< Rimljanom 3 >

1 Kaj ima torej Jud obilneje? ali kaj hasni obreza?
Kisha ni faida gani aliyo nayo Myahudi? Na faida ya tohara ni nini?
2 Mnogo, vsakakor: kajti prvič zaupali mu so se izreki Božji.
Ni vyema sana kwa kila njia. Awali ya yote, Wayahudi walikabidhiwa ufunuo kutoka kwa Mungu.
3 Pa kaj, če niso verovali nekteri? bo li njih nevera vero Božjo odpravila?
Lakini, itakuwaje iwapo baadhi ya Wayahudi hawakuwa na imani? Je, kutokuamini kwao kutafanya uaminifu wa Mungu kuwa batili?
4 Bog ne daj! nego Bog naj bo resničen, a vsak človek lažnjivec, kakor je pisano: "Da se opravičiš v svojih besedah in zmagaš, kedar te bodo sodili.",
La hasha. Badala yake, acha Mungu aonekane kuwa kweli, hata kama kila mtu ni mwongo. Kama ilivyokuwa imeandikwa, “Ya kwamba uweze kuonekana kuwa mwenye haki katika maneno yako, na uweze kushinda uingiapo katika hukumu.”
5 Če pa naša krivica Božjo pravico potrjuje, kaj porečemo? da je nepravičen Bog, kedar se jezi? Po človeku govorim.
Lakini ikiwa uovu wetu unaonesha haki ya Mungu, tuseme nini? Mungu si dhalimu atoapo ghadhabu yake, je yupo hivyo? Naongea kutokana na mantiki ya kibinadamu.
6 Bog ne daj! ker kako bo sodil Bog svet?
La hasha! Ni jinsi gani basi Mungu atauhukumu ulimwengu?
7 Kajti če se resnica Božja v mojej laži poobilša na njegovo slavo, za kaj bi bil še tudi jaz kakor grešnik sojen?
Lakini ikiwa kweli ya Mungu kupitia uongo wangu hutoa sifa tele kwa ajili yake, kwa nini ningali bado nahukumiwa kama mwenye dhambi?
8 In ne smemo li, (kakor kričé na nas in pravijo nekteri da mi govorimo), storiti hudo, da pride dobro? Teh le čaka pravična sodba.
Kwa nini tusiseme, kama tulivyosingiziwa na kama wengine wanavyothibitisha kwamba tunasema, “Tufanye uovu, ili mema yaje”? Hukumu juu yao ni ya haki.
9 Kaj torej? jeli smo bolji? nikakor: kajti prej smo dokazali, da so Judje in pa Grki vsi pod grehom.
Ni nini basi? Tunajitetea wenyewe? Hapana kabisa. Kwa kuwa sisi tayari tumewatuhumu Wayahudi na Wayunani wote pamoja, ya kuwa wapo chini ya dhambi.
10 Kakor je pisano: "Da ni pravičnega ne enega:
Hii ni kama ilivyoandikwa: “Hakuna mwenye haki, hata mmoja.
11 Ni ga, kteri bi bil razumen, ni ga, kteri bi iskal Boga.
Hakuna mtu ambaye anaelewa. Hakuna mtu ambaye anamtafuta Mungu.
12 Vsi so se uganili, ob enem so se izpridili; ni ga, kteri bi delal dobro, ni ga le enega ne."
Wote wamegeuka. Wao kwa pamoja wamekuwa hawana maana. Hakuna atendaye mema, la, hata mmoja.
13 "Grob odprt je njih grlo, s svojimi jeziki goljufno govoré: "kačji strup je pod njih ustnicami."
Makoo yao ni kaburi lililo wazi. Ndimi zao zimedanganya. Sumu ya nyoka ipo chini ya midomo yao.
14 "Njih usta so polna kletve in grenkobe."
Vinywa vyao vimejaa laana na uchungu.
15 "Hitre so njih noge, da kri prelijó."
Miguu yao ina mbio kumwaga damu.
16 "Potrtje in nadloga je na njih potih."
Uharibifu na mateso yapo katika njia zao.
17 "In poti mira niso spoznali."
Watu hawa hawajajua njia ya amani.
18 "Ni straha Božjega pred njih očmi."
Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yao.”
19 Vemo pa, da vse, kar postava govori, govori tem, kteri so v postavi, da se vsaka usta zamašé in kriv postane ves svet Bogu;
Sasa tunajua kwamba chochote sheria isemacho, husema na wale walio chini ya sheria. Hii ni ili kwamba kila kinywa kifungwe, na hivyo kwamba ulimwengu wote uweze kuwajibika kwa Mungu.
20 Kajti iz del postave se ne bo opravičilo nobeno meso pred njim, ker skozi postavo prihaja spoznanje greha.
Hii ni kwa sababu hakuna mwili utakaohesabiwa haki kwa matendo ya sheria mbele za macho yake. Kwa kuwa kupitia Sheria huja ufahamu wa dhambi.
21 Sedaj pa se je brez postave pravica Božja pokazala, spričevana od postave in prerokov.
Lakini sasa pasipo sheria, haki ya Mungu imejulikana. Ilishuhudiwa kwa sheria na Manabii,
22 A pravica Božja z vero Jezusa Kristusa v vse in na vse, kteri verujejo, ker ga ni razločka;
hiyo ni, haki ya Mungu kupitia imani katika Yesu Kristo kwa wale wote wanaoamini. Maana hakuna tofauti.
23 Kajti vsi so pregrešili ter jim manjka slave Božje,
Kwa kuwa wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.
24 In opravičujejo se daroma z njegovo milostjo po odkupljenji v Jezusu Kristusu,
Wamehesabiwa haki bure kwa neema yake kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu.
25 Kterega si je najprej odménil Bog za pomirjenje po veri v njegovej krvi, da pokaže svojo pravico z odpuščenjem prejšnjih grehov;
Kwa maana Mungu alimtoa Kristo Yesu awe upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake. Alimtoa Kristo kama ushahidi wa haki yake, kwa sababu ya kuziachilia dhambi zilizopita
26 V potrpljenji Božjem, da pokaže svojo pravico v sedanjem času, da je on pravičen in da opravičuje tega, kteri je iz vere Kristusove.
katika uvumilivu wake. Haya yote yalitokea ili kuonesha haki yake wakati huu wa sasa. Hii ilikuwa ili aweze kujithibitisha mwenyewe kuwa haki, na kuonesha kwamba humhesabia haki mtu yeyote kwa sababu ya imani katika Yesu.
27 Kje je torej hvala? Zavrgla se je. Po kakošnej postavi? jeli dél? ne, nego po postavi vere.
Kuwapi basi kujisifu? Kumetengwa. Kwa misingi ipi? Misingi ya matendo? Hapana, lakini kwa misingi ya imani.
28 Mislimo torej, da se z vero opravičuje človek, brez del postave.
Hivyo tunahitimisha kwamba mtu huhesabiwa haki kwa imani pasipo matendo ya sheria.
29 Jeli je Bog samo Judovski? jeli ni tudi poganski? Dà, tudi poganski.
Au Mungu ni Mungu wa Wayahudi tu? Je yeye si Mungu wa watu wa Mataifa pia? Ndiyo, wa mataifa pia.
30 Kajti eden je Bog, kteri bo opravičil obrezo iz vere in neobrezo po veri.
Ikiwa kwa kweli Mungu ni mmoja, atawahesabia haki walio wa tohara kwa imani, na wasiotahiriwa kwa njia ya imani.
31 Postavo torej odpravljamo z vero? Bog ne daj! nego postavo stavimo.
Je sisi twaibatilisha sheria kwa imani? La hasha! Kinyume cha hayo, sisi twaithibitisha sheria.

< Rimljanom 3 >