< Sodniki 18 >
1 V tistih dneh ni bilo kralja v Izraelu in v tistih dneh si je rod Danovcev iskal dediščino, da v njej prebiva, kajti do tistega dne jim vsa njihova dediščina ni pripadla med Izraelovimi rodovi.
Katika siku hizo Israeli walikuwa hawana mfalme. Katika siku hizo kabila la Wadani walikuwa wanatafuta mahali pao wenyewe pa kuishi, kwa sababu walikuwa hawajafika kwenye urithi wao miongoni mwa makabila ya Israeli.
2 Danovi otroci so izmed svojih družin poslali pet moških iz svojih pokrajin, junaške može iz Core in iz Eštaóla, da hodijo vzdolž dežele in da jo preiščejo. Rekli so jim: »Pojdite, oglejte deželo.« Ko so le-ti prišli do gore Efrájim, k Mihovi hiši, so se tam nastanili.
Hivyo Wadani wakatuma mashujaa watano kutoka Sora na Eshtaoli ili kupeleleza nchi na kuichunguza. Hawa watu waliwakilisha koo zao zote. Waliwaambia, “Nendeni mkaichunguze hiyo nchi.” Watu hao wakaingia katika nchi ya vilima ya Efraimu, nao wakafika nyumba ya Mika, ambako walilala usiku huo.
3 Ko so bili pri Mihovi hiši, so prepoznali glas mladeniča, Lévijevca. Obrnili so se tja in mu rekli: »Kdo te je privedel sèm? Kaj delaš na tem kraju? In kaj imaš tukaj?«
Walipofika karibu na nyumba ya Mika, waliitambua sauti ya yule kijana Mlawi; hivyo wakaingia humo na kumuuliza, “Ni nani aliyekuleta hapa? Unafanya nini mahali hapa? Kwa nini uko hapa?”
4 Odgovoril jim je: »Tako in tako je Miha postopal z menoj, me najel in sem njegov duhovnik.«
Akawaeleza yale Mika aliyomtendea, naye akasema, “Ameniajiri nami ni kuhani wake.”
5 Rekli so mu: »Prosimo te, vprašaj za nasvet od Boga, da bomo lahko vedeli katera izmed naših poti, po kateri gremo, bo uspešna.«
Kisha wakamwambia, “Tafadhali tuulizie kwa Mungu kama safari yetu itafanikiwa.”
6 Duhovnik jim je rekel: »Pojdite v miru. Vaša pot, po kateri greste, je pred Gospodom.«
Yule kuhani akawajibu, “Enendeni kwa amani. Safari yenu ina kibali cha Bwana.”
7 Potem je pet mož odpotovalo in prišlo k Láješu in videlo ljudstvo, ki je bilo tam, kako so brezskrbno prebivali po navadi Sidóncev, tiho in varno. Tam v deželi ni bilo naseljencev, da bi jih lahko v kakršnikoli stvari osramotili. Bili so daleč od Sidóncev in z nikomer niso imeli nič opraviti.
Basi hao watu watano wakaondoka na kufika Laishi, mahali ambapo waliwakuta watu wanaishi salama, kama Wasidoni, kwa utulivu na bila mashaka. Nchi yao haikupungukiwa na kitu chochote, hivyo wakawa tajiri. Pia walikaa mbali sana na Wasidoni, wala hawakushughulika na mtu yeyote.
8 Prišli so k svojim bratom do Core in Eštaóla in njihovi bratje so jim rekli: »Kaj pravite?«
Waliporudi kwa ndugu zao huko Sora na Eshtaoli, ndugu zao wakawauliza, “Mlionaje mambo huko?”
9 Odgovorili so: »Vstanite, da bomo lahko šli gor zoper njih, kajti videli smo deželo in glejte, ta je zelo dobra. In vi ste mirni? Ne bodite leni, da bi šli in vstopili, da vzamete deželo v last.«
Wakajibu, “Twendeni, tukapigane nao! Tumeona kuwa nchi ni nzuri sana. Je, hamtafanya chochote? Msisite kupanda ili kuimiliki.
10 Ko greste, boste prišli k varnemu ljudstvu in k veliki deželi, kajti Bog jo je dal v vaše roke. Prostor, kjer ni pomanjkanja česarkoli, kar je na zemlji.
Mtakapokwenda huko mtakuta watu waliotulia walio salama, nayo nchi hiyo ni kubwa na Mungu ameitia mikononi mwenu, nayo ni nchi ambayo haikupungukiwa na kitu chochote kilicho duniani.”
11 Od tod je odšla družina Danovcev na svojo pot, iz Core in iz Eštaóla, šeststo mož, opasanih z bojnim orožjem.
Ndipo watu 600 toka ukoo wa Wadani, waliojifunga silaha za vita, wakaondoka Sora na Eshtaoli.
12 Odšli so gor in se utaborili v Kirját Jearímu v Judu. Zato so ta kraj imenovali Mahané Dan do današnjega dne. Glej ta je poleg Kirját Jearíma.
Walipokuwa wakisafiri wakapiga kambi huko Kiriath-Yearimu katika Yuda. Hii ndiyo sababu sehemu ya magharibi ya Kiriath-Yearimu inaitwa Mahane-Dani mpaka leo.
13 Od tam so prešli h gori Efrájim in prišli do Mihove hiše.
Kutoka hapo wakaendelea mbele mpaka nchi ya vilima ya Efraimu na kufika katika nyumba ya Mika.
14 Potem je pet mož, ki so odšli, da ogledajo deželo Láješ, odgovorilo in reklo svojim bratom: »Ali veste, da so v teh hišah efód, družinski malik, rezana podoba in ulita podoba? Sedaj torej preudarite kaj vam je storiti.«
Ndipo wale watu watano waliopeleleza nchi ya Laishi wakawaambia ndugu zao, “Je, mwajua kuwa mojawapo ya nyumba hizi kuna naivera, sanamu ndogo za nyumbani, sanamu ya kuchonga na sanamu ya kusubu? Sasa basi fikirini mtakalofanya.”
15 Obrnili so se tja in prišli do hiše mladeniča, Lévijevca, torej k Mihovi hiši in ga pozdravili.
Basi wakaingia humo na kwenda kwenye nyumba ya yule kijana Mlawi katika nyumba ya Mika na kumsalimu.
16 Šeststo mož, opasanih s svojimi bojnimi orožji, ki so bili izmed Danovih otrok, pa je stalo pri vhodu velikih vrat.
Wale Wadani 600, waliovaa silaha za vita, wakasimama penye ingilio la lango.
17 Pet mož, ki so šli, da ogledajo deželo, je odšlo gor in vstopili so tja in vzeli rezano podobo, efód, družinskega malika in ulito podobo. Duhovnik pa je stal na vhodu velikih vrat s šeststotimi možmi, ki so bili opasani z bojnim orožjem.
Wale watu watano waliokwenda kupeleleza nchi wakaingia ndani na kuchukua ile sanamu ya kuchonga, ile naivera, na zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani pamoja na ile sanamu ya kusubu, wakati yule kuhani akiwa amesimama pale penye ingilio la lango pamoja na wale watu 600 waliokuwa wamejifunga silaha za vita.
18 Ti so odšli v Mihovo hišo in prinesli izrezljano podobo, efód, družinskega malika in ulito podobo. Potem jim je duhovnik rekel: »Kaj počnete?«
Hao watu walipoingia katika nyumba ya Mika na kuchukua ile sanamu ya kuchonga, ile naivera, na zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani, pamoja na ile sanamu ya kusubu, yule kuhani akawauliza, “Mnafanya nini?”
19 Rekli so mu: »Molči, svojo roko položi na svoja usta in pojdi z nami in nam bodi oče in duhovnik. Ali je zate bolje biti duhovnik hiši enega človeka ali da postaneš duhovnik rodu in družini v Izraelu?«
Wakamjibu, “Nyamaza kimya! Weka mkono wako juu ya kinywa chako na ufuatane nasi, uwe baba yetu na kuhani wetu. Si ni afadhali utumikie kabila na ukoo katika Israeli kama kuhani kuliko kumtumikia mtu mmoja na watu wa nyumbani mwake?”
20 Duhovnikovo srce je bilo veselo in vzel je efód, družinskega malika, rezano podobo in odšel v sredo ljudstva.
Yule kuhani akafurahi. Akachukua ile naivera, zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani, na sanamu ya kuchonga, naye akaenda pamoja na wale watu.
21 Tako so se obrnili in odšli ter predse postavili malčke, živino in vozove.
Ndipo wakageuka na kuondoka wakiwatanguliza mbele watoto wao wadogo, wanyama wao wa kufugwa na mali zao.
22 In ko so bili dobro pot od Mihove hiše, so se ljudje, ki so bili v hišah blizu Mihove hiše, zbrali skupaj in dohiteli Danove otroke.
Walipokuwa wamesafiri umbali kidogo toka nyumbani kwa Mika, watu walioishi karibu na Mika wakaitwa wakakusanyika pamoja, nao wakawafikia Wadani.
23 Klicali so k Danovim otrokom. Ti pa so obrnili svoje obraze in Mihu rekli: »Kaj te pesti, da prihajaš s takšnim spremstvom?«
Walipofuatilia wakipiga kelele Wadani wakawageukia na kumwambia Mika, “Una nini wewe hata ukaja na kundi la watu namna hii ili kupigana?”
24 Odgovoril je: »Odvzeli ste moje bogove, ki sem jih naredil in duhovnika ter odšli proč. In kaj še imam? Kaj je to, da mi pravite: ›Kaj te pesti?‹«
Akawajibu, “Mmechukua miungu yote niliyoitengeneza, mkachukua na kuhani wangu, nanyi mkaondoka. Nimebaki na nini kingine? Mnawezaje kuniuliza, ‘Una nini wewe?’”
25 Danovi otroci so mu rekli: »Tvojega glasu naj ne bo slišati med nami, da ne bi jezni ljudje stekli nadte in bi izgubil svoje življenje, z življenji svoje družine.«
Wadani wakamjibu, “Usibishane na sisi, la sivyo watu wenye hasira kali watakushambulia, nawe na watu wa nyumbani mwako mtapoteza maisha.”
26 Danovi otroci so odšli svojo pot. Ko je Miha videl, da so bili premočni zanj, se je obrnil in se vrnil nazaj k svoji hiši.
Basi Wadani wakaenda zao, naye Mika alipoona kuwa wana nguvu kumliko yeye, akageuka na kurudi nyumbani kwake.
27 Vzeli so stvari, ki jih je naredil Miha in duhovnika, ki ga je imel in prišli k Láješu, k ljudstvu, ki je bilo tiho in varno. Udarili so jih z ostrino meča in mesto zažgali z ognjem.
Kisha wakachukua vile Mika alivyokuwa ametengeneza, na kuhani wake, wakaendelea hadi Laishi, dhidi ya watu walio na amani, wasiokuwa na wasiwasi. Wakawashambulia kwa upanga na kuuteketeza mji wao kwa moto.
28 Tam ni bilo nobenega osvoboditelja, ker je bilo daleč od Sidóna in niso imeli opravka s kakršnimkoli človekom. To je bilo v dolini, ki leži pri Bet Rehóbu. In zgradili so mesto ter prebivali v njem.
Hapakuwa na yeyote wa kuwaokoa, kwa kuwa kulikuwa mbali sana na Sidoni na hawakuwa na ushirikiano na mtu mwingine yeyote. Mji ulikuwa kwenye bonde karibu na Beth-Rehobu. Wadani wakaujenga upya huo mji na kuishi humo.
29 Ime mesta so imenovali Dan, po imenu njihovega očeta Dana, ki je bil rojen Izraelu, vendar je bilo ime mesta najprej Láješ.
Wakauita ule mji Dani kwa kufuata jina la baba yao aliyezaliwa na Israeli, ingawa mji huo ulikuwa ukiitwa Laishi hapo kwanza.
30 Danovi otroci so postavili rezano podobo in Jonatan, sin Geršóma, sinú Manáseja, on in njegovi sinovi so bili duhovniki Danovemu rodu do dneva ujetništva dežele.
Kisha Wadani wakajisimamishia sanamu ile ya kuchonga, naye Yonathani mwana wa Gershomu, mwana wa Mose pamoja na wanawe walikuwa makuhani wa kabila la Wadani mpaka nchi hiyo ilipotekwa.
31 Postavili so si Mihovo rezano podobo, ki jo je naredil ves ta čas, ko je bila Božja hiša v Šilu.
Wakaisimamisha na kuiabudu hiyo sanamu ya kuchonga ya Mika aliyokuwa ameitengeneza, wakati wote ule nyumba ya Mungu ilipokuwa huko Shilo.