< 1 Crónicas 11 >

1 Entonces todos los israelitas se reunieron con David en Hebrón. Y le dijeron: “Somos tu carne y tu sangre.
Israeli yote walimjia Daudi kwa pamoja huko Hebroni wakamwambia, “Sisi ni nyama yako na damu yako.
2 En los últimos tiempos, aunque Saúl era el rey, tú eras el verdadero líder de Israel. El Señor, tu Dios, te ha dicho: ‘Tú serás el pastor de mi pueblo, y tú serás el jefe de mi pueblo Israel’”.
Zamani, wakati Sauli alikuwa mfalme, wewe ndiwe uliyeiongoza Israeli vitani, naye Bwana Mungu wako alikuambia, ‘Wewe utawachunga watu wangu Israeli, na utakuwa mtawala wao.’”
3 Todos los ancianos de Israel acudieron ante el rey en Hebrón, y David hizo un acuerdo solemne con ellos ante el Señor. Allí ungieron a David como rey de Israel, tal como el Señor lo había prometido por medio de Samuel.
Wazee wote wa Israeli walipokuwa wamewasili kwa Mfalme Daudi huko Hebroni, alifanya mapatano nao huko Hebroni mbele za Bwana, nao wakamtia Daudi mafuta awe mfalme wa Israeli, sawasawa na Bwana alivyoahidi kupitia kwa Samweli.
4 Entonces David y todos los israelitas fueron a Jerusalén (antes conocida como Jebús), donde vivían los jebuseos.
Daudi na Waisraeli wote wakaenda Yerusalemu (ndio Yebusi). Nao Wayebusi walioishi humo
5 Pero los jebuseos le dijeron a David: “No entrarás aquí”. Sin embargo, David capturó la fortaleza de Sión, ahora conocida como la Ciudad de David.
wakamwambia Daudi, “Wewe hutaingia humu.” Hata hivyo, Daudi akaiteka ngome ya Sayuni, Mji wa Daudi.
6 Y David había dicho: “El primero que ataque a los jebuseos será mi comandante en jefe”. Como Joab, hijo de Sarvia, fue el primero, se convirtió en el comandante en jefe.
Daudi alikuwa amesema, “Yeyote aongozaye mashambulizi dhidi ya Wayebusi, atakuwa jemadari mkuu.” Yoabu mwana wa Seruya akawa wa kwanza kukwea, naye akawa mkuu.
7 David decidió habitar en la fortaleza, por eso la llamaron Ciudad de David.
Daudi akafanya makao yake kwenye ngome, hivyo ukaitwa Mji wa Daudi.
8 Entonces construyó la ciudad a su alrededor, desde el Milo e hizo un circuito alrededor, mientras que Joab reparaba el resto de la ciudad.
Akajenga mji pande zote, kuanzia kwenye mito hadi kwenye ukuta kuzunguka, wakati huo huo Yoabu akajenga sehemu zingine zilizobaki za Yerusalemu.
9 David se hizo cada vez más poderoso, porque el Señor Todopoderoso estaba con él.
Daudi akazidi kuwa na nguvu zaidi na zaidi, kwa sababu Bwana Mwenye Nguvu Zote alikuwa pamoja naye.
10 Estos fueron los líderes de los poderosos guerreros de David que, junto con todos los israelitas, le dieron un fuerte apoyo para que se convirtiera en rey, tal como el Señor había prometido que sucedería con Israel.
Hawa ndio waliokuwa wakuu wa mashujaa wa Daudi: wao pamoja na Israeli wote wakauimarisha ufalme wake ili kuenea katika nchi yote, kama Bwana alivyoahidi.
11 Esta es la lista de los principales guerreros que apoyaron a David: Jasobeam, hijo de Hacmoni, líder de los Tres. Con su lanza, una vez mató a 300 hombres en una sola batalla.
Hii ndio orodha ya mashujaa wa Daudi: Yashobeamu, Mhakmoni, alikuwa mkuu wa maafisa; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua katika pambano moja.
12 Después de él vino Eleazar, hijo de Dodo, descendiente de Ahoha, uno de los Tres guerreros principales.
Aliyefuata alikuwa Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu.
13 Estaba con David en Pasdamin cuando los filisteos se reunieron para la batalla que tuvo lugar en un campo de cebada. El ejército israelita huyó cuando los filisteos atacaron,
Huyo alikuwa pamoja na Daudi huko Pas-Damimu, wakati Wafilisti walikusanyika huko kwa ajili ya vita. Huko ambapo kulikuwa na shamba lililokuwa limejaa shayiri, vikosi vya Israeli vikawakimbia Wafilisti.
14 pero David y Eleazar se apostaron en medio del campo, defendiendo su terreno y matando a los filisteos. El Señor los salvó dándoles una gran victoria.
Lakini Eleazari na Daudi wakasimama imara katikati ya lile shamba, nao wakalishindania na wakawaua Wafilisti. Naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.
15 En otra ocasión, los Tres, que formaban parte de los Treinta guerreros principales, bajaron a recibir a David cuando estaba en la cueva de Adulam. El ejército filisteo estaba acampado en el valle de Refaim.
Wakuu watatu miongoni mwa wale thelathini, walimwendea Daudi katika mwamba huko kwenye pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai.
16 En ese momento David estaba en la fortaleza, y la guarnición filistea estaba en Belén.
Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu.
17 David tenía mucha sed y dijo: “¡Ojalá alguien pudiera traerme un trago de agua del pozo que está junto a la puerta de la entrada de Belén!”
Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilichoko karibu na lango la Bethlehemu!”
18 Los Tres atravesaron las defensas filisteas, tomaron un poco de agua del pozo de la puerta de Belén y se la llevaron a David. Pero David se negó a beberla y la vertió como ofrenda al Señor.
Kwa hivyo wale watatu, wakapita katikati ya safu za Wafilisti, wakachota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini yeye akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana.
19 “¡Dios me libre de hacer esto!”, dijo. “Sería como beber la sangre de esos hombres que arriesgaron sus vidas. Ellos arriesgaron sus vidas para traerme una bebida”. Así que no la bebió. Estas son algunas de las cosas que hicieron los tres guerreros principales.
Akasema, “Mungu apishie mbali kwamba nifanye hivi! Je kweli, niinywe damu ya watu hawa waliohatarisha maisha yao?” Kwa sababu walihatarisha maisha yao kuyaleta yale maji, Daudi hakukubali kuyanywa. Huo ndio uliokuwa ujasiri wa wale mashujaa watatu.
20 Abisai, hermano de Joab, era el líder de los segundos Tres. Usando su lanza, una vez mató a 300 hombres, y se hizo famoso entre los Tres.
Abishai, ndugu yake Yoabu ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu.
21 Era el más apreciado de los Tres y era su comandante, aunque no fue uno de los primeros Tres.
Alitunukiwa heshima maradufu ya wale Watatu, akawa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.
22 Benaía, hijo de Joiada, un fuerte guerrero de Cabseel, hizo muchas cosas sorprendentes. Mató a dos hijos de Ariel de Moab. También fue tras un león a un pozo en la nieve y lo mató.
Benaya, mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba.
23 En otra ocasión mató a un egipcio, un hombre enorme que medía dos metros y medio. El egipcio tenía una lanza cuyo asta era tan gruesa como la vara de un tejedor. Benaía lo atacó sólo con un garrote, pero pudo agarrar la lanza de la mano del egipcio, y lo mató con su propia lanza.
Alimuua Mmisri aliyekuwa na urefu kama dhiraa tano. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki kama mti wa mfumaji mkononi mwake, Benaya alimwendea na rungu. Akamnyangʼanya Mmisri mkuki wake na kumuua nao.
24 Este fue el tipo de cosas que hizo Benaía y que lo hicieron tan famoso como los tres guerreros principales.
Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu.
25 Era el más apreciado de los Treinta, aunque no era uno de los Tres. David lo puso a cargo de su guardia personal.
Yeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu: Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.
26 Otros guerreros principales eran: Asael, hermano de Joab; Elhanán, hijo de Dodo, de Belén;
Wale watu mashujaa walikuwa: Asaheli nduguye Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu,
27 Sama el harodita; Heles el pelonita;
Shamothi Mharori, Helesi Mpeloni,
28 Ira, hijo de Iques, de Tecoa; Abiezer, de Anatot;
Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa, Abiezeri kutoka Anathothi,
29 Sibecai el husatita; Ilai el ahohita;
Sibekai Mhushathi, Ilai Mwahohi,
30 Maharai, de Netofa; Heled, hijo de Baana, de Netofa;
Maharai Mnetofathi, Heledi mwana wa Baana, Mnetofathi,
31 Itai, hijo de Ribai, de Guibeá, de los benjamitas; Benaía el Piratonita;
Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini, Benaya Mpirathoni,
32 Hurai de los valles de Gaas; Abiel de Arabá;
Hurai kutoka mabonde ya Gaashi, Abieli Mwaribathi,
33 Azmavet de Bahurim; Eliaba el Saalbonita;
Azmawethi Mbaharumi, Eliaba Mshaalboni,
34 Los hijos de Jasén el Gizonita; Jonatán, hijo de Sage el Ararita;
wana wa Hashemu Mgiloni, Yonathani mwana wa Shagee Mharari,
35 Ahíam, hijo de Sacar el Ararita; Elifal, hijo de Ur;
Ahiamu mwana wa Sakari Mharari, Elifale mwana wa Uru,
36 Hefer de Mequer; Ahías el pelonita;
Heferi Mmekerathi, Ahiya Mpeloni,
37 Hezro el Carmelita; Naarai, hijo de Ezbai;
Hezro Mkarmeli, Naarai mwana wa Ezbai,
38 Joel, hermano de Natán; Mibhar, hijo de Hagri;
Yoeli nduguye Nathani, Mibhari mwana wa Hagri,
39 Zelek, el amonita; Naharai, de Beerot; el escudero de Joab, hijo de Sarvia;
Seleki Mwamoni, Naharai Mbeerothi, mbeba silaha wa Yoabu mwana wa Seruya,
40 Ira, de Jatir; Gareb, de Jatir;
Ira Mwithiri, Garebu Mwithiri,
41 Urías, el hitita; Zabad, hijo de Ahlai;
Uria Mhiti, Zabadi mwana wa Alai,
42 Adina, hijo de Siza, rubenita, jefe de los rubenitas, y los treinta que estaban con él;
Adina mwana wa Shiza Mreubeni, ambaye alikuwa mkuu wa Wareubeni, akiwa pamoja na watu thelathini,
43 Hanán, hijo de Maaca; Josafat mitnita;
Hanani mwana wa Maaka, Yoshafati Mmithni,
44 Uzías de Astarot; Sama y Jeiel, los hijos de Hotam de Aroer;
Uzia Mwashterathi, Shama na Yeieli wana wa Hothamu Mwaroeri,
45 Jediael, hijo de Simri, y su hermano, Joha el tizita;
Yediaeli mwana wa Shimri, nduguye Yoha Mtizi,
46 Eliel de Mahava; Jerebai y Josavía, los hijos de Elnaam; Itma el moabita;
Elieli Mmahawi, Yeribai na Yoshavia wana wa Elnaamu, Ithma Mmoabu,
47 Eliel; Obed y Jaasiel, todos ellos de Soba.
Elieli, na Obedi na Yaasieli Mmesobai.

< 1 Crónicas 11 >