< Salmos 129 >
1 Cántico gradual. Mucho me han combatido desde mi mocedad, exclame ahora Israel;
Wimbo wa kwenda juu. Wamenionea mno tangu ujana wangu; Israeli na aseme sasa:
2 mucho me combatieron desde mi mocedad, mas no concluyeron conmigo.
wamenionea mno tangu ujana wangu, lakini bado hawajanishinda.
3 Sobre mis espaldas araron los aradores; abrieron largos surcos;
Wakulima wamelima mgongo wangu, na kufanya mifereji yao mirefu.
4 mas Yahvé, el Justo, ha cortado las coyundas de los impíos.
Lakini Bwana ni mwenye haki; amenifungua toka kamba za waovu.
5 Retrocedan confundidos cuantos odian a Sión.
Wale wote waichukiao Sayuni na warudishwe nyuma kwa aibu.
6 Sean como la hierba de los tejados, que se seca antes de crecer.
Wawe kama majani juu ya paa, ambayo hunyauka kabla hayajakua;
7 No llena de ella su mano el segador, ni su regazo el que hace gavillas.
kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake, wala akusanyaye kujaza mikono yake.
8 No dicen los transeúntes: “La bendición de Yahvé sea sobre vosotros.” “Os bendecimos en el Nombre de Yahvé.”
Wale wapitao karibu na wasiseme, “Baraka ya Bwana iwe juu yako; tunakubariki katika jina la Bwana.”