< Mihej 3 >

1 Rekel sem: »Poslušajte, prosim vas, oh Jakobovi poglavarji in vi princi Izraelove hiše: › Mar ni to za vas, da poznate sodbo?‹
Kisha nikasema, “Sikilizeni enyi viongozi wa Yakobo, enyi watawala wa nyumba ya Israeli. Je, hampaswi kujua hukumu,
2 Ki sovražite dobro in ljubite zlo, ki njihovo kožo trgate iz njih in njihovo meso iz njihovih kosti,
ninyi mnaochukia mema na kupenda maovu; ninyi mnaowachuna watu wangu ngozi na kuondoa nyama kwenye mifupa yao;
3 ki tudi jeste meso mojega ljudstva in odirate njihovo kožo iz njih; in lomijo njihove kosti in jih sekajo na koščke, kakor za lonec in kakor meso znotraj kotla.
ninyi mnaokula nyama ya watu wangu, mnaowachuna ngozi na kuvunja mifupa yao vipande vipande; mnaowakatakata kama nyama ya kuwekwa kwenye sufuria na kama nyama ya kuwekwa kwenye chungu?”
4 Potem bodo klicali h Gospodu, toda ne bo jih slišal. Ob tistem času bo celo svoj obraz skril pred njimi, kakor so se oni slabo obnašali v svojih ravnanjih.
Kisha watamlilia Bwana, lakini hatawajibu. Wakati huo atawaficha uso wake kwa sababu ya uovu waliotenda.
5 Tako govori Gospod glede prerokov, ki mojemu ljudstvu povzročajo, da se moti, ki grizejo s svojimi zobmi in kličejo: ›Mir; ‹ in kdor ne daje v njihova usta, pripravljajo celo vojno zoper njega.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kuhusu manabii wanaowapotosha watu wangu, mtu akiwalisha, wanatangaza ‘amani’; kama hakufanya hivyo, wanaandaa kupigana vita dhidi yake.
6 Zato bo nad vami noč, da ne boste imeli videnja; in ta vam bo temna, da ne boste vedeževali; in sonce bo zašlo nad preroki in dan bo otemnel nad njimi.
Kwa hiyo usiku utawajieni, msiweze kuwa na maono, na giza, msiweze kubashiri. Jua litawachwea manabii hao, nao mchana utakuwa giza kwao.
7 Takrat bodo vidci osramočeni in vedeževalci zbegani. Da, vsi bodo pokrivali svoje ustnice, kajti tam ni odgovora od Boga.
Waonaji wataaibika na waaguzi watafedheheka. Wote watafunika nyuso zao kwa sababu hakuna jibu litokalo kwa Mungu.”
8 Toda resnično, jaz sem po Gospodovem duhu poln oblasti, sodbe in moči, da Jakobu razglasim njegov prestopek in Izraelu njegov greh.
Lakini kuhusu mimi, nimejazwa nguvu, nimejazwa Roho wa Bwana, haki na uweza, kumtangazia Yakobo kosa lake, na Israeli dhambi yake.
9 Poslušajte to, prosim vas, vi poglavarji Jakobove hiše in princi Izraelove hiše, ki se vam gnusi sodba in izkrivljate vso pravico.
Sikieni hili, enyi viongozi wa nyumba ya Yakobo, enyi watawala wa nyumba ya Israeli, mnaodharau haki na kupotosha kila lililo sawa;
10 Sion gradijo s krvjo in Jeruzalem s krivičnostjo.
mnaojenga Sayuni kwa kumwaga damu na Yerusalemu kwa uovu.
11 Njihovi poglavarji sodijo zaradi nagrade in njihovi duhovniki učijo zaradi plačila in preroki vedežujejo zaradi denarja. Vendar ali se bodo naslonili na Gospoda in rekli: › Mar ni Gospod med nami? Nobeno zlo ne more priti nad nas.‹
Viongozi wake wanahukumu kwa rushwa, na makuhani wake wanafundisha kwa malipo, nao manabii wake wanatabiri kwa fedha. Hata hivyo wanamwegemea Bwana na kusema, “Je, Bwana si yumo miongoni mwetu? Hakuna maafa yatakayotupata.”
12 Zato bo zaradi vas Sion preoran kakor polje in Jeruzalem bo spremenjen v razvaline in gore [te] hiše kakor visoki kraji gozda.«
Kwa hiyo kwa sababu yenu, Sayuni italimwa kama shamba, Yerusalemu itakuwa lundo la kokoto, na kilima cha Hekalu kitakuwa kichuguu kilichofunikwa na vichaka.

< Mihej 3 >