< Matej 6 >

1 »Pazite se, da svoje miloščine ne izkazujete pred ljudmi, da bi jo le-ti videli, sicer nimate nobene nagrade od svojega Očeta, ki je v nebesih.
“Angalieni msitende wema wenu mbele ya watu ili wawaone. Kwa maana mkifanya hivyo, hamna thawabu kutoka kwa Baba yenu aliye mbinguni.
2 Zato kadar daješ svojo miloščino, ne trobi pred seboj, kakor počno hinavci v sinagogah in na ulicah, da bi lahko imeli slavo od ljudi. Resnično, povem vam: ›Imajo svojo nagrado.‹
“Hivyo mnapowapa wahitaji, msipige panda mbele yenu kama wafanyavyo wanafiki katika masinagogi na mitaani, ili wasifiwe na watu. Amin nawaambia wao wamekwisha kupokea thawabu yao.
3 Toda kadar ti daješ miloščino, naj tvoja levica ne ve kaj počne tvoja desnica,
Lakini ninyi mtoapo sadaka, fanyeni kwa siri, hata mkono wako wa kushoto usijue mkono wako wa kuume unachofanya,
4 da bo tvoja miloščina lahko na skrivnem in tvoj Oče, ki sam vidi na skrivnem, te bo javno nagradil.
ili sadaka yako iwe ni siri. Ndipo Baba yako wa mbinguni, yeye aonaye sirini atakupa thawabu kwa wazi.
5 In kadar moliš, ne bodi kakor so hinavci, kajti ti radi molijo, stoječ v sinagogah in na vogalih ulic, da jih ljudje lahko vidijo. Resnično, povem vam: ›Imajo svojo nagrado.‹
“Nanyi msalipo, msiwe kama wanafiki, maana wao hupenda kusali wakiwa wamesimama katika masinagogi na kando ya barabara ili waonekane na watu. Amin nawaambia, wao wamekwisha kupata thawabu yao.
6 Toda ti, kadar ti moliš, vstopi v svojo sobico in ko si zaprl svoja vrata, moli k svojemu Očetu, ki je na skrivnem; in tvoj Oče, ki vidi na skrivnem, te bo nagradil javno.
Lakini wewe unaposali, ingia chumbani mwako, funga mlango na umwombe Baba yako aliye sirini. Naye Baba yako aonaye sirini atakupa thawabu yako.
7 Toda ko molite, ne uporabljajte jalovih ponavljanj, kakor to počno pogani, kajti mislijo, da bodo uslišani zaradi svojega mnogega govorjenja.
Nanyi mnaposali msiseme maneno kama wafanyavyo watu wasiomjua Mungu. Kwa maana wao hudhani kwamba watasikiwa kwa sababu ya wingi wa maneno yao.
8 Ne bodite jim zato podobni, kajti vaš Oče ve, katere stvari potrebujete, preden ga prosite.
Msiwe kama wao, kwa sababu Baba yenu anajua kile mnachohitaji kabla hamjamwomba.
9 Zatorej molíte na ta način: ›Oče naš, ki si v nebesih: ›Posvečuje naj se tvoje ime.
“Hivi basi, ndivyo iwapasavyo kuomba: “‘Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe.
10 Pridi tvoje kraljestvo. Zgôdi se tvoja volja na zemlji, kakor je v nebesih.
Ufalme wako uje. Mapenzi yako yafanyike hapa duniani kama huko mbinguni.
11 Daj nam danes naš vsakdanji kruh.
Utupatie riziki yetu ya kila siku.
12 In odpusti nam naše dolge, kakor mi odpuščamo svojim dolžnikom.
Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tulivyokwisha kuwasamehe wadeni wetu.
13 In ne vôdi nas v skušnjavo, temveč nas osvobodi pred zlom, kajti tvoje je kraljestvo in moč in slava, na veke. Amen.‹
Usitutie majaribuni, bali utuokoe kutoka kwa yule mwovu [kwa kuwa Ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amen].’
14 Kajti če ljudem odpustite njihove prekrške, bo prav tako vaš nebeški Oče odpustil vam.
Kwa kuwa kama mkiwasamehe watu wengine wanapowakosea, Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi pia.
15 Toda če ljudem ne odpustite njihovih prekrškov, tudi vaš Oče ne bo odpustil vaših prekrškov.
Lakini msipowasamehe watu wengine makosa yao, naye Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.
16 Poleg tega, kadar se postite, ne bodite kakor hinavci, potrtega obličja; kajti kazijo svoje obraze, da bi bilo ljudem videti, da se postijo. Resnično, povem vam: ›Imajo svojo nagrado.‹
“Mnapofunga, msiwe wenye huzuni kama wafanyavyo wanafiki. Maana wao hukunja nyuso zao ili kuwaonyesha wengine kwamba wamefunga. Amin, amin nawaambia wao wamekwisha kupata thawabu yao kamilifu.
17 Toda kadar se ti postiš, mazili svojo glavo in umij svoj obraz,
Lakini mnapofunga, jipakeni mafuta kichwani na kunawa nyuso zenu
18 da ne bo videti ljudem, da se postiš, temveč tvojemu Očetu, ki je na skrivnem, in tvoj Oče, ki vidi na skrivnem, te bo nagradil javno.
ili kufunga kwenu kusionekane na watu wengine ila Baba yenu aketiye mahali pa siri; naye Baba yenu aonaye sirini atawapa thawabu yenu kwa wazi.
19 Ne shranjujte si zakladov na zemlji, kjer molj in rja delata razkroj in kjer tatovi vlamljajo in kradejo,
“Msijiwekee hazina duniani, mahali ambapo nondo na kutu huharibu, nao wevi huvunja na kuiba.
20 temveč si zase shranjujte zaklade v nebesih, kjer niti molj niti rja ne delata razkroja in kjer tatovi ne vlamljajo niti ne kradejo,
Lakini jiwekeeni hazina mbinguni, mahali ambapo nondo na kutu haviharibu, wala wevi hawavunji na kuiba.
21 kajti kjer je tvoj zaklad, tam bo tudi tvoje srce.
Kwa sababu mahali hazina yako ilipo, hapo ndipo pia moyo wako utakapokuwa.
22 Svetloba telesa je oko; če je torej tvoje oko enovito, bo tvoje celotno telo polno svetlobe.
“Jicho ni taa ya mwili. Kama jicho lako ni nyofu, mwili wako wote utajaa nuru.
23 Toda če bo tvoje oko hudobno, bo tvoje celotno telo polno teme. Če bo torej svetloba, ki je v tebi, tema, kako velika je ta tema!
Lakini kama jicho lako ni ovu, mwili wako wote utajawa na giza. Kwa hiyo basi, kama nuru iliyomo ndani yako ni giza, hilo ni giza kuu namna gani!
24 Nihče ne more služiti dvema gospodarjema; kajti ali bo enega sovražil in drugega ljubil, ali pa se bo držal k enemu in preziral drugega. Ne morete služiti Bogu in mamonu.
“Hakuna mtu awezaye kuwatumikia mabwana wawili. Kwa kuwa atamchukia huyu na kumpenda yule mwingine, au atashikamana sana na huyu na kumdharau yule mwingine. Hamwezi kumtumikia Mungu pamoja na Mali.
25 Zatorej vam pravim: ›Ne vznemirjajte se in ne skrbite glede svojega življenja, kaj boste jedli ali kaj boste pili niti za svoje telo, kaj boste oblekli. Kaj ni življenje več kot hrana in telo več kot oblačilo?
“Kwa hiyo nawaambia, msisumbukie maisha yenu kwamba mtakula nini au mtakunywa nini; au msumbukie miili yenu kwamba mtavaa nini. Je, maisha si zaidi ya chakula, na mwili zaidi ya mavazi?
26 Poglejte perjad neba, kajti ne seje niti ne žanje niti ne zbira v skednje, vendar jih vaš nebeški Oče hrani. Ali niste mnogo boljši kakor one?
Waangalieni ndege wa angani; wao hawapandi wala hawavuni au kuweka ghalani, lakini Baba yenu wa mbinguni huwalisha. Je, ninyi si wa thamani zaidi kuliko hao ndege?
27 Kdo izmed vas lahko z vznemirjanjem in skrbmi svoji postavi doda en komolec?
Ni nani miongoni mwenu ambaye kwa kujitaabisha kwake anaweza kujiongezea hata saa moja zaidi katika maisha yake?
28 In zakaj se vznemirjate in skrbite za oblačilo? Preudarite o lilijah travnika, kako rastejo; ne garajo niti ne predejo.‹
“Nanyi kwa nini mnajitaabisha kwa ajili ya mavazi? Fikirini maua ya shambani yameavyo. Hayafanyi kazi wala hayafumi.
29 In vendar vam povem: ›Da celó Salomon, v vsej svoji slavi, ni bil oblečen tako kakor ena izmed teh.‹
Lakini nawaambia, hata Solomoni katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo ya hayo maua.
30 Zatorej, če Bog tako oblači travo polja, ki danes je, jutri pa je vržena v peč, ali ne bo mnogo bolj oblačil vas, oh vi, maloverni?
Basi ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya shambani, ambayo leo yapo na kesho yanatupwa motoni, je, hatawavika ninyi vizuri zaidi, enyi wa imani haba?
31 Zato se ne vznemirjate in ne skrbite, rekoč: ›Kaj bomo jedli?‹ ali: ›Kaj bomo pili?‹ ali: ›S čim bomo oblečeni?‹
Kwa hiyo msiwe na wasiwasi, mkisema, ‘Tutakula nini?’ au ‘Tutakunywa nini?’ au ‘Tutavaa nini?’
32 (Kajti za vsemi temi stvarmi povprašujejo pogani), kajti vaš nebeški Oče ve, da potrebujete vse te stvari.
Watu wasiomjua Mungu ndio wanaoshindania hayo, lakini Baba yenu wa mbinguni anafahamu kuwa mnahitaji haya yote.
33 Toda iščite najprej Božje kraljestvo in njegovo pravičnost in vse te stvari vam bodo dodane.
Lakini utafuteni kwanza Ufalme wa Mungu na haki yake, na haya yote atawapa pia.
34 Zato se ne vznemirjate in ne skrbite za jutrišnji dan, kajti jutrišnji dan bo sam poskrbel za stvari. Zadostno je dnevu le tega zlo.«
Kwa hiyo msiwe na wasiwasi kuhusu kesho, kwa sababu kesho itajitaabikia yenyewe. Yatosha kwa siku masumbufu yake.

< Matej 6 >