< Luka 6 >

1 In pripetilo se je na drugi šabat za prvim, da je šel skozi žitna polja in njegovi učenci so smukali žitno klasje, ga méli v svojih rokah in jedli.
Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano, na wanafunzi wake wakaanza kukwanyua masuke ya ngano, wakaondoa punje zake kwa mikono, wakala.
2 Nekateri izmed farizejev so jim rekli: »Zakaj delate to, kar ni zakonito delati na šabatne dneve?«
Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, “Mbona mnafanya jambo ambalo si halali siku ya Sabato?”
3 Jezus jim odgovori in reče: »Mar niste brali tega, kar je storil David, ko je bil lačen on sam in ti, ki so bili z njim;
Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma jinsi alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?
4 kako je odšel v Božjo hišo in vzel in jedel hlebe navzočnosti in jih dal tudi tistim, ki so bili z njim; kar ni zakonito jésti [nikomur], razen samo duhovnikom?«
Yeye aliingia ndani ya nyumba ya Mungu, akachukua ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu, akala na kuwapa wenzake. Kisheria, ni makuhani tu peke yao ndio walioruhusiwa kula mikate hiyo.”
5 Rekel jim je: »Sin človekov je tudi Gospodar šabata.«
Hivyo akawaambia, “Mwana wa Mtu ni Bwana wa Sabato.”
6 In prav tako se je na še en šabat pripetilo, da je vstopil v sinagogo ter učil, in tam je bil človek, čigar desna roka je bila izsušena.
Siku nyingine ya Sabato, Yesu aliingia katika sunagogi, akafundisha. Mle ndani mlikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
7 In pisarji in farizeji so ga opazovali ali bo ozdravljal na šabatni dan, da bi zoper njega lahko našli obtožbo.
Walimu wa Sheria na Mafarisayo walitaka kupata kisingizio cha kumshtaki Yesu na hivyo wakawa wanangojea waone kama angemponya mtu siku ya Sabato.
8 Toda poznal je njihove misli in rekel možu, ki je imel izsušeno roko: »Vstani in stopi na sredo.« In ta je vstal ter stopil naprej.
Lakini Yesu alijua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Inuka, simama katikati.” Yule mtu akaenda akasimama katikati.
9 Potem jim je Jezus rekel: »Eno stvar vas bom vprašal: ›Ali je na šabatne dneve zakonito delati dobro ali delati zlo? Rešiti življenje ali ga uničiti?‹«
Kisha Yesu akawaambia, “Nawaulizeni, je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuyaangamiza?”
10 In ko je pogledal naokoli po vseh, je rekel možu: »Iztegni svojo roko.« In ta je storil tako in njegova roka je bila v celoti ozdravljena, tako kakor druga.
Baada ya kuwatazama wote waliokuwa pale, akamwambia yule mtu, “Nyosha mkono wako.” Naye akafanya hivyo, na mkono wake ukawa mzima tena.
11 In bili so izpolnjeni z besom in drug z drugim so se posvetovali, kaj bi lahko storili Jezusu.
Lakini wao wakakasirika sana, wakajadiliana jinsi ya kumtendea Yesu maovu.
12 In pripetilo se je v tistih dneh, da je odšel ven na goro, da moli in je vso noč vztrajal v molitvi k Bogu.
Siku moja Yesu alikwenda mlimani kusali, akakesha huko usiku kucha akimwomba Mungu.
13 In ko je bil dan, je k sebi poklical svoje učence in izmed njih jih je izbral dvanajst, ki jih je imenoval tudi apostole:
Kesho yake aliwaita wanafunzi wake, na miongoni mwao akachagua kumi na wawili ambao aliwaita mitume:
14 Simona (ki ga je imenoval tudi Peter) in njegovega brata Andreja, Jakoba in Janeza, Filipa in Bartolomeja,
Simoni (ambaye Yesu alimpa jina Petro) na Andrea ndugu yake, Yakobo na Yohane, Filipo na Bartholomayo,
15 Mateja in Tomaža, Jakoba, Alfejevega sina in Simona, imenovanega Gorečnik,
Mathayo na Thoma, Yakobo wa Alfayo na Simoni (aliyeitwa Zelote),
16 in Juda, Jakobovega brata in Juda Iškarijota, ki je bil tudi izdajalec.
Yuda wa Yakobo na Yuda Iskarioti ambaye baadaye alikuwa msaliti.
17 In z njimi je prišel dol ter stal na ravnem in skupina njegovih učencev ter velika množica ljudi iz vse Judeje in Jeruzalema in pokrajin Tira in Sidóna, ki so prišli, da ga poslušajo in da bi bili ozdravljeni svojih bolezni,
Baada ya kushuka mlimani pamoja na mitume, Yesu alisimama mahali palipokuwa tambarare. Hapo palikuwa na kundi kubwa la wanafunzi wake na umati wa watu waliotoka pande zote za Yudea na Yerusalemu na pwani ya Tiro na Sidoni. Wote walifika kumsikiliza Yesu na kuponywa magonjwa yao.
18 in tisti, ki so bili nadlegovani z nečistimi duhovi in bili so ozdravljeni.
Aliwaponya pia wote waliokuwa wanasumbuliwa na pepo wachafu.
19 In celotna množica si je prizadevala, da bi se ga dotaknila, kajti iz njega je izhajala moč in jih vse ozdravljala.
Watu wote walitaka kumgusa, kwa maana nguvu ilikuwa inatoka ndani yake na kuwaponya wote.
20 In povzdignil je svoje oči na svoje učence ter rekel: »Blagoslovljeni bodite vi ubogi, kajti vaše je Božje kraljestvo.
Yesu akawageukia wanafunzi wake, akasema: “Heri ninyi mlio maskini, maana Ufalme wa Mungu ni wenu.
21 Blagoslovljeni ste vi, ki ste sedaj lačni, kajti nasičeni boste. Blagoslovljeni ste vi, ki sedaj jokate, kajti smejali se boste.
Heri ninyi mnaosikia njaa sasa, maana baadaye mtashiba. Heri ninyi mnaolia sasa, maana baadaye mtacheka kwa furaha.
22 Blagoslovljeni ste, ko vas bodo ljudje sovražili in ko vas bodo oddvojili od svoje družbe in vas bodo grajali in zaradi Sina človekovega vaše ime zavrgli kot hudobno.
“Heri yenu ninyi iwapo watu watawachukia, watawatenga, watawatukana na kuwaharibieni jina kwa ajili ya Mwana wa Mtu!
23 Veselite se na tisti dan in poskakujte od radosti, kajti, glejte, vaša nagrada v nebesih je velika, kajti na podoben način so njihovi očetje delali prerokom.
Wakati hayo yatakapotokea, furahini na kucheza, maana hakika tuzo lenu ni kubwa mbinguni. Kwa maana wazee wao waliwatendea manabii vivyo hivyo.
24 Toda gorje vam, ki ste bogati! Kajti prejeli ste svojo tolažbo.
Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, maana mmekwisha pata faraja yenu.
25 Gorje vam, ki ste siti! Kajti lačni boste. Gorje vam, ki se sedaj smejete! Kajti žalovali boste in jokali.
Ole wenu ninyi mnaoshiba sasa, maana baadaye mtasikia njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka kwa furaha sasa, maana baadaye mtaomboleza na kulia.
26 Gorje vam, ko bodo vsi ljudje o vas lepo govorili! Kajti tako so njihovi očetje delali lažnim prerokom.
Ole wenu ninyi iwapo watu wote wanawasifu, maana wazee wao waliwafanyia manabii wa uongo vivyo hivyo.
27 Toda jaz pravim vam, ki slišite: ›Ljubite svoje sovražnike, delajte dobro tem, ki vas sovražijo,
“Lakini nawaambieni ninyi mnaonisikiliza: wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale wanaowachukieni.
28 blagoslavljajte te, ki vas preklinjajo in molite za tiste, ki vas kruto izkoriščajo.
Watakieni baraka wale wanaowalaani, na waombeeni wale wanaowatendea vibaya.
29 In tistemu, ki te udarja na eno lice, ponudi še drugo; in tistemu, ki odvzema tvoje ogrinjalo, ne prepovej vzeti tudi svojega plašča.
Mtu akikupiga shavu moja mgeuzie na la pili. Mtu akikunyang'anya koti lako mwachie pia shati lako.
30 Vsakemu človeku daj, kar prosi od tebe in od tistega, ki jemlje tvoje dobrine, ne prosi ponovno zanje.
Yeyote anayekuomba mpe, na mtu akikunyang'anya mali yako usimtake akurudishie.
31 In kakor želite, da bi ljudje storili vam, prav tako tudi vi storite njim.
Watendeeni wengine kama mnavyotaka wawatendee ninyi.
32 Kajti če ljubite te, ki ljubijo vas, kakšno hvalo imate? Kajti tudi grešniki ljubijo tiste, ki ljubijo njih.
“Na ikiwa mnawapenda tu wale wanaowapenda ninyi, je, mtapata tuzo gani? Hakuna! Kwa maana hata wenye dhambi huwapenda wale wanaowapenda wao.
33 In če delate dobro tem, ki delajo dobro vam, kakšno hvalo imate? Kajti tudi grešniki celó enako delajo.
Tena, kama mkiwatendea mema wale tu wanaowatendeeni mema, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi hufanya vivyo hivyo!
34 In če posojate tistim, od katerih upate, da prejmete, kakšno hvalo imate? Kajti tudi grešniki posojajo grešnikom, da prejmejo toliko nazaj.
Na kama mnawakopesha wale tu mnaotumaini watawalipeni, je, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi wenzao ili warudishiwe kima kilekile!
35 Toda ljubite svoje sovražnike in delajte dobro in posojajte ter se ničesar ne nadejajte v vrnitev in vaša nagrada bo velika in boste otroci Najvišjega, kajti on je prijazen do nehvaležnih in do hudobnih.
Ila nyinyi wapendeni adui zenu, na kuwatendea mema; kopesheni bila kutazamia malipo, na tuzo lenu litakuwa kubwa, nanyi mtakuwa watoto wa Mungu aliye juu. Kwa maana yeye ni mwema kwa wale wasio na shukrani na walio wabaya.
36 Bodite torej usmiljeni, kakor je tudi vaš Oče usmiljen.
Muwe na huruma kama Baba yenu alivyo na huruma.
37 Ne sodite in ne boste sojeni, ne obsojajte in ne boste obsojeni, odpuščajte in vam bo odpuščeno,
“Msiwahukumu wengine, nanyi hamtahukumiwa; msiwalaumu wengine, nanyi hamtalaumiwa; wasameheni wengine, nanyi mtasamehewa.
38 dajajte in to vam bo dano; dobro mero, potlačeno in skupaj zbrano in čez rob polno vam bodo ljudje dali v vaše naročje. Kajti z enako mero, s katero vi merite, bo tudi vam ponovno odmerjeno.‹
Wapeni wengine wanavyohitaji, nanyi mtapewa. Naam, mtapokea mikononi mwenu kipimo kilichojaa, kikashindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika. Kwa maana kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho ambacho Mungu atatumia kwenu.”
39 In spregovoril jim je prispodobo: ›Mar lahko slepi vodi slepega? Ali ne bosta oba padla v jarek?
Akawaambia mfano huu: “Je, kipofu anaweza kumwongoza kipofu mwenzake? La! Wote wataanguka shimoni.
40 Učenec ni nad svojim učiteljem, toda vsak, kdor je popoln, bo kakor njegov učitelj.
Mwanafunzi hamshindi mwalimu wake, lakini kila mwanafunzi akisha hitimu huwa kama mwalimu wake.
41 In zakaj gledaš drobec, ki je v očesu svojega brata, toda ne zaznavaš bruna, ki je v tvojem lastnem očesu?‹
Unawezaje kukiona kibanzi kilicho katika jicho la mwenzio, usione boriti iliyo katika jicho lako mwenyewe?
42 Ali kako lahko rečeš svojemu bratu: ›Brat, dovoli mi izvleči drobec, ki je v tvojem očesu, ‹ ko sam ne zapaziš bruna, ki je v tvojem lastnem očesu? Ti hinavec, vrzi ven najprej bruno iz svojega lastnega očesa in tedaj boš jasno videl izvleči drobec, ki je v očesu tvojega brata.
Au, unawezaje kumwambia mwenzako, Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi katika jicho lako, na huku huioni boriti iliyoko katika jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe! Toa kwanza boriti iliyoko jichoni mwako, na hivyo utaona sawasawa kiasi cha kuweza kuondoa kibanzi kilicho katika jicho la ndugu yako.
43 Kajti dobro drevo ne prinaša slabega sadu niti slabo drevo ne prinaša dobrega sadu.
“Mti mwema hauzai matunda mabaya, wala mti mbaya hauzai matunda mazuri.
44 Kajti vsako drevo je razpoznano po svojem lastnem sadu. Kajti ljudje fig ne nabirajo s trnja niti z robidovega grma ne nabirajo grozdja.
Watu huutambua mti kutokana na matunda yake. Ni wazi kwamba watu hawachumi tini katika michongoma, wala hawachumi zabibu katika mbigili.
45 Dober človek iz dobrega zaklada svojega srca prinaša to, kar je dobro, hudobnež pa iz zlega zaklada svojega srca prinaša to, kar je zlo, kajti iz obilja srca njegova usta govoré.
Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka katika hazina bora iliyo moyoni mwake; na mtu mbaya hutoa yaliyo mabaya katika hazina mbaya iliyo moyoni mwake, kwa maana mtu huongea kutokana na yale yaliyojaa moyoni mwake.
46 In zakaj me kličete: ›Gospod, Gospod, ‹ pa ne delate stvari, ki jih govorim?
“Mbona mwaniita Bwana, Bwana, na huku hamtimizi yale ninayosema?
47 Kdorkoli pride k meni in posluša moje besede ter jih izpolnjuje, vam bom pokazal, komu je podoben.
Nitawapeni mfano unaofaa kuonyesha alivyo yeyote yule anayekuja kwangu, akasikia maneno yangu na kuyatimiza:
48 Podoben je človeku, ki je gradil hišo in globoko kopál ter položil temelj na skalo. In ko je nastala poplava, je na to hišo silovito udaril vodni tok in je ni mogel omajati, kajti utemeljena je bila na skali.
Huyo anafanana na mtu ajengaye nyumba, ambaye amechimba chini na kuweka msingi wake juu ya mwamba; kukatokea mafuriko ya mto, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, lakini haukuweza kuitikisa, kwa sababu ilikuwa imejengwa imara.
49 Toda kdor posluša, pa ne dela, je podoben človeku, ki je na zemlji zgradil hišo brez temelja, proti kateri je silovito udaril vodni tok in ta je takoj padla in ruševina te hiše je bila velika.«
Lakini yeyote anayesikia maneno yangu lakini asifanye chochote, huyo anafanana na mtu aliyejenga nyumba juu ya udongo, bila msingi. Mafuriko ya mto yakatokea, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, ikaanguka na kuharibika kabisa!”

< Luka 6 >