< 1 Crónicas 3 >
1 He aquí los hijos de David que le nacieron en Hebrón: El primogénito Amnón, de Ahinoam de Jesreel; el segundo, Daniel, de Abigail de Carmel;
Hawa ndio waliokuwa wana wa Daudi waliozaliwa huko Hebroni: Mzaliwa wa kwanza alikuwa Amnoni ambaye mama yake aliitwa Ahinoamu wa Yezreeli; wa pili, Danieli ambaye mama yake alikuwa Abigaili wa Karmeli;
2 el tercero, Absalón, hijo de Maacá, hija de Talmai, rey de Gesur; el cuarto, Adonías, hijo de Haggit;
wa tatu alikuwa Absalomu, ambaye mama yake alikuwa Maaka, binti Talmai mfalme wa Geshuri; wa nne, Adoniya, ambaye mama yake alikuwa Hagithi;
3 el quinto, Safarías, de Abital; el sexto, Itream, de su mujer Eglá.
wa tano alikuwa Shefatia ambaye mama yake alikuwa Abitali; wa sita alikuwa Ithreamu, aliyezaliwa na mke wake Egla.
4 Estos seis le nacieron en Hebrón, donde reinó siete años y seis meses. Después reinó treinta y tres años en Jerusalén.
Hawa sita walizaliwa huko Hebroni ambako Daudi alitawala kwa miaka saba na miezi sita. Daudi alitawala Yerusalemu kwa miaka thelathini na mitatu,
5 He aquí los que le nacieron en Jerusalén: Sima, Sobab, Natán y Salomón, cuatro, de Betsabee, hija de Amiel;
nao hawa ndio watoto wa Daudi waliozaliwa huko Yerusalemu: mkewe Bathsheba, binti Amieli, alimzalia Shamua, Shobabu, Nathani na Solomoni.
6 además Ibhar, Elisamá, Elifálet,
Pia kulikuwa na wana wengine: Ibihari, Elishua, Elifeleti,
8 Elisamá, Eliadá y Elifélet, nueve.
Elishama, Eliada na Elifeleti; wote walikuwa tisa.
9 Estos son todos los hijos de David, sin contar los hijos de las mujeres secundarias. Tamar era hermana de ellos.
Hawa wote walikuwa wana wa Daudi, mbali na wale wana waliozaliwa na masuria. Naye Tamari alikuwa dada yao.
10 Hijo de Salomón: Roboam; Abías, su hijo; Asá, su hijo; Josafat, su hijo;
Mwana wa Solomoni alikuwa Rehoboamu, mwanawe huyo alikuwa Abiya, mwanawe huyo alikuwa Yehoshafati, mwanawe huyo alikuwa Asa,
11 Joram, su hijo; Ococías, su hijo; Joás, su hijo;
mwanawe huyo alikuwa Yehoramu, mwanawe huyo alikuwa Ahazia, mwanawe huyo alikuwa Yoashi,
12 Amasías, su hijo; Azarías, su hijo; Joatam, su hijo;
mwanawe huyo alikuwa Amazia, mwanawe huyo alikuwa Azaria, mwanawe huyo alikuwa Yothamu,
13 Acaz, su hijo; Ezequías, su hijo; Manasés, su hijo;
mwanawe huyo alikuwa Ahazi, mwanawe huyo alikuwa Hezekia, mwanawe huyo alikuwa Manase,
14 Amón, su hijo; Josías, su hijo.
mwanawe huyo alikuwa Amoni na mwanawe huyo alikuwa Yosia.
15 Hijos de Josías: El primogénito, Johanán; el segundo, Joakim; el tercero, Sedecías; el cuarto, Sellum.
Wana wa Yosia walikuwa: Yohanani mzaliwa wake wa kwanza, Yehoyakimu mwanawe wa pili, wa tatu Sedekia, wa nne Shalumu.
16 Hijos de Joakim: Jeconías, su hijo; Sedecías, su hijo.
Walioingia mahali pa Yehoyakimu kama wafalme ni: Yekonia mwanawe, na Sedekia.
17 Hijos de Jeconías el cautivo: Salatiel, su hijo;
Hawa ndio waliokuwa wazao wa Yekonia aliyekuwa mateka: Shealtieli mwanawe,
18 Malquiram, Fadaías, Senasar, Jecamías, Hosamá y Nadabías.
Malkiramu, Pedaya, Shenasari, Yekamia, Hoshama na Nedabia.
19 Hijos de Fadaías: Zorobabel y Semeí. Hijos de Zorobabel: Mesullam, Hananías y Salomit, su hermana,
Wana wa Pedaya walikuwa: Zerubabeli na Shimei. Wana wa Zerubabeli walikuwa: Meshulamu na Hanania. Shelomithi alikuwa dada yao.
20 Hasubá, Ohel, Baraquías, Hasadías y Jusabhésed, cinco.
Pia walikuwepo wengine watano: Hashuba, Oheli, Berekia, Hasadia na Yushab-Hesedi.
21 Hijos de Hananías: Faldas y Jesaías; los hijos de Refaías, los hijos de Arnán, los hijos de Abdías, los hijos de Sequenías.
Wazao wa Hanania walikuwa: Pelatia na Yeshaya, na wana wa Refaya, na wana wa Arnani, na wana wa Obadia, na wana wa Shekania.
22 Hijo de Sequenías: Semeías. Hijos de Semeías: Hatús, Igal, Barias, Nearías y Safat, seis.
Wazao wa Shekania: Shemaya na wanawe: Hatushi, Igali, Baria, Nearia na Shafati; jumla yao walikuwa sita.
23 Hijos de Nearías: Elioenai, Ezequías y Ezricam, tres.
Wana wa Nearia walikuwa: Elioenai, Hizkia na Azrikamu; jumla yao watatu.
24 Hijos de Elioenai: Hodaías, Eliasib, Feleías, Acub, Johanán, Dalaías y Ananí, siete.
Wana wa Elioenai walikuwa: Hodavia, Eliashibu, Pelaya, Akubu, Yohanani, Delaya na Anani; jumla yao wote saba.