< Luka 2 >

1 Zgodí se pa tiste dni, da izide povelje od cesarja Avgusta, naj se popiše ves svet.
Sasa katika siku hizo, ikatokea kwamba Kaisari Agusto alitoa agizo akielekeza kwamba ichukuliwe sensa ya watu wote wanaoishi duniani.
2 (To popisovanje prvo bilo je, ko je vladal v Siriji Cirenij.)
Hii ilikuwa ni sensa ya kwanza iliyofanyika wakati Krenio akiwa gavana wa Siria.
3 In šli so vsi, da se zapišejo, vsak v svoje mesto.
Hivyo kila mmoja akaenda mjini kwake kuandikishwa sensa.
4 Napoti se pa tudi Jožef iz Galileje, iz mesta Nazareta, v Judejo, v mesto Davidovo, ktero se imenuje Betlehem, (ker je bil iz hiše in rodovine Davidove, )
Naye Yusufu aliondoka pia katika mji wa Nazareti huko Galilaya na akasafiri Yudea katika mji wa Bethlehemu, ujulikanao kama mji wa Daudi, kwa sababu alitokea katika ukoo ya Daudi.
5 Da se zapiše z Marijo zaročeno mu ženo, ktera je bila noseča.
Alikwenda huko kujiandikisha pamoja na Mariamu, ambaye alikuwa amemposa na alikuwa akitazamia mtoto.
6 Zgodí se pa, ko sta bila tam, da se izpolnijo dnevi, da porodí.
Sasa ilitokea kwamba, wakiwa kule wakati wake wa kujifungua mtoto ukawadia.
7 In rodí sina svojega prvenca, in povije ga v plenice, in položi ga v jasli: ker jima ni bilo prostora v gostilnici.
Akajifungua mtoto wa kiume, mzaliwa wake wa kwanza, akamzungushia nguo mwilini kumkinga na baridi mtoto. Ndipo akamweka kwenye kihori cha kulishia wanyama, kwa sababu haikuwepo nafasi kwenye nyumba za wageni.
8 Bili so pa pastirji v tistem kraji, kteri so čuli in na ponočnih stražah bili pri čredi svojej.
Katika eneo hilo, walikuwapo wachungaji walioishi mashambani wakilinda makundi ya Kondoo wao usiku.
9 In glej, angelj Gospodov pristopi k njim, in slava Gospodova jih obsije; in uplašijo se z velikim strahom.
Ghafla, malaika wa Bwana akawatokea, na utukufu wa Bwana ukang'aa kuwazunguka, na wakawa na hofu sana.
10 Pa jim angelj reče: Ne bojte se! kajti glej, oznanjam vam veliko radost, ktera bo vsemu ljudstvu:
Ndipo malaika akwaambia, “Msiogope, kwasababu nawaletea habari njema ambayo italeta furaha kuu kwa watu wote.
11 Da vam se je rodil danes zveličar, kteri je Kristus Gospod, v mestu Davidovem.
Leo Mwokozi kazaliwa kwaajili yenu mjini mwa Daudi! Yeye ndiye Kristo Bwana!
12 In to vam bo znamenje: Našli boste dete povito, da leži v jaslih.
Hii ndiyo ishara ambayo mtapewa, mtamkuta mtoto amefungwa nguo na amelala kwenye hori la kulishia wanyama.”
13 In na hip se pokaže z angeljem množica nebeške vojske, kteri so Boga hvalili, govoreč:
Ghafla kukawa na jeshi kubwa la mbinguni likaungana na malaika huyo wakamsifu Mungu, wakisema,
14 Slava na višavah Bogu, in na zemlji mir; med ljudmi dobra volja.
“Utukufu kwa Mungu aliye juu sana, na amani iwe duniani kwa wote ambao anapendezwa nao.”
15 In zgodí se, ko odidejo angelji od njih na nebo, pa rekó pastirji med seboj: Pojdimo do Betlehema, in poglejmo to reč, ki se je zgodila, ki nam jo je povedal Gospod.
Ikawa kwamba malaika walipokwisha kuondoka kwenda mbinguni, wachungaji wakasemezena wao kwa wao, “Twendeni sasa kule Bethlehemu, na tukaone hiki kitu ambacho kimetokea, ambacho Bwana ametufahamisha.”
16 In pridejo jadrno, in najdejo Marijo in Jožefa, in dete, da leží v jaslih.
Wakaharakisha kule, na wakamkuta Mariamu na Yusufu, na wakamuona mtoto amelala kwenye hori la kulishia wanyama.
17 Videvši pa, povedó, kar jim je bilo rečeno za to dete.
Na walipoona hivi, wakawajulisha watu kile walichokuwa wameambiwa kumhusu mtoto.
18 In vsi, kteri so slišali, začudijo se temu, kar so jim bili povedali pastirji.
Wote waliosikia habari hii wakashangazwa na kile kilichosemwa na wachungaji.
19 A Marija je vse te besede varovala, in zlágala jih je v srcu svojem.
Lakini Mariamu akaendelea kufikiri kuhusu yote aliyokwisha kuyasikia, akiyatunza moyoni mwake.
20 In vrnejo se pastirji, slaveč in hvaleč Boga za vse, kar so slišali in videli, kakor jim je bilo povedano.
Wachungaji wakarudi wakimtukuza na kumsifu Mungu kwa ajili ya kila kitu walichokwisha sikia na kuona, kama tu ilivyokuwa imenenwa kwao.
21 In ko se izpolni osem dnî, da dete obrežejo, pa mu dadó ime Jezus, ktero je bil imenoval angelj, predno se je še začel v telesu.
Ilipofika siku ya nane na ilikuwa ni wakati wa kumtahiri mtoto, wakamwita jina Yesu, jina alilokwishapewa na yule malaika kabla mimba haijatungwa tumboni.
22 In ko se izpolnijo dnevi očiščevanja njenega, po postavi Mojzesovej, prineseta ga v Jeruzalem, da ga postavita pred Gospoda,
zao zilizotakiwa za utakaso zilipopita, kulingana na sheria ya Musa, Yusufu na Mariamu wakampeleka hekaluni kule Yerusalemu kumweka mbele za Bwana.
23 (Kakor je pisano v postavi Gospodovej: "Vsak samec, kteri odprè maternico, posvetí naj se Gospodu,")
Kama ilivyoandikwa katika sheria ya Bwana, “Kila mwanaume anayefungua tumbo ataitwa aliyetolewa wakfu kwa Bwana.”
24 In da dasta dar po tem, kar je rečeno v postavi Gospodovej: "Dve grlici ali dva golobiča."
Wao vilevile walikuja kutoa sadaka kulingana na kile kinachosemwa katika sheria ya Bwana, “Jozi ya njiwa au makinda mawili ya njiwa.”
25 In glej, bil je človek v Jeruzalemu, kteremu je bilo ime Simeon, in ta človek je bil pravičen in pobožen, in čakal je tolažbe Izraelove, in Duh sveti je bil v njem.
Tazama, palikuwa na mtu katika Yerusalemu ambaye jina lake alikuwa akiitwa Simeoni. mtu huyu alikuwa mwenye haki na mcha Mungu. Yeye alikuwa akisubiri kwa ajili ya mfariji wa Israeli, na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.
26 In razodel mu je bil sveti Duh, da ne bo videl smrti, dokler ne vidi Kristusa Gospoda.
Ilikuwa imekwisha funuliwa kwake kupitia Roho Mtakatifu kwamba yeye hangelikufa kabla ya kuwomwona Kristo wa Bwana.
27 In pride v Duhu v tempelj. In ko prineseta roditelja otroka Jezusa, da storita za-nj po šegi postave,
Siku moja alikuja ndani ya hekalu, akiongozwa na Roho Mtakatifu. Ambapo wazazi walimleta mtoto, Yesu, kumfanyia yale yaliyopasa kawaida ya sheria,
28 Pa ga on vzeme na naročje svoje, in zahvali Boga, in reče:
ndipo Simeoni alimpokea mikononi mwake, na akamsifu Mungu na kusema,
29 Sedaj odpuščaš hlapca svojega, Gospod, po besedi svojej v miru:
“Sasa ruhusu mtumishi wako aende kwa amani Bwana, kulingana na Neno lako.
30 Ker so videle očí moje zveličanje tvoje,
Kwa kuwa macho yangu yameuona wakovu wako,
31 Ktero si pripravil pred obličjem vseh narodov;
ambao umeonekana kwa macho ya watu wote.
32 Luč za razsvetljenje poganov, in slavo naroda tvojega Izraelskega.
Yeye ni nuru kwa ajili ya ufunuo kwa Wamataifa na utukufu wa watu Israeli.”
33 A Jožef in mati njegova sta se čudila temu, kar se je govorilo o njem.
Baba na Mama wa mtoto walishangazwa kwa mambo ambayo yalizungumzwa juu yake.
34 In blagoslovi ju Simeon, in reče Mariji materi njegovej: Glej, ta je postavljen na pad in vstajenje mnogim v Izraelu, in za znamenje, kteremu se bo nasprotovalo:
Ndipo Simeoni akawabariki na akasema kwa Mariamu mama yake, “Sikiliza kwa makini! Mtoto huyu atakuwa sababu ya kupotea na kuokoka kwa watu wengi katika Israeli na ni ishara ambayo watu wengi wataipinga.
35 (A tebi samej bo pa prebodel meč dušo!) da se odkrijejo iz mnogih src misli.
Pia ni upanga utakaochoma nafsi yako mwenyewe, ili kwamba mawazo ya mioyo ya wengi yadhihirike”.
36 In bila je prerokinja Ana, hči Fanuelova, od rodú Azerjevega: ta je bila zeló stara, in sedem let je bila živela z možem po devištvu svojem;
Nabii mwanamke aliyeitwa Ana pia alikuwako hekaluni. Yeye alikuwa binti wa Fanueli kutoka kabila la Asheri. Alikuwa na miaka mingi sana. Naye aliishi na mume wake kwa miaka saba baada ya kuoana,
37 In vdova okoli štiri in osemdesetih let, ktera ni odhajala od tempeljna, in je s postom in molitvami služila Bogu, noč in dan.
na ndipo akawa mjane kwa miaka themanini na minne. Naye hakuwahi kuondoka hekaluni na alikuwa akiendelea kumwabudu Mungu pamoja na kufunga na kuomba, usiku na mchana.
38 In ta ravno tisti čas pristopi, in hvalila je Gospoda, in govorila je o njem vsem, kteri so čakali odrešenja v Jeruzalemu.
Na kwa wakati huo, alikuja pale walipo akaanza kumshukuru Mungu. Aliongea kumhusu mtoto kwa kila mtu ambaye alikuwa akisubiri ukombozi wa Yerusalemu.
39 In ko vse po postavi Gospodovej dopolnijo, vrnejo se v Galilejo, v mesto svoje Nazaret.
Walipomaliza kila kitu walichotakiwa kufanya kuligana na na sheria ya Bwana, walirudi Galilaya, mjini kwao, Nazareti.
40 A dete je rastlo, in krepčalo se je v duhu, in napolnjevalo se je modrosti; in milost Božja je bila ž njim.
Mtoto alikua, na akawa na nguvu, akiongezeka katika hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.
41 In hodila sta roditelja njegova vsako leto v Jeruzalem o velikonočnem prazniku.
Wazazi wake kila mwaka walikwenda Yerusalemu kwaajili ya sikukuu ya Pasaka.
42 In ko mu je bilo dvanajst let, in sta bila šla v Jeruzalem po navadi praznika,
Alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, walikwenda tena wakati mwafaka kidesturi kwa ajili ya sikukuu.
43 In sta dní dokončala, ko sta se onadva vračala, ostal je deček Jezus v Jeruzalemu. In tega ni vedel Jožef in mati njegova.
Baada ya kubaki siku zote kwa ajili ya sikukuu, walianza kurudi nyumbani. Lakini mvulana Yesu alibaki nyuma mle Yerusalemu na wazazi wake hawakujua hili.
44 Misleč pa, da je pri druščini, prešla sta dan hodá, in iskala sta ga pri sorodnikih in pri znancih.
Walidhani kwamba yumo kwenye kundi walilokuwa wakisafiri nalo, hivyo walisafiri safari ya siku. Ndipo wakaanza kumtafuta miongoni wa ndugu na marafiki zao.
45 In ko ga nista našla, vrneta se v Jeruzalem, iskajoč ga,
Waliposhindwa kumpata, walirudi Yerusalemu na wakaanza kumtafuta humo.
46 In zgodí se po treh dnéh, da ga najdeta v tempeljnu, da sedí sredi učenikov, ter jih posluša, in jih vprašuje.
Ikatokea kwamba baada ya siku tatu, wakampata hekaluni, akiwa ameketi katikati ya waalimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
47 Čudili pa so se vsi, kteri so ga poslušali, razumu njegovemu in odgovorom njegovim.
Wote waliomsikia walishangazwa na ufahamu wake na majibu yake.
48 In ko ga ugledata, zavzemeta se; in reče mu mati njegova: Sin, kaj si nama storil tako? Glej, oče tvoj in jaz sva te z žalostjo iskala.
Walipomwona, walistaajabu. Mama yake akamwambia, “Mwanangu, kwa nini umetutendea hivi? Sikiliza, baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa wasiwasi mkubwa.”
49 Pa jima reče: Kaj, da sta me iskala? Nista li vedela, da moram biti v tem, kar je očeta mojega?
Akawaambia, “Kwa nini mmekuwa mkinitafuta? Hamkujua kwamba lazima niwe kwenye nyumba ya Baba yangu?
50 In ona nista razumela besede, ktero jima je rekel.
Lakini hawakuelewa nini alichomaanisha kwa maneno hayo.
51 Ter snide ž njima, in pride v Nazaret; in bil jima je pokoren. In mati njegova je varovala vse te besede v srcu svojem.
Ndipo akaenda pamoja nao mpaka nyumbani Nazareti na alikuwa mtii kwao. Mama yake alihifadhi mambo yote moyoni mwake.
52 In Jezus je napredoval v modrosti in rasti, in v milosti pri Bogu in ljudeh.
Lakini Yesu aliendelea kukua katika hekima na kimo, na akazidi kupendwa na Mungu na watu.

< Luka 2 >