< 1 Crónicas 20 >

1 En primavera, en la época del año en que los reyes salen a hacer la guerra, Joab dirigió el ejército israelita en los ataques contra el país de los amonitas, asediando también Rabá. Sin embargo, David se quedó en Jerusalén. Joab atacó Rabá y la destruyó.
Mwanzoni mwa mwaka mpya, wakati ambapo wafalme huenda vitani, Yoabu aliliongoza jeshi. Aliangamiza nchi ya Waamoni, na akaenda Raba na kuuzingira, lakini Daudi alibaki Yerusalemu. Yoabu akashambulia Raba na kuuacha ukiwa magofu.
2 David tomó la corona de la cabeza de su ídolo Milcom. Era de oro y estaba engastado con gemas. Pesaba un talentob y fue colocado sobre la cabeza de David. David también tomó una gran cantidad de botín de la ciudad.
Daudi akachukua taji kutoka kwa kichwa cha mfalme wao, lililokuwa na uzito wa talanta moja ya dhahabu, nayo ilizungushiwa vito vya thamani. Ikawekwa juu ya kichwa cha Daudi. Alichukua nyara nyingi kutoka mjini huo.
3 David hizo trabajar a la gente de allí con sierras, picos de hierro y hachas. También hizo lo mismo con todas las ciudades amonitas. Luego David y todo su ejército regresaron a Jerusalén.
Akawatoa watu waliokuwa humo, akawaweka wafanye kazi kwa misumeno, sululu za chuma na mashoka. Daudi akafanya hivi kwa miji yote ya Waamoni. Kisha Daudi na jeshi lake lote wakarudi Yerusalemu.
4 Algún tiempo después de esto estalló un conflicto con los filisteos en Gezer. Pero entonces Sibecai de Husa mató a Sipai, un descendiente de los refaítas, y los filisteos se vieron obligados a someterse.
Baada ya muda, kulitokea vita dhidi ya Wafilisti, huko Gezeri. Wakati huo Sibekai, Mhushathi, akamuua Sipai, aliyekuwa mmoja wa wazao wa Warefai, nao Wafilisti wakashindwa.
5 En otra batalla con los filisteos, Elhanán, hijo de Jair, mató a Lahmi, hermano de Goliat de Gat. El asta de su lanza era tan gruesa como una vara de tejedor.
Katika vita vingine na Wafilisti, Elhanani mwana wa Yairi alimuua Lahmi nduguye Goliathi, Mgiti, ambaye mkuki wake ulikuwa na mpini kama mti wa mfumaji.
6 En otra batalla en Gat, había un hombre gigantesco, que tenía seis dedos en cada mano y seis dedos en cada pie, haciendo un total de veinticuatro. También él descendía de los gigantes.
Katika vita vingine tena, vilivyopiganwa huko Gathi, kulikuwako na mtu mmoja mkubwa mwenye vidole sita katika kila mkono na vidole sita katika kila mguu: jumla vidole ishirini na vinne. Yeye alikuwa pia mzao wa Mrefai.
7 Pero cuando insultó a Israel, Jonatán, hijo de Simea, hermano de David, lo mató.
Alipowadhihaki Israeli, Yonathani, mwana wa Shimea, nduguye Daudi, akamuua.
8 Estos eran los descendientes de los gigantes en Gat, pero todos fueron muertos por David y sus hombres.
Hawa walikuwa ndio wazao wa Warefai huko Gathi, nao walianguka kwa mikono ya Daudi na watu wake.

< 1 Crónicas 20 >