< Salmos 150 >

1 ¡Hallelú Yah! Alabad al Señor en su Santuario, alabadlo en la sede de su majestad.
Msifuni Bwana. Msifuni Mungu katika patakatifu pake, msifuni katika mbingu zake kuu.
2 Alabadlo por las obras de su poder, alabadlo según su inmensa grandeza.
Msifuni kwa matendo yake makuu, msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.
3 Alabadlo al son de trompeta, alabadlo con salterio y cítara.
Msifuni kwa mvumo wa tarumbeta, msifuni kwa kinubi na zeze,
4 Alabadlo con tamboril y danza, alabadlo con cuerdas y flautas.
msifuni kwa matari na kucheza, msifuni kwa kinanda cha nyuzi na filimbi,
5 Alabadlo con címbalos sonoros, alabadlo con címbalos que atruenen.
msifuni kwa matoazi yaliayo, msifuni kwa matoazi yavumayo sana.
6 ¡Todo lo que respira alabe al Señor! ¡Hallelú Yah!
Kila chenye pumzi na kimsifu Bwana. Msifuni Bwana!

< Salmos 150 >