< 3 Mojzes 25 >

1 Gospod je na gori Sinaj spregovoril Mojzesu, rekoč:
Yahweh akazungumza na Musa kwenye Mlima wa Sinai, akisema,
2 »Govori Izraelovim otrokom in jim reci: ›Ko pridete v deželo, ki sem vam jo dal, potem bo dežela ohranjala šabat Gospodu.
“Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, “Mtakapoingia katika nchi ambayo ninawapa, kisha hiyo nchi lazima ifanywe iwe ya kuishika Sabato kwa ajili ya Yahweh.
3 Šest let boš sejal svoje polje in šest let boš obrezoval svoj vinograd in zbiral njegov sad,
Ni lazima mtapanda mazao yenu kwa miaka sita, na kwa miaka sita mtaikatia matawi mizabibu yenu na kukusanya mazao yake.
4 toda v sedmem letu bo šabatni počitek deželi, šabat za Gospoda. Niti ne boš sejal svojega polja niti obrezal svojega vinograda.
Lakini katika mwaka wa saba, Sabato ya pumziko la utulivu kwa nchi itashikwa, ni Sabato kwa Yahweh. Hamtapanda mashamba yenu wala kuikatia mizabibu yenu matawi yake.
5 Tega, kar raste samo od sebe od tvoje žetve, ne boš požel niti nabiral grozdja iz svoje neobrezane trte, kajti to je za deželo leto počitka.
Hamtasimamia mavuno yoyote ya mazao ya mizabibu iliyojiotesha yenyewe katika mashamba yenu ya mizabibu isiyokatiwa matawi. Huu utakuwa mwaka wa pumziko lenye utulivu kwa ardhi.
6 Šabatni [pridelek] dežele bo zate hrana; zate, za tvojega služabnika, za tvojo služkinjo, za tvojega najetega služabnika in za tvojega tujca, ki začasno biva s teboj
Chochote ardhi isiyofanyiwa kazi itakachotoa wakati wa Sabato ndicho kitakuwa chakula chako. Wewe mwenyewe, watumwa wako wa kiume na wa kike, watumishi wako wa kuajiriwa na wageni wanaoishi pamoja nawe mnaweza kujikusanyia chakula.
7 in ves njegov narast bo hrana za tvojo živino in za živali, ki so na tvoji zemlji.
Na wnyama wako wa kufugwa na wanyama pori waweze kula chochote ardhi itoacho.
8 Štel si boš sedem šabatnih let, sedemkrat sedem let; in obdobje sedmih šabatnih let ti bodi devetinštirideset let.
Ni lazima kwenu kuhesabu Sabato saba za miaka, yaani, saba mara miaka saba, ikifanya jumla ya miaka arobaini na tisa.
9 Potem bo šofar jubileja zadonel na deseti dan sedmega meseca. Na dan sprave boste naredili, da zvok šofarja zadoni po vsej vaši deželi.
Kisha mtapiga sauti ya tarumbeta kila mahali katika siku ya kumi ya mwezi wa saba. Katika Siku ya Upatanisho ni lazima mtapiga tarumbeta katika nchi yenu yote.
10 Posvetili boste petdeseto leto in razglasili svobodo po vsej deželi, vsem njenim prebivalcem. To vam bo jubilej, vi pa se boste vrnili vsak mož k svoji posesti in vrnili se boste vsak mož k svoji družini.
Nanyi mtautenga mwaka wa hamsini kwa ajili ya Yahweh na mtatangaza uhuru katika nchi yote kwa wakazi wote. Kutakuwa na Yubile kwa ajili yenu, ambayo kwayo mali na watumwa ni lazima warejeshwe kwa familia zao.
11 Vam bo to petdeseto leto jubilej. Ne boste niti sejali niti želi tega, kar zraste samo od sebe niti nabirali grozdja v njem od vaše neobrezane trte.
Mwaka wa saba kutakuwa na Yubile kwenu. Hamtapanda wala kusimamia mavuno ya kijioteshacho chenyewe, na kukusanya kichipukacho kwenye mizabibu isiyokatiwa matawi.
12 Kajti to je jubilej; ta vam bo svet. Jedli boste njegov donos iz polja.
Kwa sababu hiyo ni Yubile takatifu kwenu. Nanyi mtakula mazao yanayokua yenyewe kutoka mashambani.
13 V letu tega jubileja se bo vsak človek vrnil k svoji posesti.
Ni lazima muwarejeshe kila mmoja kwenye miliki yake katika mwaka huu wa Yubile.
14 Če kaj prodaš svojemu bližnjemu, ali kaj kupiš iz roke svojega bližnjega, ne boste zatirali drug drugega.
Iwapo utauza ardhi yoyote ya jirani yako au kununua ardhi yake, ni shrti msipunjane au kutendeana kwa hila.
15 Glede na število let po jubileju boš kupil od svojega bližnjega in glede na število let sadov ti bo prodal.
Iwapo unanunua ardhi kutoka kwa jirani yako, zingatia idadi ya miaka na mazao ambayo yaweza kuvunwa mpaka mwaka wa Yubile nyingine. Jirani yako anayeuza ardhi ni lazima aihesabu miaka hiyo pia.
16 Glede na množino let boš povečal njegovo ceno in glede na manjše število let boš zmanjšal njegovo ceno, kajti glede na število let sadov ti jo bo prodal.
Miaka inapoongezeka mpaka Yubile nyingine, ataongeza thamani ya ardhi, na miaka inapokuwa michache kufikia Yubile nyingine atashusha thamani, kwa sababu idadi ya mavuno inahusiana na idadi ya miaka kabla ya Yubile nyingine.
17 Zatorej ne boste zatirali drug drugega, temveč se boš bal svojega Boga, kajti jaz sem Gospod, tvoj Bog.
Msipunjane au kutendeana kwa hila, badala yake, yawapasa kumheshi Yahweh Mungu wenu.
18 Zatorej boste izpolnjevali moje zakone in se držali mojih sodb in jih izvrševali, in v varnosti boste prebivali v deželi.
Kwa hiyo basi, ni lazima muyatii maagiza, kuzitunza sheria zangu na kuzitekeleza. Nanyi mtaishi katika nchi katika usalama.
19 Dežela bo obrodila svoj sad in jedli boste svoje obilje in v njej varno prebivali.
Nayo nchi itawapa mavuno yake, nanyi mtakula matunda yenu na mtaishi humo salama.
20 In če boste rekli: ›Kaj bomo jedli sedmo leto? Glej, ne bomo sejali niti zbrali v našem narastu, ‹
Labda mtasema, Tutakula nini katika mwaka wa saba? Tazama, hatuwezi kupanda wala kukusanya mazao yetu.”
21 potem bom v šestem letu zapovedal nad vami svoj blagoslov in ta bo prinesel sad za tri leta.
Nitaiamru baraaka yangu ije juu yenu katika mwaka wa sita, nayo itatoa mavuno ya kutosha kwa miaka mitatu.
22 Sejali boste osmo leto in še jedli od starih sadov do devetega leta, dokler ne pridejo njeni sadovi, boste jedli iz starih zalog.
Mtapanda katika mwaka wa nane na mtaendelea kula mazao ya miaka iliyopita na kutoka kwenye ghala la chakula. Mpaka mavuno ya mwaka wa tisa yatakapofika, mtaweza kula kutoka kwenye riziki iliyohifadhiwa katika miaka iliyopita
23 Dežela naj ne bo prodana na veke, kajti dežela je moja, kajti vi ste tujci in začasni prebivalci z menoj.
Ardhi haitauzwa kwa mmiliki mpya wa kudumu, kwa sababu ardhi ni mali yangu. Ninyi nyote mu wageni na wakazi wa muda juu ya ardhi yangu.
24 In po vsej deželi svoje posesti boste zagotovili odkupitev za deželo.
Ni lazima muitunze haki ya ukombozi kwa ajili ya ardhi yote mtakayoimiliki; itawapasa kuruhusu ardhi inunuliwe tena na familia ambayo wewe uliinunua hiyo ardhi kutoka kwao.
25 Če tvoj brat postane reven in je prodal nekaj od svoje posesti in če pride katerikoli njegov sorodnik, da to odkupi, potem bo odkupil to, kar je njegov brat prodal.
Iwapo Mwisraeli mwenzako anakuwa masikini na kwa sababu hiyo anauza baadhi ya miliki yake, kisha jamaa yake wa karibu anaweza kuja na kuikomboa hiyo miliki ambayo jamaa yake kaiuza kwako.
26 Če mož nima nikogar, da to odkupi in je sam zmožen to odkupiti,
Iwapo mtu hana jamaa wa kuikomboa mali yake, lakini ikiwa kafanikiwa na anao uwezo wa kuikomboa,
27 potem naj prešteje leta od njegove prodaje in povrne presežek človeku, ki mu jo je prodal, da se on lahko vrne v svojo posest.
kisha atahesabu miaka tangu ardhi hiyo ilipouzwa na kurejesha kwa mtu aliyemuuzia fedha iliyosalia. Naye anaweza kuerejea kwenye miliki yake mwenyewe.
28 Toda če mu on tega ne bo zmožen povrniti, potem bo to, kar je prodal, ostalo v roki tistega, ki je to kupil, do jubilejnega leta. Na jubilej bo odšlo in on se bo vrnil v svojo posest.
Lakini ikiwa hawezi kuirejesha kwake ardhi aliyoiuza, nayo hiyo ardhi aliyoiuza itabaki katika umiliki wa yule aliyeinunua mpaka mwaka wa Yubile. Kwenye mwaka wa Yubile, ardhi itarejeshwa kwa mtu aliyeiuza, naye mmiliki wa asili atarejea kwenye mali yake.
29 Če mož proda hišo za prebivanje v mestu z obzidjem, potem jo lahko odkupi znotraj celotnega leta potem, ko je bila ta prodana. Znotraj polnega leta jo lahko odkupi.
Ikiwa mtu anauza nyumba iliyo kwenye mji uliozungushiwa ukuta, naye anaweza kuinunua tena ndani ya mwaka baada ya kuuzwa. kwa kuwa, kwa mwaka mzima atakuwa na haki ya ukombozi.
30 Če pa ta ne bo odkupljena znotraj časa polnega leta, potem bo hiša, ki je v mestu z obzidjem, utrjena na veke tistemu, ki jo je kupil, skozi vse njegove rodove. Ta v jubileju ne bo odšla.
Kama nyumba hiyo haitakombolewa kabla ya mwaka mzima, ndipo hiyo nyumba iliyoko kwenye mji uliozungushiwa ukuta itakuwa mali ya kudumu ya yule aliyeinunua, katika vizazi vyote vya uzao wake. Nyumba hiyo haitakuwa ya kurejeshwa katika mwaka wa Yubile.
31 Toda vaške hiše, ki naokoli nimajo obzidja, bodo štete kakor polja dežele. Lahko so odkupljene in na jubilej bodo odšle.
Lakini nyumba za vijijini zisizokuwa na ukuta kuzizunguuka, zitahesabiwa kuwa shamba la nchi. Zaweza kukombolewa, na ni lazima zirejeshwe katika mwaka wa Yubile.
32 Vendar lahko mesta Lévijevcev in hiše mest njihove posesti Lévijevci kadarkoli odkupijo.
Hata hivyo, nyumba zinazomilikiwa na makuhani katika miji yao zaweza kukombelewa wakati wowote.
33 Če človek kupi od Lévijevcev, potem bo hiša, ki je bila prodana in mesto njegove posesti, odšlo v jubilejnem letu, kajti hiše mest Lévijevcev so njihova posest med Izraelovimi otroki.
Iwapo mmoja wa makuhani haikombowi nyumba iliyozwa, kisha nyumba hiyo iliyouzwa katika miji ilimo, ni lazima irejeshwe katika mwaka wa Yubile, kwa kuwa nyumba za miji ya makuhani ni mali yao miongoni mwa watu wa Israeli.
34 Toda polje predmestij njihovih mest ne more biti prodano, kajti to je njihova neprestana posest.
Lakini yale mashamba yanayozunguka miji yao hayataweza kuuzwa kwa sababu hiyo ni mali ya kudumu ya Makuhani.
35 Če tvoj brat postane reven in je zaradi tebe propadel, potem ga boš razbremenil; da, čeprav je tujec ali začasni prebivalec, da bo lahko živel s teboj.
Ikiwa mwananchi mwenzako anakuwa masikini, kiasi kwamba hawezi kujihudumia, nawe utalazimika kumsaidia kama vile ungemsaidia mgeni au mwingine yeyote kutoka nje aishie miongoni mwenu.
36 Nobenih obresti ne vzemi od njega ali narasta, temveč se boj svojega Boga, da bo tvoj brat lahko živel s teboj.
Usimtoze riba au kujaribu kunufaika kutoka kwake katika njia yoyote, bali mheshimu Mungu wako ili kwamba ndugu yako aendelee kuishi nawe.
37 Svojega denarja mu ne boš dal na obresti niti svojega živeža posodil za dobiček.
Hutampa mkopo wa fedha na kumtoza riba, wala hutamuuzia chakula chako ili kupata faida.
38 Jaz sem Gospod, vaš Bog, ki vas je privedel iz egiptovske dežele, da vam dam kánaansko deželo in, da bi bil vaš Bog.
Mimi ndimi Yahweh Mungu wako, aliye kuleta wewe kutoka nchi ya Misri, ili kwamba Nikupe nchi ya Kanaani, na kwamba niwe Mungu wako.
39 Če tvoj brat, ki prebiva pri tebi, postane reven in ti je prodan, ga ne boš prisilil, da služi kakor služabnik,
Iwapo mwananchi mwenzako atakuwa masikini na kujiuza mwenyewe kwako, hutamfanyisha kazi kama mtumwa.
40 temveč kakor najeti služabnik in kakor začasni prebivalec bo on s teboj in ti bo služil do jubilejnega leta.
Mtendee kama mtumishi wa kuajiriwa. Ni lazima awe kama yule ahudumuye nawe kwa muda mpaka mwaka wa Yubile.
41 Potem bo odšel od tebe tako on in njegovi otroci z njim in se bo vrnil k svoji lastni družini in se bo vrnil na posest svojih očetov.
Kisha ataondoka kwako, yeye mwenyewe na watoto wake pamoja naye, na atarejea kwenye familia yake mwenyewe na kwenye miliki ya baba yake.
42 Kajti oni so moji služabniki, ki sem jih privedel iz egiptovske dežele. Ne bodo prodani kakor tlačani.
Kwa sababu wao ni watumishi wangu niliowaleta kutoka katika nchi ya Misri. Hawatauzwa kama watumwa.
43 Nad njim ne boš vladal s krutostjo, temveč se boš bal svojega Boga.
Usitawale juu yao kwa ukatili, bali yakupasa kumheshimu Mungu wako.
44 Tako tvoji služabniki in tvoje služabnice, ki jih boš imel, bodo izmed poganov, ki so naokoli vas; izmed njih si kupujte služabnike in služabnice.
Kwa upande wa watumwa wako wakiume na watumwa wako wa kike, unaowezao kuwapata kutok kwa mataifa yanayokuzunguka, waweza kununua watumwa kutoka kwao.
45 Poleg tega izmed otrok tujcev, ki začasno prebivajo med vami, od njih boste kupovali in od njihovih družin, ki so z vami, ki so jih zaplodili v vaši deželi; in oni bodo vaša posest.
Unaweza pia kununua watumwa kutoka kwa wageni wanaoishi miongoni mwenu, yaani, kutoka familia zao waliopamoja nawe, wale wtoto waliozaliwa katika nchi yako. Wanaweza kuwa mali yako.
46 Vzeli jih boste kakor dediščino za svoje otroke za seboj, da jih podedujejo za posest; ti bodo vaši služabniki na veke, toda nad svojimi brati, Izraelovimi otroki, ne boste s krutostjo vladali drug nad drugim.
Unaweza kuzalisha watumwa hao kama urithi kwa watoto wako baada yako, ili kuwamiliki kama mali. Kutoka kwao waweza kununua watumwa daima, lakini hamtawezi kutawala kwa ukali juu ya ndugu zenu walio miogoni mwa watu wa Israeli.
47 Če začasni prebivalec ali tujec poleg tebe obogati, tvoj brat, ki prebiva ob njem pa obuboža in se proda tujcu ali začasnemu prebivalcu ob tebi ali rodu tujčeve družine,
Iwapo mgeni anayeishi nawe kwa muda anakuwa tajiri, na ikiwa mmoja wa Waisraeli amekuwa masikini na kujuza mwenyewe kwa familia ya mgeni, au kwa mtu fulani katika familia,
48 potem, ko je ta prodan, je lahko ponovno odkupljen. Eden izmed njegovih bratov ga lahko odkupi.
baada ya Mwisraeli mwenzako kuwa amenunuliwa. Anaweza kurejeshwa kwa maliopo. Iwapo anaweza kurejeshwa. Mtu fulani katika familia yake anaweza kumkomboa.
49 Odkupi ga lahko njegov stric ali sin njegovega strica ali kdorkoli, ki je blizu sorodstva njegovi družini, ga lahko odkupi, ali če je zmožen, se lahko odkupi sam.
Anaweza kuwa mjomba wake, au mjomba wa mwanawe, anayemkomboa yeye, au yeyote aliye ndugu yake wa karibu kutoka kwa ukoo wake. Au, iwapo ni mwenye mafanikio, anaweza kujikomboa mwenyewe.
50 Poračunal bo z njim, ki ga je kupil od leta, ko mu je bil prodan, do jubilejnega leta. Cena njegove prodaje bo glede na število let, glede na čas najetega služabnika bo ta z njim.
Ni lazima apatane na mtu aliyemnunua, itawapasa kuhesabu miaka tangu mwaka aliojiuza kwa mnunuzi wake mpaka mwaka wa Yubile. Ile thamani ya ukombozi wake ihesabiwe kulingana na kiwango cha mshahara anaolipwa mtumishi aliyeajiriwa, kwa idadi ya miaka ambayo angeweza kuendelea kufanya kazi kwa yule aliyemnunua.
51 Če je zadaj še veliko let, glede na njihovo [število], bo povrnil ceno svoje odkupitve od denarja, za katerega je bil kupljen.
Endapo kutakuwa kungali na miaka mingi iliyobaki mpaka mwaka wa Yubile, atalazimika kulipa fungu kubwa la fedha kwa ajili ya ukombozi ambao ni uwino wa idadi ya miaka hiyo.
52 Če bo preostalo le nekaj let do jubilejnega leta, potem bo z njim obračunal in glede na njegova leta mu bo povrnil ceno njegove odkupitve.
Iwapo kuna miaka michache tu iliyobaki mpaka mwaka wa Yubile, atapatana na aliyemnunua ili kuipitia idadi ya miaka iliyobaki mpaka Yubile, naye atalazimika kulipia ukombozi wake kulingana na idadi ya miaka.
53 In kakor letno najeti služabnik bo z njim, in drugi nad njim v tvojem pogledu ne bo vladal s krutostjo.
Naye atatendewa kama mtu aliyeajiriwa mwaka kwa mwaka. Utahakikisha kwamba hatendewi kwa ukali.
54 Če pa ne bo odkupljen v teh letih, potem bo odšel v jubilejnem letu, tako on in njegovi otroci z njim.
Iwapo hakukombolewa katika njia hizi, basi atatumika mpaka mwaka wa Yubile, yeye pamoja na watoto wake.
55 Kajti Izraelovi otroci so mi služabniki; oni so moji služabniki, ki sem jih privedel iz egiptovske dežele. Jaz sem Gospod, vaš Bog.‹«
Kwangu mimi watu wa Israeli ni watumishi. Wao ni watumishi wangu ambao Niliwatoa katika nchi ya Misri. Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.

< 3 Mojzes 25 >