< Proverbios 19 >
1 Más vale el pobre que vive rectamente, que el rico fatuo y de lengua perversa.
Bora mtu masikini ambaye huenenda katika uadilifu wake kuliko mwenye ukaidi katika maneno yake na ni mpumbavu.
2 Es un mal si el alma carece de ciencia, pues tropieza el que anda precipitado.
Tena, si vizuri kuwa na hamu bila maarifa na mwenye kukimbia haraka sana hukosea njia.
3 La necedad le tuerce al hombre sus caminos, y luego murmura su corazón contra Yahvé.
Upuuzi wa mtu unaharibu maisha yake na moyo wake hughadhabika dhidi ya Yehova.
4 Las riquezas aumentan mucho el número de los amigos, el pobre, empero, es abandonado de su propio compañero.
Utajiri huongeza marafiki wengi, bali mtu masikini hutengwa na rafiki zake.
5 Testigo falso no quedará sin castigo, y no se librará el que profiere mentiras.
Shahidi wa uongo hatakosa adhabu na mwenye kupumua uongo hataokoka.
6 El dadivoso tiene muchos aduladores; todos son amigos del que da regalos.
Wengi wataomba fadhila kutoka kwa mtu mkarimu na kila mtu ni rafiki wa yule anayetoa zawadi.
7 Si al pobre le aborrecen todos sus hermanos, ¡Cuánto más se alejarán de él sus amigos! Quiere ganarlos con palabras pero no están a su alcance.
Mtu masikini huchukiwa na ndugu zake wote; je marafiki wengi kiasi gani hujitenga kutoka kwake! Anawaita, lakini wameondoka.
8 El que adquiere inteligencia ama su alma, quien se acomoda a la prudencia hallará la dicha.
Anayepata hekima huyapenda maisha yake mwenyewe; yeye atunzaye ufahamu atapata kilicho chema.
9 El testigo falso no quedará impune, y el que propala mentiras perecerá.
Shahidi wa uongo hatakosa kuadhibiwa, bali mwenye kupumua uongo ataangamia.
10 No está bien al necio una vida regalada, mucho menos a un esclavo el mandar a los príncipes.
Haifai kwa mpumbavu kuishi kwa anasa- wala kwa mtumwa kutawala juu ya wafalme.
11 El hombre sabio detiene su ira; su gloria es olvidar las injurias.
Busara humfanya mtu achelewe kukasirika na utukufu wake ni kusamehe kosa.
12 Como rugido de león es la ira del rey; y su favor cual rocío sobre el césped.
Ghadhabu ya mfalme ni kama muungurumo wa simba kijana, bali fadhila yake ni kama umande kwenye majani.
13 Dolor de su padre es el hijo insensato, y gotera continua la mujer rencillosa.
Mwana mpumbavu ni uharibifu kwa baba yake na mke mgomvi ni maji yanayochuruzika daima.
14 Casa y riqueza se heredan de los padres, pero la mujer discreta es don de Yahvé.
Nyumba na utajiri ni urithi kutoka kwa wazazi, bali mke mwenye busara hutoka kwa Yehova.
15 La pereza trae el sueño, y la indolencia el hambre.
Uvivu unamtupa mtu kwenye usingizi mzito, bali asiyetamani kufanya kazi atakwenda njaa.
16 Quien guarda los mandamientos, guarda su alma; mas el que menosprecia los caminos de (Yahvé) morirá.
Yeye anayetii amri huyaongoza maisha yake, bali mtu asiyefikiri juu ya njia zake atakufa.
17 Quien se apiada del pobre, presta a Yahvé, el cual le recompensará su obra.
Mwenye ukarimu kwa masikini humkopesha Yehova na atalipwa kwa kile alichofanya.
18 Castiga a tu hijo, pues hay esperanza; pero no te dejes llevar a darle muerte.
Mrudi mwanao wakati kuna matumaini na usiwe na shauku ya kumweka katika mauti.
19 El que mucho se aíra sufrirá penas, de las cuales aun cuando le libras has de sacarle siempre de nuevo.
Mtu mwenye hasira kali lazima alipe adhabu; kama ukimwokoa, utafanya hivyo mara mbili.
20 Escucha el consejo, y acepta la corrección, para que seas sabio en tu fin.
Sikiliza ushauri na ukubali maelekezo, ili uweze kuwa na hekima mwishoni mwa maisha yako.
21 Muchos proyectos hay en el corazón del hombre, pero siempre se cumple el designio de Yahvé.
Moyoni mwa mtu kuna mipango mingi, bali kusudi la Yehova ndilo litakalo simama.
22 Al hombre le gusta ser compasivo; más vale ser pobre que mentiroso.
Shauku ya mtu ni uaminifu na mtu masikini ni bora kuliko muongo.
23 El temor de Yahvé conduce a la vida; así queda (el hombre) satisfecho y libre de todo mal.
Kumheshimu Yehova huwaelekeza watu kwenye uzima; mwenye nayo atashibishwa na hatadhurika kwa madhara.
24 El haragán mete su mano en el plato, pero no la lleva a su boca.
Mtu goigoi huuzika mkono wake ndani ya dishi; hataurudisha juu ya kinywa chake.
25 Castiga al burlador, y se hace cuerdo el necio; amonesta al sensato y entenderá la sabiduría.
Kama utampiga mwenye mzaha, wajinga watakuwa na hekima; mwelekeze mwenye ufahamu, naye atapata maarifa.
26 Quien maltrata a su padre y echa de sí a su madre, es un hijo desvergonzado y sin honor.
Anayempora baba yake na kumfukuza mama yake ni mwana anayeleta aibu na shutuma.
27 Hijo mío, si dejas de oír consejos, te desviarás de las palabras de la sabiduría.
Mwanangu, kama utaacha kusikiliza maelekezo, utapotea kutoka kwenye maneno ya maarifa.
28 El testigo perverso se ríe de la justicia; y la boca de los impíos se traga la iniquidad.
Shahidi mpotofu huidhihaki haki na kinywa cha waovu humeza uovu.
29 Los castigos han sido hechos para los burladores, y los azotes para las espaldas de los insensatos.
Hukumu ipo tayari kwa wenye dhihaka na mjeledi kwa migongo ya wapumbavu.