< Salmos 108 >
1 Cántico. Salmo. De David. Mi corazón está pronto, oh Dios; quiero cantar y entonar salmos; mi alma está despierta.
Wimbo. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
2 Salterio y lira, despertaos; despiértese la aurora (a nuestro canto).
Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
3 Te alabaré, Yahvé, entre los pueblos, te cantaré himnos ante las naciones.
Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
4 Porque tu misericordia es más grande que los cielos, y tu fidelidad hasta las nubes.
Kwa maana upendo wako ni mkuu, ni juu kuliko mbingu; uaminifu wako unazifikia anga.
5 Muéstrate excelso, oh Dios, sobre los cielos, y brille tu gloria sobre toda la tierra,
Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
6 para que sean libertados los que Tú amas; socorre con tu diestra y escúchanos.
Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
7 Lo dijo Dios por su santidad: “Triunfaré; repartiré a Siquem, y mediré el valle de Sucot.
Mungu amenena kutoka patakatifu pake: “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi na kulipima Bonde la Sukothi.
8 Mía es la tierra de Galaad, mía la tierra de Manasés; Efraím es el yelmo de mi cabeza, y Judá, mi cetro;
Gileadi ni yangu, Manase ni yangu, Efraimu ni kofia yangu ya chuma, nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
9 Moab, la vasija de mi lavatorio; sobre Edom echaré mi calzado, sobre Filistea cantaré victoria.”
Moabu ni sinia langu la kunawia, juu ya Edomu natupa kiatu changu; nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
10 ¿Quién me conducirá a la ciudad inaccesible? ¿Quién me llevará hasta Edom?
Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
11 ¿No serás Tú, oh Dios, que nos has rechazado y que ya no sales con nuestros ejércitos?
Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
12 Ven en nuestro auxilio contra el adversario, porque vano es el concurso de los hombres.
Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
13 Con Dios haremos proezas; Él hollará a nuestros enemigos.
Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.