< 1 Korinčanom 12 >
1 A za duhovne stvari ne čem, bratje, da bi ničesar ne znali.
Ndugu, kuhusu vipaji vya kiroho, napenda mfahamu vizuri mambo haya:
2 Veste, da ste pogani bili in hodili k nemim malikom, kakor so vas vodili;
Mnajua kwamba, kabla ya kuongoka kwenu, mlitawaliwa na kupotoshwa na sanamu tupu.
3 Za to vam dajem na znanje, da nikdor v duhu Božjem govoreč ne govori prekletstva Jezusu, in nikdor ne more reči Gospoda Jezusa razen v Duhu svetem.
Basi, jueni kwamba mtu yeyote anayeongozwa na Roho wa Mungu hawezi kusema: “Yesu alaaniwe!” Hali kadhalika, mtu yeyote hawezi kusema: “Yesu ni Bwana,” asipoongozwa na Roho Mtakatifu.
4 So pa razločki darov, ali eden je Duh,
Vipaji vya kiroho ni vya namna nyingi, lakini Roho avitoaye ni mmoja.
5 In so razločki službe, ali eden je Gospod.
Kuna namna nyingi za kutumikia, lakini Bwana anayetumikiwa ni mmoja.
6 In so razločki del, ali eden je Bog, kteri dela vse v vsem.
Kuna namna mbalimbali za kufanya kazi ya huduma, lakini Mungu ni mmoja, anayewezesha kazi zote katika wote.
7 A vsakemu se daje razodetje Duha na korist.
Kila mtu hupewa mwangaza wa Roho kwa faida ya wote.
8 Kajti enemu se po Duhu daje beseda modrosti, a drugemu beseda znanja po ravno tistem Duhu,
Roho humpa mmoja ujumbe wa hekima, na mwingine ujumbe wa elimu apendavyo Roho huyohuyo.
9 Drugemu pa vera v ravno tistem Duhu, a drugemu dar ozdravljanja v ravno tistem Duhu;
Roho huyohuyo humpa mmoja imani, na humpa mwingine kipaji cha kuponya;
10 A drugemu dela moči, drugemu pa preroštvo, a drugemu razločevanje duhov, drugemu pa raznovrstnost jezikov, a drugemu razkladanje jezikov.
humpa mmoja kipaji cha kufanya miujiza, mwingine kipaji cha kusema ujumbe wa Mungu, mwingine kipaji cha kubainisha vipaji vitokavyo kwa Roho na visivyo vya Roho; humpa mmoja kipaji cha kusema lugha ngeni, na mwingine kipaji cha kuzifafanua.
11 A vse to dela ravno tisti Duh, razdeljujoč po svojej volji vsakemu kakor hoče.
Hizo zote ni kazi za Roho huyohuyo mmoja, ambaye humpa kila mtu kipaji tofauti, kama apendavyo mwenyewe.
12 Kajti kakor je telo eno in ude ima mnogo, a vsi udje enega telesa, če tudi jih je mnogo, eno so telo; tako tudi Kristus.
Kama vile mwili ulivyo mmoja wenye viungo vingi, na viungo hivyo vyote—ingawaje ni vingi—hufanya mwili mmoja, ndivyo ilivyo pia kwa Kristo.
13 Ker smo se v enem Duhu mi vsi v eno telo krstili, bodi si Judje, bodi si Grki, bodi si sužnji, bodi si svobodni, in vsi smo se v enega Duha napojili.
Maana sisi, tukiwa Wayahudi au watu wa mataifa mengine, watumwa au watu huru, sote tumebatizwa kwa Roho mmoja katika mwili huo mmoja; na sote tukanyweshwa Roho huyo mmoja.
14 Kajti telo ni eden ud, nego mnogi.
Mwili hauna kiungo kimoja tu, bali una viungo vingi.
15 Če reče noga: "nisem roka, nisem od telesa," je li za to ni od telesa?
Kama mguu ungejisemea: “Kwa kuwa mimi si mkono, basi mimi si mali ya mwili”, je, ungekoma kuwa sehemu ya mwili? La hasha!
16 In če reče uho: "nisem oko, nisem od telesa," jeli za to ni od telesa?
Kama sikio lingejisemea: “Kwa vile mimi si jicho, basi mimi si mali ya mwili”, je, kwa hoja hiyo lingekoma kuwa sehemu ya mwili? La!
17 Ko bi bilo celo telo oko, kje bi bil sluh? ko bi bilo celo sluh, kje bi bil voh?
Kama mwili wote ungekuwa jicho, sikio lingekuwa wapi? Na kama mwili wote ungekuwa sikio, mtu angewezaje kunusa?
18 Sedaj je pa Bog postavil ude enega vsakega izmed njih po telesu, kakor je hotel.
Lakini kama ilivyo, Mungu alizipanga sehemu hizo tofauti katika mwili kama alivyopenda.
19 Ko bi bili pa vsi eden ud, kje bi bilo telo?
Kama sehemu zote zingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
20 Sedaj so pa mnogi udje, a telo eno.
Ukweli ni kwamba, sehemu za mwili ni nyingi, lakini mwili ni mmoja.
21 Pa oko ne more reči roki: "ni mi to treba," ali zopet glava nogama: "ni mi vaju treba."
Basi, jicho haliwezi kuuambia mkono: “Sikuhitaji wewe”, wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu: “Siwahitaji ninyi.”
22 Nego s tem bolje so potrebnejši udje telesa, kteri se slabejši zdé;
Zaidi ya hayo, inaonekana kwamba sehemu zile za mwili zinazoonekana kuwa ni dhaifu ndizo zilizo muhimu zaidi.
23 In kteri nam se zdé manje častni na telesu, okoli teh stavimo obilnejšo čast, in naši nespodobni imajo obilnejšo spodobnost.
Tena, viungo vile tunavyovifikiria kuwa havistahili heshima kubwa, ndivyo tunavyovitunza kwa uangalifu zaidi; viungo vya mwili ambavyo havionekani kuwa vizuri sana, huhifadhiwa zaidi,
24 A našim spodobnim pa tega ni treba. Ali Bog je zložil telo, davši pomanjkljivemu večo čast,
ambapo viungo vingine havihitaji kushughulikiwa. Mungu mwenyewe ameuweka mwili katika mpango, akakipa heshima zaidi kiungo kile kilichopungukiwa heshima,
25 Da bi ne bilo razpora v telesu, nego da bi udje enako skrbeli eden za drugega.
ili kusiweko na utengano katika mwili bali viungo vyote vishughulikiane.
26 In če trpi eden ud, ž njim trpé vsi udje, a če se slavi eden ud, ž njim se veselé vsi udje.
Kama kiungo kimoja kinaumia viungo vyote huumia pamoja nacho. Kiungo kimoja kikisifiwa viungo vingine vyote hufurahi pamoja nacho.
27 Vi pa ste telo Kristusovo in udje med seboj;
Basi, ninyi nyote ni mwili wa Kristo; kila mmoja wenu ni kiungo cha mwili huo.
28 In nektere si je postavil Bog v cerkvi prvič za aposteljne, drugič za preroke, tretjič za učitelje; po tem moči, za tem dari ozdravljanja, pomaganja, vladanja, raznovrstnost jezikov.
Mungu ameweka katika kanisa: kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu; kisha ameweka wale wenye kipaji cha kufanya miujiza, kuponya, kusaidia; viongozi na wenye kusema lugha ngeni.
29 Jeli so vsi aposteljni? jeli vsi preroki? jeli vsi učitelji? jeli vsi moči?
Je, wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni walimu? Wote ni wenye kipaji cha kufanya miujiza?
30 Jeli imajo vsi darove ozdravljanja? jeli vsi jezike govoré? jeli vsi razkladajo?
Je, wote ni wenye kipaji cha kuponya? Wote ni wenye kipaji cha kusema lugha ngeni? Je, wote hufafanua lugha?
31 Hrepenite pa za boljšimi darovi, in še boljšo pot vam kažem.
Muwe basi, na tamaa ya kupata vipaji muhimu zaidi. Nami sasa nitawaonyesheni njia bora zaidi kuliko hizi zote.