< 3 Mojzes 16 >

1 Gospod je spregovoril Mojzesu po smrti Aronovih dveh sinov, ko sta darovala pred Gospodom in umrla,
Bwana akasema na Mose baada ya kifo cha wale wana wawili wa Aroni waliokufa walipokaribia mbele za Bwana.
2 in Gospod je rekel Mojzesu: »Govori svojemu bratu Aronu, da ne pride ob vseh časih v sveti prostor znotraj zagrinjala, pred sedež milosti, ki je na skrinji, da ne umre, kajti jaz se bom v oblaku prikazal nad sedežem milosti.
Bwana akamwambia Mose: “Mwambie ndugu yako Aroni asije wakati wowote atakavyo yeye ndani ya Patakatifu pa Patakatifu, nyuma ya pazia pale mbele ya kiti cha rehema kile kilichoko juu ya Sanduku la Agano, la sivyo atakufa, kwa sababu huwa ninatokea ndani ya wingu juu ya kile kiti cha rehema.
3 Tako bo Aron prišel na sveti kraj: z mladim bikcem za daritev za greh in ovnom za žgalno daritev.
“Hivi ndivyo Aroni atakavyoingia katika mahali patakatifu: atachukua fahali mchanga kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa.
4 Nadel si bo svet lanen plašč, na svojem mesu bo imel kratke platnene hlače, opasan bo z lanenim pasom in okrašen z lanenim turbanom. To so sveta oblačila, zato bo svoje meso umil v vodi in si jih tako nadel.
Atavaa koti takatifu la kitani, pamoja na nguo za ndani za kitani; atafunga mshipi wa kitani kiunoni, na kuvaa kilemba cha kitani. Haya ni mavazi matakatifu, kwa hiyo ni lazima aoge kwa maji kabla ya kuyavaa mavazi hayo.
5 Od zbora Izraelovih otrok bo vzel dva kozlička od koz za daritev za greh in enega ovna za žgalno daritev.
Atachukua mbuzi dume wawili kutoka kwa jumuiya ya Israeli kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa.
6 Aron bo daroval svojega bikca daritve za greh, ki je zanj ter opravil spravo zase in za svojo hišo.
“Aroni atamtoa huyo fahali kwa ajili ya sadaka yake ya dhambi ili afanye upatanisho kwa ajili yake mwenyewe na nyumba yake.
7 Vzel bo dva kozla in ju postavil pred Gospoda, pri vratih šotorskega svetišča skupnosti.
Kisha atawachukua wale mbuzi dume wawili na kuwaleta mbele za Bwana kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
8 Aron bo metal žrebe med dvema kozloma. En žreb za Gospoda, drugi žreb pa za ubežnega kozla.
Aroni atapiga kura kwa ajili ya hao mbuzi wawili, mmoja kwa ajili ya Bwana na mwingine kwa ajili ya kubebeshwa dhambi.
9 Aron bo privedel kozla, na katerega je padel Gospodov žreb in ga daroval za daritev za greh.
Aroni atamleta yule mbuzi ambaye kura ya Bwana imemwangukia na kumtoa dhabihu kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
10 Toda kozel, na katerega pade žreb, da bo ubežen kozel, bo živ postavljen pred Gospoda, da z njim opravi spravo in da ga za ubežnega kozla spusti v divjino.
Lakini mbuzi aliyechaguliwa kwa kura kuwa wa kubebeshwa dhambi atatolewa akiwa hai mbele za Bwana, atumike kwa kufanya upatanisho kwa kumwacha aende jangwani akiwa amebebeshwa dhambi.
11 Aron bo privedel bikca daritve za greh, ki je zanj in opravil spravo zase in za svojo hišo in zaklal bo bikca daritve za greh, ki je zanj,
“Aroni atamleta yule fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi yake mwenyewe, ili kufanya upatanisho kwa ajili yake na nyumba yake, naye atamchinja huyo fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi yake mwenyewe.
12 in izpred oltarja, pred Gospodom, bo vzel kadilnico, polno gorečega ognjenega oglja in svoji roki polni drobno zdrobljenega dišečega kadila in to bo prinesel znotraj zagrinjala.
Atachukua chetezo kilichojaa makaa yanayowaka kutoka madhabahuni mbele za Bwana, na konzi mbili za uvumba laini uliosagwa vizuri wenye harufu, na kuvipeleka nyuma ya pazia.
13 Kadilo bo položil na ogenj pred Gospodom, da oblak kadila lahko pokrije sedež milosti, ki je nad pričevanjem, da ne umre.
Ataweka uvumba juu ya moto mbele za Bwana, na moshi wa uvumba utafunika kile kiti cha rehema kilicho juu ya Ushuhuda, ili asife.
14 Vzel bo od krvi bikca in jo s svojim prstom poškropil nad sedežem milosti proti vzhodu. Pred sedežem milosti bo s svojim prstom sedemkrat poškropil kri.
Atachukua sehemu ya damu ya fahali, na kwa kidole chake atanyunyiza sehemu ya mbele ya kiti cha rehema; kisha atanyunyiza sehemu ya hiyo damu kwa kidole chake mara saba mbele ya kiti cha rehema.
15 Potem bo zaklal kozla daritve za greh, ki je za ljudstvo in njegovo kri prinesel znotraj zagrinjala in s to krvjo storil, kakor je storil s krvjo bikca in jo poškropil nad sedežem milosti in pred sedežem milosti.
“Kisha atamchinja mbuzi wa sadaka ya dhambi kwa ajili ya watu, na kuichukua damu yake nyuma ya pazia, na aifanyie kama alivyofanya kwa damu ya fahali: Atanyunyiza juu ya kiti cha rehema na mbele yake.
16 Zaradi nečistosti Izraelovih otrok in zaradi njihovih prestopkov v vseh njihovih grehih bo opravil spravo za svet kraj in tako bo storil za šotorsko svetišče skupnosti, ki ostaja med njimi v sredi njihove nečistosti.
Kwa njia hii atafanya upatanisho kwa ajili ya Patakatifu pa Patakatifu kwa sababu ya unajisi na uasi wa Waisraeli, kwa dhambi zao zozote. Atafanya hivyo kwa ajili ya Hema la Kukutania, ambalo liko miongoni mwao katikati ya unajisi wao.
17 Tam ne bo nobenega moža v šotorskem svetišču skupnosti, ko gre vanj, da opravi spravo na svetem kraju, dokler ne pride ven in je opravil spravo zase, za svojo družino in za vso Izraelovo skupnost.
Mtu yeyote haruhusiwi kuwa ndani ya Hema la Kukutania, kuanzia wakati Aroni anapoingia kufanya upatanisho katika Patakatifu pa Patakatifu, hadi atakapotoka nje, baada ya kujifanyia upatanisho yeye mwenyewe na nyumba yake, pamoja na jumuiya yote ya Israeli.
18 Odšel bo ven, k oltarju, ki je pred Gospodom in opravil spravo zanj. Vzel bo od krvi bikca in od krvi kozla in to položil naokoli, na oltarne rogove.
“Kisha atatoka aje kwenye madhabahu yaliyo mbele za Bwana na kufanya upatanisho kwa ajili yake. Atachukua sehemu ya damu ya fahali na sehemu ya damu ya mbuzi, na kuiweka kwenye pembe za madhabahu.
19 S svojim prstom bo nanj sedemkrat poškropil od krvi, ga očistil in ga posvetil pred nečistostjo Izraelovih otrok.
Atanyunyiza baadhi ya hiyo damu juu ya madhabahu kwa kidole chake mara saba, ili kuitakasa na kuiweka wakfu kutokana na unajisi wa Waisraeli.
20 Ko zaključi očiščenje svetega kraja, šotorskega svetišča skupnosti in oltarja, bo privedel živega kozla,
“Aroni atakapokuwa amemaliza kufanya upatanisho kwa ajili ya Patakatifu pa Patakatifu, Hema la Kukutania na madhabahu, atamleta mbele yule mbuzi aliye hai.
21 in Aron bo obe svoji roki položil na glavo živega kozla in nad njim priznal vse krivičnosti Izraelovih otrok in vse njihove prestopke v vseh njihovih grehih, s tem, da jih položi na glavo kozla in ga po roki primernega moža pošlje proč, v divjino.
Aroni ataweka mikono yake miwili juu ya kichwa cha mbuzi aliye hai na kuungama juu yake uovu wote na uasi wa Waisraeli, yaani dhambi zao zote, ili kuziweka juu ya kichwa cha huyo mbuzi. Atamwachia huyo mbuzi akimbilie jangwani kwa uangalizi wa mtu aliyepewa wajibu huo.
22 Kozel bo na sebi nosil vse njihove krivičnosti v nenaseljeno deželo in kozla bo spustil v divjino.
Yule mbuzi atachukua juu yake dhambi zao zote mpaka mahali pasipo na watu; naye yule mtu atamwachia akimbilie jangwani.
23 Aron bo prišel v šotorsko svetišče skupnosti in odložil lanene obleke, ki jih je oblekel, ko je odšel v sveti kraj in jih bo pustil tam.
“Kisha Aroni ataenda ndani ya Hema la Kukutania na kuvua yale mavazi ya kitani aliyoyavaa kabla ya kuingia katika Patakatifu pa Patakatifu, naye atayaacha pale.
24 Svoje meso bo z vodo umil na svetem kraju in si nadel svoje obleke in prišel naprej ter daroval svojo žgalno daritev, žgalno daritev za ljudstvo in opravil spravo zase in za ljudstvo.
Ataoga kwa maji katika mahali patakatifu na kuvaa mavazi yake ya kawaida. Kisha atatoka na kutoa dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa kwa ajili yake na sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya watu, ili kufanya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe, na kwa ajili ya watu.
25 Tolščo daritve za greh bo sežgal na oltarju.
Pia atachoma mafuta ya mnyama wa sadaka ya dhambi juu ya madhabahu.
26 Tisti, ki je spustil kozla za ubežnega kozla, bo opral svoja oblačila in svoje meso umil v vodi in potem pride v tabor.
“Yule mtu anayemwachia yule mbuzi wa kubebeshwa dhambi ni lazima afue nguo zake na kuoga kwa maji; baadaye anaweza kuingia kambini.
27 Bikca daritve za greh in kozla daritve za greh, čigar kri je bila prinesena, da opravi spravo na svetem kraju, bo nekdo odnesel zunaj tabora, v ognju pa bodo sežgali njihove kože, njihovo meso in njihov iztrebek.
Yule fahali na mbuzi waliotolewa kwa ajili ya sadaka za dhambi, ambao damu yao ilikuwa imeletwa Patakatifu pa Patakatifu kwa ajili ya kufanya upatanisho, ni lazima watolewe nje ya kambi. Ngozi zao, nyama, na matumbo pamoja na mavi vitateketezwa kwa moto.
28 Kdor jih zažiga bo opral svoja oblačila in svoje telo umil v vodi in potem bo prišel v tabor.
Mtu atakayevichoma ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji; baadaye ataweza kuingia kambini.
29 To bo med vami zakon na veke, da boste v sedmem mesecu, na deseti dan meseca, ponižali svoje duše in sploh ne boste počeli nobenega dela; naj bo to nekdo iz vaše lastne dežele ali tujec, ki začasno prebiva med vami,
“Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yenu: Katika siku ya kumi ya mwezi wa saba ni lazima mfunge, wala msifanye kazi yoyote, iwe mzawa au mgeni anayeishi miongoni mwenu,
30 kajti na ta dan bo duhovnik opravil spravo za vas, da vas očisti, da boste pred Gospodom lahko čisti pred vsemi svojimi grehi.
kwa sababu siku hii upatanisho utafanyika kwa ajili yenu ili kuwatakasa. Kisha mtakuwa safi mbele za Bwana kutokana na dhambi zenu zote.
31 To vam bo šabatni počitek in svoje duše boste strli, po zakonu na veke.
Ni Sabato ya mapumziko, na lazima mfunge; ni agizo la kudumu.
32 Duhovnik, ki ga bo mazilil in ki ga bo uméstil, da služi v duhovniški službi na mestu njegovega očeta, bo opravil spravo in si nadel lanena oblačila, torej sveta oblačila,
Kuhani ambaye ametiwa mafuta na kuwekwa wakfu ili kuingia mahali pa baba yake kama kuhani mkuu atafanya upatanisho. Atavaa mavazi matakatifu ya kitani,
33 in ta bo opravil spravo za sveto svetišče in ta bo opravil spravo za šotorsko svetišče skupnosti in za oltar in ta bo opravil spravo za duhovnike in za vse ljudstvo skupnosti.
na kufanya upatanisho kwa ajili ya Patakatifu pa Patakatifu, Hema la Kukutania na madhabahu, na pia kwa ajili ya makuhani, pamoja na jumuiya yote ya watu.
34 To vam bodi večen zakon, da enkrat letno opravite spravo za Izraelove otroke, za vse njihove grehe.« In storil je, kakor je Gospod zapovedal Mojzesu.
“Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yenu: Upatanisho utafanywa mara moja tu kwa mwaka kwa ajili ya dhambi zote za Waisraeli.” Ndivyo ilivyofanyika, kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.

< 3 Mojzes 16 >