< 1 Crónicas 24 >
1 Los hijos de Aarón fueron colocados en divisiones de la siguiente manera. Los hijos de Aarón eran Nadab, Abiú, Eleazar e Itamar.
Hii ndiyo migawanyo ya wana wa Aroni: Aroni alikuwa na wana wanne: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
2 Pero Nadab y Abiú murieron antes que su padre, y no tuvieron hijos. Sólo Eleazar e Itamar continuaron como sacerdotes.
Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao, nao hawakuwa na wana; kwa hiyo ndugu zao Eleazari na Ithamari wakahudumu kama makuhani.
3 Con la ayuda de Sadoc, descendiente de Eleazar, y de Itamar, descendiente de Ahimelec, David los colocó en divisiones según sus funciones asignadas.
Akisaidiwa na Sadoki mwana wa Eleazari na Ahimeleki mwana wa Ithamari, Daudi aliwapanga wazao wa Aroni katika migawanyo kufuatana na wajibu wa huduma zao.
4 Como los descendientes de Eleazar tenían más jefes que los de Itamar, se dividieron así: dieciséis jefes de familia de los descendientes de Eleazar, y ocho de los descendientes de Itamar.
Idadi kubwa ya viongozi walipatikana miongoni mwa wazao wa Eleazari, kuliko miongoni mwa wazao wa Ithamari, nao waligawanywa kwa uwiano: Viongozi kumi na sita kutoka jamaa ya wazao wa Eleazari na viongozi wanane kutoka jamaa ya wazao wa Ithamari.
5 Se dividieron echando suertes, sin preferencia, porque había oficiales del santuario y oficiales de Dios tanto de los hijos de Eleazar como de los hijos de Itamar.
Waliwagawanya bila upendeleo kwa kupiga kura, kwa kuwa kulikuwa na maafisa wa mahali patakatifu na maafisa wa Mungu miongoni mwa wazao wale wa Eleazari na wale wa Ithamari.
6 Semaías hijo de Netanel, un levita, era el secretario. Anotó los nombres y las asignaciones en presencia del rey, de los funcionarios, del sacerdote Sadoc, de Ahimelec hijo de Abiatar y de los jefes de familia de los sacerdotes y levitas. Una familia de Eleazar y otra de Itamar fueron elegidas por turno.
Mwandishi Shemaya mwana wa Nethaneli, Mlawi, aliorodhesha majina yao mbele ya Mfalme Daudi na maafisa: Kuhani Sadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa jamaa za makuhani na za Walawi: jamaa moja ikitoka upande wa Eleazari na nyingine upande wa Ithamari.
7 La primera suerte recayó en Joiarib. El segundo a Jedaías.
Kura ya kwanza ilimwangukia Yehoyaribu, ya pili Yedaya,
8 La tercera a Harim. El cuarto a Seorim.
ya tatu Harimu, ya nne Seorimu,
9 La quinta a Malquías. La sexta a Mijamín.
ya tano Malkiya, ya sita Miyamini,
10 La séptima a Cos. La octava a Abías.
ya saba Hakosi, ya nane Abiya,
11 La novena a Jesúa. La décima por Secanías.
ya tisa Yeshua, ya kumi Shekania,
12 La undécima por Eliasib. La duodécima a Jacim.
ya kumi na moja Eliashibu, ya kumi na mbili Yakimu,
13 La decimotercera por Hupah. La decimocuarta por Jeshebeab.
ya kumi na tatu Hupa, ya kumi na nne Yeshebeabu,
14 La decimoquinta por Bilga. El decimosexto a Immer.
ya kumi na tano Bilga, ya kumi na sita Imeri,
15 El decimoséptimo a Hezir. El decimoctavo a Afisés.
ya kumi na saba Heziri, ya kumi na nane Hapisesi,
16 La decimonovena a Petaías. El vigésimo a Hezequiel.
ya kumi na tisa Pethahia, ya ishirini Yehezkeli,
17 El vigésimo primero a Jaquín. El vigésimo segundo a Gamul.
ya ishirini na moja Yakini, ya ishirini na mbili Gamuli,
18 El vigésimo tercero a Delaía. El vigésimo cuarto a Maazías.
ya ishirini na tatu Delaya, ya ishirini na nne Maazia.
19 Este era el orden en que cada grupo debía servir cuando entraba en la casa del Señor, siguiendo el procedimiento que les había definido su antepasado Aarón, según las instrucciones del Señor, el Dios de Israel.
Huu ulikuwa ndio utaratibu wao uliokubalika wa kuhudumu walipoingia katika Hekalu la Bwana kulingana na masharti waliyoelekezwa na Aroni baba yao, kama Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa amemwamuru.
20 Estos fueron el resto de los hijos de Leví: de Los hijos de Amram: Shubael; de Los hijos de Shubael: Jehdeiah.
Kuhusu wazao wa Lawi waliobaki: Kutoka kwa wana wa Amramu: alikuwa Shubaeli; kutoka kwa wana wa Shubaeli: alikuwa Yedeya.
21 Para Rehabía, de sus hijos Isías (el primogénito).
Kwa wa Rehabia, kutoka kwa wanawe: Ishia alikuwa wa kwanza.
22 De los Izharitas: Shelomoth; de Los hijos de Shelomoth: Jahat.
Kutoka kwa Waishari: alikuwa Shelomithi, kutoka kwa wana wa Shelomithi: alikuwa Yahathi.
23 Los hijos de Hebrón: Jeriah (el mayor), Amariah (el segundo), Jahaziel (el tercero) y Jecamán (el cuarto).
Wana wa Hebroni: Yeria alikuwa mkuu, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, na Yekameamu wa nne.
24 El hijo de Uziel: Miqueas; de Los hijos de Miqueas: Shamir.
Mwana wa Uzieli: alikuwa Mika; kutoka kwa wana wa Mika: alikuwa Shamiri.
25 El hermano de Micaías: Isías; de Los hijos de Isías: Zacarías.
Ndugu yake Mika: alikuwa Ishia; na kutoka kwa wana wa Ishia: alikuwa Zekaria.
26 Los hijos de Merari: Mahli y Musi. El hijo de Jaaziah: Beno.
Wana wa Merari: walikuwa Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia: alikuwa Beno.
27 Los hijos de Merari: de Jaaziah: Beno, Shoham, Zaccur e Ibri.
Wana wa Merari: kutoka kwa Yaazia: ni Beno, Shohamu, Zakuri na Ibri.
28 De Mahli: Eleazar, que no tuvo hijos.
Kutoka kwa Mahli: alikuwa Eleazari, ambaye hakuwa na wana.
29 De Cis: el hijo de Cis, Jerajmeel.
Kutoka kwa Kishi: mwana wa Kishi: alikuwa Yerameeli.
30 Los hijos de Musi: Mahli, Eder y Jerimot. Estos eran los hijos de los levitas, según sus familias.
Nao wana wa Mushi: walikuwa Mahli, Ederi na Yeremothi. Hawa walikuwa Walawi kulingana na jamaa zao.
31 También echaron suertes de la misma manera que sus parientes los descendientes de Aarón. Lo hicieron en presencia del rey David, de Sadoc, de Ahimelec y de los jefes de familia de los sacerdotes y de los levitas, tanto de los jefes de familia como de sus hermanos menores.
Pia walipiga kura kama vile ndugu zao wazao wa Aroni walivyofanya, mbele ya Mfalme Daudi, Sadoki, Ahimeleki na mbele ya viongozi wa jamaa ya makuhani na ya Walawi. Jamaa za ndugu wakubwa zilitendewa sawasawa na zile za ndugu wadogo.