< Žalostinke 4 >
1 Kako je zlato postalo zatemnjeno! Kako se je najbolj čisto zlato spremenilo! Kamni svetišča so izliti na vrhu vsake ulice.
Jinsi dhahabu ilivyopoteza mngʼao wake, dhahabu iliyo safi haingʼai! Vito vya thamani vimetawanywa kwenye mwanzo wa kila barabara.
2 Dragoceni sionski sinovi, primerljivi čistemu zlatu, kako so cenjeni, kakor lončeni vrči, delo lončarjevih rok!
Wana wa Sayuni wenye thamani, ambao mwanzo uzito wa thamani yao ulikuwa wa dhahabu, sasa wanaangaliwa kama vyungu vya udongo, kazi ya mikono ya mfinyanzi!
3 Celo morske pošasti iztegnejo prsi, dajejo piti svojim mladičem. Hči mojega ljudstva je postala kruta, podobna nojem v divjini.
Hata mbweha hutoa matiti yao kunyonyesha watoto wao, lakini watu wangu wamekuwa wasio na huruma kama mbuni jangwani.
4 Jezik doječega otroka se zaradi žeje lepi na nebo njegovih ust. Mladi otroci prosijo kruha, pa jim ga noben človek ne nalomi.
Kwa sababu ya kiu ulimi wa mtoto mchanga umegandamana na kaakaa la kinywa chake, watoto huomba mkate, lakini hakuna yeyote awapaye.
5 Tisti, ki so se prefinjeno hranili, so zapuščeni na ulicah. Tisti, ki so bili vzgojeni v škrlatu, objemajo gnojišča.
Wale waliokula vyakula vya kifahari ni maskini barabarani. Wale waliokuzwa wakivaa nguo za zambarau sasa wanalalia majivu.
6 Kajti kazen krivičnosti hčere mojega ljudstva je večja kakor kazen za greh Sódome, ki je bila v hipu zrušena in nobene roke se je niso dotaknile.
Adhabu ya watu wangu ni kubwa kuliko ile ya Sodoma, ambayo ilipinduliwa ghafula bila kuwepo mkono wa msaada.
7 Njeni nazirci so bili čistejši od snega, bolj so bili beli kakor mleko, po telesu so bili bolj rdečkasti kakor rubini, njihova gladkost je bila [podobna] safirju.
Wakuu wao walikuwa wamengʼaa kuliko theluji na weupe kuliko maziwa, miili yao ilikuwa myekundu kuliko marijani, kuonekana kwao kama yakuti samawi.
8 Njihov videz je bolj črn kakor oglje; na ulicah niso prepoznavni. Njihova koža se lepi na njihove kosti; izsušena je, postala je kakor palica.
Lakini sasa ni weusi kuliko masizi; hawatambulikani barabarani. Ngozi yao imeshikamana juu ya mifupa yao, imekuwa mikavu kama fimbo.
9 Tisti, ki so umorjeni z mečem, so boljši kakor tisti, ki so umorjeni z lakoto, kajti ti hirajo, zadeti zaradi potrebe po poljskem sadu.
Wale waliouawa kwa upanga ni bora kuliko wale wanaokufa njaa; wanateseka kwa njaa, wanatokomea kwa kukosa chakula kutoka shambani.
10 Roke sočutnih žensk so kuhale svoje lastne otroke. Bili so njihova hrana v uničenju hčere mojega ljudstva.
Kwa mikono yao wenyewe wanawake wenye huruma wanapika watoto wao wenyewe, waliokuwa chakula chao watu wangu walipoangamizwa.
11 Gospod je dovršil svojo razjarjenost; izlil je svojo kruto jezo in prižgal ogenj na Sionu in ta je požrl njegove temelje.
Bwana ametoa nafasi kamilifu ya ghadhabu yake; ameimwaga hasira yake kali. Amewasha moto katika Sayuni ambao umeteketeza misingi yake.
12 Kralji zemlje in vsi prebivalci zemeljskega [kroga] niso hoteli verjeti, da bosta nasprotnik in sovražnik vstopila v velika vrata Jeruzalema.
Wafalme wa dunia hawakuamini, wala mtu yeyote wa duniani, kwamba adui na watesi wangeweza kuingia kwenye malango ya Yerusalemu.
13 Zaradi grehov njenih prerokov in krivičnosti njenih duhovnikov, ki so prelivali kri pravičnih v njeni sredi,
Lakini hili lilitokea kwa sababu ya dhambi za manabii wake, na maovu ya makuhani wake, waliomwaga ndani yake damu ya wenye haki.
14 klatili so se kakor slepi možje po ulicah, oskrunili so se s krvjo, tako da se možje niso mogli dotakniti njihovih oblek.
Sasa wanapapasa papasa barabarani kama watu ambao ni vipofu. Wamenajisiwa kabisa kwa damu, hata hakuna anayethubutu kugusa mavazi yao.
15 Klicali so jim: »Odidite; to je nečisto; odidite, odidite, ne dotikajte se.« Ko so pobegnili in se potikali so med pogani govorili: »Nič več ne bodo začasno prebivali tam.
Watu wanawapigia kelele, “Ondokeni! Ninyi ni najisi! Ondokeni! Ondokeni! Msituguse!” Wanapokimbia na kutangatanga huku na huko, watu miongoni mwa mataifa wanasema, “Hawawezi kukaa hapa zaidi.”
16 Gospodova jeza jih je razdelila; ne bo se več oziral nanje. Niso spoštovali oseb duhovnikov, niso bili naklonjeni starešinam.
Bwana mwenyewe amewatawanya; hawaangalii tena. Makuhani hawaonyeshwi heshima, wazee hawakubaliki.
17 Kar se tiče nas, so naše oči doslej odpovedovale zaradi naše prazne pomoči. V svojem oprezanju smo oprezali za narodom, ki nas ni mogel rešiti.
Zaidi ya hayo, macho yetu yalichoka, kwa kutazamia bure msaada; tuliangalia kutoka minara yetu kwa taifa lisiloweza kutuokoa.
18 Lovijo naše korake, da ne moremo iti na svoje ulice. Naš konec je blizu, naši dnevi so izpolnjeni, kajti naš konec je prišel.
Watu walituvizia katika kila hatua hata hatukuweza kutembea katika barabara zetu. Mwisho wetu ulikuwa karibu, siku zetu zilikuwa zimetimia, kwa maana mwisho wetu ulikuwa umefika.
19 Naši preganjalci so hitrejši kakor orli neba. Zasledovali so nas po gorah, na nas so prežali v divjini.
Waliotufuatia walikuwa wepesi kuliko tai angani; walitusaka juu milimani na kutuvizia jangwani.
20 Dih naših nosnic, Gospodov maziljenec, je bil odveden v njihove jame, o katerem smo rekli: »Pod njegovo senco bomo živeli med pogani.«
Mpakwa mafuta wa Bwana, pumzi ya uhai wetu hasa, alinaswa katika mitego yao. Tulifikiri kwamba chini ya kivuli chake tungeliweza kuishi miongoni mwa mataifa.
21 Razveseljuj se in bodi vesela, oh edómska hči, ki prebivaš v deželi Uc; prav tako bo čaša prešla k tebi. Opijanjena boš in razgalila se boš.
Shangilia na ufurahi, ee Binti Edomu, wewe unayeishi nchi ya Usi. Lakini kwako pia kikombe kitapitishwa, Utalewa na kuvuliwa nguo ubaki uchi.
22 Kazen tvoje krivičnosti je dovršena, oh hči sionska; nič več te ne bo odvedel v ujetništvo. Obiskal bo tvojo krivičnost, oh hči edómska; odkril bo tvoje grehe.
Ee Binti Sayuni, adhabu yako itaisha, hatarefusha muda wako wa kukaa uhamishoni. Lakini, ee Binti Edomu, ataadhibu dhambi yako, na atafunua uovu wako.