< Job 32 >

1 Desistieron aquellos tres hombres de responder a Job; porque este estaba convencido de su inocencia.
Hivyo hawa watu watatu walikoma kumjibu Ayubu kwasababu alikuwa ni mwenye haki katika macho yake mwenyewe.
2 Entonces montó en cólera Eliú, hijo de Baraquel bucita, de la familia de Ram. Montó en cólera contra Job, porque pretendía ser más justo que Dios.
Ndipo iliwaka hasira ya Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi, wa familia ya Ramu, iliwaka dhidi ya Ayubu kwa kuwa alijihesabia haki mwenyewe kuliko Mungu.
3 Se irritó también contra sus tres amigos, por cuanto no habían hallado qué contestar a Job, y con todo lo condenaban.
Hasira ya Elihu iliwaka pia kinyume cha marafiki zake watatu kwasababu hawakupata jibu kwa ajili ya Ayubu, na bado walimhukumu Ayubu.
4 Siendo ellos de mayor edad que él, Eliú había tardado en contestar a Job.
Sasa Elihu alikuwa amemsubiri Ayubu ili aweze kuzungumza naye kwa kuwa watu wengine walikuwa wakubwa kuliko yeye.
5 Mas cuando vio que no había más respuesta en la boca de aquellos tres hombres, se indignó sobremanera. Tomó Eliú, hijo de Baraquel, bucita, la palabra y dijo:
Hata hivyo, wakati Elihu alipoona ya kuwa hapakuwa na jibu katika midomo ya watu hawa watatu, hasira yake iliwaka.
6 “Siendo yo joven, y vosotros ancianos, tuve miedo, y no me atreví a manifestar mi parecer.
Ndipo Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi alinena na kusema, “Mimi ni mdogo, na ninyi ni wazee. Hii ndio sababu nilijizuia na sikuthubutu kuzungumza mawazo yangu mwenyewe.
7 Yo me decía: Los días han de hablar, y en los muchos años se dará a conocer la sabiduría.
Nilisema, “Urefu wa siku utazungumza; na wingi wa miaka utatufundisha hekima.
8 Pero hay espíritu que reside en el hombre; es el soplo del Todopoderoso el que les da la inteligencia.
Lakini kuna roho ndani ya mtu; pumzi ya Mwenye nguvu humpa yeye ufahamu.
9 No es lo mismo ser viejo que sabio, no son (siempre) los ancianos los que entienden de justicia.
Si tu watu wakubwa ndio wenye hekima, wala watu wazee pekee ambao hufahamu haki.
10 Por eso dije: Escuchadme; quiero también yo manifestar mi parecer.
Hivyo basi nakwambia wewe, “Nisikilizeni mimi; Nitakwambia pia uelewa wangu.'
11 He aquí que he esperado mientras hablabais, di oídos a vuestros razonamientos hasta el fin de vuestra disputa.
Tazama, niliyasubiria maneno yenu; nilisikiliza hoja zenu wakati mlipokuwa mnafikiri juu ya kile cha kusema.
12 Sí, os he prestado atención, más ninguno ha convencido a Job; ninguno de vosotros sabe responder a sus palabras.
Hakika, niliwajali sana ninyi, lakini, tazama, hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kumshawishi Ayubu wala ambaye aliweza kumjibu maneno yake.
13 No digáis, pues: «Hemos hallado la sabiduría; es Dios quien le castiga, y no hombre alguno.»
Iweni waangalifu msije mkasema, 'Tumepata hekima!' Mungu atakuwa amemshinda Ayubu; mtu wa kawaida hawezi akafanya hivyo.
14 No contra mí ha dirigido él sus palabras; y yo no voy a contestarle con vuestros argumentos.
Kwa kuwa Ayubu hajasema mojamoja maneno yake juu yangu, basi sitamjibu kwa maneno yenu.
15 Desconcertados ya no responden nada, faltándoles otras palabras.
Hawa watu watatu wamep igwa bumbuwazi; hawawezi kuendelea kumjibu Ayubu; hawana neno zaidi la kusema.
16 He esperado hasta que se callasen, hasta que quedasen atascados sin poder contestar.
Je ninapaswa kusubiria kwasababu hawazungumzi, kwa kuwa wamesimama pale kimya na wala hawajibu zaidi?
17 Comenzaré yo a hablar, manifestaré por mi parte mi saber.
La, nitajibu pia upande wangu; Nitawaambia pia ufahamu wangu.
18 Pues lleno estoy de palabras, me aprieta el espíritu en mi interior.
Kwa kuwa nimejawa na maneno mengi, roho ndani yangu inanisukuma.
19 Mi pecho es como vino encerrado, cual odre nuevo pronto a reventar.
Tazama, kifua changu ni kama divai yenye chachu ambayo haina tundu; kama viriba vipya, kiko tayari kupasuka.
20 Hablaré para desahogarme; abriré mis labios y responderé.
Nitazungumza ili kwamba niweze kuburudishwa; nitafungua kimya changu na kusema.
21 No haré acepción de personas, no adularé a ningún mortal.
Sitaonesha upendeleo; wala sitatoa sifa za majina kwa mtu yeyote.
22 Pues no sé adular; (si lo hiciera), dentro de poco me llevaría mi Creador.”
Kwa kuwa sijui namna ya kutoa sifa; kama nitafanya hivyo, Muumba wangu atanikatilia mimi mbali.

< Job 32 >