< 1 Crónicas 23 >

1 Cuando David envejeció, habiendo vivido una larga vida, nombró a su hijo Salomón rey de Israel.
Daudi alipokuwa mzee aliyeshiba siku, akamfanya Solomoni mwanawe kuwa mfalme juu ya Israeli.
2 También convocó a todos los jefes de Israel, a los sacerdotes y a los levitas.
Pia akawakusanya pamoja viongozi wote wa Israeli, pamoja na makuhani na Walawi.
3 Se contaron los levitas mayores de treinta años, y fueron 38.000 en total.
Walawi waliokuwa na umri wa miaka thelathini au zaidi walihesabiwa, nayo hesabu ya wanaume ilikuwa 38,000.
4 “De ellos, 24.000 estarán a cargo de las obras de la casa del Señor, mientras que 6.000 serán oficiales y jueces”, instruyó David.
Daudi akasema, “Miongoni mwa hawa, 24,000 watasimamia kazi ya Hekalu la Bwana na 6,000 watakuwa maafisa na waamuzi,
5 “Y 4.000 serán porteros, mientras que 4.000 alabarán al Señor usando los instrumentos musicales que he proporcionado para la alabanza”.
na 4,000 watakuwa mabawabu, na wengine 4,000 watamsifu Bwana kwa ala za uimbaji nilizotoa kwa ajili ya kusudi hilo.”
6 David los dividió en secciones correspondientes a Los hijos de Levi: Gersón, Coat y Merari.
Daudi akawagawa Walawi katika makundi kufuatana na wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
7 Los hijos de Gersón: Ladán y Simei.
Wana wa Wagershoni walikuwa wawili: Ladani na Shimei.
8 Los hijos de Ladan: Jehiel (el jefe de familia), Zetham y Joel, tres en total.
Wana wa Ladani walikuwa watatu: Yehieli wa kwanza, Zethamu na Yoeli.
9 Los hijos de Simei: Selomit, Haziel y Harán, tres en total. Estos eran los jefes de las familias de Ladán.
Wana wa Shimei walikuwa watatu: Shelomothi, Hazieli na Harani. Hawa watatu walikuwa viongozi wa jamaa za Ladani.
10 Los hijos de Simei: Jahat, Ziza, Jeús y Bería, cuatro en total.
Nao wana wa Shimei walikuwa wanne: Yahathi, Zina, Yeushi na Beria.
11 Jahat (el jefe de familia), y Ziza (el segundo); pero como Jeús y Bería no tuvieron muchos hijos, fueron contados como una sola familia.
Yahathi alikuwa wa kwanza na Ziza wa pili, lakini Yeushi na Beria hawakuwa na wana wengi; kwa hiyo walihesabiwa kama jamaa moja, wakapewa wajibu kwa pamoja.
12 Los hijos de Coat: Amram, Izhar, Hebrón y Uziel-un total de cuatro.
Wana wa Kohathi walikuwa wanne: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
13 Los hijos de Amram: Aarón y Moisés. Aarón estaba dedicado al servicio con las cosas más sagradas, para que él y sus hijos presentaran siempre ofrendas al Señor, y ministraran ante él, y dieran bendiciones en su nombre para siempre.
Wana wa Amramu walikuwa: Aroni na Mose. Aroni waliwekwa wakfu, yeye na wazao wake milele, wawe wakiweka wakfu vitu ambavyo ni vitakatifu mno, kutoa dhabihu mbele za Bwana, kuhudumu mbele zake na kutamka baraka katika Jina la Bwana milele.
14 En cuanto a Moisés, el hombre de Dios, sus hijos estaban incluidos en la tribu de Leví.
Wana wa Mose mtu wa Mungu walihesabiwa kama sehemu ya kabila la Lawi.
15 Los hijos de Moisés: Gersón y Eliezer.
Wana wa Mose walikuwa: Gershomu na Eliezeri.
16 Los hijos de Gersón: Sebuel (el jefe de familia).
Wazao wa Gershomu: Shebueli alikuwa wa kwanza.
17 Los hijos de Eliezer: Rehabías (el jefe de familia). Eliezer no tuvo más hijos, pero Rehabías tuvo muchos hijos.
Wazao wa Eliezeri: Rehabia alikuwa wa kwanza. Eliezeri alikuwa na mwana mmoja tu, lakini wana wa Rehabia walikuwa wengi sana.
18 Los hijos de Izhar: Selomit (el jefe de familia).
Wana wa Ishari: Shelomithi alikuwa wa kwanza.
19 Los hijos de Hebrón: Jeria (el jefe de familia), Amarías (el segundo), Jahaziel (el tercero) y Jecamán (el cuarto).
Wana wa Hebroni walikuwa: Yeria alikuwa wa kwanza, wa pili Amaria, wa tatu Yahazieli, na wa nne Yekameamu.
20 Los hijos de Uziel: Micaías (el jefe de familia) e Isías (el segundo).
Wana wa Uzieli walikuwa: Mika wa kwanza na Ishia wa pili.
21 Los hijos de Merari: Mahli y Musi. Los hijos de Mahli: Eleazar y Cis.
Wana wa Merari walikuwa: Mahli na Mushi. Wana wa Mahli walikuwa: Eleazari na Kishi.
22 Eleazar murió sin tener hijos, sólo hijas. Sus primos, Los hijos de Cis, se casaron con ellas.
Eleazari akafa bila ya kuwa na wana: alikuwa na binti tu. Binamu zao, wana wa Kishi, wakawaoa.
23 Los hijos de Musi: Mahli, Eder y Jeremot, tres en total.
Wana wa Mushi: Mahli, Ederi na Yeremothi; wote walikuwa watatu.
24 Estos eran los descendientes de Leví por familias, los jefes de familia enumerados individualmente por su nombre: los que tenían veinte años o más y servían en la casa del Señor.
Hawa walikuwa wazao wa Lawi kwa jamaa zao. Wakuu wa jamaa kama walivyoandikwa kwa majina yao na kuhesabiwa kila mmoja, yaani, wenye uwezo wa kufanya kazi kuanzia miaka ishirini au zaidi, waliohudumu katika Hekalu la Bwana.
25 Porque David dijo: “El Señor, el Dios de Israel, ha dado la paz a su pueblo, y vivirá en Jerusalén para siempre.
Kwa maana Daudi alikuwa amesema, “Kwa vile Bwana, Mungu wa Israeli amewapa watu wake raha na amekuja kuishi Yerusalemu milele,
26 Así que los levitas ya no necesitan llevar la Tienda ni nada necesario para su servicio”.
Walawi hawahitaji tena kubeba Maskani wala chombo chochote cha utumishi wake.”
27 De acuerdo con las instrucciones finales de David, se contaron los levitas de veinte años o más.
Kulingana na maagizo ya mwisho ya Daudi, Walawi waliohesabiwa ni wale wa kuanzia umri wa miaka ishirini au zaidi.
28 Su misión era ayudar a los descendientes de Aarón en el servicio de la casa del Señor. Eran responsables de los patios y las habitaciones, de la limpieza de todas las cosas sagradas y del trabajo del servicio de la casa de Dios.
Wajibu wa Walawi ulikuwa kuwasaidia wazao wa Aroni kuhudumu katika Hekalu la Bwana: Kuwa wasimamizi wa nyua, vyumba vya pembeni, kutakasa vyombo vitakatifu na utendaji mwingine wowote katika nyumba ya Mungu.
29 También eran responsables del pan de la proposición que se ponía sobre la mesa, de la harina especial para las ofrendas de grano, de los panes sin levadura, de la cocción, de la mezcla y del manejo de todas las cantidades y medidas.
Walikuwa wasimamizi wa mikate iliyowekwa mezani, unga kwa ajili ya sadaka za nafaka, mikate isiyotiwa chachu, uokaji na uchanganyaji, pamoja na vipimo vyote vya wingi na ukubwa.
30 También debían ponerse de pie todas las mañanas para dar gracias y alabar al Señor, y hacer lo mismo al atardecer,
Pia ulikuwa wajibu wao kila asubuhi kumshukuru na kumsifu Bwana. Iliwapasa pia kufanya hivyo jioni
31 y siempre que se presentaran holocaustos al Señor, ya fuera en los sábados, lunas nuevas y días festivos. Debían servir regularmente ante el Señor según el número que se les exigiera.
na wakati wowote sadaka za kuteketezwa zilipotolewa kwa Bwana siku za Sabato na kwenye sikukuu za Mwezi Mwandamo na katika sikukuu nyingine zilizoamriwa. Iliwapasa kuhudumu mbele za Bwana mara kwa mara kwa idadi maalum na kwa namna waliyokuwa wamepewa maelekezo.
32 Así, los levitas debían cumplir con la responsabilidad de cuidar la Tienda del Encuentro y el santuario, y con sus hermanos los descendientes de Aarón, servían a la casa del Señor.
Hivyo Walawi wakafanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, katika Mahali Patakatifu chini ya uongozi wa ndugu zao wazao wa Aroni, kwa ajili ya utumishi katika Hekalu la Bwana.

< 1 Crónicas 23 >