< Matej 26 >

1 In pripetilo se je, ko je Jezus končal vse te govore, da je rekel svojim učencem:
Yesu alipomaliza kusema hayo yote, akawaambia wanafunzi wake,
2 »Veste, da je čez dva dni praznik pashe in Sin človekov je izdan, da bi bil križan.«
“Kama mnavyojua, baada ya siku mbili itakuwa Pasaka, naye Mwana wa Adamu atasalitiwa ili asulubiwe.”
3 Tedaj so se skupaj zbrali visoki duhovniki in pisarji ter starešine izmed ljudstva, k palači vélikega duhovnika, ki mu je bilo ime Kajfa
Basi viongozi wa makuhani na wazee wa watu wakakusanyika katika jumba la utawala la kuhani mkuu, jina lake Kayafa.
4 in se posvetovali, da bi lahko Jezusa s premetenostjo prijeli ter ga ubili.
Wakafanya shauri ili kumkamata Yesu kwa siri na kumuua.
5 Toda rekli so: »Ne na prazničen dan, da med ljudmi ne bi bilo vstaje.«
Lakini wakasema, “Isiwe wakati wa Sikukuu, kusitokee ghasia miongoni mwa watu.”
6 Torej ko je bil Jezus v Betaniji, v hiši Simona gobavca,
Yesu alikuwa Bethania nyumbani mwa Simoni aliyekuwa na ukoma,
7 je prišla k njemu ženska, ki je imela alabastrno škatlo zelo dragocenega mazila in ko je sedel pri mizi, ga je izlila na njegovo glavo.
naye mwanamke mmoja akamjia akiwa na chupa ya marhamu yenye manukato ya thamani kubwa; akayamimina kichwani mwa Yesu alipokuwa ameketi mezani kula chakula.
8 Toda ko so njegovi učenci to videli, so bili ogorčeni, rekoč: »S kakšnim namenom je ta potrata?
Lakini wanafunzi wake walipoona hayo wakakasirika, wakasema, “Upotevu huu wote ni wa nini?
9 Kajti to mazilo bi bilo lahko drago prodano in dano revnim.«
Manukato haya yangeuzwa kwa bei kubwa, na fedha hizo wakapewa maskini.”
10 Ko je Jezus to spoznal, jim je rekel: »Zakaj nadlegujete žensko? Kajti na meni je storila dobro delo.
Yesu, akijua jambo hili, akawaambia, “Mbona mnamsumbua huyu mwanamke? Yeye amenitendea jambo zuri sana.
11 Kajti revne imate vedno s seboj, toda mene nimate vedno.
Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.
12 Ker je to mazilo izlila na moje telo, je to storila za moj pokop.
Alipomiminia haya manukato kwenye mwili wangu, amefanya hivyo ili kuniandaa kwa ajili ya maziko yangu.
13 Resnično, povem vam: ›Kjerkoli se bo ta evangelij oznanjal po vsem svetu, tam se bo tudi to, kar je ta ženska storila, pripovedovalo v spomin nanjo.‹«
Amin, nawaambia, mahali popote ulimwenguni ambapo hii Injili itahubiriwa, jambo hili alilolitenda huyu mwanamke litatajwa pia kwa ukumbusho wake.”
14 Tedaj je eden izmed dvanajsterih, imenovan Juda Iškarijot, odšel k visokim duhovnikom
Kisha mmojawapo wa wale kumi na wawili, aitwaye Yuda Iskariote, alikwenda kwa viongozi wa makuhani
15 in jim rekel: »Kaj mi boste dali in vam ga bom izročil?« In z njim so se sporazumeli za trideset koščkov srebra.
na kuuliza, “Mtanipa nini nikimtia Yesu mikononi mwenu?” Wakamlipa vipande thelathini vya fedha.
16 In od tedaj je iskal priložnost, da ga izda.
Tangu wakati huo Yuda akawa anatafuta wakati uliofaa wa kumsaliti Yesu.
17 Učenci so torej prvi dan [praznika] nekvašenega kruha prišli k Jezusu in mu rekli: »Kje želiš, da ti pripravimo, da boš jedel pashalno jagnje?«
Siku ya kwanza ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, wanafunzi walimjia Yesu wakamuuliza, “Unataka twende wapi ili tukuandalie mahali pa kula Pasaka?”
18 In rekel je: »Pojdite v mesto k temu in temu človeku ter mu recite: ›Učitelj pravi: ›Moj čas je blizu; s svojimi učenci bom v tvoji hiši praznoval pasho.‹«
Akajibu, “Nendeni kwa mtu fulani huko mjini, mkamwambie, ‘Mwalimu asema hivi: Saa yangu imekaribia. Nitaiadhimisha Pasaka pamoja na wanafunzi wangu katika nyumba yako.’”
19 In učenci so storili, kakor jim je Jezus določil; in pripravili so pashalno jagnje.
Hivyo wanafunzi wakafanya kama vile Yesu alivyokuwa amewaelekeza, nao wakaandaa Pasaka.
20 Torej, ko je prišel večer, se je z dvanajsterimi usedel.
Ilipofika jioni, Yesu alikuwa ameketi mezani pamoja na wale wanafunzi wake kumi na wawili.
21 In ko so jedli, je rekel: »Resnično, povem vam, da me bo eden izmed vas izdal.«
Nao walipokuwa wakila, Yesu akasema, “Amin, nawaambia, mmoja wenu atanisaliti.”
22 Bili so silno žalostni in začeli so mu vsak izmed njih govoriti: »Gospod, ali sem jaz?«
Wakahuzunika sana, wakaanza kumuuliza mmoja baada ya mwingine, “Je, ni mimi Bwana?”
23 In odgovoril je ter rekel: »Kdor pomaka svojo roko z menoj v skledo, ta isti me bo izdal.
Yesu akawaambia, “Yule aliyechovya mkono wake katika bakuli pamoja nami ndiye atakayenisaliti.
24 Sin človekov gre, kakor je pisano o njem, toda gorje temu človeku, po katerem je Sin človekov izdan! Dobro bi bilo za tega človeka, če se ne bi rodil.«
Mwana wa Adamu anaenda zake kama vile alivyoandikiwa. Lakini ole wake mtu yule amsalitiye Mwana wa Adamu. Ingekuwa heri kwake mtu huyo kama hangezaliwa!”
25 Potem je Juda, ki ga je izdal, odgovoril in rekel: »Učitelj, ali sem jaz?« Rekel mu je: »Ti si rekel.«
Kisha Yuda, yule mwenye kumsaliti, akasema, “Je, ni mimi Rabi?” Yesu akajibu, “Naam, wewe mwenyewe umesema.”
26 In medtem ko so jedli je Jezus vzel kruh in ga blagoslovil in ga razlomil ter ga dal učencem in rekel: »Vzemite, jejte; to je moje telo.«
Walipokuwa wanakula, Yesu akachukua mkate, akashukuru, akaumega, na kuwapa wanafunzi wake, akisema, “Twaeni, mle; huu ndio mwili wangu.”
27 In vzel je čašo in se zahvalil ter jim jo dal, rekoč: »Pijte iz nje vsi,
Kisha akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, akisema, “Nyweni nyote katika kikombe hiki.
28 kajti to je moja kri nove zaveze, ki je prelita za mnoge v odpuščanje grehov.
Hii ndiyo damu yangu ya Agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.
29 Toda povem vam: ›Odslej ne bom pil od tega sadu vinske trte do tistega dne, ko bom z vami pil novega v kraljestvu svojega Očeta.‹«
Lakini ninawaambia, tangu sasa sitakunywa tena katika uzao huu wa mzabibu, hadi siku ile nitakapounywa mpya pamoja nanyi katika Ufalme wa Baba yangu.”
30 In ko so odpeli hvalnico, so odšli ven na Oljsko goro.
Walipokwisha kuimba wimbo, wakatoka wakaenda Mlima wa Mizeituni.
31 Tedaj jim Jezus reče: »Vsi se boste to noč pohujšali zaradi mene, kajti pisano je: ›Udaril bom pastirja in ovce tropa bodo razkropljene naokoli.‹
Kisha Yesu akawaambia, “Usiku huu, ninyi nyote mtaniacha, kwa maana imeandikwa: “‘Nitampiga mchungaji, nao kondoo wa hilo kundi watatawanyika.’
32 Toda potem, ko bom obujen, bom pred vami šel v Galilejo.«
Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.”
33 Peter je odgovoril in mu rekel: »Čeprav se bodo vsi ljudje pohujšali zaradi tebe, se vendarle jaz nikoli ne bom pohujšal.«
Petro akajibu, “Hata kama wote watakuacha, kamwe mimi sitakuacha.”
34 Jezus mu je rekel: »Resnično, povem ti: ›Da me boš to noč, preden petelin zapoje, trikrat zatajil.‹«
Yesu akamjibu, “Amin, nakuambia, usiku huu, kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
35 Peter mu je rekel: »Čeprav bi moral umreti s teboj, te vendarle ne bom zatajil.« Tudi vsi učenci so enako govorili.
Lakini Petro akasisitiza, “Hata kama itabidi kufa pamoja nawe, sitakukana kamwe.” Nao wanafunzi wale wengine wote wakasema vivyo hivyo.
36 Tedaj pride Jezus z njimi na kraj, imenovan Getsemani in reče učencem: »Sédite tukaj, medtem ko grem in tamle molim.«
Kisha Yesu akaenda pamoja na wanafunzi wake mpaka kwenye bustani iitwayo Gethsemane, akawaambia, “Kaeni hapa, nami niende kule nikaombe.”
37 In s seboj je vzel Petra ter dva Zebedejeva sinova in postajal je žalosten ter zelo potrt.
Akamchukua Petro pamoja na wale wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuhuzunika na kufadhaika.
38 Tedaj jim reče: »Moja duša je silno žalostna, celó do smrti; zadržujte se tukaj in bedite z menoj.«
Kisha Yesu akawaambia, “Moyo wangu umejawa na huzuni kiasi cha kufa. Kaeni hapa na mkeshe pamoja nami.”
39 In odšel je še malce dlje ter padel na svoj obraz in molil, rekoč: »Oh moj Oče, če je to mogoče, naj gre ta čaša mimo mene, vendar ne kakor jaz hočem, temveč kakor hočeš ti.«
Akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akaomba akisema, “Baba yangu, kama inawezekana, kikombe hiki na kiniondokee. Lakini si kama nipendavyo mimi, bali kama upendavyo wewe.”
40 In pride k učencem in jih najde speče ter reče Petru: »Kaj, eno uro niste zmogli bedeti z menoj?
Kisha akarudi kwa wanafunzi wake, akawakuta wamelala. Akamuuliza Petro, “Je, ninyi hamkuweza kukesha pamoja nami hata kwa saa moja?
41 Bedite in molíte, da ne pridete v skušnjavo. Duh je zares voljan, toda meso je šibko.«
Kesheni na mwombe, msije mkaingia majaribuni. Roho iko radhi, lakini mwili ni mdhaifu.”
42 Zopet je, drugič, odšel proč in molil, rekoč: »Oh moj Oče, če ta čaša ne more iti mimo mene, ne da jo izpijem, zgôdi se tvoja volja.«
Akaenda tena mara ya pili na kuomba, “Baba yangu, kama haiwezekani kikombe hiki kiniepuke nisikinywe, basi mapenzi yako yafanyike.”
43 In prišel je ter jih ponovno našel speče, kajti njihove oči so bile težke.
Aliporudi, akawakuta tena wamelala kwa sababu macho yao yalikuwa mazito.
44 In zapustil jih je ter ponovno odšel proč in tretjič molil, govoreč iste besede.
Hivyo akawaacha akaenda zake tena mara ya tatu na kuomba akisema maneno yale yale.
45 Potem pride k svojim učencem in jim reče: »Spite torej in vzemite si [svoj] počitek; glejte, ura je blizu, in Sin človekov je izdan v roke grešnikov.
Kisha akarudi kwa wanafunzi wake, akawaambia, “Bado mmelala na kupumzika? Tazameni, saa imefika ambapo Mwana wa Adamu anasalitiwa na kutiwa mikononi mwa wenye dhambi.
46 Vstanite, pojdimo. Glejte, tisti, ki me izdaja, je blizu.«
Inukeni, twende zetu! Tazameni, msaliti wangu yuaja!”
47 In medtem ko je še govoril, glej, je prišel Juda, eden izmed dvanajsterih in z njim velika množica z meči in palicami, od visokih duhovnikov in starešin izmed ljudstva.
Alipokuwa bado anazungumza, Yuda, mmoja wa wale Kumi na Wawili, akafika. Alikuwa amefuatana na umati mkubwa wa watu wenye panga na marungu, waliokuwa wametumwa na viongozi wa makuhani na wazee wa watu.
48 Torej tisti, ki ga je izdal, jim je dal znamenje, rekoč: »Kogarkoli bom poljubil, ta isti je on; trdno ga primite.«
Basi msaliti alikuwa amewapa hao watu ishara, kwamba: “Yule nitakayembusu ndiye. Mkamateni.”
49 In nemudoma je prišel k Jezusu in rekel: »Pozdravljen, učitelj, « ter ga poljubil.
Mara Yuda akamjia Yesu na kumsalimu, “Salamu, Rabi!” Akambusu.
50 Jezus pa mu je rekel: »Prijatelj, zakaj si prišel?« Tedaj so prišli in na Jezusa položili roke ter ga prijeli.
Yesu akamwambia, “Rafiki, fanya kile ulichokuja kufanya hapa.” Kisha wale watu wakasogea mbele, wakamkamata Yesu.
51 In glej, eden izmed njih, ki je bil z Jezusom, je iztegnil svojo roko ter dvignil svoj meč in udaril služabnika vélikega duhovnika in odbil njegovo uho.
Ghafula mmoja wa wale waliokuwa na Yesu alipoona hivyo, akaushika upanga wake, akauchomoa na kumpiga mtumishi wa kuhani mkuu, akamkata sikio.
52 Tedaj mu je Jezus rekel: »Vtakni svoj meč ponovno na njegovo mesto, kajti vsi tisti, ki primejo za meč, bodo z mečem pokončani.
Ndipo Yesu akamwambia, “Rudisha upanga wako mahali pake, kwa maana wote watumiao upanga watakufa kwa upanga.
53 Ali mislite, da ne morem sedaj moliti k svojemu Očetu in bi mi takoj dal več kot dvanajst legij angelov?
Je, unadhani siwezi kumwomba Baba yangu naye mara moja akaniletea zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika?
54 Toda kako naj se potem izpolnijo pisma, da mora biti tako?«
Lakini je, yale Maandiko yanayotabiri kwamba ni lazima itendeke hivi yatatimiaje?”
55 In v tej isti uri je Jezus rekel množicam: »Ali ste prišli ven kot proti razbojniku, z meči in palicami, da me primete? Dnevno sem sedel z vami ter učil v templju, pa me niste prijeli.
Wakati huo, Yesu akawaambia ule umati wa watu, “Je, mmekuja na panga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyangʼanyi? Siku kwa siku niliketi Hekaluni nikifundisha, mbona hamkunikamata?
56 Toda vse to je bilo storjeno, da se lahko izpolnijo pisma prerokov.« Tedaj so ga vsi učenci zapustili in pobegnili.
Lakini haya yote yametukia ili maandiko ya manabii yapate kutimia.” Ndipo wanafunzi wake wote wakamwacha na kukimbia.
57 Tisti pa, ki so Jezusa zgrabili, so ga odpeljali proč h Kajfu, vélikemu duhovniku, kjer so bili zbrani pisarji in starešine.
Wale waliokuwa wamemkamata Yesu wakampeleka kwa Kayafa, kuhani mkuu, mahali ambapo walimu wa sheria pamoja na wazee walikuwa wamekusanyika.
58 Toda Peter mu je od daleč sledil do palače vélikega duhovnika in vstopil ter sédel s služabniki, da vidi konec.
Lakini Petro akamfuata kwa mbali hadi uani kwa kuhani mkuu. Akaingia ndani, akaketi pamoja na walinzi ili aone litakalotukia.
59 Visoki duhovniki in starešine in ves véliki zbor so torej iskali krivih prič zoper Jezusa, da bi ga usmrtili,
Viongozi wa makuhani na Baraza la Wayahudi lote wakatafuta ushahidi wa uongo dhidi ya Yesu ili wapate kumuua.
60 toda niso našli nobene; da, čeprav je prišlo mnogo krivih prič, vendar niso našli nobene. Na koncu sta prišli dve krivi priči
Lakini hawakupata jambo lolote, ingawa mashahidi wengi wa uongo walijitokeza. Hatimaye wakajitokeza mashahidi wawili wa uongo
61 in rekli sta: »Ta je rekel: ›Zmožen sem uničiti Božji tempelj in ga v treh dneh zgraditi.‹«
na kusema, “Huyu mtu alisema, ‘Ninaweza kulivunja Hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa siku tatu.’”
62 In véliki duhovnik je vstal ter mu rekel: »Nič ne odgovarjaš? Kaj je to, kar ti priči pričujeta zoper tebe?«
Kisha kuhani mkuu akasimama na kumwambia Yesu, “Je, wewe hutajibu? Ni ushahidi gani hawa watu wanauleta dhidi yako?”
63 Toda Jezus je ohranil svoj mir. In véliki duhovnik je odgovoril ter mu rekel: »Zaklinjam te pri živem Bogu, da nam poveš, ali si ti Kristus, Božji Sin.«
Lakini Yesu akakaa kimya. Ndipo kuhani mkuu akamwambia, “Nakuapisha mbele za Mungu aliye hai. Tuambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu.”
64 Jezus mu reče: »Ti si rekel, vendar ti jaz pravim: ›Odslej boste videli Sina človekovega sedeti na desnici moči in prihajati na oblakih neba.‹«
Yesu akajibu, “Wewe umenena. Lakini ninawaambia nyote: Siku za baadaye, mtamwona Mwana wa Adamu akiwa ameketi mkono wa kuume wa Mwenye Nguvu, na akija juu ya mawingu ya mbinguni.”
65 Tedaj je véliki duhovnik raztrgal svoja oblačila, rekoč: »Govoril je bogokletje; imamo kakšno dodatno potrebo po pričah? Glejte, sedaj ste slišali njegovo bogokletje.
Ndipo kuhani mkuu akararua mavazi yake na kusema, “Amekufuru! Tuna haja gani tena ya mashahidi zaidi? Tazama, sasa ninyi mmesikia hayo makufuru.
66 Kaj vi mislite?« Oni pa so odgovorili in rekli: »Kriv je smrti.«
Uamuzi wenu ni gani?” Wakajibu, “Anastahili kufa.”
67 Tedaj so mu pljuvali v njegov obraz in ga klofutali; in drugi so ga udarjali z dlanmi svojih rok,
Kisha wakamtemea mate usoni na wengine wakampiga ngumi. Wengine wakampiga makofi
68 rekoč: »Prerokuj nam, ti Kristus: ›Kdo je tisti, ki te je udaril?‹«
na kusema, “Tutabirie, wewe Kristo! Ni nani aliyekupiga?”
69 Peter je torej sedèl zunaj v palači; in k njemu je prišla gospodična, rekoč: »Tudi ti si bil z Jezusom iz Galileje.«
Wakati huu Petro alikuwa amekaa nje uani. Mtumishi mmoja wa kike akamjia na kumwambia, “Wewe pia ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.”
70 Toda on je pred vsemi njimi zanikal, rekoč: »Ne vem, kaj govoriš.«
Lakini Petro akakana mbele yao wote akisema, “Sijui hilo usemalo.”
71 In ko je odšel ven v preddverje, ga je videla druga služabnica in rekla tem, ki so bili tam: »Ta je bil prav tako z Jezusom Nazarečanom.«
Alipotoka nje kufika kwenye lango, mtumishi mwingine wa kike alimwona, akawaambia watu waliokuwepo, “Huyu mtu alikuwa pamoja na Yesu, Mnazareti.”
72 In ponovno je s prisego zanikal: »Ne poznam tega človeka.«
Akakana tena kwa kiapo akisema, “Mimi simjui huyo!”
73 In čez nekaj časa so prišli k njemu tisti, ki so stali ob strani ter rekli Petru: »Zagotovo si ti eden izmed njih, kajti tvoje narečje te izdaja.«
Baada ya muda mfupi, wale waliokuwa wamesimama pale wakamwendea Petro, wakamwambia, “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana usemi wako ni kama wao.”
74 Tedaj je začel preklinjati in prisegati, rekoč: »Ne poznam [tega] človeka.« In petelin je takoj zapel.
Ndipo Petro akaanza kujilaani na kuwaapia, “Mimi simjui mtu huyo!” Papo hapo jogoo akawika.
75 In Peter se je spomnil Jezusove besede, ki mu jo je rekel: »Preden petelin zapoje, me boš trikrat zatajil.« In odšel je ven ter se bridko zjokal.
Ndipo Petro akakumbuka lile neno Yesu alilokuwa amesema: “Kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.” Naye akaenda nje, akalia kwa majonzi.

< Matej 26 >