< Matej 9 >

1 In vstopil je na ladjo in se peljal čez ter prišel v svoje lastno mesto.
Yesu akaingia kwenye chombo, akavuka na kufika katika mji wa kwao.
2 In glej, k njemu so prinesli moža, bolnega zaradi paralize, ki je ležal na postelji. Ko pa je Jezus videl njihovo vero, je rekel bolnemu zaradi paralize: »Sin, bodi dobre volje, tvoji grehi so ti odpuščeni.«
Wakati huo huo wakamletea mtu aliyepooza, akiwa amelazwa kwenye mkeka. Yesu alipoiona imani yao, alimwambia yule mtu aliyepooza, “Mwanangu, jipe moyo mkuu. Dhambi zako zimesamehewa.”
3 In glej, nekateri izmed pisarjev so v sebi govorili: »Ta človek preklinja.«
Kwa ajili ya jambo hili, baadhi ya walimu wa sheria wakasema mioyoni mwao, “Huyu mtu anakufuru!”
4 Ker pa je Jezus poznal njihove misli, je rekel: »Zakaj v svojih srcih razmišljate hudobno?
Lakini Yesu akiyafahamu mawazo yao, akawaambia, “Kwa nini mnawaza maovu mioyoni mwenu?
5 Kajti ali je lažje reči: ›Tvoji grehi so ti odpuščeni‹ ali reči: ›Vstani in hôdi?‹
Je, ni lipi lililo rahisi zaidi: kusema, ‘Umesamehewa dhambi zako,’ au kusema, ‘Inuka, uende’?
6 Toda da boste lahko vedeli, da ima Sin človekov na zemlji oblast odpuščati grehe, « (tedaj reče bolnemu zaradi paralize), »vstani, vzemi svojo posteljo in pojdi v svojo hišo.«
Lakini, ili mpate kujua kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani kusamehe dhambi…” Ndipo akamwambia yule aliyepooza, “Inuka, chukua mkeka wako, uende nyumbani kwako.”
7 In ta je vstal in odšel v svojo hišo.
Yule mtu akasimama, akaenda nyumbani kwake.
8 Toda ko so množice to videle, so se čudile in slavile Boga, ki je ljudem dal takšno oblast.
Makutano walipoyaona haya, wakajawa na hofu ya Mungu, wakamtukuza Mungu ambaye alikuwa ametoa mamlaka kama haya kwa wanadamu.
9 In ko je Jezus šel naprej od tam, je zagledal moža, imenovanega Matej, ki je sedel pri kraju plačevanja davkov in mu rekel: »Sledi mi.« In ta je vstal ter mu sledil.
Yesu alipokuwa akienda kutoka huko, alimwona mtu mmoja jina lake Mathayo akiwa ameketi forodhani mahali pa kutoza ushuru. Yesu akamwambia, “Nifuate.” Mathayo akaondoka, akamfuata.
10 In pripetilo se je, da ko je Jezus v hiši sedel pri obedu, glej, je prišlo mnogo davkarjev in grešnikov ter sédlo z njim in njegovimi učenci.
Yesu alipokuwa akila chakula ndani ya nyumba ya Mathayo, watoza ushuru wengi na “wenye dhambi” wakaja kula pamoja naye na wanafunzi wake.
11 In ko so farizeji to videli, so njegovim učencem rekli: »Zakaj vaš Učitelj jé z davkarji in grešniki?«
Mafarisayo walipoona mambo haya, wakawauliza wanafunzi wake, “Kwa nini Mwalimu wenu anakula pamoja na watoza ushuru na ‘wenye dhambi’?”
12 Toda ko je Jezus to zaslišal, jim je rekel: »Tisti, ki so zdravi, ne potrebujejo zdravnika, temveč tisti, ki so bolni.
Lakini Yesu aliposikia hayo, akawaambia, “Watu wenye afya hawahitaji tabibu, lakini wale walio wagonjwa ndio wanaohitaji tabibu.
13 Toda pojdite in se naučite, kaj pomeni to: ›Usmiljenje hočem imeti, ne pa žrtve, kajti nisem prišel, da kličem pravične, temveč grešnike h kesanju.‹«
Nendeni mkajifunze maana ya maneno haya: ‘Nataka rehema, wala si dhabihu.’ Kwa maana sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi.”
14 Tedaj so k njemu prišli Janezovi učenci, rekoč: »Zakaj se mi in farizeji često postimo, tvoji učenci pa se ne postijo?«
Wanafunzi wa Yohana Mbatizaji wakaja na kumuuliza Yesu, “Imekuwaje kwamba sisi na Mafarisayo tunafunga, lakini wanafunzi wako hawafungi?”
15 Jezus jim je rekel: »Ali lahko otroci svatovske sobe žalujejo, dokler je z njimi ženin? Toda prišli bodo dnevi, ko bo ženin odvzet od njih in tedaj se bodo postili.
Yesu akawajibu, “Wageni wa bwana arusi wawezaje kuomboleza wakati angali pamoja nao? Wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kwao. Hapo ndipo watakapofunga.
16 Nihče ne polaga koščka novega oblačila na staro obleko, kajti to, kar je vstavljeno, da jo zapolni, trga iz obleke in nastane hujša raztrganina.
“Hakuna mtu anayeshonea kiraka kipya kwenye nguo iliyochakaa, kwa maana kile kiraka kitachanika kutoka kwenye hiyo nguo, nayo hiyo nguo itachanika zaidi.
17 Niti ljudje novega vina ne dajejo v stare mehove. Sicer mehovi počijo in vino izteče ven in mehovi propadejo; temveč novo vino vlivajo v nove mehove in je oboje ohranjeno.«
Wala watu hawaweki divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Kama wakifanya hivyo, viriba vitapasuka nayo divai itamwagika, navyo viriba vitaharibika. Lakini divai mpya huwekwa kwenye viriba vipya, na hivyo divai na viriba huwa salama.”
18 Medtem ko jim je govoril vse te besede, glej, je prišel nek vladar in ga oboževal, rekoč: »Moja hči je pravkar umrla, toda pridi in položi nanjo svojo roko in bo živela.«
Yesu alipokuwa akiwaambia mambo haya, mara akaingia kiongozi wa sinagogi akapiga magoti mbele yake, akamwambia, “Binti yangu amekufa sasa hivi. Lakini njoo uweke mkono wako juu yake, naye atakuwa hai.”
19 In Jezus je vstal in mu sledil in tako so storili tudi njegovi učenci.
Yesu akaondoka akafuatana naye, nao wanafunzi wake pia wakaandamana naye.
20 In glej, ženska, ki je bila dvanajst let bolna s težavo krvi, je prišla za njim ter se dotaknila obšiva njegove obleke,
Wakati huo huo, mwanamke mmoja, ambaye alikuwa na ugonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili, akaja nyuma ya Yesu, akagusa upindo wa vazi lake,
21 kajti v sebi je rekla: »Če se lahko samo dotaknem njegove obleke, bom postala zdrava.«
kwa maana alisema moyoni mwake, “Kama nikigusa tu vazi lake, nitaponywa.”
22 Toda Jezus se je obrnil in ko jo je zagledal, je rekel: »Hči, bodi dobro potolažena, tvoja vera te je naredila zdravo.« In ženska je bila od te ure zdrava.
Yesu akageuka, naye alipomwona akamwambia, “Binti, jipe moyo mkuu, imani yako imekuponya.” Naye yule mwanamke akapona kuanzia saa ile ile.
23 Ko je Jezus prišel v vladarjevo hišo in videl flavtiste in množico, ki je delala hrup,
Yesu alipofika nyumbani kwa yule kiongozi wa sinagogi na kuwaona waombolezaji wakipiga filimbi za maombolezo na watu wengi wakipiga kelele,
24 jim je rekel: »Dajte prostor, kajti deklica ni mrtva, temveč spi.« Oni pa so se mu smejali do norčevanja.
akawaambia, “Ondokeni! Kwa maana binti huyu hakufa, bali amelala.” Wakamcheka kwa dhihaka.
25 Toda ko je bila množica porinjena ven, je vstopil ter jo prijel za roko in deklica je vstala.
Lakini watu walipokwisha kutolewa nje, akaingia mle ndani na kumshika yule binti mkono, naye akaamka.
26 In slôves o tem je šel daleč po vsej tej deželi.
Habari hizi zikaenea katika maeneo yale yote.
27 In ko je Jezus odšel od tam, sta mu sledila dva slepa človeka, ki sta vpila in govorila: » Ti, Davidov Sin, usmili se naju.«
Yesu alipokuwa akiondoka mahali pale, vipofu wawili wakamfuata wakipiga kelele kwa nguvu na kusema, “Mwana wa Daudi, tuhurumie!”
28 In ko je prišel v hišo, sta k njemu prišla slepa človeka in Jezus jima reče: »Ali verujeta, da sem zmožen to storiti?« Rekla sta mu: »Da, Gospod.«
Alipoingia mle nyumbani wale vipofu wakamjia. Naye Yesu akawauliza, “Mnaamini kwamba ninaweza kufanya jambo hili?” Wakamjibu, “Ndiyo, Bwana.”
29 Tedaj se je dotaknil njunih oči, rekoč: »Naj se vama zgodi glede na vajino vero.«
Ndipo Yesu akagusa macho yao na kusema, “Iwe kwenu sawasawa na imani yenu.”
30 In njune oči so bile odprte in Jezus jima je strogo naročil, rekoč: »Glejta, da tega nihče ne izve.«
Macho yao yakafunguka. Yesu akawaonya vikali, akisema, “Angalieni mtu yeyote asijue kuhusu jambo hili.”
31 Toda ko sta onadva odšla, sta v vsej tej deželi povsod razširila njegov slôves.
Lakini wao wakaenda na kueneza habari zake katika eneo lile lote.
32 Ko sta odšla ven, glej, so k njemu prinesli nemega moža, obsedenega s hudičem.
Walipokuwa wanatoka, mtu mmoja aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu na ambaye hakuweza kuongea aliletwa kwa Yesu.
33 In ko je bil hudič izgnan, je nemi spregovoril in množice so se čudile, rekoč: »Nikoli ni bilo tega videti v Izraelu.«
Yule pepo mchafu alipotolewa, yule mtu aliyekuwa bubu akaongea. Ule umati wa watu ukastaajabu na kusema, “Jambo kama hili kamwe halijapata kuonekana katika Israeli.”
34 Toda farizeji so rekli: »Hudiče izganja s pomočjo princa hudičev.«
Lakini Mafarisayo wakasema, “Huyo anatoa pepo wachafu kwa uwezo wa mkuu wa pepo wachafu.”
35 In Jezus je hodil naokrog po vseh mestih in vaseh in učil v njihovih sinagogah ter oznanjal evangelij kraljestva in med ljudmi ozdravljal vsako slabost in vsako bolezen.
Yesu akazunguka katika miji yote na vijiji vyote, akifundisha katika masinagogi yao, akihubiri habari njema za Ufalme, na akiponya kila ugonjwa na kila aina ya maradhi.
36 Toda ko je videl množice, je bil prevzet s sočutjem do njih, ker so oslabeli in so bili razkropljeni naokoli kakor ovce brez pastirja.
Alipoona makutano, aliwahurumia kwa sababu walikuwa wanasumbuka bila msaada, kama kondoo wasiokuwa na mchungaji.
37 Tedaj reče svojim učencem: »Žetev je resnično obilna, toda delavcev je malo.
Ndipo akawaambia wanafunzi wake, “Mavuno ni mengi lakini watendakazi ni wachache.
38 Prosite torej Gospoda žetve, da bo poslal delavce na svojo žetev.«
Kwa hiyo mwombeni Bwana wa mavuno, ili apeleke watendakazi katika shamba lake la mavuno.”

< Matej 9 >