< Psalmi 36 >
1 Prestopek zlobnega znotraj mojega srca pravi, da pred njegovimi očmi ni Božjega strahu.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana. Kuna neno moyoni mwangu kuhusu hali ya dhambi ya mwovu. Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
2 Kajti v svojih lastnih očeh si laska, dokler se ne najde njegova krivičnost, da je vreden sovraštva.
Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.
3 Besede iz njegovih ust so krivičnost in prevara. Prenehal je biti moder in delati dobro.
Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu, ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
4 Na svoji postelji snuje vragolijo, postavlja se na pot, ki ni dobra, zla ne prezira.
Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya, hujitia katika njia ya dhambi na hakatai lililo baya.
5 Tvoje usmiljenje, oh Gospod, je v nebesih; in tvoja zvestoba sega do oblakov.
Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni, uaminifu wako hadi kwenye anga.
6 Tvoja pravičnost je podobna velikim goram, tvoje sodbe so zelo globokoumne. Oh Gospod, ti ohranjaš človeka in žival.
Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama kilindi kikuu. Ee Bwana, wewe huwahifadhi mwanadamu na mnyama.
7 Kako odlična je tvoja ljubeča skrbnost, oh Bog! Zato človeški otroci svoje trdno upanje polagajo pod senco tvojih peruti.
Upendo wako usiokoma ni wa thamani mno! Watu wakuu na wadogo hujificha uvulini wa mbawa zako.
8 Obilno bodo nasičeni z obiljem tvoje hiše in primoral jih boš piti iz reke svojih radosti.
Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako, nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
9 Kajti s teboj je studenec življenja, v tvoji svetlobi bomo videli svetlobo.
Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima, katika nuru yako twaona nuru.
10 Oh nadaljuj svoje ljubeče skrbnosti tem, ki te poznajo, in svojo pravičnost do iskrenih v srcu.
Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe, haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
11 Naj proti meni ne pride stopalo ponosnega in naj me roka zlobnega ne odstrani.
Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu, wala mkono wa mwovu usinifukuze.
12 Tam so padli delavci krivičnosti. Podrti so in ne bodo mogli vstati.
Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka: wametupwa chini, hawawezi kuinuka!