< Salmos 55 >

1 Al maestro de coro. Para instrumentos de cuerda. Maskil de David. Escucha oh Dios, mi oración, y no te escondas de mi súplica.
Kwa mwimbishaji. Na ala za uimbaji. Utenzi wa Daudi. Ee Mungu, sikiliza maombi yangu, wala usidharau hoja yangu.
2 Atiéndeme, inclina tu oído. Vago gimiendo y sobresaltado [y estoy turbado]
Nisikie na unijibu. Mawazo yangu yananisumbua na nimehangaishwa
3 ante las amenazas del enemigo y la opresión del inicuo; se acumulan calamidades sobre mí y me asaltan con furor.
kwa sauti ya adui, kwa kukaziwa macho na waovu, kwa sababu wananiletea mateso juu yangu na kunitukana kwa hasira zao.
4 El corazón tiembla en mi pecho, y me acometen mortales angustias.
Moyo wangu umejaa uchungu, hofu ya kifo imenishambulia.
5 El temor y el terror me invaden, y me envuelve el espanto.
Woga na kutetemeka vimenizunguka, hofu kuu imenigharikisha.
6 Y exclamo: “¡Oh si tuviera yo alas como la paloma para volar en busca de reposo!”
Nilisema, “Laiti ningekuwa na mbawa za njiwa! Ningeruka niende mbali kupumzika.
7 Me iría bien lejos a morar en el desierto.
Ningalitorokea mbali sana na kukaa jangwani,
8 Me escaparía al instante del torbellino y de la tempestad.
ningaliharakisha kwenda mahali pa salama, mbali na tufani kali na dhoruba.”
9 Piérdelos, Señor; divide sus lenguas, pues en la ciudad veo la violencia y la discordia
Ee Bwana, uwatahayarishe waovu na uwachanganyishie semi zao, maana nimeona jeuri na ugomvi mjini.
10 rondar día y noche sobre sus muros; y en su interior hay opresión y ruina.
Usiku na mchana wanazunguka juu ya kuta zake, uovu na dhuluma vimo ndani yake.
11 La insidia impera en medio de ella, y de sus plazas no se apartan la injuria y el engaño.
Nguvu za uharibifu zinatenda kazi mjini, vitisho na uongo haviondoki mitaani mwake.
12 Si me insultara un enemigo, lo soportaría; si el que me odia se hubiese levantado contra mí, me escondería de él simplemente.
Kama aliyenitukana ni adui yangu, ningevumilia, kama mtu mwovu angejiinua dhidi yangu, ningejificha asinione.
13 Pero eres tú, mi compañero, mi amigo y mi confidente,
Kumbe ni wewe, mwenzangu, mshiriki na rafiki yangu wa karibu,
14 con quien vivía yo en dulce intimidad, y subíamos en alegre consorcio a la casa de Dios.
ambaye awali tulifurahia ushirika mzuri, tulipokuwa tukienda na umati hekaluni mwa Mungu.
15 Sorpréndalos la muerte; vivos aún desciendan al sepulcro, porque la maldad reina en sus moradas [y en ellos mismos]. (Sheol h7585)
Kifo na kiwajie adui zangu ghafula, na washuke kuzimu wangali hai, kwa maana uovu upo ndani yao. (Sheol h7585)
16 Mas yo clamaré a Dios, y Yahvé me salvará.
Lakini ninamwita Mungu, naye Bwana huniokoa.
17 Me lamentaré y lloraré a la tarde, a la mañana, a mediodía, y Él oirá mi voz.
Jioni, asubuhi na adhuhuri ninalia kwa huzuni, naye husikia sauti yangu.
18 Me sacará sano y salvo de los asaltos, aunque son muchos contra mí.
Huniokoa nikawa salama katika vita vilivyopangwa dhidi yangu, ingawa watu wengi hunipinga.
19 Me escuchará Dios y los humillará Él, que es eternamente. Porque no hay modo de convertirlos, y no temen a Dios.
Mungu anayemiliki milele, atawasikia na kuwaadhibu, watu ambao hawabadilishi njia zao, wala hawana hofu ya Mungu.
20 Cada cual levanta su mano contra el amigo, y violan la fe jurada.
Mwenzangu hushambulia rafiki zake, naye huvunja agano lake.
21 Más blando que manteca es su rostro, pero su corazón es feroz; sus palabras, más untuosas que el aceite, son espadas desnudas.
Mazungumzo yake ni laini kama siagi, hata hivyo vita vimo moyoni mwake. Maneno yake ni mororo kuliko mafuta, hata hivyo ni upanga mkali uliofutwa.
22 Deja tu cuidado a cargo de Yahvé, y Él te sostendrá. Nunca permitirá que el justo caiga;
Mtwike Bwana fadhaa zako, naye atakutegemeza, hatamwacha kamwe mwenye haki wake aanguke.
23 mas a ellos, oh Dios, los harás descender a la fosa. No llegarán a la mitad de sus días esos hombres sanguinarios y fraudulentos. Yo, empero, pongo en Ti mi confianza, oh Señor.
Lakini wewe, Ee Mungu, utawashusha waovu katika shimo la uharibifu. Wenye kiu ya kumwaga damu na wenye hila, hawataishi nusu ya siku zao. Lakini mimi ninakutumaini wewe.

< Salmos 55 >