< Proverbios 5 >
1 Hijo mío, presta atención a mi sabiduría, inclina tu oído a mi enseñanza,
Mwanangu, zingatia hekima yangu; sikiliza kwa makini ufahamu wangu,
2 para que guardes los consejos y tus labios conserven la instrucción.
ili ujifunze busara na midomo yako iweze kuhifadhi maarifa.
3 Pues los labios de la mujer extraña destilan miel, y su paladar es más suave que el aceite;
Maana midomo ya malaya hutiririsha asali na kinywa chake ni laini kuliko mafuta,
4 pero su fin es amargo como el ajenjo, cortante como espada de dos filos.
lakini mwishoni anakuwa mchungu kama mnyoo, hukata kama upunga mkali.
5 Sus pies se encaminan hacia la muerte, sus pasos llevan al scheol. (Sheol )
Miguu yake huelekea mauti; hatua zake huelekea njia yote ya kuzimu. (Sheol )
6 No anda por la senda de la vida, va errando por caminos sin saber adónde.
Hafikirii njia ya uzima. Hatua za miguu yake hupotea, maana hajui anakwenda wapi.
7 Pues bien, escuchadme, hijos, y no os apartéis de las palabras de mi boca;
Sasa, wanangu, nisikilizeni; wala msiache kusikiliza maneno ya kinywa changu.
8 desvía de ella tu camino, y no te acerques a la puerta de su casa.
Lindeni njia yenu mbali naye wala msiende karibu na mlango wa nyumba yake.
9 No sacrifiques tu honor a gente extraña ni tus años a un tirano,
Kwa njia hiyo hamtawapa wengine heshima yenu au miaka ya uzima wenu kwa mtu mkatiri;
10 no sea que extraños se harten de tus bienes, y tus fatigas beneficien a casas ajenas,
wageni usije kufanya karamu kwa utajiri wenu; kazi mliyoifanya haitaenda katika nyumba ya wageni.
11 y al fin tengas que gemir, después de consumir tu carne,
Mwishoni mwa maisha yenu mtajuta ambapo nyama na mwili wenu vitaangamia.
12 y hayas de exclamar: “¡Cómo he podido aborrecer la instrucción, y rehusar en mi corazón la corrección!
Nanyi mtasema, “Namna gani nilichukia fundisho na moyo wangu ulidharau sahihisho!
13 Desoí la voz de los que me adoctrinaban y no quise oír a mis maestros.
Sikuweza kuwatii walimu wangu au kuwasikiliza walionielekeza.
14 Casi he llegado al colmo de los males, en medio del pueblo y de la asamblea.”
Nilikuwa nimeharibika kabisa katikati ya kusanyiko, miongoni mwa makutano ya watu.”
15 Bebe el agua de tu aljibe y los raudales que manan de tu pozo.
Munywe maji kutoka kwenye birika lenu mwenyewe na munywe maji yanatiririka kutoka kwenye kisima chenu.
16 ¿Por qué derramar fuera tus fuentes, por las plazas las corrientes de tu agua?
Je inapaswa chemichemi yenu ifurike popote na mifereji yenu ya maji itiririke katika njia kuu?
17 ¡Sean para ti solo, y no para los extraños a tu lado!
Yawe yenu wenyewe peke yenu wala si kwa wageni.
18 ¡Sea tu fuente bendita, y alégrate con la esposa de tu mocedad!
Chemichemi yako ibarikiwe na umfurahie mke wa ujana wako.
19 ¡Sea ella la gacela de tu amor, una cierva graciosa, embriáguenle sus pechos perpetuamente, y su amor te encante en todo tiempo!
Maana ni ayala apendezaye na kulungu mwenye uzuri. Matiti yake na yakujaze furaha muda wote; daima na utekwe na upendo wake.
20 ¿Por qué, hijo mío, dejarte embaucar por la mujer extraña y abrazar el seno de la ajena?
Mwanangu, kwa nini uwe mateka wa malaya, kwa nini uyakumbatie matiti ya mwanamke mgeni?
21 Pues ante Yahvé están los caminos del hombre. Él mira todos sus pasos.
Yehova huona kila kitu afanyacho mtu na huangalia mapito yake yote.
22 El hombre malo será presa de sus propias iniquidades, y quedará enredado en los lazos de su pecado.
Mtu mwovu atatekwa na makosa yake mwenyewe; kamba za dhambi yake zitamnasa kwa nguvu.
23 Perecerá por falta de disciplina, y andará perdido a causa de su gran necedad.
Atakufa kwa kukosa maonyo; atapotelea mbali kwa upumbavu wake wingi.