< Janez 11 >

1 Torej nek mož je bil bolan, po imenu Lazar, iz Betanije, mesta Marije in njene sestre Marte.
Basi mtu mmoja jina lake Lazaro alikuwa mgonjwa. Yeye alikuwa akiishi Bethania kijiji cha Maria na Martha dada zake.
2 (Marija je bila tista, ki je Gospoda mazilila z mazilom in je s svojimi lasmi obrisala njegova stopala, katere brat Lazar je bil bolan.)
Huyu Maria, ambaye Lazaro kaka yake alikuwa mgonjwa, ndiye yule ambaye alimpaka Bwana mafuta na kuifuta miguu yake kwa nywele zake.
3 Zato sta njegovi sestri poslali k njemu, rekoč: »Gospod, glej, tisti, ki ga imaš rad, je bolan.«
Hivyo hawa dada wawili walituma ujumbe kwa Yesu kumwambia, “Bwana, yule umpendaye ni mgonjwa.”
4 Ko je Jezus to slišal, je rekel: »Ta bolezen ni za smrt, temveč za Božjo slavo, da bo Božji Sin s tem lahko proslavljen.«
Lakini Yesu aliposikia hayo, akasema, “Ugonjwa huu hautaleta mauti bali umetokea ili kudhihirisha utukufu wa Mungu, ili Mwana wa Mungu apate kutukuzwa kutokana na ugonjwa huu.”
5 Torej Jezus je ljubil Marto in njeno sestro ter Lazarja.
Pamoja na hivyo, ingawa Yesu aliwapenda Martha, Maria na Lazaro ndugu yao,
6 Ko je torej slišal, da je bil bolan, je še dva dni ostal na istem kraju, kjer je bil.
baada ya kusikia kwamba Lazaro ni mgonjwa, aliendelea kukawia huko alikokuwa kwa siku mbili zaidi.
7 Šele nató reče svojim učencem: »Ponovno pojdimo v Judejo.«
Ndipo akawaambia wanafunzi wake, “Haya, turudi Uyahudi.”
8 Njegovi učenci mu rečejo: »Učitelj, Judje so si nedavno prizadevali, da te kamnajo, ti pa greš ponovno tja?«
Wanafunzi wake wakamwambia, “Rabi, Wayahudi walikuwa wanataka kukupiga mawe, nawe unataka kurudi huko?”
9 Jezus je odgovoril: »Ali ni v dnevu dvanajst ur? Če katerikoli človek hodi podnevi, se ne spotika, ker vidi svetlobo tega sveta.
Yesu akawajibu, “Si kuna saa kumi na mbili za mchana katika siku moja? Wala watembeao mchana hawawezi kujikwaa kwa maana wanaona nuru ya ulimwengu huu.
10 Toda če človek hodi ponoči, se spotika, ker v njem ni svetlobe.«
Lakini wale watembeao usiku hujikwaa kwa sababu hakuna nuru ndani yao.”
11 Te besede je rekel in nató jim reče: »Naš prijatelj Lazar spi, vendar grem, da ga lahko zbudim iz spanja.«
Baada ya kusema haya, Yesu akawaambia, “Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini naenda kumwamsha.”
12 Tedaj so njegovi učenci rekli: »Gospod, če spi, bo okreval.«
Wanafunzi wakamwambia, “Bwana, kama amelala usingizi ataamka.”
13 Vendar je Jezus govoril o njegovi smrti, toda mislili so, da je govoril o počitku v spanju.
Hata hivyo, Yesu alikuwa anazungumzia kuwa Lazaro amekufa, lakini wanafunzi wake hawakuelewa, walidhani kwamba anasema Lazaro amelala usingizi tu.
14 Tedaj jim je Jezus odkrito povedal: »Lazar je mrtev.
Kwa hiyo Yesu akawaambia waziwazi, “Lazaro amekufa.
15 Zaradi vas pa sem vesel, da nisem bil tam, z namenom, da boste lahko verovali, vendar pojdimo k njemu.«
Hata hivyo nafurahi kwa kuwa sikuwepo huko kabla ya Lazaro kufa, ili mpate kuamini. Lakini sasa twendeni kwake.”
16 Tedaj je Tomaž, ki se je imenoval Dvojček, rekel svojim součencem: »Naj gremo tudi mi, da bomo lahko umrli z njim.«
Tomaso aliyeitwa Pacha akawaambia wanafunzi wenzake, “Sisi nasi twendeni tukafe pamoja naye.”
17 Potem ko je Jezus prišel, je odkril, da je že štiri dni ležal v grobu.
Yesu alipowasili huko alikuta Lazaro amekuwa kaburini siku nne.
18 Torej Betanija je bila blizu Jeruzalema, okoli petnajst dolžin brazd proč
Basi Bethania ulikuwa karibu na Yerusalemu umbali wa karibu maili mbili,
19 in mnogi izmed Judov so prišli k Marti in Mariji, da ju tolažijo glede njunega brata.
na Wayahudi wengi walikuwa wamekuja kuwafariji Martha na Maria kwa ajili ya kufiwa na ndugu yao.
20 Potem je Marta, takoj ko je slišala, da je prihajal Jezus, odšla in ga srečala, toda Marija je še vedno sedela v hiši.
Martha aliposikia kwamba Yesu anakuja, alitoka kwenda kumlaki, ila Maria alibaki nyumbani.
21 Tedaj je Marta rekla Jezusu: »Gospod, če bi bil ti tukaj, moj brat ne bi umrl.
Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, ndugu yangu hangalikufa.
22 Toda jaz vem, da celó sedaj, karkoli hočeš prositi od Boga, ti bo Bog to dal.«
Lakini sasa ninajua kuwa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa.”
23 Jezus ji reče: »Tvoj brat bo ponovno vstal.«
Yesu akamwambia, “Ndugu yako atafufuka.”
24 Marta mu reče: »Vem, da bo ponovno vstal na vstajenje ob poslednjem dnevu.«
Martha akamjibu, “Ninajua ya kuwa atafufuka wakati wa ufufuo wa wafu siku ya mwisho.”
25 Jezus ji je rekel: »Jaz sem vstajenje in življenje. Kdor vame veruje, četudi bi bil mrtev, bo vendarle živel.
Yesu akamwambia, “Mimi ndiye huo ufufuo na uzima. Yeye aniaminiye mimi, hata akifa atakuwa anaishi
26 In kdorkoli živi in veruje vame, ne bo nikoli umrl. Veruješ to?« (aiōn g165)
na yeyote aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je, unasadiki haya?” (aiōn g165)
27 Ona mu reče: »Da, Gospod. Verujem, da si ti Kristus, Božji Sin, ki naj bi prišel na svet.«
Martha akamwambia, “Ndiyo Bwana, ninaamini ya kuwa wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yeye ajaye ulimwenguni.”
28 In ko je tako rekla, je šla svojo pot in na skrivnem poklicala svojo sestro Marijo, rekoč: »Učitelj je prišel in te kliče.«
Baada ya kusema haya Martha alikwenda, akamwita Maria dada yake faraghani na kumwambia, “Mwalimu yuko hapa anakuita.”
29 Brž ko je ona to zaslišala, je hitro vstala in prišla k njemu.
Maria aliposikia hivyo, akaondoka upesi akaenda mpaka alipokuwa Yesu.
30 Torej Jezus še ni prišel v mesto, temveč je bil na kraju, kjer ga je srečala Marta.
Yesu alikuwa hajaingia kijijini, bali alikuwa bado yuko mahali pale alipokutana na Martha.
31 Ko so Judje, ki so bili z njo v hiši in jo tolažili, videli Marijo, da je v naglici vstala in odšla ven, so ji potem sledili, rekoč: »H grobu gre, da bi tam jokala.«
Wale Wayahudi waliokuwa pamoja na Maria nyumbani wakimfariji walipoona ameondoka haraka na kutoka nje, walimfuata wakidhani ya kwamba alikuwa anakwenda kule kaburini kulilia huko.
32 Torej ko je Marija prišla tja, kjer je bil Jezus in ga zagledala, je padla dol k njegovim stopalom in mu rekla: »Gospod, če bi bil ti tukaj, moj brat ne bi umrl.«
Maria alipofika mahali pale Yesu alipokuwa, alipiga magoti miguuni Pake na kusema, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, ndugu yangu hangalikufa.”
33 Ko jo je Jezus torej videl jokajočo in jokajoče tudi Jude, ki so prišli z njo, je v duhu zastokal in bil vznemirjen
Yesu alipomwona Maria akilia na wale Wayahudi waliokuja pamoja naye pia wakilia, Yesu alisikia uchungu moyoni, akafadhaika sana.
34 ter rekel: »Kam ste ga položili?« Rekli so mu: »Gospod, pridi in poglej.«
Akauliza, “Mmemweka wapi?” Wakamwambia, “Bwana, njoo upaone.”
35 Jezus se je zjokal.
Yesu akalia machozi.
36 Tedaj so Judje rekli: »Glejte, kako ga je imel rad!«
Ndipo Wayahudi wakasema, “Tazama jinsi alivyompenda Lazaro!”
37 Nekateri izmed njih pa so rekli: »Mar ni mogel ta človek, ki je slepemu odprl oči, storiti, da ta mož sploh ne bi umrl?«
Lakini wengine wakasema, “Je, yule aliyefungua macho ya kipofu, hakuweza kumfanya na huyu asife?”
38 Jezus torej, v sebi ponovno stokajoč, pride h grobu. To je bila votlina in nanjo je bil položen kamen.
Yesu kwa mara nyingine akiwa amefadhaika sana, akafika penye kaburi. Hilo kaburi lilikuwa pango ambalo jiwe lilikuwa limewekwa kwenye ingilio lake.
39 Jezus je rekel: »Odstranite kamen proč.« Marta, sestra tega, ki je bil mrtev, mu reče: »Gospod, do sedaj že zaudarja, kajti mrtev je štiri dni.«
Yesu akasema, “Liondoeni hilo jiwe.” Martha ndugu yake yule aliyekuwa amekufa akasema, “Lakini Bwana, wakati huu atakuwa ananuka kwani amekwisha kuwa kaburini siku nne.”
40 Jezus ji reče: »Kaj ti nisem rekel, da če boš verovala, boš videla Božjo slavo?«
Yesu akamwambia, “Sikukuambia kwamba kama ukiamini utauona utukufu wa Mungu?”
41 Tedaj so odstranili kamen z mesta, kamor je bil mrtvi položen. Jezus pa je povzdignil svoje oči in rekel: »Oče, hvala ti, da si me uslišal.
Kwa hiyo wakaliondoa lile jiwe kutoka kaburini. Yesu akainua macho yake juu akasema, “Baba, ninakushukuru kwa kuwa wanisikia.
42 In vedel sem, da me ti vedno uslišiš, toda to sem rekel zaradi množice, ki stoji zraven, da bi lahko verovala, da si me ti poslal.«
Ninajua ya kuwa wewe hunisikia siku zote, lakini nimesema haya kwa ajili ya umati huu uliosimama hapa, ili wapate kuamini ya kuwa wewe umenituma.”
43 In ko je tako govoril, je z močnim glasom zaklical: »Lazar, pridi naprej.«
Baada ya kusema haya, Yesu akapaza sauti yake akaita, “Lazaro, njoo huku!”
44 In tisti, ki je bil mrtev, je prišel naprej, z rokami in nogami, povezanimi s pogrebnimi oblačili in njegov obraz je bil naokoli povezan s prtičem. Jezus jim reče: »Odvežite ga in ga pustite oditi.«
Yule aliyekuwa amekufa akatoka nje, mikono yake na miguu yake ikiwa imeviringishiwa vitambaa vya kitani na leso usoni pake. Yesu akawaambia, “Mfungueni, mwacheni aende zake.”
45 Potem so mnogi izmed Judov, ki so prišli k Mariji in videli stvari, ki jih je Jezus storil, verovali vanj.
Hivyo Wayahudi wengi waliokuwa wamekuja kumfariji Maria, walipoona yale Yesu aliyoyatenda wakamwamini.
46 Toda nekateri izmed njih so odšli po svojih poteh k farizejem in jim povedali, kakšne stvari je Jezus storil.
Lakini baadhi yao wakaenda kwa Mafarisayo na kuwaambia mambo Yesu aliyoyafanya.
47 Tedaj so visoki duhovniki in farizeji zbrali véliki zbor ter rekli: »Kaj [naj] storimo? Kajti ta človek dela mnoge čudeže.
Kwa hiyo viongozi wa makuhani na Mafarisayo wakaita mkutano wa baraza. Wakaulizana, “Tufanyeje? Huyu mtu anafanya ishara nyingi.
48 Če ga pustimo tako pri miru, bodo vsi ljudje verovali vanj in prišli bodo Rimljani in odvzeli tako naš prostor kakor narod.«
Kama tukimwacha aendelee hivi, kila mtu atamwamini, nao Warumi watakuja na kupaharibu mahali petu patakatifu na taifa letu.”
49 In eden izmed njih, po imenu Kajfa, ki je bil to isto leto véliki duhovnik, jim je rekel: »Vi čisto nič ne veste,
Mmoja wao aliyeitwa Kayafa, ambaye alikuwa kuhani mkuu mwaka huo, akasema, “Ninyi hamjui kitu chochote!
50 niti ne preudarite, da je za nas koristno, da naj bi en človek umrl za ljudi, ne pa da propade celoten narod.«
Hamjui kwamba ni afadhali mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, kuliko taifa lote liangamie?”
51 To pa ni govoril [sam] od sebe, temveč ker je bil tisto leto véliki duhovnik, je prerokoval, da naj bi Jezus umrl za ta narod,
Hakusema haya kutokana na mawazo yake mwenyewe bali kama kuhani mkuu mwaka huo, alitabiri kuwa Yesu angelikufa kwa ajili ya taifa la Wayahudi,
52 in ne samo za ta narod, temveč da naj bi tudi Božje otroke, ki so bili razkropljeni naokoli, skupaj zbral v enem.
wala si kwa ajili ya taifa hilo pekee, bali pia kwa ajili ya watoto wa Mungu waliotawanyika, ili kuwaleta pamoja na kuwafanya wawe wamoja.
53 Torej so se od tega dne dalje skupaj posvetovali, da ga usmrtijo.
Hivyo tangu siku hiyo wakawa wanafanya mipango ili wamuue Yesu.
54 Jezus torej med Judi ni več hodil javno, temveč je od tam odšel v deželo poleg divjine, v mesto, imenovano Efrájim in tam ostal s svojimi učenci.
Kwa hiyo Yesu akawa hatembei hadharani miongoni mwa Wayahudi, bali alijitenga akaenda sehemu iliyo karibu na jangwa kwenye kijiji kiitwacho Efraimu. Akakaa huko na wanafunzi wake.
55 In blizu je bila judovska pasha in mnogi iz dežele so pred pasho odšli gor v Jeruzalem, da se očistijo.
Basi Pasaka ya Wayahudi ilipokuwa imekaribia, watu wengi walitoka vijijini wakaenda Yerusalemu kabla ya Pasaka ili wakajitakase.
56 Medtem ko so stali v templju, so torej iskali Jezusa in med seboj govorili: »Kaj mislite, da ne bo prišel na praznik?«
Watu wakawa wanamtafuta Yesu, nao waliposimama kwenye eneo la Hekalu waliulizana, Je, mtu huyu hatakuja kamwe kwenye Sikukuu?
57 Torej tako visoki duhovniki kakor farizeji so izdali zapoved, da če katerikoli človek ve, kje bi bil, naj to pokaže, da bi ga lahko prijeli.
Viongozi wa makuhani na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kuwa yeyote atakayejua mahali Yesu aliko, lazima atoe taarifa ili wapate kumkamata.

< Janez 11 >