< Job 9 >
2 “Bien sé que es así. ¿Cómo puede el hombre ser justo frente a Dios?
“Naam, najua hili ni kweli. Lakini mwanadamu awezaje kuwa mwadilifu mbele za Mungu?
3 Si pretendiera contender con él, de mil (cargos) no respondería a uno solo.
Ingawa mtu angetaka kushindana naye, asingaliweza kumjibu Mungu hata mara moja miongoni mwa elfu moja.
4 Él es sabio de corazón, poderoso y fuerte; ¿quién se le opuso y le salió bien?
Hekima yake ni kubwa sana na ana uwezo mwingi mno. Ni nani aliyempinga naye akawa salama?
5 Él traslada los montes, sin que sepan quién los trastorna en su ira.
Aiondoa milima bila yenyewe kujua na kuipindua kwa hasira yake.
6 Él remueve la tierra de su sitio, y sus columnas son sacudidas.
Aitikisa dunia kutoka mahali pake na kuzifanya nguzo zake zitetemeke.
7 Él manda al sol, y este no sale, y encierra bajo sello las estrellas.
Husema na jua, nalo likaacha kuangaza; naye huizima mianga ya nyota.
8 Él solo extiende los cielos, y anda sobre las olas del mar.
Yeye peke yake huzitandaza mbingu na kuyakanyaga mawimbi ya bahari.
9 Él hizo la Osa, el Orión y las Pléyades, las constelaciones del cielo austral.
Yeye ndiye Muumba wa nyota za Dubu, na Orioni, Kilimia, na makundi ya nyota za kusini.
10 Él hace cosas grandes e insondables, y maravillas sin cuento y número.
Hutenda maajabu yasiyopimika, miujiza isiyoweza kuhesabiwa.
11 He aquí que pasa junto a mí, y yo no le veo; y si se retira, tampoco lo advierto.
Anapopita karibu nami, siwezi kumwona; apitapo mbele yangu, simtambui.
12 Si Él toma una presa ¿quién hará que la devuelva? ¿quién podrá decirle: «¿Qué es lo que haces?»
Anapochukua kwa ghafula, ni nani awezaye kumzuia? Ni nani awezaye kumwambia, ‘Unafanya nini?’
13 Él es Dios, no hay quien pueda doblegar su ira; debajo de Él se encorvan los auxiliares de Rahab.
Mungu hataizuia hasira yake; hata jeshi kubwa la Rahabu lenye nguvu linajikunyata miguuni pake.
14 ¿Cuánto menos podré yo responderle, elegir mis palabras frente a Él?
“Ni vipi basi mimi nitaweza kubishana naye? Nawezaje kupata maneno ya kuhojiana naye?
15 Aun teniendo yo razón, nada le respondería; imploraría la clemencia del que me juzga.
Ingawa sikuwa na hatia, sikuweza kumjibu; ningeweza tu kumsihi Mhukumu wangu anihurumie.
16 Aun cuando respondiera a mis clamores, no creería que había escuchado mi voz,
Hata kama ningemwita kwenye shauri, naye akakubali, siamini kama angenisikiliza.
17 Él, que me aplasta con un torbellino, y multiplica mis llagas sin causa.
Yeye angeniangamiza kwa dhoruba na kuongeza majeraha yangu pasipo na sababu.
18 No me deja respirar y me harta de amargura.
Asingeniacha nipumue bali angenifunika kabisa na huzuni kuu.
19 Si se trata de fuerza, el poderoso es Él, y si de justicia (dice): «¿Quién me emplazará?»
Kama ni suala la nguvu, yeye ni mwenye nguvu! Kama ni suala la haki, ni nani awezaye kumwita mahakamani?
20 Aun cuando yo tuviera razón mi boca me condenaría, aunque fuera inocente, me declararía culpable.
Hata kama sikuwa na hatia, kinywa changu kingenihukumu; kama sikuwa na kosa, kingenitangaza kuwa mwenye hatia.
21 Soy inocente, pero no me importa mi existencia, no hago caso de mi vida.
“Ingawa mimi sina kosa, haileti tofauti katika nafsi yangu; nauchukia uhai wangu.
22 Es todo lo mismo; por eso he dicho: «Él acaba con el inocente como con el impío.»
Hayo yote ni sawa; ndiyo sababu nasema, ‘Yeye huwaangamiza wasio na makosa pamoja na waovu.’
23 ¡Si al menos el azote matase de repente! Él se ríe de la prueba de los inocentes.
Wakati pigo liletapo kifo cha ghafula, yeye hudhihaki kule kukata tamaa kwa yule asiye na kosa.
24 La tierra ha sido entregada en manos de los malvados; Él mismo tapa el rostro de sus jueces. Si no es Él, ¿quién lo será?
Wakati nchi inapoangukia mikononi mwa waovu, yeye huwafunga macho mahakimu wake. Kama si yeye, basi ni nani?
25 Mis días pasaron más veloces que un correo, huyen sin ver cosa buena;
“Siku zangu zapita mbio kuliko mkimbiaji; zinapita upesi bila kuona furaha hata kidogo.
26 pasan como las naves de junco, cual águila que se arroja sobre la presa.
Zinapita upesi kama mashua ya mafunjo, mfano wa tai ayashukiaye mawindo kwa ghafula.
27 Si digo: «Olvidaré mis quejas, voy a mudar mi semblante, y me regocijaré»,
Kama nikisema, ‘Nitayasahau malalamiko yangu, nitabadili sura ya uso wangu na kutabasamu,’
28 me espantan todos mis dolores, pues sé que Tú no me declaras inocente.
bado ninahofia mateso yangu yote, kwa kuwa ninajua hutanihesabu kuwa sina hatia.
29 Y si soy juzgado culpable, ¿por qué fatigarme en vano?
Kwa kuwa nimeonekana mwenye hatia, kwa nini basi nitaabishwe bure?
30 Aunque me lavara con agua de nieve, y con lejía limpiara mis manos,
Hata kama ningejiosha kwa sabuni na kutakasa mikono yangu kwa magadi,
31 Tú me sumergirías en el fango, y hasta mis vestidos me darían asco.
wewe ungenitupa kwenye shimo la utelezi kiasi kwamba hata nguo zangu zingenichukia sana.
32 Porque Él no es un hombre como yo, a quien se pudiera decir: «¡Vamos juntos a juicio!»
“Yeye si mwanadamu kama mimi ili niweze kumjibu, ili kwamba tuweze kushindana naye mahakamani.
33 No hay entre nosotros árbitro que ponga la mano sobre entrambos.
Laiti angelikuwepo mtu wa kutupatanisha kati yetu, aweke mkono wake juu yetu sote wawili,
34 Aparte Él de mí su vara, y no me espante su terror:
mtu angeliiondoa fimbo ya Mungu juu yangu, ili utisho wake usiendelee kunitia hofu.
35 entonces hablaré, sin tenerle miedo, porque así como estoy, no me conozco a mí mismo.”
Ndipo ningenena naye, bila kumwogopa, lakini kama ilivyo kwangu sasa, sitaweza.