< Job 24 >

1 “¿Por qué el Todopoderoso no fija tiempos (para el juicio)? ¿y por qué los que le conocen no saben el día fijado por Él?
Kwa nini nyakati za kuwahukumu waovu hazikuwekwa na Mwenyezi? Kwa nini siyo wale waliowaaminifu kwa Mungu huziona siku za hukumu zikija?
2 Hay quienes remueven mojones, roban rebaños y los apacientan;
Kuna waovu waondoao alama za mipaka; kuna waovu walichukua kundi kwa nguvu na kulifanya lao.
3 se llevan el asno de los huérfanos, toman en prenda el buey de la viuda;
Wanawadhurumu wanyonge punda wao; wanachukua ng'ombe wa mjane kuwa dhamana.
4 no dejan pasar a los pobres por el camino, y todos los humildes del país se esconden.
Wanawaondoa wahitaji katika njia zao kwa lazima; masikini wa dunia yote wanajificha kutoka kwao.
5 Mira cómo estos salen a su trabajo como los asnos monteses del desierto, buscando una presa hasta la tarde, sin hallar alimento para sus hijos.
Tazama, masikini hawa huenda kufanya kazi kama punda-mwitu mwituni, akitafuta chakula kwa uangalifu; pengine Araba itawapatia chakula kwa ajili ya watoto wao.
6 En el campo cortan el trigo (ajeno), y vendimian la viña del inicuo.
Masikini huvuna katika mashamba ya wengine usiku; wanakusanya zabibu kidogo kutokana na mapato ya waovu.
7 Pasan la noche desnudos, por falta de ropa, no tienen abrigo contra el frío.
Wana lala bila kujifunika wakati wa usiku; hawana cha kujifunika wakati wa baridi.
8 Mojados con las lluvias de las montañas se acurrucan contra las peñas, porque no tienen donde abrigarse.
Wanalowanishwa na mvua ya milimani; wanalala pembeni mwa miamba mikubwa kwani hawana makao.
9 (Y hay opresores que) arrancan al huérfano del pecho, y toman en prenda la ropa de los pobres,
Kuna waovu wanaowapokonya yatima katika kifua cha mama zao, na waovu wawachukuao watoto kama dhamana kutoka kwa masikini.
10 que andan desnudos sin vestidos, cargan hambrientos con las gavillas;
Lakini masikini wanatembea uchi; wajapokaa na njaa, wanabebea wengine chakula.
11 exprimen el aceite entre sus muros, y sedientos pisan sus lagares.
Masikini wanazalisha vinono ndani ya nyumba za waovu; wanakanyaga mashinikizo ya waovu, lakini wanakiu.
12 Desde la ciudad se oyen gemidos y clama el alma de los muertos; pero Dios no atiende su oración.
Watu wananung'unika mjini; waliojeruhiwa wanaomboleza, lakini Mungu hasikilizi maombi yao.
13 Y hay quienes aborrecen la luz; no conocen sus caminos, ni quieren atenerse a sus senderos.
Baadhi ya waovu hawa wanaiasi nuru; hawafahamu njia zake, wala kukaa katika njia zake.
14 Al alba se levanta el homicida para matar al desvalido y al pobre, y en la oscuridad sale como ladrón.
Muaji huinuka na nuru; huuwa masikini na waitaji; ni kama mwizi wakati wa usiku.
15 Aguarda la noche el ojo del adúltero, diciendo: «No me verá ojo alguno» y se emboza la cara.
Pia, mzinifu hungoja wakati wa usiku; husema, 'Hakuna anionaye.' Hujibadilisha.
16 Otros de noche fuerzan las casas, y de día se esconden, pues no quieren ver la luz.
Waovu huingia katika nyumba gizani, lakini hujifungia wakati wa mchana; hawajari nuru.
17 Para todos ellos el alba es sombra de muerte; más los terrores de la noche les son familiares;
Kwa kuwa asubuhi kwao wote ni kama giza totoro; wanaamani na vitisho vya giza totoro.
18 (huyen) veloces sobre la superficie de las aguas. ¡Maldita su prole sobre la tierra! ¡No ande por el camino de sus viñas!
Wanapotea polepole, lakini, kama povu juu ya maji; shamba lao limelaaniwa; hakuna anayekwenda kufanya kazi katika mashamba yao ya mizabibu.
19 Como la sequía y el calor absorben las aguas de la nieve, así (engulle) el scheol al pecador. (Sheol h7585)
Kiangazi na joto huondoa barafu; ndivyo kuzimu pia kunavyowaaribu waliotenda dhambi. (Sheol h7585)
20 Se olvida de él el seno materno, gusanos le comen como dulce manjar, no quedará memoria de su nombre. Como árbol será deshecha la maldad.
Mama yake atamsahau; polepole funza watamuuma; hatakumbukwa tena; kwa hiyo, waovu watavunjika kama mti.
21 Porque alimentaba a la estéril, que no tenía hijos, y no hacía bien a la viuda.
Mwovu anamrarua mgumba; hawatendi jema lolote kwa mjane.
22 Pero (Dios) con su fuerza derriba a los poderosos; se levanta, y ninguno está seguro de su vida.
Bado Mungu huwaondoa wenye nguvu kwa nguvu zake; huinuka na kuwadhoofisha.
23 Los deja vivir en seguridad y confianza, pero sus ojos velan sobre los caminos de ellos.
Mungu huwaacha wajione wako salama, na wanalifurahia hilo, lakini anayaangalia maisha yao.
24 Se ven ensalzados por un poco, y luego desaparecen, son derribados y cosechados como todos los hombres; son segados como espigas del trigal.
Watu hawa wanatukuzwa; bado, kitambo tu, watapotea; hakika, watashushwa; watakusanywa kama wengine wote; wataondolewa kama sehemu ya juu ya masikio ya nafaka.
25 Si no es así, ¿quién me desmentirá y declarará nula mi palabra?”
Ikiwa sivyo, nani atanithibitisha kuwa mwongo; atakaye fanya maneno yangu kuwa si kitu?”

< Job 24 >