< 1 Crónicas 6 >
1 Los hijos de Levi: Gersón, Coat y Merari.
Wana wa Levi walikuwa Gerishoni, Kohathi, na Merari.
2 Los hijos de Coat: Amram, Izhar, Hebrón y Uziel.
Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
3 Los hijos de Amram: Aarón, Moisés y Miriam. Los hijos de Aarón: Nadab, Abiú, Eleazar e Itamar.
Wana wa Amramu walikuwa Aruni, Musa, Miriamu. Wana wa Aruni walikuwa Nadabu, Abihu, Eleazari, na Ithamari.
4 Eleazar fue el padre de Finehas. Finehas fue el padre de Abisúa.
Eleazari akawa baba wa Finehasi, na Finehasi akawa baba wa Abishua.
5 Abisúa fue el padre de Buqui. Buqui fue el padre de Uzi;
Abishua akawa baba wa Buki, na Buki akawa baba wa Uzi.
6 Uzi fue el padre de Zeraías. Zeraías fue el padre de Meraioth.
Uzi akawa baba wa Zerahia, na Zerahia akawa baba wa Meraioti.
7 Meraiot fue el padre de Amarías. Amarías fue el padre de Ajitub.
Meraioti akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
8 Ajitub fue el padre de Sadok. Sadok fue el padre de Ahimaas.
Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Ahimazi.
9 Ahimaas fue el padre de Azarías. Azarías fue el padre de Johanán.
Ahimazi akawa baba wa Azaria, na Azaria akawa baba wa Yohanani.
10 Johanán fue el padre de Azarías (quien sirvió como sacerdote cuando Salomón construyó el Templo en Jerusalén).
Yohanani akawa baba wa Azaria, aliye hudumu katika hekalu alilo lijenga Sulemani ndaniya Yerusalemu.
11 Azarías fue el padre de Amarías. Amarías fue el padre de Ajitub.
Azaria akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
12 Ajitub fue el padre de Sadoc. Sadoc fue el padre de Salum.
Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Shalumu.
13 Salum fue el padre de Hilcías. Hilcías fue el padre de Azarías.
Shalumu akawa baba wa Hilikia, na Hilikia akawa baba wa Azaria.
14 Azarías fue el padre de Seraías, y Seraías fue el padre de Josadac.
Azaria akawa baba Seraia, na Seraia akawa baba wa Yehozadaki.
15 Josadac fue llevado al cautiverio cuando el Señor usó a Nabucodonosor para enviar a Judá y a Jerusalén al exilio.
Yehozadaki akaenda matekani Yahweh alipo wapeleka utumwani Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Nebukadneza.
16 Los hijos de Leví: Gersón, Coat y Merari.
Wana wa Levi walikuwa Gerishomu, Kohathi, na Merari.
17 Estos son los nombres de los hijos de Gersón: Libni y Simei.
Wana wa Gerishomu walikuwa Libini na Shimei.
18 Los hijos de Coat: Amram, Izhar, Hebrón y Uziel.
Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
19 Los hijos de Merari: Mahli y Musi. Estas son las familias de los levitas, que estaban ordenadas según sus padres:
Wana wa Merari walikuwa Mahili na Mushi. Hawa walikuwa koo za Walawi kwa familia za baba zao.
20 Los descendientes de Gersón: Libni su hijo, Jehat su hijo, Zima su hijo,
Uzao wa Gerishomu ulianza na mwanae Libini. Mwana wa Libini alikuwa Jahathi. Mwanae alikuwa Zima.
21 Joa su hijo, Iddo su hijo, Zera su hijo y Jeatherai su hijo.
Mwanae alikuwa Yoa. Mwanae alikuwa alikuwa Ido. Mwanae alikuwa Zera. Mwanae alikuwa Yeatherai.
22 Los descendientes de Coat: Aminadab su hijo; Coré su hijo; Asir su hijo,
Uzao wa Kohathi ulianza na mwanae Aminadabu. Mwanae alikuwa Kora. Mwanae alikuwa Asiri.
23 Elcana su hijo; Ebiasaf su hijo; Asir su hijo;
Mwanae alikuwa Elikana. Mwanae alikuwa Ebiasa. Mwanae alikuwa Asiri.
24 Tahat su hijo; Uriel su hijo; Uzías su hijo, y Saúl su hijo.
Mwanae alikuwa Tahathi. Mwanae alikuwa Urieli. Mwanae alikuwa uzia. Mwanae alikuwa Shauli.
25 Los descendientes de Elcana: Amasai, Ahimot,
Wana wa Elikana walikuwa Amasai, Ahimothi, na Elikana.
26 Elcana su hijo; Zofai su hijo; Nahat su hijo;
Mwana wa huyu Elikana wa pili alikuwa Zofai. Mwanae alikuwa Nahathi.
27 Eliab su hijo, Jeroham su hijo; Elcana su hijo, y Samuel su hijo.
Mwanae alikuwa Eliabu. Mwanae alikuwa Yehoramu. Mwanae alikuwa Elikana.
28 Los hijos de Samuel: Joel (primogénito) y Abías (el segundo).
Wana wa Samwali walikuwa mzaliwa wa kwanza, Yoeli, na Abija, wa pili.
29 Los descendientes de Merari: Mahli, su hijo Libni, su hijo Simei, su hijo Uza,
Mwana wa Merari alikuwa Mahili. Mwanae alikuwa Libini.
30 su hijo Simea, su hijo Haguía y su hijo Asaías.
Mwanae alikuwa Shimei. Mwanae alikuwa Uza. Mwanae alikuwa Shimea. Mwanae alikuwa Hagia. Mwana alikuwa Asaia.
31 Estos son los músicos que David designó para dirigir la música en la casa del Señor una vez que el Arca fuera colocada allí.
Haya ndio majina ya wanaume ambao Daudi waliwaeka kusimamia muziki katika nyumba ya Yahweh, baada ya sanduku kuja hapo.
32 Ellos dirigieron la música y el canto ante el Tabernáculo, la Tienda de Reunión, hasta que Salomón construyó el Templo del Señor en Jerusalén. Servían siguiendo el reglamento que se les había dado.
Walitumika kwa kuimba mbele ya hema, hema la kukutania, mpaka Sulemani alipo jenga nyumba ya Yahweh ndani ya Yerusalemu. Walikamilisha wajibu wao kwa kadiri ya maelekezo waliopewa.
33 Estos son los hombres que servían, junto con sus hijos: De los coatitas Hemán, el cantor, el hijo de Joel, el hijo de Samuel,
Hawa walitumika pamoja na wana wao. Katika makabila ya Wakohathi alitoka Hemani mwana muziki. Babu zake walikuwa hawa, kurudi nyuma ya wakati: Hemani alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Samweli.
34 hijo de Elcana, hijo de Jeroham, hijo de Eliel, hijo de Toa,
Samweli alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Yerohamu. Yerohamu alikuwa mwana wa Elieli. Elieli alikuwa mwana wa Toa.
35 hijo de Zuf, ehijo de Elcana, hijo de Mahat, hijo de Amasai,
Toa alikuwa mwana wa Zufi. Zufi alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Mahathi. Mahathi alikuwa mwana wa Amasai. Amasai alikuwa mwana wa Elikana.
36 hijo de Elcana, hijo de Joel, hijo de Azarías, hijo de Sofonías,
Elikana alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Azaria. Azaria alikuwa mwana wa Zefania.
37 hijo de Tahat, hijo de Asir, hijo de Ebiasaf, hijo de Coré,
Zefania alikuwa mwana wa Tahathi. Tahathi alikuwa mwana wa Asiri. Asiri alikuwa mwana wa Ebiasa. Ebiasa alikuwa mwana wa Kora.
38 hijo de Izhar, hijo de Coat, hijo de Leví, hijo de Israel.
Kora alikuwa mwana wa Izhari. Izhari alikuwa mwana wa Kohathi. Kohathi alikuwa mwana wa Levi. Levi alikuwa mwana wa Israeli.
39 Asaf, pariente de Hemán, que servía junto a él a la derecha: Asaf hijo de Berequías, hijo de Simea,
Msaidizi wa Hemani alikuwa Asafu, aliye simama mkono wake wa kuume. Asafu alikuwa mwana Berekia. Berekia alikuwa mwana wa Shimea.
40 hijo de Miguel, hijo de Baasías, hijo de Malaquías,
Shimea alikuwa mwana Mikaeli. Mikaeli alikuwa mwana wa Baaseia. Baaseia alikuwa mwana wa Malikiya.
41 hijo de Etni, hijo de Zera, hijo de Adaías,
Malikiya alikuwa mwana wa Ethini. Ethini alikuwa mwana wa Zera. Zera alikuwa mwana wa Adaia.
42 hijo de Etán, hijo de Zima, hijo de Simei,
Adaia alikuwa mwana wa Ethani. Ethani alikuwa mwana wa Zima. Zima alikuwa mwana wa Shimei.
43 hijo de Jahat, hijo de Gersón, hijo de Leví.
Shimei alikuwa mwana wa Yahathi. Yahathi alikuwa mwana wa Gerishomu. Gerishomu alikuwa mwana wa Levi.
44 A la izquierda de Hemán sirvieron los hijos de Merari: Etán hijo de Quisi, el hijo de Abdi, hijo de Malluch,
Upande wa mkono wa koshoto wa Hemani walikuwa wasaidizi wake wana wa Merari. Alikuwa Ethani mwana wa Kishi. Kishi alikuwa mwana wa Abdi. Abdi alikuwa mwana wa Maluki.
45 hijo de Hasabiah, hijo de Amasías, hijo de Hilcías,
Maluki alikuwa mwana wa Hashabia. Hashabia alikuwa mwana wa Amazia. Amazia alikuwa mwana wa Hilikia.
46 hijo de Amzi, hijo de Bani, hijo de Semer,
Hilikia alikuwa mwana wa Amzi. Amzi alikuwa mwana wa Bani. Bani alikuwa mwana wa Shemeri.
47 hijo de Mahli, hijo de Musi, hijo de Merari, hijo de Levi.
Shemeri alikuwa mwana wa Mahili. Mahili alikuwa mwana wa Mushi. Mushi alikuwa mwana wa Merari. Merari alikuwa mwana wa Levi.
48 Los demás levitas desempeñaban todas las demás funciones en el Tabernáculo, la casa de Dios.
Walawi, alipangiwa kufanya kazi zote za hema, nyumba ya Mungu.
49 Sin embargo, eran Aarón y sus descendientes quienes daban ofrendas en el altar de los holocaustos y en el altar del incienso y hacían todo el trabajo en el Lugar Santísimo, haciendo la expiación por Israel según todo lo que había ordenado Moisés, el siervo de Dios.
Aruni na wana wake walitoa sadaka katika madhabahu kwa ajili ya sadaka za kuteketeza; na sadaka katika madhabahu ya uvumba kwa kazi zote katika pa patakatifu. Hizi sadaka zilifanya maombezi kwa ajili ya Waisraeli, kwa kadiri ya yote ambayo Musa mtumishi wa Mungu aliwaamuru.
50 Los descendientes de Aarón fueron: Eleazar su hijo, Finees su hijo, Abisúa su hijo,
Uzao wa Aruni una kumbukwa kama ifuatavyo: Mwana wa Aruni alikuwa Eleazari. Mwana Eleazari alikuwa Finehasi. Mwana wa Finehasi alikuwa Abishua.
51 Buqui su hijo, Uzi su hijo, Zeraías su hijo,
Mwana wa Abishua alikuwa Buki. Mwana wa Buki alikuwa Uzi. Mwana wa Buki alikuwa Zerahia.
52 Meraioth su hijo, Amariah su hijo, Ahitub su hijo,
Mwana wa Zerahia alikuwa Meraiothi. Mwana wa Meraiothi alikuwa Amaria. Mwana wa Amaria alikuwa Ahitubi.
53 Zadok su hijo, y su hijo Ahimaas.
Mwana wa Ahitubi alikuwa Zadoki. Mwana wa Zadoki alikuwa Ahimazi.
54 Estos fueron los lugares que se les dieron para vivir como territorio asignado a los descendientes de Aarón, comenzando por el clan coatita, porque el suyo fue el primer lote:
Hizi ni sehemu ambazo wazao wa Aruni walipangiwa kuishi, wazao wa Aruni ambao walitoka katika koo za Wakohathi (maeneo ya kwanza yalikuwa yao).
55 Recibieron Hebrón, en Judá, junto con los pastos que la rodean.
Walipewa Hebroni katika nchi ya Yuda na nchi ya malisho,
56 Pero los campos y las aldeas cercanas a la ciudad fueron entregados a Caleb hijo de Jefone.
lakini maeneo ya mji na vijiji alipewa Kalebu mwana wa Yefune.
57 Así, los descendientes de Aarón recibieron Hebrón, una ciudad de refugio, Libna, Jatir, Estemoa,
Kwa wazao wa Aruni waliwapa: Hebroni ( mji wa makimblio), na Libina pamoja na nchi ya malisho, Yatiri, Eshitemoa pamoja na nchi ya malisho,
Hileni pamoja na nchi ya malisho, na Debiri pamoja na nchi ya malisho.
59 Asán, Juta y Bet Semes, junto con sus pastizales.
Waliwapa uzao wa Aruni: Ashani pamoja na nchi ya malisho na Bethi Shemeshi pamoja na nchi ya malisho;
60 De la tribu de Benjamín recibieron Gabaón, Geba, Alemeth y Anathoth, junto con sus pastizales. Tenían un total de trece ciudades entre sus familias.
na kutoka katika kabila la Benjamini walipewa Geba pamoja na nchi ya malisho, Alemethi pamoja na nchi ya malisho, na Anothothi na nchi ya malisho. Jumla ya miji yao ilikuwa kumi na tatu.
61 Los demás descendientes de Coat recibieron por sorteo diez ciudades de la media tribu de Manasés.
Uzao mwengine wa Kohathi waliwapa kwa sehemu miji kumi kutoka kwa kabila la Manase.
62 Los descendientes de Gersón, por familia, recibieron trece ciudades de las tribus de Isacar, Aser y Neftalí, y de la media tribu de Manasés en Basán.
Kwa uzao wa Gerishomu kwa koo zao tofauti walipewa miji kumi na tatu kutoka kwa makabila ya Isakari, Asheri, Naftali, na nusu ya kabila la Manase huko Bashani.
63 Los descendientes de Merari, por familia, recibieron doce ciudades de las tribus de Rubén, Gad y Zabulón.
Kwa uzao wa Merari walipewa miji kumi, kulingana na koo zao, kutoka kwa makabila ya Rubeni, Gadi, na Zebuluni.
64 El pueblo de Israel dio a los levitas estas ciudades y sus pastizales.
Hivyo watu wa Israeli walitoa hii miji pamoja na nchi za malisho kwa Walawi.
65 A las ciudades ya mencionadas les asignaron por nombre las de las tribus de Judá, Simeón y Benjamín.
Walitoa kwa sehemu miji iliyo tajwa awali kutoka katika kabila la Yuda, Simeoni, na Benjamini.
66 Algunas de las familias coatitas recibieron como territorio ciudades de la tribu de Efraín.
Kwa baadhi ya koo za Wakohathi walitoa miji kutoka kwa kabila la Efraimu.
67 Se les dio Siquem, una ciudad de refugio, en la región montañosa de Efraín, Gezer,
Waliwapa: Shekemu ( mji wa makimbilio) pamoja na nchi ya malisho katika milima ya Efraimu, Gezeri na nchi ya malisho,
Jokimeamu pamoja na nchi ya malisho, Bethi Horoni pamoja na nchi ya malisho,
69 Aijalon y Gat Rimmon, junto con sus pastizales.
Aiyaloni pamoja na nchi ya malisho, na Gathi Rimoni pamoja na nchi ya malisho.
70 De la mitad de la tribu de Manasés, el pueblo de Israel dio Aner y Bileam, junto con sus pastizales, al resto de las familias coatitas.
Nusu ya kabila la Manase waliwapa Wakohathi: Aneri pamoja na nchi ya malisho na Bileamu pamoja na nchi ya malisho. Hizi zikawa mali za koo za Wakohathi.
71 Los descendientes de Gersón recibieron lo siguiente. De la familia de la media tribu de Manasés Golán en Basán, y Astarot, junto con sus pastizales;
Kwa uzao wa Gerishomu kutoka koo za nusu ya kabila la Manase, waliwapa: Golani huko Baashani na nchi ya malisho na Ashitarothi pamoja na nchi ya malisho.
72 de la tribu de Isacar: Cedes, Daberat,
Kabila la Isakari liliwapa uzao wa Gerishomu: Kedeshi pamoja na nchi ya malisho, Dabera pamoja na nchi ya malisho,
73 Ramot y Anem, junto con sus pastizales;
Ramothi pamoja na nchi ya malisho, na Anemu pamoja na nchi ya malisho.
74 de la tribu de Aser: Masal, Abdón,
Isakari alipokea kutoka kwa kabila la Asheri: Mashali pamoja na nchi ya malisho, Abdoni pamoja na nchi ya malisho,
75 Hucoc y Rehob, junto con sus pastizales;
Hukoki pamoja na nchi ya malisho, na Rehobu pamoja na nchi ya malisho.
76 y de la tribu de Neftalí: Cedes en Galilea, Hamón y Quiriatím, con sus pastizales.
Walipokea kutoka kabila la Naftali: Kedeshi iliyo Galileya pamoja na nchi ya malisho, Hamoni pamoja na nchi ya malisho, na Kiriathaimu pamoja na nchi ya malisho.
77 Los demás descendientes de Merari recibieron lo siguiente. De la tribu de Zabulón Jocneam, Carta, Rimón y Tabor, con sus pastizales;
Kwa Walawi wengine, uzao wa Merari, walipewa kutoka kabila la Zebuluni: Rimono pamoja na nchi ya malisho na Tabori pamoja na nchi ya malisho.
78 de la tribu de Rubén, al este del Jordán, frente a Jericó: Beser (en el desierto), Jahzá,
Kwa wao pia walipewa, upande wa pili wa Yordani huko Yeriko, kwa upande wa mashariki mwa mto: Bezeri katika jangwa pamoja na nchi ya malisho, Yahzahi pamoja na nchi ya malisho,
79 Cedemot y Mefat, con sus pastizales
Kedemothi pamoka na nchi ya malisho, ma Mefathi pamoja na nchi ya malisho. Hizi zilitolewa kutoka kabila la Rubeni.
80 y de la tribu de Gad: Ramot de Galaad, Mahanaim,
Walawi walipokea kutoka kabila la Gadi: Ramothi ya Gileadi pamoja na nchi ya malisho, Mahanaimu pamoja na nchi ya malisho,
81 Hesbón y Jazer, con sus pastizales.
Heshiboni pamoja na nchi ya malisho, na Yazeri pamoja na nchi ya malisho.