< Sofonija 1 >

1 Gospodova beseda, ki je prišla Sofoniju, sinu Kušíja, sinú Gedaljája, sinú Amarjá, sinú Hezekija, v dneh Jošíja, Amónovega sina, Judovega kralja.
Hili ni neno la Yahwe ambalo lilikuja kwa Sefania mwana wa Kushi mwana wa Gedalia mwana wa Amaria mwana Hezekia, katika siku za Yosia mwana wa Amoni, mfalme wa Yuda. “
2 »Popolnoma bom použil vse stvari iz dežele, « govori Gospod.
Nitaangamiza kabisa kila kitu kutoka usoni mwa dunia - hili ni tamko la Bwana mwenyewe.
3 »Použil bom človeka in žival. Z zlobnimi bom použil perjad neba in ribe morja in kamne spotike in človeka bom iztrebil iz dežele, « govori Gospod.
Nitamwangamiza mtu na mnyama; Nitawaangamiza ndege wa mbinguni na samaki wa baharini, uharibifu pamoja na waovu. Hivyo nitamfutilia mbali mtu kutoka uso wa dunia - hili ni tamko la Bwana mwenyewe.
4 »Prav tako bom svojo roko iztegnil nad Juda in nad vse prebivalce Jeruzalema in iztrebil bom preostanek Báala iz tega mesta in ime Kemarimov z duhovniki;
Nitafika kwa mkono wangu juu ya Yuda na wote wenyeji wa Yerusalemu. Nitafutilia mbali kila mabaki ya Baali kutoka sehemu hii na majina ya watu waabuduo sanamu miongoni mwa makuhani,
5 in tiste, ki obožujejo vojsko neba na hišnih strehah; in tiste, ki obožujejo in ki prisegajo pri Gospodu in prisegajo pri Milkómu;
watu ambao juu ya nyumba huabudu miili ya mbinguni, na watu ambao huabudu na kuapa kwa Yahwe bali ambao pia huapa kwa mfalme wao.
6 in tiste, ki so obrnjeni nazaj od Gospoda; in tiste, ki niso iskali Gospoda niti poizvedovali za njim.«
Nitawafutilia mbali pia wale ambao wamegeuka nyuma kutoka kumfuata Yahwe, wale ambao pia humtafuta Yahwe pasipo kuuliza ulinzi wake.
7 Mirujte ob prisotnosti Gospoda Boga, kajti dan Gospodov je pri roki, kajti Gospod je pripravil klavno daritev, povabil je svoje goste.
Uwe kimya mbele ya Bwana Yahwe! Kwa kuwa siku ya Yahwe ni karibu, Yahwe ameandaa dhabihu na amewatenga wageni wake.
8 »In zgodilo se bo, na dan Gospodove klavne daritve, da bom kaznoval prince in kraljeve otroke in vse tiste, ki so oblečeni s tujo obleko.
“Itakuja katika siku ya dhabihu ya Bwana, hivyo nitawapiga wakuu na wana wa mfalme, na kila mmoja aliyevikwa mavazi ya kigeni.
9 V istem dnevu bom kaznoval tudi vse tiste, ki poskakujejo na pragu, ki napolnjujejo hiše svojih gospodarjev z nasiljem in prevaro.
Katika siku hiyo nitawapiga wote wale ambao huruka juu ya kizingiti, wale ambao hujaza nyumba ya bwana wao kwa vurugu na udanganyifu.
10 Na tisti dan se bo zgodilo, « govori Gospod, » da bo glas vpitja od Ribjih velikih vrat in tuljenja od drugih in veliko lomljenje s hribov.
Itakuwa katika siku ile - hili ni tangazo la Yahwe - kwamba kilio cha huzuni kitakuja kutoka kwenye mlango wa samaki, ikipiga yowe kutoka Wilaya ya Pili, na sauti ya kishindo kikuu kutoka vilimani.
11 Tulite, vi prebivalci Maltarke, kajti vse trgovsko ljudstvo je posekano. Vsi tisti, ki nosijo srebro, so iztrebljeni.
Pigeni yowe, wenyeji wa Soko la Wilaya, kwa wote wafanyabiashara watakuwa wameharibiwa, wote wale ambao hupima fedha watakuwa wamefutiliwa mbali.
12 Ob tistem času se bo zgodilo, da bom Jeruzalem preiskal s svetilkami in kaznoval ljudi, ki so naseljeni na svojih usedlinah, ki v svojem srcu pravijo: › Gospod ne bo storil dobrega niti ne bo storil zlega.‹
Itakuwa katika siku ile nitaitafuta Yerusalemu kwa taa na kuwapiga wanaume ambao watakuwa wamekaa kwenye mvinyo wao na kusema mioyoni mwao, 'Yahwe hatafanya chochote, ama kizuri au kiovu.'.
13 Zato bodo njihove dobrine postale plen in njihove hiše opustošenje. Prav tako bodo gradili hiše, toda ne bodo jih poselili in sadili bodo vinograde, toda od njihovega vina ne bodo pili.«
Mali zao zitakuja kuporwa, na nyumba zao zitakuwa zimetelekezwa kwa maangamizi! Watajenga nyumba lakini hawataishi humo, na kupanda mizabibu lakini hawatakunywa mvinyo wake.
14 Gospodov véliki dan je blizu, ta je blizu in silno hiti, celó glas Gospodovega dneva. Mogočen človek bo tam grenko jokal.
Siku kubwa ya Yahwe ni karibu, karibu na inaharakisha upesi! Sauti ya siku ya Yahwe itakuwa ya kilio cha uchungu wa kishujaa!
15 Tisti dan je dan besa, dan stiske in tegobe, dan pustote in opustošenja in dan teme in mračnosti, dan oblakov in goste teme,
Siku hiyo itakuwa siku ya ghadabu, siku ya huzuni na uchungu, siku ya dhoruba na maangamizi, siku ya giza na utusitusi, siku ya mawingu na giza nene.
16 dan šofarja in alarma zoper utrjena mesta in zoper visoke stolpe.
Itakuwa siku ya parapanda na kengele dhidi ya ngome mijini na buruji ndefu.
17 »Na ljudi bom privedel tegobo, da bodo hodili kakor slepi ljudje, ker so grešili zoper Gospoda in njihova kri bo izlita kakor prah in njihovo meso kakor gnoj.«
Hivyo nitaleta dhiki juu ya wanadamu, kwa hiyo watatembea karibu kama wanaume vipofu tangu walipofanya dhambi dhidi ya Yahwe. Damu yao itamwagwa kama vumbi, na sehemu zao za ndani kama kinyesi.
18 Niti jih njihovo srebro niti njihovo zlato ne bo moglo osvoboditi na dan Gospodovega besa, temveč bo celotna dežela použita z ognjem njegove ljubosumnosti, kajti celo zelo hitro se bo znebil vseh tistih, ki prebivajo v deželi.«
Wala fedha zao wala dhahabu zao hazitaweza kuwaokoa juu ya ghadhabu ya Yahwe. Ndani ya moto wa wivu wake dunia yote itateketezwa, hivyo ataleta ukamilifu, miwisho wa kutisha kwa wote wakaao duniani.”

< Sofonija 1 >