< 1 Corintios 16 >
1 En cuanto a la colecta para los santos, según he ordenado a las Iglesias de Galacia, haced también vosotros.
Sasa kuhusu michango kwa ajili ya waumini, kama nilivyo elekeza makanisa ya Galatia, vivyo hivyo mwapaswa kufanya.
2 El primer día de la semana, cada uno de vosotros ponga aparte para sí lo que sea de su agrado, reservándolo, no sea que cuando llegue yo, se hagan entonces las colectas.
Katika siku ya kwanza ya wiki, kila mmoja wenu aweke kitu fulani kando na kukihifadhi, kama muwezavyo. Fanyeni hivyo ili kwamba kusiwe na michango wakati nikija.
3 Y cuando yo haya llegado, a aquellos que vosotros tuviereis a bien, los enviaré con cartas, para que lleven vuestro don a Jerusalén;
Na nitakapofika, yeyote mtakayemchagua, nitamtuma pamoja na barua kutoa sadaka yenu huko Yerusalem.
4 y si conviene que vaya también yo, irán conmigo.
Na kama ni sahihi kwa mimi kwenda pia, watakwenda pamoja nami.
5 Iré a veros después de recorrer la Macedonia; pues por Macedonia tengo que pasar.
Lakini nitakuja kwenu, wakati ninapitia Makedonia. Kwa kuwa nitapitia Makedonia.
6 Y puede ser que me detenga entre vosotros y aun pase el invierno; para que me despidáis a dondequiera que vaya.
Labda naweza kukaa nanyi au hata kumaliza majira ya baridi, ili kwamba muweze kunisaidia katika safari yangu, popote niendako.
7 Porque esta vez no quiero veros de paso, y espero permanecer algún tiempo entre vosotros, si el Señor lo permite.
Kwa kuwa sitarajii kuwaona sasa kwa muda mfupi. Kwani ninatumaini kukaa nanyi kwa muda fulani, kama Bwana ataniruhusu.
8 Me quedaré en Éfeso hasta Pentecostés;
Lakini nitakaa Efeso mpaka Pentekoste,
9 porque se me ha abierto una puerta grande y eficaz, y los adversarios son muchos.
kwa kuwa mlango mpana umefunguliwa kwa ajili yangu, na kuna maadui wengi wanipingao.
10 Si Timoteo llega, mirad que esté entre vosotros sin timidez, ya que él hace la obra del Señor lo mismo que yo.
Sasa wakati Timotheo akija, muoneni kwamba yuko na ninyi pasipo kuogopa, anafanya kazi ya Bwana, kama ninavyofanya.
11 Que nadie, pues, le menosprecie; despedidle en paz para que venga a mí, porque le estoy esperando con los hermanos.
Mtu yeyote asimdharau. Mumsaidie katika njia yake kwa amani, ili kwamba aweze kuja kwangu. Kwa kuwa ninamtarajia aje pamoja na ndugu.
12 En cuanto al hermano Apolo, mucho le encarecí que fuese a vosotros con los hermanos, mas no tuvo voluntad alguna de ir ahora; irá cuando tenga oportunidad.
Sasa kuhusiana na ndugu yetu Apolo. Nilimtia moyo sana kuwatembelea ninyi pamoja na ndugu. Lakini aliamua kutokuja kwa sasa. Hata hivyo, atakuja wakati ana nafasi.
13 Velad; estad firmes en la fe; portaos varonilmente; confortaos.
Muwe macho, simameni imara, mtende kama wanaume, muwe na nguvu.
14 Todas vuestras cosas se hagan con amor.
Basi yote myafanyayo yafanyike katika upendo.
15 Os exhorto, hermanos —porque conocéis la casa de Estéfanas, que es primicias de Acaya y que se han consagrado al servicio de los santos—,
Mnaijua kaya ya Stefana. Mnajua kwamba walikuwa waamini wa kwanza huko Akaya, na kwamba walijiweka wenyewe kwenye huduma ya waumini. Na sasa nawasihi, kaka na dada zangu,
16 que también vosotros os pongáis a disposición de ellos y de todo el que colabore y se afane.
kuweni wanyenyekevu kwa watu kama hao, na kwa kila mtu anayesaidia katika kazi na watenda kazi pamoja nasi.
17 Me regocijo de la llegada de Estéfanas, Fortunato y Acaico; porque ellos han suplido vuestra falta,
Na ninafurahi kwa ujio wa Stefana, Fotunato, na Akiko. Wamesimama mahali ambapo ninyi mgepaswa kuwa.
18 recreando mi espíritu y el vuestro. Estimádselo, pues, a hombres como ellos.
Kwa kuwa wameifurahisha roho yangu na yenu. Kwa hiyo sasa, watambueni watu kama hawa.
19 Os saludan las Iglesias de Asia. Os mandan muchos saludos en el Señor, Aquila y Prisca, junto con la Iglesia que está en su casa.
Makanisa ya Asia wametuma salamu kwenu. Akila na Priska wanawasalimu katika Bwana, pamoja na kanisa lililoko nyumbani kwao.
20 Os saludan todos los hermanos. Saludaos unos a otros en ósculo santo.
Kaka na dada zangu wote wanawasalimu. Salimianeni kwa busu takatifu.
21 Va la salutación de mi propio puño: Pablo.
Mimi, Paulo, naandika hivi kwa mkono wangu.
22 Si alguno no ama al Señor, sea anatema. ¡Maran-atha!
Kama yeyote hampendi Bwana, basi laana iwe juu yake. Bwana wetu, njoo!
23 La gracia del Señor Jesús sea con vosotros.
Neema ya Bwana Yesu iwe nanyi.
24 Mi amor está con todos vosotros, en Cristo Jesús.
Upendo wangu uwe pamoja nanyi katika Kristo Yesu.