< Psalmi 48 >
1 Velik je Gospod in silno bodi hvaljen v mestu našega Boga, na gori njegove svetosti.
Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
2 Lepa zaradi lege, radost celotne zemlje, je gora Sion na straneh severa, mesto vélikega Kralja.
Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
3 Bog je v njenih palačah razpoznan za zatočišče.
Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
4 Kajti, glej, kralji so bili zbrani, skupaj so šli mimo.
Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
5 Videli so to in tako so se čudili; bili so vznemirjeni in odhiteli.
walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
6 Tam sta jih prevzela strah in bolečina kakor žensko v porodnih mukah.
Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
7 Z vzhodnikom lomiš ladje iz Taršíša.
Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
8 Kakor smo slišali, tako smo videli v mestu Gospoda nad bojevniki, v mestu svojega Boga. Bog ga bo utrdil na veke. (Sela)
Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
9 Premišljevali smo o tvoji ljubeči skrbnosti, oh Bog, v sredi tvojega templja.
Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
10 Glede na tvoje ime, oh Bog, taka je tvoja hvala do koncev zemlje. Tvoja desnica je polna pravičnosti.
Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
11 Naj se gora Sion veseli, naj bodo Judove hčere radostne zaradi tvojih sodb.
Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
12 Hodite okoli Siona in ga obhodite, štejte njegove stolpe.
Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
13 Dobro označite njegove branike, opazujte njegove palače, da boste to lahko pripovedovali naslednjemu rodu.
yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
14 Kajti ta Bog je naš Bog na veke vekov. On bo naš vodnik celó do smrti.
Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.