< Job 37 >

1 “Por esto tiembla mi corazón, y salta de su lugar.
“Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
2 Oíd, oíd el trueno de su voz, el ruido que sale de su boca.
Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
3 Lo hace retumbar por toda la extensión del cielo, y su fulgor brilla hasta los confines de la tierra.
Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
4 Tras de Él se oye una voz rugiente; pues truena con la voz de su majestad; y no retiene más (los rayos) cuando se oye su voz.
Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
5 Truena la voz de Dios y obra maravillas, hace cosas grandes e inescrutables.
Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
6 Pues a la nieve dice: «¡Baja a la tierra!» Él (envía) la lluvia y los aguaceros torrenciales.
Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
7 Sobre la mano de todos pone un sello, para que todos conozcan Su obra.
Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
8 Las fieras se retiran a sus cubiles, y descansan en sus guaridas.
Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
9 De sus cámaras sale el huracán, y del norte viene el frío.
Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
10 Al soplo de Dios se forma el hielo, y en su derretimiento se ensanchan las aguas.
Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
11 Él carga con vapor la nube, y la nube esparce sus fulgores,
Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
12 que dando vueltas según sus planes hacen lo que Él manda sobre la redondez de la tierra;
Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
13 ora para corrección de su tierra, ora para mostrar su misericordia.
Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
14 Esto, oh Job, escúchalo bien, detente, y considera las maravillas de Dios.
“Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
15 ¿Sabes tú cómo Dios las realiza, y cómo hace relampaguear la luz de sus nubes?
Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
16 ¿Conoces tú el balanceo de las nubes, las maravillas de Aquel que es perfecto en saber?
Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
17 ¿ (Sabes) tú por qué se calientan tus vestidos, cuando la tierra se calla bajo el soplo del Austro?
Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
18 ¿Extendiste tú con Él el firmamento, tan sólido como un espejo fundido?
je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
19 Díganos qué debemos responderle, ya que no sabemos qué decirle, siendo como somos ignorantes.
“Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
20 Mas ¿hay que contarle lo que yo digo? pues el hombre, por más que hable, no es más que una nada.
Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
21 Ahora ya no se ve la luz, aquel resplandor en el firmamento; pasó el viento, y lo deja despejado.
Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
22 Del norte viene áureo (brillo), la terrible majestad, que envuelve a Dios.
Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
23 Él Todopoderoso, el inaccesible, es grande en poder y juicio, es rico en justicia, y no oprime a nadie.
Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
24 Por eso han de temerlo los hombres: no mira Él a los que se creen sabios.”
Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”

< Job 37 >