< Janez 6 >

1 Po teh besedah se je Jezus peljal preko Galilejskega morja, kar je Tiberijsko morje.
Baada ya haya, Yesu alikwenda ngʼambo ya Bahari ya Galilaya, ambayo pia huitwa Bahari ya Tiberia.
2 Sledila mu je velika množica, ker so videli njegove čudeže, ki jih je storil na teh, ki so bili bolni.
Umati mkubwa wa watu uliendelea kumfuata, kwa sababu waliona ishara nyingi za miujiza alizofanya kwa wagonjwa.
3 In Jezus je odšel gor na goro ter tam sédel s svojimi učenci.
Kisha Yesu akapanda mlimani akaketi huko pamoja na wanafunzi wake.
4 In blizu je bila pasha, judovski praznik.
Pasaka ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.
5 Ko je Jezus tedaj povzdignil svoje oči in zagledal k njemu prihajati veliko skupino, reče Filipu: »Od kod naj kupimo kruha, da bodo ti lahko jedli?«
Yesu alipotazama na kuuona ule umati mkubwa wa watu ukimjia, akamwambia Filipo, “Tutanunua wapi mikate ili watu hawa wale?”
6 To pa je rekel, da bi ga preizkusil, kajti sam je vedel, kaj bo storil.
Aliuliza swali hili kumpima, kwa maana alishajua la kufanya.
7 Filip mu je odgovoril: »Dvesto denarjev kruha zanje ni zadosti, da bi vsak izmed njih lahko nekaj vzel.«
Filipo akamjibu, “Hata fedha kiasi cha dinari mia mbili, hazitoshi kununua mikate ya kuwapa watu hawa ili kila mtu apate kidogo.”
8 Eden izmed njegovih učencev, Andrej, brat Simona Petra, mu reče:
Mmoja wa wanafunzi wake aitwaye Andrea, ndugu yake Simoni Petro, akamwambia,
9 »Tukaj je deček, ki ima pet ječmenovih hlebov in dve majhni ribi. Toda kaj je to med tako mnogimi?«
“Hapa kuna mvulana mmoja mwenye mikate mitano ya shayiri na samaki wawili wadogo. Lakini hivi vitatosha nini kwa umati huu wote?”
10 In Jezus je dejal: »Storite, da se ljudje usedejo.« Torej na tem kraju je bilo mnogo trave. Tako so se ljudje usedli, po številu okoli pet tisoč.
Yesu akasema, “Waketisheni watu chini.” Palikuwa na majani mengi katika eneo lile, nao watu wakaketi. Palikuwa na wanaume wapatao 5,000.
11 In Jezus je vzel hlebe in ko se je zahvalil, je razdelil učencem in učenci tem, ki so se usedli, in podobno od rib, toliko, kolikor so hoteli.
Ndipo Yesu akachukua ile mikate, akamshukuru Mungu na kuwagawia wale watu waliokuwa wameketi. Akafanya vivyo hivyo na wale samaki. Kila mtu akapata kadiri alivyotaka.
12 Ko so bili nasičeni, je svojim učencem rekel: »Zberite odlomke, ki ostanejo, da ne bo nič izgubljeno.«
Watu wote walipokwisha kula na kushiba, akawaambia wanafunzi wake, “Kusanyeni vipande vilivyobaki vya ile mikate, kisipotee chochote.”
13 Zato so jih zbrali skupaj in napolnili dvanajst košar z odlomki od petih ječmenovih hlebov, ki so ostali vrh tega tem, ki so jedli.
Hivyo wakavikusanya, wakajaza vikapu kumi na viwili kwa vipande vya ile mikate mitano ya shayiri na samaki wale wawili wadogo vilivyobakishwa na waliokula.
14 Tedaj so ti ljudje, ko so videli čudež, ki ga je Jezus storil, rekli: »To je resnično ta prerok, ki naj bi prišel na svet.«
Baada ya watu kuona muujiza ule Yesu aliofanya, walianza kusema, “Hakika huyu ndiye Nabii ajaye ulimwenguni!”
15 Ko je torej Jezus zaznal, da bodo prišli in ga s silo odvedli, da ga postavijo za kralja, je ponovno sam odšel na goro.
Yesu akijua kwamba walitaka kuja kumfanya awe mfalme wao, kwa nguvu, akajitenga nao akaenda milimani peke yake.
16 In sedaj, ko je prišel večer, so njegovi učenci odšli dol k morju
Ilipofika jioni, wanafunzi wake waliteremka kwenda baharini.
17 in vstopili na ladjo ter se preko morja peljali proti Kafarnáumu. Bilo pa je že temno in Jezus ni prišel k njim.
Wakaingia kwenye mashua, wakaanza kuvuka bahari kwenda Kapernaumu. Wakati huu kulikuwa tayari giza na Yesu alikuwa hajajumuika nao.
18 Zaradi velikega vetra, ki je pihal, se je morje vzdignilo.
Bahari ikachafuka kwa sababu upepo mkali ulikuwa unavuma.
19 Ko so preveslali že okoli petindvajset ali trideset dolžin brazd, so zagledali Jezusa hoditi po morju in prihajati bliže k ladji in bili so prestrašeni.
Wanafunzi walipokuwa wamekwenda mwendo wa karibu maili tatu au nne, walimwona Yesu akitembea juu ya maji akikaribia mashua, nao wakaogopa sana.
20 Toda on jim reče: »Jaz sem, ne bodite prestrašeni.«
Lakini Yesu akawaambia, “Ni mimi. Msiogope.”
21 Potem so ga voljno sprejeli na ladjo in ladja je bila takoj pri deželi, kamor so šli.
Ndipo wakamkaribisha kwa furaha ndani ya mashua, na mara wakafika ufuoni walikokuwa wakienda.
22 Naslednjega dne, ko je množica, ki je stala na drugi strani morja, videla, da tam ni bilo nobenega drugega čolna, razen tistega, v katerega so vstopili njegovi učenci in da Jezus s svojimi učenci ni vstopil na čoln, temveč, da so njegovi učenci odšli sami
Siku iliyofuata, wale watu waliokuwa wamebaki ngʼambo waliona kwamba palikuwepo na mashua moja tu na kwamba Yesu hakuwa ameondoka pamoja na wanafunzi wake, ila walikuwa wameondoka peke yao.
23 (čeprav so iz Tiberije prišli drugi čolni v bližino kraja, kjer so jedli kruh, potem ko se je Gospod zahvalil);
Lakini zikaja mashua nyingine kutoka Tiberia zikafika karibu na mahali pale walipokula mikate baada ya Bwana kumshukuru Mungu.
24 ko je množica torej videla, da Jezusa ni bilo tam niti njegovih učencev, so se tudi sami, ker so iskali Jezusa, vkrcali in prišli v Kafarnáum.
Mara wale watu wakatambua kwamba Yesu hakuwepo hapo, wala wanafunzi wake. Wakaingia kwenye mashua hizo, wakaenda Kapernaumu ili kumtafuta Yesu.
25 In ko so ga našli na drugi strani morja, so mu rekli: »Rabi, kdaj si prišel sèm?«
Walipomkuta Yesu ngʼambo ya bahari wakamuuliza, “Rabi, umefika lini huku?”
26 Jezus jim je odgovoril in rekel: »Resnično, resnično, povem vam: ›Ne iščete me, ker ste videli čudeže, temveč ker ste jedli od hlebov in bili nasičeni.‹
Yesu akawajibu, “Amin, amin nawaambia, ninyi hamnitafuti kwa kuwa mliona ishara na miujiza, bali kwa sababu mlikula ile mikate mkashiba.
27 Ne trudite se za jed, ki propada, temveč za jed, ki vzdrži v večno življenje, ki vam jo bo dal Sin človekov, kajti njega je potrdil Oče Bog.« (aiōnios g166)
Msishughulikie chakula kiharibikacho, bali chakula kidumucho hata uzima wa milele, ambacho Mwana wa Adamu atawapa. Yeye ndiye ambaye Mungu Baba amemtia muhuri.” (aiōnios g166)
28 Tedaj so mu rekli: »Kaj naj storimo, da bomo lahko delali Božja dela?«
Ndipo wakamuuliza, “Tufanye nini ili tupate kuitenda kazi ya Mungu?”
29 Jezus je odgovoril in jim rekel: »Božje delo je to, da verujete v tistega, ki ga je on poslal.«
Yesu akawajibu, “Kazi ya Mungu ndiyo hii: Mwaminini yeye aliyetumwa naye.”
30 Rekli so mu torej: »Kakšno znamenje torej pokažeš, da bomo lahko videli in ti verovali? Kaj delaš?
Hivyo wakamuuliza, “Utafanya ishara gani ya muujiza, ili tuione tukuamini? Utafanya jambo gani?
31 Naši očetje so v puščavi jedli mano, kakor je pisano: ›Kruh iz nebes jim je dajal jesti.‹«
Baba zetu walikula mana jangwani, kama ilivyoandikwa, ‘Aliwapa mikate kutoka mbinguni ili wale.’”
32 Potem jim je Jezus rekel: »Resnično, resnično, povem vam: ›Ni vam Mojzes dal tega kruha iz nebes, temveč vam moj Oče daje resničen kruh iz nebes.‹
Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, si Mose aliyewapa mikate kutoka mbinguni, bali Baba yangu ndiye anawapa mkate wa kweli kutoka mbinguni.
33 Kajti Božji kruh je tisti, ki prihaja dol iz nebes in daje svetu življenje.«
Kwa maana mkate wa Mungu ni yule ashukaye kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima.”
34 Tedaj so mu rekli: »Gospod, vselej nam daj tega kruha.«
Wakamwambia, “Bwana, kuanzia sasa tupatie huo mkate siku zote.”
35 In Jezus jim je rekel: »Jaz sem kruh življenja. Kdor prihaja k meni, ne bo nikoli lačen. In kdor vame veruje, ne bo nikoli žejen.
Yesu akawaambia, “Mimi ndimi mkate wa uzima. Yeye ajaye kwangu, hataona njaa kamwe na yeye aniaminiye, hataona kiu kamwe.
36 Toda rekel sem vam: ›Da ste me vi tudi videli, pa ne verujete.‹
Lakini kama nilivyowaambia, mmeniona lakini bado hamwamini.
37 Vse, kar mi daje Oče, bo prišlo k meni, in tistega, ki prihaja k meni, nikakor ne bom izgnal ven.
Wale wote anipao Baba watakuja kwangu na yeyote ajaye kwangu, sitamfukuzia nje kamwe.
38 Kajti prišel sem dol iz nebes, ne da delam svojo lastno voljo, temveč voljo tistega, ki me je poslal.
Kwa kuwa nimeshuka kutoka mbinguni si ili kufanya mapenzi yangu, bali mapenzi yake yeye aliyenituma.
39 In to je volja Očeta, ki me je poslal, da od vsega, kar mi je dal, ne bi ničesar izgubil, temveč bi ob poslednjem dnevu to ponovno dvignil.
Haya ndiyo mapenzi yake yeye aliyenituma, kwamba, nisimpoteze hata mmoja wa wale alionipa, bali niwafufue siku ya mwisho.
40 In to je volja tistega, ki me je poslal, da bo vsakdo, ki vidi Sina in veruje vanj, lahko imel večno življenje in jaz ga bom dvignil na poslednji dan.« (aiōnios g166)
Kwa maana mapenzi ya Baba yangu ni kwamba kila mmoja amtazamaye, Mwana na kumwamini awe na uzima wa milele, nami nitawafufua siku ya mwisho.” (aiōnios g166)
41 Judje so tedaj godrnjali nad njim, ker je rekel: »Jaz sem kruh, ki je prišel dol iz nebes.«
Wayahudi wakaanza kunungʼunika kwa kuwa alisema, “Mimi ndimi mkate ulioshuka kutoka mbinguni.”
42 In govorili so: »Ali ni to Jezus, Jožefov sin, katerega očeta in mater poznamo? Kako to potem, da pravi: ›Prišel sem dol iz nebes?‹«
Wakasema, “Huyu si Yesu, mwana wa Yosefu, ambaye baba yake na mama yake tunawajua? Anawezaje basi sasa kusema, ‘Nimeshuka kutoka mbinguni’?”
43 Jezus je torej odgovoril in jim rekel: »Ne godrnjajte med seboj.
Hivyo Yesu akawaambia, “Acheni kunungʼunikiana ninyi kwa ninyi.
44 Nihče ne more priti k meni, razen če ga ne pritegne Oče, ki me je poslal in jaz ga bom dvignil na poslednji dan.
Hakuna mtu awezaye kuja kwangu kama asipovutwa na Baba aliyenituma, nami nitamfufua siku ya mwisho.
45 V prerokih je pisano: ›In vsi bodo poučeni od Boga.‹ Vsak torej, ki je slišal in se naučil od Očeta, prihaja k meni.
Imeandikwa katika Manabii, ‘Wote watafundishwa na Mungu.’ Yeyote amsikilizaye Baba na kujifunza kutoka kwake, huyo huja kwangu.
46 Ne da je katerikoli človek videl Očeta, samo tisti, ki je od Boga, on je videl Očeta.
Hakuna mtu yeyote aliyemwona Baba isipokuwa yeye atokaye kwa Mungu, yeye ndiye peke yake aliyemwona Baba.
47 Resnično, resnično, povem vam: ›Kdor veruje vame, ima večno življenje.‹ (aiōnios g166)
Amin, amin nawaambia, yeye anayeamini anao uzima wa milele. (aiōnios g166)
48 Jaz sem ta kruh življenja.
Mimi ni mkate wa uzima.
49 Vaši očetje so v divjini jedli mano in so mrtvi.
Baba zenu walikula mana jangwani, lakini wakafa.
50 To je kruh, ki prihaja dol iz nebes, da lahko človek od tega jé in ne umre.
Lakini hapa kuna mkate utokao mbinguni, ambao mtu yeyote akiula, hatakufa.
51 Jaz sem živi kruh, ki je prišel dol iz nebes. Če katerikoli človek od tega kruha jé, bo živel večno, in kruh, ki ga bom jaz dal, je moje meso, ki ga bom dal za življenje sveta.« (aiōn g165)
Mimi ni mkate wa uzima ule uliotoka mbinguni. Mtu yeyote akiula mkate huu, ataishi milele. Mkate huu ni mwili wangu, ambao nitautoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.” (aiōn g165)
52 Judje so se torej med seboj prepirali, rekoč: »Kako nam lahko ta človek da jesti svoje meso?«
Ndipo Wayahudi wakaanza kuhojiana vikali wao kwa wao wakisema, “Mtu huyu awezaje kutupatia mwili wake tuule?”
53 Tedaj jim je Jezus rekel: »Resnično, resnično, povem vam: ›Razen, če ne jeste mesa Sina človekovega in ne pijete njegove krvi, v sebi nimate življenja.
Hivyo Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, msipoula mwili wa Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu.
54 Kdorkoli jé moje meso in pije mojo kri, ima večno življenje in jaz ga bom dvignil na poslednji dan.‹ (aiōnios g166)
Mtu yeyote aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, anao uzima wa milele. Nami nitamfufua siku ya mwisho. (aiōnios g166)
55 Kajti zares je moje meso hrana in zares je moja kri pijača.
Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli na damu yangu ni kinywaji cha kweli.
56 Kdor jé moje meso in pije mojo kri, prebiva v meni in jaz v njem.
Yeyote alaye mwili wangu na kunywa damu yangu, atakaa ndani yangu nami nitakaa ndani yake.
57 Kakor me je poslal živi Oče in jaz živim po Očetu. Ravno tako, kdor mene jé, celó ta bo živel po meni.
Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, na kama nami ninavyoishi kwa sababu ya Baba, hivyo anilaye mimi ataishi kwa sababu yangu.
58 To je ta kruh, ki je prišel dol iz nebes. Ne kakor vaši očetje, ki so jedli mano in so mrtvi. Kdor jé od tega kruha, bo živel večno.« (aiōn g165)
Huu ndio mkate ushukao kutoka mbinguni, si kama ule mkate baba zenu waliokula nao wakafa. Lakini yeye aulaye mkate huu ataishi milele.” (aiōn g165)
59 Te stvari je povedal v sinagogi, ko je učil v Kafarnáumu.
Yesu alisema maneno haya alipokuwa akifundisha katika sinagogi huko Kapernaumu.
60 Zatorej so mnogi izmed njegovih učencev, ko so to slišali, rekli: »To je trda beseda, kdo jo lahko posluša?«
Wengi wa wafuasi wake waliposikia jambo hili wakasema, “Mafundisho haya ni magumu. Ni nani awezaye kuyapokea?”
61 Potem ko je Jezus v sebi vedel, da so njegovi učenci nad tem godrnjali, jim je rekel: »Ali vas to pohujšuje?
Yesu alipojua kwamba wafuasi wake wananungʼunika kuhusu mafundisho yake, akawaambia, “Je, jambo hili limewaudhi?
62 Kaj pa, če boste videli Sina človekovega dvigniti se gor, kjer je bil prej?
Ingekuwaje basi kama mngemwona Mwana wa Adamu akipaa kwenda zake huko alipokuwa kwanza?
63 Duh je, ki oživlja, meso nič ne koristi. Besede, ki vam jih govorim, te so duh in te so življenje.
Roho ndiye atiaye uzima, mwili haufai kitu. Maneno haya niliyowaambia ni Roho tena ni uzima.
64 Toda tam so nekateri izmed vas, ki ne verujejo.« Kajti Jezus je že od začetka vedel kdo so bili ti, ki niso verovali in kdo naj bi ga izdal.
Lakini baadhi yenu hamwamini.” Kwa maana Yesu alifahamu tangu mwanzo wale ambao hawangemwamini miongoni mwao na yule ambaye angemsaliti.
65 In rekel je: »Zato sem vam rekel, da nihče ne more priti k meni, razen če mu ni dano od mojega Očeta.«
Akaendelea kusema, “Hii ndiyo sababu niliwaambia kwamba hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba yangu.”
66 Od tega časa je mnogo izmed njegovih učencev odšlo nazaj in niso več hodili z njim.
Tangu wakati huo wafuasi wake wengi wakarejea nyuma wakaacha kumfuata.
67 Tedaj je Jezus dvanajsterim rekel: »Ali hočete tudi vi oditi?«
Hivyo Yesu akawauliza wale wanafunzi wake kumi na wawili, “Je, ninyi pia mnataka kuondoka?”
68 Potem mu je Simon Peter odgovoril: »Gospod, h komu naj gremo? Ti imaš besede večnega življenja. (aiōnios g166)
Simoni Petro akamjibu, “Bwana, tuondoke twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele. (aiōnios g166)
69 In mi verujemo in smo prepričani, da si ti ta Kristus, Sin živega Boga.«
Tunaamini na kujua kuwa wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu.”
70 Jezus jim je odgovoril: »Ali vas nisem izbral dvanajst in je eden izmed vas hudič?«
Ndipo Yesu akajibu, “Je, sikuwachagua ninyi kumi na wawili? Lakini mmoja wenu ni ibilisi.”
71 Govoril je o Judu Iškarijotu, Simonovem sinu, kajti on je bil ta, ki naj bi ga izdal in je izmed dvanajsterice.
(Hapa alikuwa anasema juu ya Yuda, mwana wa Simoni Iskariote. Ingawa alikuwa mmoja wa wale kumi na wawili, ndiye ambaye baadaye angemsaliti Yesu.)

< Janez 6 >