< Jozue 6 >
1 Torej Jeriha je bila strogo zaprta zaradi Izraelovih otrok. Nihče ni odšel ven in nihče ni prišel noter.
Basi malango ya Yeriko yalifungwa kwa uthabiti kwa ajili ya Waisraeli. Hakuna mtu yeyote aliyetoka au kuingia.
2 Gospod je rekel Józuetu: »Poglej, v tvojo roko sem izročil Jeriho in njenega kralja in močne junaške može.
Kisha Bwana akamwambia Yoshua, “Tazama, nimeitia Yeriko mikononi mwako, pamoja na mfalme wake na watu wake wa vita.
3 Obdali boste mesto, vsi vi bojevniki in enkrat obhodili mesto. Tako boste počeli šest dni.
Zunguka mji mara moja pamoja na watu wote wenye silaha. Fanya hivi kwa siku sita.
4 Sedem duhovnikov bo pred skrinjo nosilo sedem šofarjev iz ovnovih rogov, in sedmi dan boste sedemkrat obkrožili mesto in duhovniki bodo zatrobili s šofarji.
Uwe na makuhani saba wakibeba mabaragumu ya pembe za kondoo dume mbele ya Sanduku. Siku ya saba, mzunguke mji mara saba, nao makuhani wakipiga baragumu hizo.
5 In zgodilo se bo, da ko bodo z ovnovim rogom naredili dolgo trobljenje in ko zaslišite zvok šofarja, naj vse ljudstvo zavpije z velikim krikom in mestno obzidje bo plosko padlo dol in ljudstvo se bo povzpelo, vsak človek naravnost pred seboj.«
Utakapowasikia wamepaliza sauti kubwa ya baragumu, watu wote wapige kelele kwa sauti kuu, kisha ukuta wa mji utaanguka na watu watapanda, kila mtu akiendelea mbele.”
6 Nunov sin Józue je poklical duhovnike ter jim rekel: »Vzdignite skrinjo zaveze in sedem duhovnikov naj pred Gospodovo skrinjo nosi sedem šofarjev iz ovnovih rogov.«
Ndipo Yoshua mwana wa Nuni akaita makuhani na kuwaambia, “Chukueni Sanduku la Agano la Bwana na makuhani saba wachukue baragumu za pembe za kondoo dume mbele yake.”
7 Ljudstvu pa je rekel: »Pojdite naprej in obkrožite mesto in naj tisti, ki je oborožen, gre naprej pred Gospodovo skrinjo.«
Naye akawaagiza watu, “Songeni mbele! Mkauzunguke mji, na walinzi wenye silaha watangulie mbele ya Sanduku la Bwana.”
8 Pripetilo se je, ko je Józue govoril ljudstvu, da je sedem duhovnikov, nosečih sedem šofarjev iz ovnovih rogov, šlo naprej pred Gospodom in trobilo s šofarji in skrinja Gospodove zaveze jim je sledila.
Baada ya Yoshua kuzungumza na watu, wale makuhani saba wenye kuzibeba zile baragumu saba mbele za Bwana, wakatangulia mbele, wakipiga baragumu zao na Sanduku la Agano la Bwana likawafuata.
9 Oboroženi možje so šli pred duhovniki, ki so trobili na šofarje in zadnja straža je prišla za skrinjo. Duhovniki pa so hodili in trobili s šofarji.
Walinzi waliokuwa na silaha wakaenda mbele ya hao makuhani waliopiga hizo baragumu na hao walinzi wa nyuma wakafuata Sanduku. Wakati wote huu baragumu zilikuwa zikipigwa.
10 Józue je zapovedal ljudstvu, rekoč: »Ne boste kričali niti naredili nobenega hrupa z vašim glasom niti ne bo nobena beseda izšla iz vaših ust do dneva, ko vam zapovem kričati; potem boste kričali.«
Bali Yoshua alikuwa amewaagiza watu, “Msipige kelele ya vita, msipaze sauti zenu, wala kusema neno lolote mpaka siku ile nitakayowaambia mpige kelele. Ndipo mtapiga kelele!”
11 Tako je Gospodova skrinja obkrožila mesto, ga enkrat obhodila in prišli so v tabor in prenočili v taboru.
Basi akalipeleka Sanduku la Bwana kuzungushwa huo mji, likizungushwa mara moja. Kisha watu wakarudi kambini kulala.
12 Józue je vstal zgodaj zjutraj in duhovniki so dvignili Gospodovo skrinjo.
Yoshua akaamka mapema asubuhi iliyofuata nao makuhani wakalichukua Sanduku la Bwana.
13 Sedem duhovnikov, ki so pred Gospodovo skrinjo nosili sedem šofarjev iz ovnovih rogov, je nenehno hodilo naprej in trobilo s šofarji in oboroženi možje so šli pred njimi, toda zadnja straža je prišla za Gospodovo skrinjo, duhovniki hodeč naprej in trobeč s šofarji.
Wale Makuhani saba wakizibeba zile baragumu saba wakatangulia mbele ya Sanduku la Bwana wakizipiga. Watu wenye silaha wakatangulia mbele yao na walinzi wa nyuma wakalifuata Sanduku la Bwana, huku baragumu hizo zikiendelea kulia.
14 Drugi dan so enkrat obkrožili mesto in se vrnili v tabor. Tako so počeli šest dni.
Siku ya pili wakauzunguka mji mara moja na kurudi kambini. Wakafanya hivi kwa siku sita.
15 Na sedmi dan se je pripetilo, da so vstali zgodaj, ob jutranjem svitanju in na isti način sedemkrat obkrožili mesto. Samo ta dan so mesto obkrožili sedemkrat.
Siku ya saba, wakaamka asubuhi na mapema wakauzunguka mji kama walivyokuwa wakifanya, isipokuwa siku ile waliuzunguka mji mara saba.
16 Pripetilo se je sedmič, ko so duhovniki zatrobili s šofarji, da je Józue rekel ljudstvu: »Kričite, kajti Gospod vam je dal mesto.
Walipouzunguka mara ya saba, makuhani walipopiga baragumu kwa sauti kubwa, Yoshua akawaamuru watu akisema, “Pigeni kelele! Kwa maana Bwana amewapa mji huu!
17 Mesto bo prekleto Gospodu, celó to in vse, kar je v njem. Samo pocestnica Rahába bo živela, ona in vsi, ki so z njo v hiši, ker je skrila poslanca, ki smo ju poslali.
Mji huu pamoja na vyote vilivyomo ndani yake utawekwa wakfu kwa Bwana. Ila Rahabu tu, yule kahaba na wote ambao wako pamoja naye nyumbani mwake ndio watakaosalimishwa, kwa sababu aliwaficha wale wapelelezi tuliowatuma.
18 Vi pa se zagotovo zadržite pred prekleto stvarjo, da se ne bi naredili preklete, ko vzamete od preklete stvari in naredite tabor Izraelcev prekletstvo in ga vznemirite.
Lakini mjiepushe na vitu vilivyowekwa wakfu, msije mkachukua chochote katika hivyo, msije mkajiletea maangamizi katika maskani ya Israeli na kuiletea taabu.
19 Toda vse srebro, zlato in posode iz brona in železa so posvečeni Gospodu. Pridejo naj v Gospodovo zakladnico.«
Fedha yote na dhahabu, vyombo vya shaba na chuma ni vitakatifu kwa Bwana, lazima viletwe katika hazina yake.”
20 Tako je ljudstvo zakričalo, ko so duhovniki zatrobili s šofarji in pripetilo se je, ko je ljudstvo zaslišalo zvok šofarja in je ljudstvo zavpilo z velikim krikom, da je obzidje plosko padlo dol, tako da je ljudstvo odšlo gor v mesto, vsak mož naravnost pred seboj in zavzeli so mesto.
Wakati baragumu zilipopigwa, watu walipiga kelele, na katika sauti ya baragumu, na watu kupaza sauti, ukuta ukaanguka; hivyo kila mtu akapanda akiendelea mbele na kuuteka mji.
21 Popolnoma so uničili vse, kar je bilo v mestu, tako moškega kakor žensko, mladega, starega, vola, ovco in osla, z ostrino meča.
Wakauweka mji wakfu kwa Bwana, na kila chenye uhai ndani yake walikiangamiza kwa upanga, wanaume kwa wanawake, vijana kwa wazee, ngʼombe, kondoo na punda.
22 Toda Józue je rekel dvema možema, ki sta ogledovala deželo: »Pojdita v hišo pocestnice in od tam privedita žensko in vse, kar ima, kakor sta ji prisegla.«
Yoshua akawaambia wale watu wawili waliokuwa wameipeleleza nchi, “Nendeni nyumbani kwa yule kahaba, mleteni pamoja na wote waliomo nyumbani mwake, kulingana na kiapo chenu kwake.”
23 Mladeniča, ki sta bila oglednika, sta vstopila in privedla ven Rahábo, njenega očeta, njeno mater, njene brate in vse, kar je imela in ven sta privedla vse njeno sorodstvo in jih pustila zunaj tabora Izraelcev.
Basi wale vijana waliofanya upelelezi wakaenda kumleta Rahabu, baba yake na mama yake, na ndugu zake na watu wote waliokuwa pamoja naye. Wakaleta jamaa yake yote na kuwaweka mahali nje ya kambi ya Israeli.
24 Mesto pa so požgali z ognjem in vse, kar je bilo v njem. Samo srebro, zlato in posode iz brona in iz železa, so dali v zakladnico Gospodove hiše.
Kisha wakauchoma mji wote na kila kitu kilichokuwamo ndani yake. Lakini fedha, dhahabu, vyombo vya shaba na vya chuma wakaviweka katika hazina ya nyumba ya Bwana.
25 Józue je rešil pocestnico Rahábo živo in družino njenega očeta in vse, kar je imela. V Izraelu prebiva do današnjega dne, ker je skrila poslanca, ki ju je Józue poslal, da ogledata Jeriho.
Lakini Yoshua akamhifadhi Rahabu yule kahaba, jamaa yake yote na wote waliokuwa wa kwake, kwa sababu aliwaficha watu waliotumwa na Yoshua kuipeleleza Yeriko, naye anaishi miongoni mwa Waisraeli hata leo.
26 Ob tistem času jih je Józue zaprisegel, rekoč: »Preklet bodi mož pred Gospodom, ki dvigne in pozida to mesto Jeriho. Njen temelj bo položil v svojem prvorojencu in v njegovem najmlajšem sinu bo postavil njena velika vrata.«
Wakati ule Yoshua akatamka kiapo hiki akasema, “Aliyelaaniwa mbele za Bwana ni mtu atakayeinuka kuujenga tena mji huu wa Yeriko: “Kwa gharama ya mzaliwa wake wa kwanza wa kiume ataiweka misingi yake; kwa gharama ya mtoto wake wa mwisho atayaweka malango yake.”
27 Tako je bil Gospod z Józuetom in njegova slava je bila razglašena po vsej deželi.
Hivyo Bwana alikuwa pamoja na Yoshua, na sifa zake zikaenea katika nchi yote.