< Pregovori 28 >

1 Zlobni zbežijo, kadar jih noben človek ne preganja, toda pravični so pogumni kakor lev.
Mtu mwovu hukimbia ingawa hakuna yeyote anayemfukuza, bali wenye haki ni wajasiri kama simba.
2 Zaradi prestopka dežele so številni njeni princi, toda s človekom razumevanja in spoznanja bo njihova država podaljšana.
Wakati nchi inapokuwa na uasi, inakuwa na viongozi wengi, bali mwenye ufahamu na maarifa hudumisha utaratibu.
3 Revež, ki zatira ubogega, je podoben pometajočemu dežju, ki ne zapušča nobene hrane.
Mtu maskini amwoneaye yeye aliye maskini zaidi ni kama mvua ya dhoruba isiyosaza mazao.
4 Tisti, ki zapuščajo postavo, hvalijo zlobne, toda tisti, ki se držijo postave, se z njimi pričkajo.
Wale waiachao sheria huwasifu waovu, bali wale waishikao sheria huwapinga.
5 Hudobneži ne razumejo sodbe, toda tisti, ki iščejo Gospoda, razumejo vse stvari.
Watu wabaya hawaelewi haki, bali wale wamtafutao Bwana wanaielewa kikamilifu.
6 Boljši je ubogi, ki hodi v svoji poštenosti, kakor kdor je sprevržen na svojih poteh, četudi je bogat.
Afadhali maskini ambaye mwenendo wake hauna lawama kuliko tajiri ambaye njia zake ni potovu.
7 Kdorkoli ohranja postavo, je moder sin, toda kdor je družabnik upornih ljudi, svojega očeta spravlja v sramoto.
Yeye ashikaye sheria ni mwana mwenye ufahamu, bali rafiki wa walafi humwaibisha baba yake.
8 Kdor z obrestmi in nepravičnim zaslužkom povečuje svoje imetje, ga bo zbiral za tistega, ki bo pomiloval ubogega.
Yeye aongezaye utajiri wake kwa riba kubwa mno hukusanya kwa ajili ya mwingine, ambaye atawahurumia maskini.
9 Kdor svoje uho obrača stran od poslušanja postave, bo celo njegova molitev ogabnost.
Kama mtu yeyote akikataa kusikia sheria, hata maombi yake ni chukizo.
10 Kdorkoli pravičnemu povzroči, da zaide na zlo pot, bo tudi sam padel v svojo lastno jamo, toda pošteni bodo imeli v posesti dobre stvari.
Yeye ambaye humwongoza mwenye haki kwenye mapito mabaya, ataanguka kwenye mtego wake mwenyewe, bali wasio na lawama watapokea urithi mwema.
11 Bogataš je moder v svoji lastni domišljavosti, toda revni, ki ima razumevanje, ga preiskuje.
Mtu tajiri anaweza kuwa na hekima machoni pake mwenyewe, bali mtu maskini mwenye ufahamu atamfichua.
12 Kadar se pravični ljudje razveseljujejo, je velika slava, toda kadar vstanejo zlobni, je človek skrit.
Mwenye haki ashindapo, kuna furaha kubwa, bali waovu watawalapo, watu hujificha.
13 Kdor prikriva svoje grehe, ne bo uspešen, toda kdorkoli jih priznava in se jim odreka, bo imel usmiljenje.
Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali yeyote aziungamaye na kuziacha hupata rehema.
14 Srečen je človek, ki se vedno boji, toda kdor svoje srce zakrkne, bo padel v vragolijo.
Amebarikiwa mtu ambaye siku zote humcha Bwana, bali yeye afanyaye moyo wake kuwa mgumu huangukia kwenye taabu.
15 Kakor rjoveč lev in pohajkujoč medved, tak je zloben vladar nad ubogim ljudstvom.
Kama simba angurumaye au dubu ashambuliaye, ndivyo alivyo mtu mwovu atawalaye wanyonge.
16 Princ, ki mu manjka razumevanja, je prav tako velik zatiralec, toda kdor sovraži pohlepnost, bo podaljšal svoje dni.
Mtawala dhalimu hana akili, bali yeye achukiaye mapato ya udhalimu atafurahia maisha marefu.
17 Človek, ki počne nasilje krvi kateregakoli človeka, bo zbežal v jamo; naj ga noben človek ne zadržuje.
Mtu mwenye kusumbuliwa na hatia ya kuua atakuwa mtoro mpaka kufa; mtu yeyote na asimsaidie.
18 Kdorkoli živi pošteno, bo rešen, toda kdor je na svojih poteh sprevržen, bo naenkrat padel.
Yeye ambaye mwenendo wake hauna lawama hulindwa salama, bali yeye ambaye njia zake ni potovu ataanguka ghafula.
19 Kdor obdeluje svojo zemljo, bo imel obilo kruha, toda kdor sledi ničevim osebam, bo imel dosti revščine.
Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yule afuataye mambo ya upuzi atakuwa na umaskini wa kumtosha.
20 Zvest človek bo obilen z blagoslovi, toda kdor hiti biti bogat, ne bo nedolžen.
Mtu mwaminifu atabarikiwa sana, bali yeye atamaniye kupata utajiri kwa haraka hataacha kuadhibiwa.
21 Ozirati se na osebe ni dobro, kajti za košček kruha se bo ta človek pregrešil.
Kuonyesha upendeleo si vizuri, hata hivyo mtu atafanya kosa kwa kipande cha mkate.
22 Kdor hiti biti bogat, ima hudobno oko in ne upošteva, da bo nadenj prišla revščina.
Mtu mchoyo ana tamaa ya kupata utajiri, naye hana habari kuwa umaskini unamngojea.
23 Kdor graja človeka, bo kasneje našel večjo naklonjenost, kakor kdor laska z jezikom.
Yeye amkemeaye mtu mwishoni hupata kibali zaidi, kuliko mwenye maneno ya kusifu isivyostahili.
24 Kdorkoli krade svojemu očetu ali svoji materi in pravi: » To ni prestopek, « isti je družabnik uničevalcu.
Yeye amwibiaye babaye au mamaye na kusema, “Si kosa,” yeye ni mwenzi wa yule aharibuye.
25 Kdor je ponosnega srca, razvnema prepir, toda kdor svoje trdno upanje polaga v Gospoda, bo narastel.
Mtu mwenye tamaa huchochea fitina, bali yule amtegemeaye Bwana atafanikiwa.
26 Kdor zaupa v svoje lastno srce, je bedak, toda kdorkoli hodi modro, bo osvobojen.
Yeye ajitumainiaye mwenyewe ni mpumbavu, bali yeye atembeaye katika hekima hulindwa salama.
27 Kdor daje ubogemu, ne bo trpel pomanjkanja, toda kdor zagrinja svoje oči, bo mnogim [v] kletev.
Yeye ampaye maskini hatapungukiwa na kitu chochote, bali yeye awafumbiaye maskini macho hupata laana nyingi.
28 Kadar zlobni vstajajo, se ljudje skrivajo, toda kadar oni izginejo, pravični narastejo.
Wakati waovu watawalapo, watu huenda mafichoni, bali waovu wanapoangamia, wenye haki hufanikiwa.

< Pregovori 28 >