< Apostolska dela 13 >
1 Bili so pa v cerkvi, ktera je bila v Antijohiji, nekteri preroki in učeniki: Barnaba in Simeon, ki se je imenoval Niger, in Lucij Cirenec, in Manahen, s Herodom četrtnikom odgojen, in Savel.
Sasa katika kanisa la Antiokia, palikuwa na baadhi ya manabii na walimu. Walikua Barnaba, Simeoni (aliyeitwa Nigeri). Lukio wa Kirene, Manaeni( ndugu asiye wa damu wa Herode kiongozi wa mkoa), na Sauli.
2 Ko so pa oni službo Gospodu opravljali in se postili, reče sveti Duh: Odločite mi Barnaba in Savla za delo, na ktero sem ju poklizal.
Walipokuwa wakimwabudu Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu alisema, “Niteengeeni pembeni Barnaba na Sauli, waifanye kazi niliyo waitia.”
3 Tedaj, postivši se in molivši, položé roke na nju, ter ju odpusté.
Baada ya Kanisa kufunga, kuomba, na kuweka mikono yao juu ya watu hawa, wakawaacha waende.
4 Ta torej, poslana od Duha svetega, snideta v Selevcijo, in odtod se odpeljeta po morji na Ciper.
Kwa hiyo Barnabas na Sauli walimtii Roho Mtakatifu na walitelemka kuelekea Seleukia; Kutoka huko walisafiri baharini kuelekea kisiwa cha Kipro.
5 In ko sta prišla v Salamino, oznanjevala sta besedo Božjo po shajališčih Judovskih; imela sta pa tudi Janeza za služabnika.
Walipokuwa katika mji wa Salami, walilitangaza neno la Mungu katika Masinagogi ya Wayahudi. Pia walikuwa pamoja na Yohana Marko kama msaidizi wao.
6 In ko sta prešla otok noter do Pafa, najdeta nekega vražarja, lažnjivega preroka Juda, kteremu je bilo ime Barjezu,
Walipokwenda katika kisiwa chote mpaka Pafo, walikuta mtu fulani mchawi, Myahudi nabii wa uongo, ambaye jina lake lilikuwa Bar Yesu.
7 In je bil z namestnikom Sergijem Pavlom, pametnim možem. Ta, poklicavši Barnaba in Savla, želel je slišati besedo Božjo.
Mchawi huyu alishirikiana na Liwali Sergio Paulus, aliyekuwa mtu mwenye akili. Mtu huyu aliwaalika Barnaba na Sauli, kwa sababu alihitaji kusikia neno la Mungu.
8 Ali ustavljal jima se je Elima, vražar (tako namreč se tolmači ime njegovo), gledajoč, da bi namestnika odvrnil od vere.
Lakini Elima “yule mchawi” (hivyo ndivyo jina lake lilivyo tafsiriwa) aliwapinga; alijaribu kumgeuza yule liwali atoke kwenye imani.
9 Savel pa, ki se tudi Pavel imenuje, poln Duha svetega, pogledavši na-nj,
Lakini Sauli aliyeitwa Paulo, alikuwa amejazwa na Roho Mtakatikfu, akamkazia macho
10 Reče: O polni vsake zvijače in vsake hudobije, sin hudičev, sovražnik vsake pravice! ali ne boš nehal prevračati pravih potov Gospodovih?
na akasema “Ewe mwana wa Ibilisi, umejazwa na aina zote za udanganyifu na udhaifu. Wewe ni adui wa kila aina ya haki. Hautakoma kuzigeuza njia za Bwana, zilizonyooka, je utaweza?
11 In sedaj, glej, roka Gospodova je zoper té, in slep boš in ne boš videl solnca do časa. In pri tej priči je padel na-nj mrak in tema, in tipajoč okoli, iskal je vodnika.
Sasa tazama, mkono wa Bwana upo juu yako, na utakuwa kipofu. Hautaliona Jua kwa muda” mara moja ukungu na giza vilianguka juu ya Elimas; alianza kuzunguka pale akiomba watu wamwongoze kwa kumshika mkono.
12 Tedaj je namestnik, ko je videl, kaj se je zgodilo, veroval, in čudil se je nauku Gospodovemu.
Baada ya liwali kuona kilichotokea, aliamini, kwa sababu alishangazwa kwa mafundisho kuhusu Bwana.
13 Odpeljavši pa se iz Pafa Pavel in kteri so bili ž njim, pridejo v Pergo Pamfilijsko. Janez pa se loči od nju, in vrne se v Jeruzalem.
Sasa Paulo na rafiki zake walisafiri majini kutoka Pafo na wakafika Perge katika Pamfilia. Lakini Yohana aliwaacha na kurudi Yerusalemu.
14 Ona pa, ko sta bila odšla iz Perge, prideta v Antijohijo Pisidijsko, in vnideta v sobotni dan v shajališče, in sedeta.
Paulo na rafiki yake walisafiri kutoka Perge na wakafika Antiokia ya Pisidia. Huko walikwenda katika sinagogi siku ya Sabato na kukaa chini.
15 Po branji postave in prerokov pa pošljejo poglavarji shajališča k njima, govoreč: Moža brata! če je v vaju beseda tolažbe za ljudstvo, govorita.
Baada ya kusoma sheria na manabii, viongozi wa sinagogi aliwatumia ujumbe wakisema, “Ndugu, kama mnao ujumbe wa kutia moyo watu hapa, semeni”
16 Vstavši torej Pavel, pomigne z roko, naj umolknejo, ter reče: Možjé Izraelci, in kteri se bojite Boga, poslušajte!
Kwa hiyo Paulo alisimama na kuwapungia mkono; alisema, “Wanaume wa Israeli na enyi mnao mtii Mungu, sikilizeni.
17 Bog naroda tega Izraelovega je izvolil očete naše, in povišal je ljudstvo, ko so prebivali v zemlji Egiptovskej, in s povzdigneno roko jih je izpeljal iž nje.
Mungu wa hawa watu wa Israeli aliwachagua baba zetu na kuwafanya watu wengi walipokaa katika nchi Misri, na kwa mkono wake kuinuliwa aliwaongoza nje yake.
18 In okoli štirideset let je potrpel ž njih šegami v puščavi.
Kwa miaka arobaini aliwavumilia katika jangwa.
19 In pokončavši sedem narodov v zemlji Kanaanskej, razdelil jim je po kocki njih zemljo.
Baada ya kuyaharibu mataifa saba katika nchi ya Kaanani, aliwapa watu wetu nchi yao kwa urithi.
20 In po tem, kakih štiri sto in petdeset let, dal jim je sodnike do Samuela preroka.
Matukio haya yote yalitokea zaidi ya miaka mia nne na hamsini. Baada ya vitu hivi vyote, Mungu aliwapa waamuzi mpaka Samweli Nabii.
21 In odtlej so zahtevali kralja, in dal jim je Bog Savla sina Kisovega, moža iz rodú Benjaminovega, štirideset let.
Baada ya haya, watu waliomba mfalme, hivyo Mungu aliwapa Sauli mwana wa Kishi, mtu wa kabila la Benjamini, kuwa mfalme kwa miaka arobaini.
22 In ko je bil tega zavrgel, obudil jim je Davida za kralja, kteremu je tudi rekel, pričevaje: "Našel sem Davida Jesejevega, moža po srcu svojem, kteri bo izpolnjeval vso voljo mojo."
Kisha baada ya Mungu kumuondoa katika ufalme, alimwinua Daudi kuwa mfalme wao. Ilikuwa ni kuhusu Daudi kwamba Mungu alisema, 'Nimempata Daudi mwana wa Yese kuwa mtu apendezwaye na moyo wangu; ambaye atafanya kila kitu nipendacho.'
23 Iž njegovega semena je Bog po obljubi obudil Izraelu zveličarja Jezusa,
Kutoka kwenye ukoo wa mtu huyu Mungu ameiletea Israeli mkombozi, Yesu, kama alivyoahidi kufanya.
24 Ko je oznanil Janez pred prihodom njegovim krst pokore vsemu ljudstvu Izraelovemu.
Hili lilianza kutokea, kabla ya Yesu kuja, Yohana kwanza alitangaza ubatizo wa toba kwa watu wote wa Israeli.
25 Ko je pa Janez tek svoj dopolnjeval, govoril je: "Kdo menite, da sem jaz? Nisem jaz, nego glej, prišel bo za menoj, komur nisem vreden obutala odvezati z nog."
Naye Yohana alipokuwa akimalizia kazi yake, alisema, 'Mwanifikiri mimi ni nani? mimi si yule. Lakini sikilizeni, ajaye nyuma yangu, sisitahili kulegeza viatu vya miguu yake.'
26 Možjé bratje, sinovi rodú Abrahamovega, in kteri se med vami bojé Boga! vam se je poslala beseda tega življenja.
Ndugu, watoto wa ukoo wa Abrahamu, na wale ambao kati yenu mnamwabudu Mungu, ni kwa ajili yetu kwamba ujumbe huu wa ukombozi umetumwa.
27 Kajti tí, kteri prebivajo v Jeruzalemu, in njih poglavarji, ker tega niso poznali, odsodili so ga, in tako so glasove prerokov, kteri se vsako soboto beró, dopolnili;
Kwa wale waishio Yerusalemu, na watawala wao, hawakumtambua kwa uhalisia, na wala hawakuutambua ujumbe wa manabii ambao husomwa kila Sabato; kwa hiyo walitimiliza ujumbe wa manabii kwa kumhukumu kifo Yesu.
28 In nobene krivice smrtne niso našli, in prosili so Pilata, naj ga pogubí.
Japokuwa hawakupata sababu nzuri kwa kifo ndani yake, walimwomba Pilato amuue.
29 In ko so dopolnili vse, kar je bilo pisano za njega, sneli so ga z lesa in položili v grob.
Walipomaliza mambo yote yaliyoandikwa kuhusu yeye, walimshusha kutoka mtini na kumlaza kaburini.
30 A Bog ga je obudil iz mrtvih,
Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu.
31 In pokazoval se je več dnî tem, kteri so bili ž njim vred prišli iz Galileje v Jeruzalem, kteri so priče njegove pred ljudstvom.
Alionekana kwa siku nyingi kwa wale waliokwenda pamoja naye kutoka Galilaya kuelekea Yerusalemu. Watu hawa sasa ni mashahidi wa watu.
32 In mi vam oznanjujemo obljubo, ktera se je obljubila očetom, da je to Bog izpolnil nam njih otrokom, obudivši Jezusa,
Hivyo tunawaletea habari njema kuhusu ahadi walizopewa mababu zetu.
33 Kakor je tudi v drugem psalmu pisano: "Sin moj si ti; jaz sem te danes rodil."
Mungu aliweka ahadi hizi kwetu, watoto wao, katika hilo alimfufua Yesu na kumrudisha tena katika uhai. Hili pia liliandikwa katika Zaburi ya pili: 'Wewe ni Mwanangu, leo nimekuwa Baba yako'
34 Da ga je pa obudil iz mrtvih, da se ne vrne več v trohnenje, rekel je tako: "Dal vam bom svetinjo Davidovo zvesto."
Pia kuhusu ukweli ni kwamba alimfufua kutoka wafu ili kwamba mwili wake usiharibike, ameongea hivi: 'Nitakupatia utakatifu na baraka halisi za Daudi'
35 Za to pravi tudi na drugem mestu: "Ne boš dal, da bi svetnik tvoj videl trohnenje."
Hii ndiyo sababu kasema pia katika zaburi nyingine, 'Hautaruhusu mtakatifu wako kuuona uozo.'
36 Kajti David, ko je bil ob času svojem poslužil volji Božjej, zaspal je, in položili so ga k očetom njegovim, in videl je trohnenje.
Kwa kuwa baada ya Daudi kutumikia mapenzi ya Mungu katika kizazi chake, alilala, alilazwa pamoja na baba zake, na aliuona uaharibifu,
37 Ta pa, ki ga je Bog obudil, ni videl trohnenja.
Lakini aliyefufuliwa na Mungu hakuuona uharibifu.
38 Znano vam torej bodi, možjé bratje! da vam se po njem odpuščanje grehov oznanjuje;
Hivyo na ifahamike kwenu, ndugu, kupitia mtu huyu, msamaha wa dhambi umehubiriwa.
39 In od vsega, od česar se v Mojzesovej postavi niste mogli opravičiti, opravičil se bo v tem vsak, kdor veruje.
Kwa yeye kila aaminiye anahesabiwa haki na mambo yote ambayo sheria ya Musa isingewapatia haki.
40 Glejte torej, da ne pride na vas, kar je rečeno v prerokih:
Hivyo basi kuweni waangalifu kwamba kitu walichokiongelea manabii kisitokee kwenu:
41 "Glejte, zaničevalci! in čudite se in izginite; kajti delo bom jaz storil v dnéh vaših, delo, kteremu ne boste verovali, če vam kdo pové."
'Tazama, enyi mnaodharau, na mkashangae na mkaangamie; kwa vile nafanya kazi katika siku zenu, Kazi ambayo hamwezi kuiamini, hata kama mtu atawaeleza.”
42 Ko sta pa izšla iz shajališča Judovskega, prosili so ju pogani, naj bi jim drugo soboto govorila te besede.
Wakati Paulo na Barnaba walipoondoka, watu wakawaomba waongee maneno haya siku ya Sabato ijayo.
43 In ko se je zbor razšel, odšlo je veliko Judov in pobožnih izpreobrnencev za Pavlom in Barnabom, ktera sta, govoreč jim, prigovarjala, naj ostanejo v milosti Božjej.
Wakati mkutano wa sinagogi ulipokwisha, Wayahudi wengi na waongofu thabiti waliwafuata Paulo na Barnaba, ambao waliongea nao na waliwahimiza waendelee katika neema ya Mungu.
44 A drugo soboto se je skoro vse mesto zbralo, da bi slišali besedo Božjo.
Sabato iliyofuata, karibu mji mzima ulikusanyika kusikia neno la Mungu.
45 Videč pa Judje ljudstvo, napolnijo se nenavidnosti, in govorili so zoper to, kar je pravil Pavel, nasprotujoč in preklinjajoč.
Wayahudi walipoona makutano, walijawa na wivu na kuongea maneno yaliyopinga vitu vilivyosemwa na Paulo na walimtukana.
46 Tedaj Pavel in Barnaba srčno rečeta: Vam se je morala najprej govoriti beseda Božja; ko jo pa zametujete, in se nevredne štejete večnega življenja, glej, obračava se do poganov. (aiōnios )
Lakini Paulo na Barnaba waliongea kwa ujasiri na kusema, “Ilikuwa ni muhimu kwamba neno la Mungu liongelewe kwanza kwenu. Kwa kuwa mnalisukumia mbali kutoka kwenu nakujiona kuwa hamkusitahili uzima wa milele, angalieni tutawageukia Mataifa. (aiōnios )
47 Kajti tako nam je zapovedal Gospod: "Postavil sem te za luč poganom, da boš na zveličanje noter do kraja zemlje."
Kama ambavyo Bwana ametuamuru, akisema, 'Nimewaweka ninyi kama nuru kwa watu wa mataifa, kwamba mlete wokovu kwa pande zote za dunia.”
48 Ko so pa pogani to slišali, veselili so se, in slavili so besedo Gospodovo, in verovali so, kolikor jih je bilo odločenih za večno življenje. (aiōnios )
Mataifa waliposikia hili, walifurahi na kulisifu neno la Bwana. Wengi waliochaguliwa kwa uzima wa milele waliamini. (aiōnios )
49 In razširjala se je beseda Gospodova po vsej deželi.
Neno la Bwana lilienea nchi yote.
50 Judje pa nadražijo pobožne in poštene žene in prvake mestne, in zbudé preganjanje zoper Pavla in Barnaba, in izženó ju iz svojih krajev.
Lakini wayahudi waliwasihi waliojitoa na wanawake muhimu, pia na viongozi wa mji. Haya yalichochea mateso dhidi ya Paulo na Barnaba na waliwatupa nje ya mipaka ya mji.
51 A ona sta otresla prah z nog svojih na njih, in prišla sta v Ikonijo.
Lakini Paulo na Barnaba walikung'uta vumbi ya miguu yao. Kisha walienda kwenye mji wa Ikonia.
52 Učenci pa so so napolnjevali radosti in Duha svetega.
Na wanafunzi walijawa na furaha pamoja na Roho mtakatifu.