< 4 Mojzes 23 >
1 Bileám je rekel Baláku: »Tukaj mi zgradi sedem oltarjev in mi pripravi sedem volov ter sedem ovnov.«
Balaamu akamwabia Balaki, “Jenga madhabahu saba kwa ajili yangu na uandae mafahari saba na kondoo dume saba.”
2 Balák je storil, kakor je Bileám govoril, in Balák in Bileám sta na vsakem oltarju darovala bikca in ovna.
Kwa hiyo Balaki akafanya kama Balaamu alivyoomba. Kisha Balaki na Balaamu wakatoa sadaka ya fahari mmoja na kondoo dume mmoja kwa kila madhabahu.
3 Bileám je rekel Baláku: »Stoj pri svoji žgalni daritvi, jaz pa bom šel. Morda bo prišel Gospod, da me sreča in karkoli mi pokaže, ti bom povedal.« In odšel je na visok kraj.
Ndipo Balaamu alipomwamiba Balaki, “Simama kwenye sadaka yako ya kuteketezwa na mimi nitaenda. Labda BWANA atakuja kukutana na mimi. Chochote atakachoniambia nitakuambia.” Kwa hiyo akaenda juu ya mlima usiokuwa na miti.
4 Bog je srečal Bileáma in ta mu je rekel: »Pripravil sem sedem oltarjev in na vsakem oltarju sem daroval bikca in ovna.«
Wakati bado akiwa juu ya mlima. Mungu akakutana naye, na Balaamu akamwambia, “Nimejenga madhabahu saba, na nimetoa sadaka ya fahari na kondoo dume kwa kila madhabahu.”
5 Gospod je v Bileámova usta položil besedo ter rekel: »Vrni se k Baláku in tako boš govoril.«
BWANA akaweka ujumbe kwenye kinywa cha Baalamu akasema, “Rudi kwa Balaki ukamwambie.”
6 Vrnil se je k njemu in glej, ta je stal poleg svoje žgalne daritve, on in vsi Moábovi princi.
Kwa hiyo Balaamu akarudi kwa Balaki aliyekuwa amesimama karibu na sadaka yake ya kuteketezwa, na viongozi wote wa Moabu walikuwa pamoja naye.
7 Vzel je njegovo prispodobo ter rekel: »Moábski kralj Balák me je privedel iz Aráma, iz vzhodnih gora, rekoč: ›Pridi, prekolni mi Jakoba in pridi izzivat Izraela.‹
Ndipo Balaamu alipoanza kunena unabii wake akisema, “Balaki amenileta kutoka Aramu, Mfalme wa Moabu kutoka katika milima ya mashariki, 'Njoo, nilaanie Yakobo kwa ajili yangu,' alisema, 'Njoo umtie unajisi Israeli,'
8 Kako naj prekolnem, kogar Bog ni preklel? Kako naj izzivam, kogar Gospod ni izzival?
Nawezaje kuwalaani wale ambao Mungu hajawalaani? Nawezaje kuwapinga wale ambao Mungu hawapingi?
9 Kajti od vrha skal ga vidim in od hribov ga gledam. Glej, ljudstvo bo prebivalo samo in ne bo šteto med narode.
Kwa kuwa kutoka juu ya miamba Ninamwona; kutoka kwenye milima ninamtazama. Kuna watu wanaoishi pekee yao na hawajioni wenyewe kama ni taifa la kawaida.
10 Kdo lahko prešteje Jakobov prah in število četrtine Izraela? Naj umrem smrt pravičnega in naj bo moj zadnji konec podoben njegovemu!«
Nani awezaye kuyahesabu mavumbi ya Yakobo au kuhesabu hata robo ya Israeli? Naomba nife kifo cha mtu mwenye haki, na mwisho wa maisha yangu uwe kama wake!”
11 Balák pa je rekel Bileámu: »Kaj si mi storil? Vzel sem te, da prekolneš moje sovražnike in glej, ti si jih vse skupaj blagoslovil.«
Balaki akamwambia Balaamu, “Umenifanyia nini? Nilikuleta ili uwalaani maadui wangu, lakini ona, umewabariki,”
12 Ta je odgovoril in rekel: »Mar ne morem paziti, da govorim to, kar je Gospod položil v moja usta?«
Balaamu akajibu akasema, “Kwa nini nisiwe mwangalifu kusema kile ambacho BWANA anaweka kinywani mwangu?”
13 Balák mu je rekel: »Pridi, prosim te, z menoj na drug kraj, od koder jih lahko vidiš. Videl boš le njihov skrajni del, ne boš pa videl vseh, in od tam mi jih prekolni.«
Basi Balaki akamwambia, “Hebu uje nami kwenye eneo jingine ili uwaone. Utakaowaona ni wale wa karibu tu, huwezi kuwaona wote. Huko sasa unaweza kunilaania hawa watu.”
14 Privedel ga je na polje Zofim, k vrhu Pisge in zgradil sedem oltarjev in na vsakem oltarju daroval bikca in ovna.
Kwa hiyo akampeleka Balaamu kwenye shamba la Zofimu, lililo juu ya Mlima Pisiga, na kule akajenga madhabau zingine saba. Akatoa sadaka ya fahari mmoja na kondoo dume kwa kila madhabahu.
15 Baláku je rekel: »Stoj tukaj pri svoji žgalni daritvi, medtem ko tam srečam Gospoda.«
Kisha Balaamu akamwambia Balaki, “Simama hapa karibu na sadaka zako, wakati mimi naenda kukutana na BWANA kule.”
16 Gospod je srečal Bileáma in v njegova usta položil besedo ter rekel: »Ponovno pojdi k Baláku in tako povej.«
Kwa hiyo BWANA akakutana na Balaamu na kumwekea ujumbe kinywani mwake. Alimwambia, “Rudi kwa Balaki ukamwambie huu ujumbe toka kwangu.”
17 Ko je prišel k njemu, glej, je ta stal pri svoji žgalni daritvi in princi Moába z njim. In Balák mu je rekel: »Kaj je Gospod govoril?«
Balaamu akamrudia, na tazama, alikuwa amesimama karibu na sadaka zake za kuteketezwa, na vionigozi wa Moabu walikuwa pamoja naye. Balaki akamwuliza, “BWANA amekwambiaje?”
18 Ta je vzel njegovo prispodobo ter rekel: »Vstani, Balák in poslušaj; prisluhni mi, ti, Cipórjev sin.
Balaamu akaanza kutoa unabii. Akasema, “Inuka, Balaki na usikilize. Nisikilize mimi wewe mwana wa Zippori.
19 Bog ni človek, da bi lagal; niti človeški sin, da bi se moral kesati. Je rekel in tega ne bi storil? Je govoril in ali tega ne bi dobro naredil?
Mungu siyo mtu, kwamba umdanganye, au mwanadamu awezaye kubadili mawazo. Je, alishawahi kuahidi kitu pasipo kukitekeleza? Je, alishawahi kusema kuwa atafanya kitu bila kufanya kama alivyosema?
20 Glej, prejel sem zapoved, da blagoslovim in on je blagoslovil in tega ne morem razveljaviti.
Tazama, Mimi nimeamriwa kuwabariki. Mungu ametoa baraka, nami siwezi kuibadilisha.
21 Ni zagledal krivičnosti v Jakobu niti ni videl perverznosti v Izraelu. Gospod, njegov Bog, je z njim in krik kralja je med njimi.
Hajawahi kuona magumu katika Yakobo au tabu katika Israeli. BWANA Mungu wao yuko pamoja nao, na kelele za wafalme wao ziko pamoja nao.
22 Bog jih je privedel iz Egipta; moč ima, kakor bi bila moč od samoroga.
Mungu aliwatoa Misri kwa nguvu kama za nyati.
23 Zagotovo tam ni izrekanja uroka zoper Jakoba niti tam ni nobenega vedeževanja zoper Izraela. Glede na ta čas bo to rečeno o Jakobu in o Izraelu; ›Kaj je Bog storil!‹
Hakuna uganga utakaofanikiwa dhidi ya Yakobo, na hakuna uchawi utakaomwumiza Israeli. Badala yake, itasemwa juu ya Yakobo na Israeli, 'Tazama kile ambacho Mungu amefanya!'
24 Glej, ljudstvo bo vstalo kakor velik lev in se dvignilo kakor mlad lev. On se ne bo ulegel, dokler ne jé od plena in ne pije krvi umorjenega.«
Tazama, watu wanainuka kama simba jike, kama vile simba ainukavyo na kuvamia. Halali chini mpaka ale windo lake na kunywa damu ya windo lake,”
25 Balák je rekel Bileámu: »Niti jih sploh ne preklinjaj niti jih sploh ne blagoslavljaj.«
Kisha Balaki akamwambia Balaamu, “Kamwe usiwalaani wala kuwabariki.”
26 Toda Bileám je odgovoril in rekel Baláku: »Mar ti nisem rekel, rekoč: ›Vse, kar Gospod govori, to moram storiti?‹«
Lakini Balaamu akamjibu Balaki, “Sijakuambia kuwa nitasema yote ambayo BWANA ananiambia kusema?
27 Balák je rekel Bileámu: »Pridi, prosim te, privedel te bom na drug kraj. Morda bo to ugajalo Bogu, da mi jih boš od tam preklel.«
Balaki akamwambia Balaamu, “Njoo sasa, Nami nitakupeleka mahali pengine. Labda kule itampendeza Mungu kunilaania hawa hawa watu.”
28 In Balák je privedel Bileáma na vrh Peórja, ki gleda proti Ješimonu.
Kwa hiyo Balaki akampeleka Balaamu juu ya Mlima Peori, ambao unalitazama chini lile jangwa,
29 Bileám je rekel Baláku: »Tukaj mi zgradi sedem oltarjev in tukaj mi pripravi sedem bikcev in sedem ovnov.«
Balaamu akamwambia Balaki, “Nijengee madhabahu saba hapa na uniandalie mafahari saba na kondoo duume saba.
30 Balák je storil kakor je Bileám rekel in na vsakem oltarju daroval bikca in ovna.
“Kwa hiyo Balaki akafanya kama alivyoambiwa; akatoa sadaka ya fahari na kondoo mume kwenye kila madhabahu.