael, Seraías, Obadías y Hanán. Todos ellos eran los hijos de Azel.
Aseli alikuwa na wana sita; haya ndiyo majina yao: Azrikamu, Bokeru, Ishmaeli, Shearia, Obadia na Hanani. Hawa wote ndio waliokuwa wana wa Aseli.
39 Los hijos de su hermano Esec fueron Ulam (primogénito), Jeús (el segundo) y Elifelet (el tercero).
Wana wa Esheki, nduguye Aseli, walikuwa: Mzaliwa wake wa kwanza alikuwa Ulamu, wa pili Yeushi na wa tatu Elifeleti.
40 Los hijos de Ulam eran fuertes guerreros y hábiles arqueros. Tuvieron muchos hijos y nietos, un total de 150. Todos ellos fueron los hijos de Benjamín.
Wana wa Ulamu walikuwa mashujaa hodari walioweza kutumia upinde. Alikuwa na wana wengi na wajukuu, jumla yao 150. Hawa wote ndio walikuwa wazao wa Benyamini.

< 1 Crónicas 8 >