< Incito 16 >

1 Paulo mpwalashika ku Debe, walaya ne ku Lusitala, uko kwalikuba shikwiya naumbi, lina lyakendi Timoti. Banyina balikuba Bayuda bashoma Lesa, baishi balikuba bagiliki.
Paulo akafika Derbe na kisha Listra, ambako kulikuwa na mwanafunzi mmoja jina lake Timotheo, ambaye mama yake alikuwa Myahudi aliyeamini, lakini baba yake alikuwa Myunani.
2 Banse baku Lusitala ne baku Ikoniya balikumulumba Timoti.
Alikuwa amesifiwa sana na wale ndugu waliokuwa wameamini huko Listra na Ikonio
3 Neco Paulo walikuyanda kumumanta kwambeti bendenga pamo. Nomba Bayuda bonse balikwikala uko balikwinshibeti baishi Timoti ni Bagiliki, Paulo walamupalula Timoti.
Paulo alitaka Timotheo afuatane naye, hivyo akamchukua na kumtahiri kwa sababu ya Wayahudi waliokuwa wanaishi eneo lile kwa maana wote walimjua baba yake ni Myunani.
4 Mpobalikuya kupita mu minshi balikuya kubenshibisha bashoma kwambeti, bakonkele milawo yalabikwa ne batumwa, pamo ne bamakulene ba mubungano wa mu Yelusalemu.
Walipokuwa wakienda mji kwa mji, wakawa wanawapa maamuzi yaliyotolewa na mitume na wazee huko Yerusalemu ili wayafuate.
5 Neco mibungano ya bashoma yalaba ne lushomo lwayuma, busuba ne busuba bantu balatatika kufulilako.
Hivyo makanisa yakawa imara katika imani na kuongezeka kiidadi kila siku.
6 Paulo ne banendi balapitilila cimpansha ca Fuligiya ne Galatiya, pakwinga Mushimu Uswepa walabakanisha kukambauka maswi a Lesa mucimpansha ca Asiya.
Paulo pamoja na wenzake wakasafiri sehemu za Frigia na Galatia, kwa kuwa Roho Mtakatifu hakuwaruhusu kulihubiri neno huko Asia.
7 Mpobalashika kunyinsa yacishi ca Misiya, balayanda kwingila mucimpansha ca Bituniya, nsombi Mushimu wa Yesu walabakanisha.
Walipofika mpaka wa Misia, wakajaribu kuingia Bithinia lakini Roho wa Yesu hakuwaruhusu.
8 Neco balapitilila Misiya ne kuya kushika ku Tulowa.
Kwa hiyo wakapita Misia, wakafika Troa.
9 Cindi ca mashiku Paulo walabona cimbonimboni camuntu waku Makedoniya, kali wemana ne kusengeti, “Kamutampukilani ku Makedoniya kuno, mwise mutunyamfwe.”
Wakati wa usiku Paulo akaona maono, mtu wa Makedonia amesimama akimsihi, “Vuka uje huku Makedonia utusaidie.”
10 Pacindi copeleco Paulo mpwalabona muntu mucimbonimboni, twalalibambila bulwendo bwakuya ku Makedoniya, pakwinga twalenshibeti Lesa layandeti twenga akukambauka Mulumbe Waina ku bantu baku Makedoniya.
Baada ya Paulo kuona maono haya, tulijiandaa kwa haraka kuondoka kwenda Makedonia tukiwa tumesadiki kuwa Mungu alikuwa ametuita kuhubiri habari njema huko.
11 Kufuma ku Tulowa twalenda mubwato kululama ku nsumbu ya Samotilase, mpobwalaca mumene twalapitilila mpaka twalashika ku Niyapoli.
Tukasafiri kwa njia ya bahari kutoka Troa na kwenda moja kwa moja hadi Samothrake, kesho yake tukafika Neapoli.
12 Kufuma ku Niyapoli, twalaya ku Filipi, munshi unene wa mucibela ca Makedoniya, walikwendeleshewa ne mfulumende ya Ciloma. Twalekala masuba angi mu munshi uwu.
Kutoka huko tukasafiri hadi Filipi, mji mkuu wa jimbo hilo la Makedonia, uliokuwa koloni ya Warumi. Nasi tukakaa huko siku kadhaa.
13 Pabusuba bwa Sabata twalapulilako kunsa kwamunshi ne kuya ku mulonga uko nkotwali kuyeyeti kuli musena mpobakute kupailila Bayuda. Twalekala panshi katubandika ne batukashi balikuba babungana kopeloko.
Siku ya Sabato tukaenda nje ya lango la mji kando ya mto, mahali ambapo tulitarajia tungepata mahali pa kufanyia maombi. Tukaketi, tukaanza kuongea na baadhi ya wanawake waliokuwa wamekusanyika huko.
14 Pakati pabo palikuba mutukashi naumbi, lina lyakendi Lidiya. Kucomwabo niku Tiyatila, ncito yakendi yalikuba yakulisha bikwisa byafubeluka. Walikuba mutukashi wali kupaila Lesa, neco Lesa walamucalula moyo wakendi kwambeti anyumfwishishe ne kushoma ncalikwamba Paulo.
Mmoja wa wale wanawake waliotusikiliza aliitwa Lidia, mfanyabiashara wa nguo za zambarau, mwenyeji wa mji wa Thiatira, aliyekuwa mcha Mungu. Bwana akaufungua moyo wake akaupokea ujumbe wa Paulo.
15 Lidiya ne bamung'anda yakendi mpobalabatishiwa, walatusengeti, “Mbuli ncemulabono kwambeti nkute lushomo muli Lesa, katuyani kung'anda kwakame muye mwikale nenjame,” Walatukakatisha neco twalaya.
Basi alipokwisha kubatizwa yeye na watu wa nyumba yake, alitukaribisha nyumbani kwake akisema, “Kama mmeona kweli mimi nimemwamini Bwana, karibuni mkae nyumbani mwangu.” Naye akatushawishi.
16 Cindi nacimbi mpotwalaya kumusena nkobalikupailila, twalakumanyako mutukashi musebenshi walikuba wekatwa ne mushimu waipa wakulaluka. Kufumina muncito yakendi ya kulaluka, baleli bakendi balikucanamo mali angi.
Siku moja, tulipokuwa tukienda mahali pa kusali, tulikutana na mtumwa mmoja wa kike ambaye alikuwa na pepo wa uaguzi. Naye alikuwa amewapa mabwana zake mapato makubwa ya fedha kwa ubashiri.
17 Uyu mutukashi walikukonkela Paulo pamo ne njafwe, kabilikisheti, “Bantu aba ni basebenshi ba Lesa Mukulene Wapita Byonse! Balamukambaukilinga nshila yalupulusho.”
Huyu msichana alikuwa akimfuata Paulo na sisi akipiga kelele, “Watu hawa ni watumishi wa Mungu Aliye Juu Sana, wao wanawatangazieni njia ya wokovu.”
18 Uyu mutukashi walikwinseco kwa masuba angi. Neco Paulo calamucima, walacebuka ne kuwambila mushimu waipa, “Mulina lya Yesu Klistu, ndakwambilinga omushimu waipa, fuma mu muntuyu.” Pacindi copeleco mushimu waipa walapulamo.
Akaendelea kufanya hivi kwa siku nyingi, lakini Paulo akiwa ameudhika sana, akageuka na kumwambia yule pepo mchafu, “Ninakuamuru katika jina la Yesu Kristo, umtoke!” Yule pepo mchafu akamtoka saa ile ile.
19 Baleli bamutukashuyu, mpobalabona kwambeti nteti abacaninenga mali, balekata Paulo ne Sailasi, ne kubakwekweshela kumusena wa makwebo, kubomboloshi.
Basi mabwana wa yule mtumwa wa kike walipoona kuwa tumaini lao la kuendelea kujipatia fedha limetoweka, wakawakamata Paulo na Sila wakawaburuta mpaka sokoni mbele ya viongozi wa mji.
20 Mpobalashika nabo kubeshi kombolosha, balambeti, “Aba bantu ni Bayuda, balapenshe bantu mu munshi mwetu muno.
Baada ya kuwafikisha mbele ya mahakimu wakawashtaki wakisema, “Hawa watu wanaleta ghasia katika mji wetu, nao ni Wayahudi.
21 Baleyishinga miyambo byabula kusuminishiwa, kayi nkatwelela kwitambula nambi kwikonkela afwe Baloma.”
Wanafundisha desturi ambazo sisi raiya wa Kirumi hatuwezi kuzikubali au kuzitimiza.”
22 Likoto lyalikubapo lyalatatika kuma Paulo ne Sailasi, beshikombolosha milandu nabo ebalapesheti bantu batwamune byakufwala bya Paulo ne Sailasi ne kubambileti, babakwapule bikoti.
Umati wa watu waliokuwepo wakajiunga katika kuwashambulia Paulo na Sila na wale mahakimu wakaamuru wavuliwe nguo zao na wachapwe viboko.
23 Mpobalabakwapula bikoti tunkanda twingi, balabawala mujele ne kwambila mulonda wajele kwambeti abalame cena.
Baada ya kuwachapa sana, wakawatupa gerezani na kumwagiza mkuu wa gereza awalinde kikamilifu.
24 Neco pacebo camaswi awa, mulonda wajele walabacalila mucipinda camukati mujele, ne kubapinka myendo yabo pakati pa minkulu ibili.
Kufuata maelekezo haya, yule mkuu wa gereza akawaweka katika chumba cha ndani sana mle gerezani, na akawafunga miguu yao kwa minyororo.
25 Pakati pa mashiku Paulo ne Sailasi balikupaila, ne kwimbila nyimbo shakutembaula Lesa, bakaili banabo balikunyumfwako.
Ilipokaribia usiku wa manane, Paulo na Sila walikuwa wakiomba na kuimba nyimbo za kumsifu Mungu, nao wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza.
26 Mwakutengashila kwalaba mukunkumo wangofu, cakwinseti lulindi lwa ng'anda ya jele yonse lwalatenkana, bisasa byonse byalashonkauka, ncetani nshebalikuba basunga kaili uliyense shalalaka panshi mbwee.
Ghafula pakatokea tetemeko kubwa la ardhi, hata msingi wa gereza ukatikisika. Mara milango ya gereza ikafunguka na ile minyororo iliyowafunga kila mmoja ikafunguka.
27 Mulonda wajele usa mpwalapashamuka, ne kubona bisasa bya jele byonse byashonkauka, walayeyeti bakaili bonse balafwambamo. Walapulisha cibeshi kwambeti alishine.
Yule mkuu wa gereza alipoamka na kuona milango ya gereza iko wazi, akachomoa upanga wake akataka kujiua, akidhani ya kuwa wafungwa wote wametoroka.
28 Paulo walabilikisheti, “Kotalishina! Twense motuli muno!”
Lakini Paulo akapiga kelele kwa sauti kubwa, akasema, “Usijidhuru kwa maana sisi sote tuko hapa!”
29 Mulonda usa walambila naumbi kwambeti alete lampi, walafwambila mukati katutuma njenjenje, ne kuya kuliwala pamyendo ya Paulo ne Sailasi.
Yule askari wa gereza akaagiza taa ziletwe, akaingia ndani ya kile chumba cha gereza, akapiga magoti akitetemeka mbele ya Paulo na Sila.
30 Walabapulisha kunsa ne kubepusheti, “Nkambo! Nicani ncetinyinse kwambeti mpuluke?”
Kisha akawaleta nje akisema, “Bwana zangu, nifanye nini nipate kuokoka?”
31 Balo balamukumbuleti, “Koshoma muli Mwami Yesu, obe ne ba mung'anda yakobe nimukapuluke.”
Wakamjibu, “Mwamini Bwana Yesu Kristo, nawe utaokoka, pamoja na watu wa nyumbani mwako.”
32 Balamukambaukila maswi a Mwami, pamo ne ba mung'anda yakendi.
Wakamwambia neno la Bwana yeye pamoja na wote waliokuwako nyumbani mwake.
33 Nekukabeti calikuba cindi camashiku, walabamanta ne kuya kubasuka bilonda. Popelapo mulonda usa ne ba mung'anda yakendi balabatishiwa.
Wakati ule ule, yule mkuu wa gereza akawachukua, akawaosha majeraha yao, kisha akabatizwa yeye pamoja na wote waliokuwa nyumbani mwake bila kuchelewa.
34 Panyuma pakendi, walaya nabo kung'anda yakendi, kuya kubapa cakulya. Mulonda uyu ne bonse ba mung'anda yakendi balakondwa cebo ca kushoma Lesa.
Akawapandisha nyumbani mwake akawaandalia chakula, yeye pamoja na nyumba yake yote wakafurahi sana kwa kuwa sasa walikuwa wamemwamini Mungu.
35 Mpobwalaca, beshikombolosha balatuma bashilikali kuya kumwambila usa mulonda wajele kwambeti, “Basungulule abo bantu benga.”
Kulipopambazuka wale mahakimu wakawatuma maafisa wao kwa mkuu wa gereza wakiwa na agizo linalosema, “Wafungue wale watu, waache waende zao.”
36 Usa mulonda wajele walamwambila Paulo kwambeti, “Beshikombolosha balatumu maswi akwambeti tumusungulule. Neco, kamupulani, kamuyani mulumuno.”
Mkuu wa gereza akamwambia Paulo “Mahakimu wameagiza niwaache huru, kwa hiyo tokeni na mwende zenu kwa amani.”
37 Paulo walabambila bashilikali abo, kwambeti “Batukwapula bikoti bantu bangi kabebelela, kwakubula kutombolosha nanshi, kakuli afwe tobene Loma, kayi batuwala mujele. Inga lino balayandanga kutupulisheconi kampunampuna, nkacelela kubeco sobwe! Kamuyani mubambile balamutumu bese batupulishe bene.”
Lakini Paulo akawaambia wale maafisa, “Wametupiga hadharani bila kutufanyia mashtaka na kutuhoji, nao wakatutupa gerezani, hata ingawa sisi ni raiya wa Rumi. Nao sasa wanataka kututoa gerezani kwa siri? Hapana! Wao na waje wenyewe watutoe humu gerezani.”
38 Basa bashilikali balaya kubambila beshikombolosha maswi awa. Mpobalanyumfweti Paulo ne Sailasi ni bene Loma, balatina.
Wale maafisa wakarudi na kuwaambia wale mahakimu maneno haya, wakaogopa sana walipofahamu kuwa Paulo na Sila ni raiya wa Rumi.
39 Neco beshikombolosha balesa kulilekelela kuli Paulo ne Sailasi. Panyuma pakendi balabapulisha mujele, ne kubasengeti bafumemo mu munshi uwo.
Kwa hiyo wakaja wakawaomba msamaha, wakawatoa gerezani, wakawaomba waondoke katika ule mji.
40 Paulo ne Sailasi mpobalapula mujele, balabwelela ku ng'anda kwa Lidiya, nkobalakabonana ne banabo. Panyuma pakubayuminisha, balafuma mu mushi.
Baada ya Paulo na Sila kutoka gerezani walikwenda nyumbani kwa Lidia, ambapo walikutana na wale ndugu walioamini, wakawatia moyo, ndipo wakaondoka.

< Incito 16 >