< Salmos 36 >

1 Al maestro de coro. De David, siervo de Dios. La rebeldía instiga al impío en su corazón; a sus ojos no hay temor de Dios.
Dhambi hunena kama unabii katika moyo wa mwovu; machoni mwake hamna hofu ya Mungu.
2 Por tanto, se lisonjea en su mente de que su culpa no será hallada ni aborrecida.
Kwa maana yeye hujifariji mwenyewe, akifikiria kuwa dhambi zake hazitagundulika na kuchukiwa.
3 Las palabras de su boca son malicia y fraude, no se cuida de entender para obrar bien.
Maneno yake ni yenye dhambi na udanganyifu; hataki kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
4 En su lecho medita la iniquidad; anda siempre en malos caminos. La maldad no le causa horror.
Alalapo kitandani, hupanga namna ya kutenda dhambi; yeye hukaa nje kwenye nja ya uovu; yeye hakatai uovu.
5 Yahvé, tu misericordia toca el cielo; tu fidelidad, las nubes.
Uaminifu wa agano lako, Yahwe, unafika mbinguni; uaminifu wako unafika mawinguni.
6 Tu justicia es alta como los montes de Dios; profundos como el mar, tus juicios. Tú, Yahvé, socorres al hombre y al animal.
Haki yako ni kama milima ya Mungu; hukumu yako ni kama kina kirefu. Yahwe, wewe huwahifadhi wote wanadamu na wanyama.
7 ¡Cuán preciosa es, oh Dios, tu largueza! los hijos de los hombres se abrigan a la sombra de tus alas.
Ni jinsi gani uaminifu wa aganao lako ni wa thamani, Mungu! Watu hukimbilia usalama chini ya uvuli wa mbawa zako.
8 Se sacian con la abundancia de tu casa, y los embriagas en el río de tus delicias.
Nao watatoshelezwa tele na utajiri wa chakula nyumbani mwako; utawafanya wanywe kutoka katika mto wa baraka zako za thamani.
9 Pues en Ti está la fuente de la vida, y en tu luz vemos la luz.
Kwa kuwa mna chemichemi ya uzima; na katika mwanga wako tutaiona nuru.
10 Despliega tu bondad sobre los que te conocen, y tu justicia sobre los de corazón recto.
Uupanue uaminifu wa agano lako kikamilifu kwa wale wanao kujua wewe, ulinzi wako uwe juu ya wanyoofu wa moyo.
11 No me aplaste el pie del soberbio ni me haga vacilar la mano del impío.
Usiuache mguu wa mwenye kiburi unisogelee. Usiiache mkono wa mwovu unitoweshe.
12 He aquí derribados a los obradores de la iniquidad, caídos para no levantarse más.
Kule wafanyao maovu wameanguka; wameharibiwa hawawezi kuinuka.

< Salmos 36 >