< Jona 1 >

1 Torej Gospodova beseda je prišla k Jonu, Amitájevemu sinu, rekoč:
Neno la Bwana lilimjia Yona mwana wa Amitai:
2 »Vstani, pojdi v Ninive, to veliko mesto in kliči zoper njega, kajti njihova zlobnost je prišla predme.«
“Nenda katika mji mkubwa wa Ninawi ukahubiri juu yake, kwa sababu uovu wake umekuja juu mbele zangu.”
3 Toda Jona se je dvignil, da pred Gospodovo prisotnostjo zbeži v Taršíš in je odšel dol v Jopo in našel ladjo, ki je šla v Taršíš. Tako je plačal njeno voznino in odšel dol vanjo, da gre z njimi v Taršíš, proč od Gospodove prisotnosti.
Lakini Yona alimkimbia Bwana na kuelekea Tarshishi. Alishuka mpaka Yafa, ambapo alikuta meli iliyokuwa imepangwa kuelekea bandari ile. Baada ya kulipa nauli, akapanda melini na kuelekea Tarshishi ili kumkimbia Bwana.
4 Toda Gospod je na morje odposlal velik veter in tam na morju je bil mogočen vihar, tako da je ladjo hotel zlomiti.
Ndipo Bwana akatuma upepo mkali baharini, nayo dhoruba kali sana ikavuma hata meli ikawa hatarini kuvunjika.
5 Potem so bili mornarji prestrašeni in vsak je klical k svojemu bogu in odvrgli [so] blago, ki je bilo na ladji, v morje, da jo olajšajo. Jona pa je odšel dol med ladijske boke in legel ter trdno zaspal.
Mabaharia wote waliogopa na kila mmoja akamlilia mungu wake mwenyewe. Nao wakatupa mizigo baharini ili meli ipungue uzito. Lakini Yona alikuwa ameteremkia chumba cha ndani ya meli, mahali ambapo alilala na kupatwa na usingizi mzito.
6 Tako je kapitan prišel k njemu in mu rekel: »Kaj ti misliš, oh zaspanec? Vstani, kliči k svojemu Bogu, če je tako, da bo Bog mislil na nas, da se ne pogubimo.«
Nahodha akamwendea na kusema, “Wewe unawezaje kulala? Amka ukamwite mungu wako! Huenda akatuangalia, tusiangamie.”
7 In rekli so vsak svojemu tovarišu: »Pridimo in mečimo žrebe, da bomo lahko izvedeli zaradi čigavega vzroka je nad nami to zlo.« Tako so metali žrebe in žreb je padel na Jona.
Kisha mabaharia wakasemezana wao kwa wao, “Njooni, tupige kura tumtafute anayehusika na maafa haya.” Wakapiga kura, kura ikamwangukia Yona.
8 Potem so mu rekli: »Povej nam, prosimo te, zaradi čigavega vzroka je nad nami to zlo. Kakšen je tvoj poklic? In od kod prihajaš? Katera je tvoja dežela? In iz katerega ljudstva si?«
Kwa hiyo walimuuliza, “Tuambie, ni nani anayehusika kwa kutuletea tatizo hili lote? Unafanya kazi gani? Umetoka wapi? Nchi yako ni ipi? Wewe ni kutoka taifa lipi?”
9 Rekel jim je: »Jaz sem Hebrejec in se bojim Gospoda, Boga nebes, ki je naredil morje in kopno zemljo.«
Akajibu, “Mimi ni Mwebrania, nami namwabudu Bwana, Mungu wa Mbinguni, aliyeumba bahari na nchi kavu.”
10 Potem so bili ljudje silno prestrašeni in mu rekli: »Zakaj si to storil?« Kajti ljudje so vedeli, da je pobegnil izpred Gospodovega obličja, ker jim je povedal.
Hili liliwaogopesha nao wakamuuliza, “Umefanya nini?” (Walijua alikuwa anamkimbia Bwana, kwa sababu alishawaambia hivyo.)
11 Potem so mu rekli: »Kaj naj ti storimo, da se nam morje lahko umiri?« Kajti morje se je maščevalo in bilo viharno.
Bahari ilikuwa inazidi kuchafuka. Kwa hiyo walimuuliza, “Tukutendee nini ili kufanya bahari itulie kwa ajili yetu?”
12 Rekel jim je: »Vzemite me in me vrzite v morje. Tako se vam bo morje umirilo, kajti vem, da je zaradi mene ta veliki vihar nad vami.«
Akawajibu, “Niinueni mnitupe baharini, nayo itakuwa shwari. Ninajua mawimbi haya makubwa yamewatokea kwa ajili ya kosa langu.”
13 Kljub temu so možje trdo veslali, da jo privedejo k obali, toda niso mogli, kajti morje se je maščevalo in bilo viharno proti njim.
Badala yake, wale watu walijitahidi kupiga makasia wawezavyo ili wapate kurudi pwani. Lakini hawakuweza, kwa kuwa bahari ilizidi kuchafuka kuliko mwanzo.
14 Zato so klicali h Gospodu in rekli: »Rotimo te, oh Gospod, rotimo te, naj se ne pogubimo zaradi življenja tega moža in ne položi na nas nedolžne krvi, kajti ti, oh Gospod, si storil, kakor ti je ugajalo.«
Ndipo wakamlilia Bwana, “Ee Bwana, tafadhali usituue kwa kuondoa uhai wa mtu huyu. Usituhesabie hatia kwa kuutoa uhai wa mtu asiyekuwa na hatia, kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umefanya kama ilivyokupendeza.”
15 Tako so vzeli Jona in ga vrgli v morje in morje je odnehalo od svojega besnenja.
Kisha walimchukua Yona, wakamtupa baharini nayo bahari iliyokuwa imechafuka ikatulia.
16 Potem so se možje silno zbali Gospoda in Gospodu darovali klavno daritev in naredili zaobljube.
Katika jambo hili watu wakamwogopa Bwana sana, wakamtolea Bwana dhabihu na kumwekea nadhiri.
17 Torej Gospod je pripravil veliko ribo, da je pogoltnila Jona. In Jona je bil v ribjem trebuhu tri dni in tri noči.
Lakini Bwana akamwandaa nyangumi kummeza Yona, naye Yona alikuwa ndani ya tumbo la nyangumi kwa siku tatu, usiku na mchana.

< Jona 1 >