< Pregovori 26 >

1 Kakor sneg poleti in kakor dež ob času žetve, tako se čast ne poda bedaku.
Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno, ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.
2 Kakor ptica s potepanjem, kakor lastovka z letenjem, tako prekletstvo brez razloga ne bo prišlo.
Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.
3 Bič za konja, uzda za osla in palica za hrbet bedaka.
Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!
4 Bedaku ne odgovori glede na njegovo neumnost, da ne bi bil tudi ti podoben njemu.
Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.
5 Odgovori bedaku glede na njegovo neumnost, da on ne bi bil moder v svoji lastni domišljavosti.
Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.
6 Kdor pošilja sporočilo po roki bedaka, si odseka stopala in pije škodo.
Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara, ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.
7 Nogi hromega nista enaki; takšna je prispodoba v ustih bedakov.
Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.
8 Kakor kdor poveže kamen v pračo, tak je, kdor daje čast bedaku.
Kama kufunga jiwe kwenye kombeo, ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.
9 Kakor gre trn v roko pijanca, taka je prispodoba v ustih bedakov.
Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.
10 Velik Bog, ki je ustvaril vse stvari, nagrajuje tako bedaka kakor prestopnike.
Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo, ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.
11 Kakor se pes vrača k svojemu izbljuvku, tako se bedak vrača k svoji neumnosti.
Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake, ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.
12 Ali vidiš modrega človeka v njegovi lastni domišljavosti? Več upanja je za bedaka kakor zanj.
Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
13 Len človek pravi: » Tam je lev na poti, lev je na ulicah.«
Mvivu husema, “Yuko simba barabarani, simba mkali anazunguka mitaa!”
14 Kakor se vrata obračajo na svojih tečajih, tako se leni na svoji postelji.
Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.
15 Leni skriva svojo roko v svojem naročju, žalosti ga, da jo ponovno prinese k svojim ustom.
Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.
16 Lenuh je modrejši v svoji lastni domišljavosti, kakor sedem mož, ki lahko izkažejo razlog.
Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.
17 Kdor gre mimo in se vmešava v prepir, ki mu ne pripada, je podoben tistemu, ki psa zgrabi za ušesa.
Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.
18 Kakor zmešan človek, ki meče kose tlečega lesa, puščice in smrt,
Kama mtu mwendawazimu atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,
19 tak je človek, ki zavaja svojega bližnjega in pravi: »Ali nisem na zabavi?«
ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”
20 Kjer ni nobenega lesa, tam ogenj poide. Tako, kjer ni tožljivca, prepir preneha.
Bila kuni moto huzimika; pasipo uchongezi ugomvi humalizika.
21 Kakor je oglje za vročo žerjavico in drva za ogenj, tako je prepirljiv človek za podžiganje prepira.
Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.
22 Besede tožljivca so kakor rane in gredo navzdol v najnotranjejše dele trebuha.
Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
23 Goreče ustnice in zlobno srce sta podobna črepinji, pokriti s srebrovo žlindro.
Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.
24 Kdor sovraži, prikriva s svojimi ustnicami in znotraj sebe shranjuje prevaro;
Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.
25 kadar govori lepo, mu ne verjemi, kajti sedem ogabnosti je v njegovem srcu.
Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini, kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.
26 Čigar sovraštvo je pokrito s prevaro, bo njegova zlobnost razkazana pred celotno skupnostjo.
Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu, lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.
27 Kdorkoli koplje jamo, bo padel vanjo, in kdor vali kamen, se bo le-ta vrnil nadenj.
Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake, kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.
28 Lažniv jezik sovraži tiste, ki so prizadeti z njim in prilizovanje ust dela propad.
Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza, nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.

< Pregovori 26 >