< Salmos 73 >
1 De Asaf. ¡Cuán bueno es Dios para Israel, el Señor para los que son rectos de corazón!
Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale walio na moyo safi.
2 Pero, mis pies casi resbalaron, cerca estuve de dar un mal paso;
Lakini kwangu mimi, kidogo tu miguu yangu iteleze; miguu yangu karibu iteleze kutoka kwangu
3 porque envidiaba a los jactanciosos al observar la prosperidad de los pecadores.
kwa sababu niliwaonea wivu wenye kiburi nilipoona mafanikio ya waovu.
4 No hay para ellos tribulaciones; su cuerpo está sano y robusto.
Kwa maana hawana maumivu hadi kufa kwao, lakini wana nguvu na wameshiba.
5 No conocen las inquietudes de los mortales, ni son golpeados como los demás hombres.
Wako huru dhidi ya mizigo ya watu wengine; nao hawateswi kama watu wengine.
6 Por eso la soberbia los envuelve como un collar; y la violencia los cubre como un manto.
Kiburi kinawapamba kama mkufu kwenye shingo zao; jeuri huwavika kama vazi.
7 De su craso corazón desborda su iniquidad; desfogan los caprichos de su ánimo.
Katika upofu wa jinsi hii dhambi huja; mawazo maovu hupita mioyoni mwao.
8 Zahieren y hablan con malignidad, y altivamente amenazan con su opresión.
Wao hudhihaki na kuongea kwa namna ya uovu; kwa kiburi chao hutishia mateso.
9 Su boca se abre contra el cielo, y su lengua se pasea por toda la tierra.
Wameweka vinywa vyao dhidi ya mbingu, na ndimi zao hutanga tanga duniani.
10 Así el pueblo se vuelve hacia ellos y encuentra sus días plenos;
Kwa hiyo watu wake huwageukia na maji yaliyojaa hukaushwa.
11 y dice: “¿Acaso lo sabe Dios? ¿Tiene conocimiento el Altísimo?
Nao husema, “Mungu anajuaje? Yako maarifa kwake yeye aliye juu?”
12 Ved cómo tales impíos están siempre tranquilos y aumentan su poder.
Fahamu: watu hawa ni waovu; mara zote hawajali, wakifanyika matajiri na matajiri.
13 Luego, en vano he guardado puro mi corazón, y lavado mis manos en la inocencia,
Hakika nimeutunza moyo wangu bure na nimenawa mikono yangu pasipo kukosa.
14 pues padezco flagelos todo el tiempo y soy atormentado cada día.”
Maana mchana kutwa nimeteswa na kuadhibiwa kila asubuhi.
15 Si yo dijere: “Hablaré como ellos”, renegaría del linaje de tus hijos.
Kama ningesema, “Ningesema mambo haya,” kumbe nigewasaliti kizazi hiki cha watoto wenu.
16 Me puse, pues, a reflexionar para comprender esto; pero me pareció demasiado difícil para mí.
Ingawa nilijaribu kuyaelewa mambo haya, yalikuwa ni magumu sana kwangu.
17 Hasta que penetré en los santos arcanos de Dios, y consideré la suerte final de aquellos hombres.
Ndipo nilipoingia patakatifu pa Mungu na kuelewa hatma yao.
18 En verdad Tú los pones en un camino resbaladizo y los dejas precipitarse en la ruina.
Hakika wewe huwaweka penye utelezi; huwaangusha mpaka palipoharibika.
19 ¡Cómo se deslizaron de golpe! Son arrebatados, consumidos por el terror,
Jinsi gani wamekuwa ukiwa kwa muda mfupi! Wamefika mwisho nao wamemaliza kwa utisho.
20 son como quien despierta de un sueño; así Tú, Señor, al despertar despreciarás su ficción.
Wao ni kama ndoto wakati wa mtu kuamka; Bwana, utakapo inuka, utazidharau ndoto zao.
21 Cuando, pues, exasperaba mi mente y se torturaban mis entrañas,
Maana moyo wangu ulipata uchungu, nami nilijeruhiwa sana.
22 era yo un estúpido que no entendía; fui delante de Ti como un jumento.
Nilikuwa mjinga na sijui neno; nilikuwa kama mnyama tu mbele yako.
23 Mas yo estaré contigo siempre, Tú me has tomado de la mano derecha.
Lakini mimi nipo pamoja nawe daima; umenishika mkono wa kuume.
24 Por tu consejo me conducirás, y al fin me recibirás en la gloria.
Utaniongoza kwa shauri lako na baadaye utanipokea katika utukufu.
25 ¿Quién hay para mí en el cielo sino Tú? Y si contigo estoy ¿qué podrá deleitarme en la tierra?
Ni nani niliye naye mbinguni isipokuwa wewe? Hakuna nimtamaniye duniani isipokuwa wewe.
26 La carne y el corazón mío desfallecen, la roca de mi corazón es Dios, herencia mía para siempre.
Mwili wangu na moyo wangu huwa dhaifu, bali Mungu ndiye nguvu ya moyo wangu daima.
27 Pues he aquí que cuantos de Ti se apartan perecerán; Tú destruyes a todos los que se prostituyen, alejándose de Ti.
Wale walio mbali nawe wataangamia; utawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
28 Mas para mí la dicha consiste en estar unido a Dios. He puesto en el Señor Dios mi refugio para proclamar todas tus obras en las puertas de la hija de Sión.
Lakini mimi, linipasalo kufanya ni kumkaribia Mungu. Nimemfanya Bwana Yahwe kimbilio langu. Nami nitayatangaza matendo yako yote.