< Psalmi 140 >
1 Načelniku godbe, psalm Davidov. Reši me, Gospod, hudobnih ljudî; mož presilovitih brani me,
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, niokoe, kutoka kwa watu waovu; nilinde na watu wenye jeuri,
2 Kateri mislijo hudo v srci; vsak dan se shajajo – na vojsko.
ambao hupanga mipango mibaya mioyoni mwao, na kuchochea vita siku zote.
3 Brusijo jezik svoj, podoben kačjemu; strup gadji je pod njih ustnami.
Wao hufanya ndimi zao kali kama za nyoka, sumu ya nyoka iko midomoni mwao.
4 Reši me, Gospod, rok krivičnih, mož presilovitih brani me, ki mislijo izpodbiti mi noge.
Ee Bwana, niepushe na mikono ya waovu; nilinde na watu wenye jeuri wanaopanga kunikwaza miguu yangu.
5 Skrivali so mi prevzetniki zanko in vrvi; razgrinjali mi mrežo poleg pota.
Wenye kiburi wameficha mtego wa kuninasa, wametandaza kamba za wavu wao, wametega mitego kwenye njia yangu.
6 Rekel sem Gospodu; Bog mogočni si moj; čuj, Gospod, molitev mojih glas.
Ee Bwana, ninakuambia, “Wewe ni Mungu wangu.” Ee Bwana, usikie kilio changu na kunihurumia.
7 Gospod, Bog, moč blaginje moje; glavo si mojo pokril o boja času.
Ee Bwana Mwenyezi, Mwokozi wangu mwenye nguvu, unikingaye kichwa changu siku ya vita:
8 Ne dopústi, Gospod, kar želi krivični; pregrešne misli njegove ne pospešuj; povzdigovali bi se presilno.
Ee Bwana, usiwape waovu matakwa yao, usiache mipango yao ikafanikiwa, wasije wakajisifu.
9 Glave njih, ki me obdajajo, – ustnic njih nadloga naj jih pokrije.
Vichwa vya wanaonizunguka vifunikwe na shida zinazosababishwa na midomo yao.
10 Žarjavica pridi nadnje; v ogenj naj jih vrže, v jame, da ne vstanejo.
Makaa ya mawe ya moto na yawaangukie! Na watupwe motoni, katika mashimo ya matope, wasiinuke tena kamwe.
11 Mož prokleti ne utrdi se na zemlji; mož silovitosti, njega naj udari pogin.
Wasingiziaji wasifanikiwe katika nchi; maafa na yawawinde watu wenye jeuri.
12 Vem, da bode Gospod pravdo vodil siromaku, pravico potrebnim.
Najua kwamba Bwana huwapatia maskini haki, na kuitegemeza njia ya mhitaji.
13 Dà, pravični bodo slavili ime tvoje; pošteni sedeli pred tvojim obličjem.
Hakika wenye haki watalisifu jina lako, na waadilifu wataishi mbele zako.