< 1 Crónicas 26 >

1 Esta es una lista de las divisiones de los porteros. De los corasitas: Meselemías hijo de Coré, uno de Los hijos de Asaf.
Hii ndiyo migawanyo ya mabawabu: Kutoka kwa wana wa Kora alikuwa: Meshelemia mwana wa Kore, mmoja wa wana wa Asafu.
2 Los hijos de Meselemías: Zacarías (el mayor), Jediael (el segundo), Zebadías (el tercero), Jatniel (el cuarto),
Meshelemia alikuwa na wana wafuatao: Zekaria mzaliwa wa kwanza, Yediaeli wa pili, Zebadia wa tatu, Yathnieli wa nne,
3 Elam (el quinto), Johanán (el sexto) y Elioenai (el séptimo).
Elamu wa tano Yehohanani wa sita na Eliehoenai wa saba.
4 Los hijos de Obed-edom: Semaías (el mayor), Jozabad (el segundo), Joa (el tercero), Sacar (el cuarto), Natanel (el quinto),
Obed-Edomu naye alikuwa na wana wafuatao: Shemaya mzaliwa wa kwanza, Yehozabadi wa pili, Yoa wa tatu, Sakari wa nne, Nethaneli wa tano,
5 Ammiel (el sexto), Isacar (el séptimo) y Peuletai (el octavo), porque Dios había bendecido a Obed-edom.
Amieli wa sita, Isakari wa saba, na Peulethai wa nane. (Kwa kuwa Mungu alikuwa amembariki Obed-Edomu.)
6 Semaías, hijo de Obed-edom, tenía hijos que eran líderes capaces y tenían gran autoridad en la familia de su padre.
Shemaya mwanawe pia alikuwa na wana, waliokuwa viongozi katika jamaa ya baba yao kwa sababu walikuwa watu wenye uwezo mkubwa.
7 Los hijos de Semaías: Othni, Refael, Obed y Elzabad. Sus parientes, Elihú y Semaquías, también eran hombres capaces.
Wana wa Shemaya ni: Othni, Refaeli, Obedi na Elizabadi; jamaa zake Elihu na Semakia walikuwa pia watu wenye uwezo.
8 Todos estos descendientes de Obed-edom, más sus hijos y nietos, un total de sesenta y dos, eran hombres capaces, bien calificados para su servicio.
Hawa wote walikuwa wazao wa Obed-Edomu; wao na wana wao na jamaa zao walikuwa watu wenye uwezo pamoja na nguvu za kufanya kazi. Wazao wa Obed-Edomu jumla yao walikuwa sitini na wawili.
9 Los dieciocho hijos y hermanos de Meselemías también eran hombres capaces.
Meshelemia alikuwa na wana na jamaa zake, waliokuwa watu wenye uwezo: jumla yao watu kumi na wanane.
10 Hosa, uno de los hijos de Merari, puso a Simri como líder entre sus hijos, aunque no era el primogénito.
Hosa, Mmerari, alikuwa na wana wafuatao: Shimri alikuwa mkuu wao (baba yake alikuwa amemweka yeye kuwa mkuu ijapokuwa hakuwa mzaliwa wa kwanza),
11 Entre sus otros hijos estaban Hilcías (el segundo), Tebalías (el tercero) y Zacarías (el cuarto). El total de los hijos y parientes de Osa era de trece.
Hilkia wa pili, Tabalia wa tatu na Zekaria wa nne. Wana na jamaa za Hosa jumla yao walikuwa watu kumi na watatu.
12 Estas divisiones de los porteros, a través de sus jefes de familia, servían en la casa del Señor, al igual que sus hermanos.
Hii migawanyo ya mabawabu, kupitia wakuu wao, walikuwa na zamu za kuhudumu hekaluni mwa Bwana kama jamaa zao walivyokuwa nazo.
13 Cada puerta fue asignada por sorteo a diferentes familias, la menos importante igual a la más importante.
Kura zilipigwa kwa kila lango, kufuatana na jamaa zao, wakubwa kwa wadogo.
14 La suerte de la puerta oriental recayó en Meselemías. Entonces echaron suertes sobre su hijo Zacarías, consejero sabio y perspicaz, y la suerte de la puerta del norte le correspondió a él.
Kura ya Lango la Mashariki ilimwangukia Shelemia. Kisha wakapiga kura kwa Zekaria mwanawe, aliyekuwa mshauri mwenye hekima, nayo kura ya Lango la Kaskazini ikamwangukia.
15 La suerte de la puerta del sur correspondió a Obed-edom, y la del almacén a sus hijos.
Kura ya Lango la Kusini ikamwangukia Obed-Edomu, nayo kura ya maghala ikawaangukia wanawe.
16 Supim y Hosa recibieron la puerta del oeste y la puerta de Salet en el camino que sube. Estaban siempre vigiladas.
Kura za Lango la Magharibi na Lango la Shalekethi kwenye barabara ya juu zikawaangukia Shupimu na Hosa. Zamu za walinzi ziligawanywa kwa usawa:
17 Había seis levitas de servicio cada día en la puerta oriental, cuatro en la puerta norte, cuatro en la puerta sur y dos a la vez en el almacén.
Kulikuwa na Walawi sita kila siku upande wa mashariki, wanne upande wa kaskazini, wanne upande wa kusini, na wawili wawili kwa mara moja kwenye ghala.
18 Seis estaban de servicio todos los días en la puerta oeste, cuatro en el camino principal y dos en el patio.
Kuhusu ukumbi kuelekea magharibi, kulikuwa na wanne barabarani na wawili kwenye ukumbi wenyewe.
19 Estas eran las divisiones de los porteros de Los hijos de Coré y Los hijos de Merari.
Hii ndiyo iliyokuwa migawanyo ya mabawabu waliokuwa wazao wa Kora na wa Merari.
20 Otros levitas bajo el mando de Ahías estaban a cargo de los tesoros de la casa de Dios y de los tesoros de lo que había sido dedicado a Dios.
Katika Walawi, Ahiya alikuwa mwangalizi wa hazina za nyumba ya Mungu na mwangalizi wa hazina za vitu vilivyowekwa wakfu.
21 De Los hijos de Ladán, que eran los descendientes de los gersonitas a través de Ladán, y eran los jefes de familia de Ladán el gersonita: Jehieli.
Wazao wa Ladani, waliokuwa Wagershoni kupitia Ladani na waliokuwa viongozi wa jamaa za Ladani Mgershoni, walikuwa Yehieli,
22 Los hijos de Jehieli, Zetam y su hermano Joel, estaban a cargo de los tesoros de la casa del Señor.
wana wa Yehieli, wana wa Zethamu na wa nduguye Yoeli. Wao walikuwa waangalizi wa hazina za Hekalu la Bwana.
23 De los amramitas, los izaritas, los hebronitas y los uzielitas:
Kutoka kwa wana wa Amramu, wana wa Ishari, wana wa Hebroni na wana wa Uzieli:
24 Sebuel, descendiente de Gersón, hijo de Moisés, era el principal encargado de los tesoros.
Shebueli, mzao wa Gershomu mwana wa Mose, alikuwa afisa mwangalizi wa hazina.
25 Sus parientes por parte de Eliezer fueron Rehabías, Jesaías, Joram, Zicri y Selomot.
Jamaa zake kutoka kwa Eliezeri, wanawe walikuwa: Rehabia, Yeshaya, Yoramu, Zikri na Shelomithi.
26 Selomot y sus parientes estaban a cargo de todos los tesoros de todo lo que había sido dedicado por el rey David, por los jefes de familia que eran los comandantes de millares y de centenas, y por los comandantes del ejército.
Shelomithi na jamaa zake walikuwa waangalizi wa hazina zote za vitu vile vilivyowekwa wakfu na Mfalme Daudi, kwa viongozi wa jamaa waliokuwa majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, na kwa maafisa wengine wa jeshi.
27 Dedicaron una parte del botín que habían ganado en la batalla para ayudar a mantener la casa del Señor.
Baadhi ya nyara zilizotekwa vitani waliziweka wakfu kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu la Bwana.
28 Selomot y sus parientes también se encargaron de las ofrendas dedicadas al Señor por Samuel el vidente, Saúl hijo de Cis, Abner hijo de Ner y Joab hijo de Sarvia. Todas las ofrendas dedicadas eran responsabilidad de Selomot y sus parientes.
Kila kitu kilichokuwa kimewekwa wakfu na Samweli mwonaji, na Sauli mwana wa Kishi, Abneri mwana wa Neri, na Yoabu mwana wa Seruya, pamoja na vitu vingine vyote vilivyokuwa vimewekwa wakfu, vyote vilikuwa chini ya uangalizi wa Shelomithi na jamaa zake.
29 De los izaritas: Quenanías y sus hijos recibieron funciones externas como funcionarios y jueces sobre Israel.
Kutoka kwa wana wa Ishari: Kenania na wanawe walipewa kazi nje ya Hekalu kama maafisa na waamuzi juu ya Israeli.
30 De los hebronitas: Hasabías y sus parientes, 1.700 hombres capaces, fueron puestos a cargo del Israel al oeste del Jordán, responsables de todo lo relacionado con la obra del Señor y el servicio del rey.
Kutoka kwa wana wa Hebroni: Hashabia na jamaa zake, watu 1,700 wenye uwezo, waliwajibika katika Israeli magharibi ya Yordani kwa ajili ya kazi zote za Bwana na utumishi wa mfalme.
31 También de los hebronitas salió Jericó, el líder de los hebronitas según las genealogías familiares. En el año cuarenta del reinado de David se examinaron los registros, y se descubrieron hombres de gran capacidad en Jazer de Galaad.
Kuhusu wana wa Hebroni, Yeria alikuwa mkuu wao kufuatana na orodha ya jamaa yao. Katika mwaka wa arobaini wa utawala wa Daudi uchunguzi ulifanyika katika kumbukumbu, nao watu wenye uwezo miongoni mwa wana wa Hebroni wakapatikana huko Yazeri katika Gileadi.
32 Entre los parientes de Jericó había 2.700 hombres capaces que eran líderes familiares. El rey David los puso a cargo de las tribus de Rubén y Gad y de la media tribu de Manasés. Eran responsables de todo lo relacionado con la obra del Señor y el servicio del rey.
Yeria alikuwa na jamaa ya watu 2,700 waliokuwa watu wenye uwezo na viongozi wa jamaa, naye Mfalme Daudi akawaweka kuangalia Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila Manase kuhusu kila jambo lililomhusu Mungu na shughuli za mfalme.

< 1 Crónicas 26 >